Wednesday, December 21, 2011

WANACHUO WAPEWA MBINU ZA KUFAULU...


Wanafunzi wanahudhuria vipindi na kuandika kumbukumbu zao
wenyewe wana nafasi kubwa ya kufanya vyema zaidi katika
mitihani yao kuliko wale wenyekuandika nukuu za rafiki zao



 Wanachuo wakifuatilia mhadhara maalumu chuoni kwao. Kumbe mafanikio katika majaribio na mitihani huanza toka mwanzoni kabisa. Jinsi ambavyo mwanafunzi anasoma na kuandika kile anachofundishwa na kujisomea ni muhimu kwa kuwa hiyo humsaidia pia katika utunzaji wa kumbukumbu akili. Hivyo wale waliozoea kuchukua maandishi ya wenzao wapunguze tabia hiyo na badala yake wahudhuria vipindi wawo wenyewe. Kwa habari zaidi soma hapa.

1. Start Studying in School

Studying for tests and quizzes actually starts way before you even know you'll have a test.Good study techniques begin in the classroom as you take notes. Note-taking is a way of remembering what you were taught or what you've read about.
Where's your favorite place to study?
Some keys to note-taking are to write down facts that a teacher mentions or writes on the board during class.If you miss something, ask your teacher to go over the facts with you after class.
Keep your notes organized by subject and making sure they're easy to read and review. This may mean that you need to recopy some notes at home or during a free period while the class is still fresh in your mind.
Unfortunately, most schools don't have classes that teach you how to take notes. When it comes to taking good notes, it can take some experimenting to figure out what works, so don't give up.
Original link:

Saturday, December 17, 2011

Unamfahamu mwanaAfrika huyu?



Thomas Sankara( Desemba 21, 1949 – Oktoba 15, 1987), Che Guevara wa Burkina Faso
Mwana Afrika halisi, mtu mnyofu, mwadilifu, mkweli na mzalendo wa kweli!
Mwanamapinzuzi na rais wa zamani wa Burkina Faso Thomas Isidore Sankara ( 1949 -1987) wiki moja kabla ya kifo chake alisema: “ Wakati wanamapinduzi kama watu binafsi wanaweza kuuwawa, kamwe huwezi kuziua fikra zao za kimapinduzi.”

Thomas Sankara ndiye mtu aliyebadilisha jina la nchi yake; hapo kabla ilijulikana kwa jina la Upper Volta; yeye alibadilisha na kuiita nchi yake Burkina Faso yaani NCHI YA WATU WAADILIFU – Pays des hommes integre” ama land of the upright people” hujulikana pia kama Che Guevara wa Burkina Faso


Kaburi la kawaida kabisa la MwanaAfrika huyo
likiwa limezungukwa na makaburi ya walinzi wake












 Thomas Noel Isidore Sankara alizaliwa Desemba 21, 1949. Alikuwa rais Agost 4, 1983 na huyu ndio hasa kiongozi wa kwanza aliyetambulika kwa kuwa na upendo dhahiri wa nchi yake na ambaye alihimiza kuindeleza nchi yake, kukuza na kuzitambulisha tunu za nchi hiyo na kufanya zifahamike kwa wananchi na kwa mataifa ya nje.

Sankara alipitia mafunzo mbalimbali ya kijeshi. Mwaka 1970 alikwenda Madagaska, 1978 alikwenda Moroko. Alishiriki katika vita ya Mali na Burkina Faso mwaka 1974.


Katika siasa alikuwa na mafanikio; 1981 alikuwa waziri wa habari, waziri mkuu mwaka 1982. Na kati ya 1981 na 82 alifungwa kwa tuhuma za rushwa. Na mwisho katika wigo wa kisiasa aliongoza Chama Kidemokrasia na cha Kimapinduzi hadi alipofanya mapinduzi maarufu ya Agosti 4

Kitu muhimu sana ambacho Sankara alipenda kufanya baada ya kuwa rais ni kuwataka watu wote wawe waadilifu. Alitaka serikali yake ifanye hivyo ili kutoa mfano mzuri kwa vijana na vizazi. Rushwa ilipigwa vita kwa nguvu zote. Mpango huo ulianza rasmi pale alipobadalisha jina la nchi yake. Zaidi alibadilisha pia motto, nembo ya taifa na kuwa " Nchi yetu ama kifo, Tutashinda" wananchi walihimizwa kuwa wazalendo kwa kuungana, kuilinda na kuipenda nchi yao. 
Sankara alikuwa karibu na wananchi alipiga gitaa, alicheza mpira, aliendesha baisikeli na kufanya mambo mengi ambayo yalimuweka karibu na wananchi. Kuhusu uchumi aliwapatia wananchi ardhi wapate maeneo ya kulima, aliondoa mambo kadhaa ya kuwapendelea viongozi; alifanya viongozi wawe kweli watumishi wa wananchi.
















Alifanya mambo mengi sana mazuri; hata hivyo kama wasemavyo waswahili, kizuri hakidumu. Thomas Sankara aliuwawa miaka minne baadaye. Ndani ya miaka minne aliweza kuleta mabadiliko makubwa kuliko ya miongo kadhaa. Vijana wengi barani Afrika walilia hadharani kwa kuwa waliona kuwa ile ndoto ya kuwa na mabadiliko barani Afrika iliondolewa. Wazo muhimu hapa ni je, wewe kijana unachangia nini kuleta maendeleo ya kweli kwa familia yako, jamii yako na kwa upana zaidi kwa nchi yako? Unaweza kusoma zaidi hapa











Sunday, December 11, 2011

Elimu ya kweli ni vitendo!



Elimu ikitafsiriwa kwenye matendo ndo haswa Elimu!























Chuo kikuu cha Makerere, kikishirikiana na vyuo vikuu vingine kimeshiriki katika mradi wa kutengeneza gari linalotumia nguvu ya umeme. Magari ya aina hii yatasaidia katika utunzaji wa mazingira kwani hayatoi moshi na hivyo kutunza mazingira. Changamoto ni kwa vyuo vikuu vingine hususani vile vikongwe, Afrika Mashariki vinafanya nini?

Kupata maelezo vizuri juu ya mradi huu soma hapa



Sehemu tofauti za gari hilo!


Siku za Usoni Chuo Kikuu cha Makerere kikishirikiana na vyuo vikuu vingine kitatengeneza gari la aina hii. Je, huu ni ukombozi wa kweli kwa bara letu la Afrika? 

Saturday, December 10, 2011

Sala / Swala kabla na baada ya kazi


File:Flag of Tanzania.svgTanzania ni nchi isiyo na dini ila watanzania wana imani na dini zao. Tanzania, ni nchi na si binadamu, mtanzania ni binadamu na wala si nchi. Hivyo watanzania hawa kwa kuwa wanamwamini Mungu basi katika mambo muhimu na rasmi yanayohusu nchi, watanzania hawa huyaanza kwa kumuomba na kumshukuru Mungu. Huu ni wito tosha kwetu sote pamoja na viongozi wetu kusali kabla na baada ya shughuli zetu.Changamoto mpya kwa maendeleo ya nchi yetu - Hofu ya Mungu na upendo kwa Jirani ni muhimu hasa!




WIMBO WA TAIFA WA TANZANIA


Mungu ibariki Afrika                                                   God bless Africa


Wabariki Viongozi wake                                             Bless its leaders
Hekima Umoja na Amani                                            Wisdom, unity and peace
Hizi ni ngao zetu                                                         These are our shields

Afrika na watu wake.                                                  Africa and its people

Kiitikio:                                                              Chorus

Ibariki Afrika, Ibariki Afrika                                   Bless Africa, Bless Africa

Tubariki watoto wa Afrika.                                    Bless us, the children of Africa


Mungu ibariki Tanzania                                           God bless Tanzania
Dumisha uhuru na Umoja                                        Grant eternal freedom and unity
Wake kwa Waume na Watoto                                To its women, men and children
Mungu Ibariki Tanzania na watu wake.                     God bless Tanzania and its people


Kiitikio:                                                               Chorus:
Ibariki Tanzania, Ibariki Tanzania                              Bless Tanzania, Bless Tanzania
Tubariki watoto wa Tanzania.                                   Bless us, the children of Tanzania












Friday, December 9, 2011

Uhuru wa Tanzania Bara na Maoni


Sehemu ya wadau kwenye maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru

















Maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania Bara, ama ya iliyokuwa Jamuhuri ya Tanganyika, mkoani Mtwara yalifanyika kwa mdahalo wa kitaaluma Katika Chuo Kikuu cha STEMMUCO.

Kulikuwa na mada kedekede zenye kuangalia hali halisi ya nchi hii toka ijipatie uhuru wake toka mikononi mwa walezi wa kiingereza miaka hamsini kamili hivi leo. Asilimia kubwa ya washiriki ni wale waliozaliwa kisha uhuru. Baadhi yao ni watu waliopata fursa za kuzunguka sehemu mbalimbali duniani. Wengine walikuwa ni watu wenye taaluma kubwa kwa maana ya ujuzi na vyeti. Hata hivyo walikuwepo pia washiriki wachache waliokuwa hai wakati Tanganyika ikijipatia uhuru wake.

Matokeo ya mjadala, hususani ya wasomi wengi, yalidhihirisha kuwa toka uhuru, ukitilia maanani rasilimali nyingi tulizonazo, nchi hii haijapiga hatua kabisa. Mengi yaliyofanyika ni hovyo mno na kwamba juhudi kubwa na za haraka zinahitajika sana ili tupate nafuu. Hivyo kauli mbiu ya “Tumethubutu, tumeweza na tunasonga mbele” haina ukweli kabisa labda kama ni kuthubutu kuihujumu nchi. Ilhali wazee wachache walioshiriki mjadala huo na kuongea, japo kwa muda mfupi, walisema bila kificho kuwa nchi imepiga hatua kubwa ingawa bado kuna haja ya kutenda zaidi.

Binafsi naungana sana na wazee na wengine wenye mtazamo huo kuwa; nchi yetu imefanya mambo mengi mazuri na kuna juhudi zinaendelezwa ili tufanye vyema mara dufu. Hata hivyo kutokana na utajiri wa kiasili ulio katika maliasili ya nchi yetu, basi kweli, utaona kwamba tunatakiwa kuwa mbali sana kimaendeleo. Shida yetu kubwa kila mmoja wetu ni ubinafsi; kila mmoja anataka kunufaika yeye na familia yake kwanza, na kisha hapo ndo aangalie uwezekano wa kuwakumbuka wengine, uwezekano. Tuache ubinafsi na tujifunze toka kwa waasisi wa nchi yetu kujitoa muhanga kwa maendeleo ya watu na taifa letu. Sina hakika kama Mwalimu Nyerere, Mzee Kawawa, Shujaa Moringe Sokoine waliacha pesa kwenye akaunti nje ya nchi.

Utawala bora uimarishwe; wenye makosa washitakiwe na sheria ifanye kazi yake kwa uwazi na uhuru. Tuliambiwa ili tuendelee tunahitaji watu, ardhi, siasa safi na uongozi bora. Mambo haya yote na tuyazingatiwe na hatimaye tutaweza kufika tunakopaswa kuwa kulingana na rasilimali tulizonazo.

Watu wetu tuwapate elimu ya maana zaidi; shule za kata tuziboreshe tuongeze walimu katika shule hizo na hivyo tutakuwa na watu walio tayari kuijenga nchi.Kupitia ELIMU ukombozi wa kweli utapatikana. Wanafunzi wetu tuwafunze kujitegemea kwa maana ya kujenga udadisi wao, kuimarisha ubunifu wao na kuwawekea misingi ya kuwa na fikra zao binafsi. Ili Tanzania na Afrika kwa ujumla tuweze kuendelea tunahitaji FIKRA ZETU WENYEWE fikra tunazotumia ni za kuazima; haziwezi kutufikisha mbali. Tutapata fikra zetu wenyewe tutakapowaweka wanafunzi wetu kwenye mazingira ya kufikiri, kutafakari, kupenda hesabu na masomo ya sayansi. Kwa kuanzia tufundishe masomo ya FALSAFA kwa shule zote za sekondari.

Ardhi tunayo tena ya kutosha; tuilinde na kuwapatia wananchi kwa usawa hatutaki kuingia kwenye migogoro ya Zimbabwe, Kenya, na sehemu zingine duniani.


 
Siasa zetu: Siasa ni muhimu mno. Kwa maoni yangu hii nd’o hutoa mwongozo ama dira kwa nchi, ukiwa na siasa mbaya basi huendi popote. Tanzania kwa sasa hatuna siasa nzuri; hili ni dhahiri, sisi si wajamaa wala si mabepari na mfumo tulionao haufahamiki, walu siufahamu. Kama hatujui kinachotuongoza basi hatuwezi kwenda popote. Siasa ndo hasa itatoa mwongozo kwenye uchumi wa nchi na hatimaye kwenye mambo ya kijamii.


Uongozi bora. Uongozi bora ni rahisi sana. Ili uongozi uitwe bora una kazi moja tu; kutafsiri katika vitendo sera zake yenyewe, sera ambazo zinakubaliwa na wananchi walio wengi. Kuwe na utawala wa sheria ambao ni huru na wenye uwezo wa kusimamia mambo yake bila kuingiliwa. Kwa kufanya hivyo tutapiga hatua kubwa na kufanya wananchi wetu waishi maisha yanayomfaa binadamu huru kama inavyotakikana.

Mungu Ibariki Afrika, Mungu Ibariki Tanzania

Thursday, December 8, 2011

UHURU NIGHT


















Wanachuo wa STELLA MARIS MTWARA UNIVERSITY COLLEGE wameendesha mjadala juu ya uhuru wa Tanzania bara. Ni jambo jema mno kusikiliza mawazo na malubano ya kihoja ya wanataaluma / wanazuoni.

Hapa chini kuna sehemu kidogo tu ya yaliyojiri katika mazungumzo hayo. Mijadala ndo hasa fursa za vijana kujifunza kujenga hoja na kuwa na mawazo yetu binafsi jambo hili ni muhimu sana.

Independence and Freedom of TanzaniaJe, Tanzania ipo huru?

Wanachuo wa STELLA MARIS MTWARA UNIVERSITY COLLEGE jioni ya leo wameandaa mdahalo kuadhimisha Jubilei ya dhahabu ya Uhuru wa Tanzania bara, kipindi hicho ikiitwa Tanganyika.

Tanganyika, sasa Tanzania bara, ilipata uhuru wake toka kwa waangalizi wa kiingereza. Waingereza walipatiwa mamlaka ya kuilinda Tanganyika ili itakapokuwa tayari waipatie uhuru wake… maelezo zaidi ni historia ya uhuru wa Tanzania…

Wanachuo wamejadiliana juu ya masuala mengi ya msingi kwa taifa la Tanzania. Wameangalia muda uliopita, uliopo na ujao. Wameangalia mafanikio, changamoto, kufeli kwa viongozi na taifa kwa jumla. Lakini wanachuo wameangalia nafasi na mchango wao pia katika maendeleo ya Tanzania.

Wanachuo waliuchambua uhuru kupitia nyanja kuu tatu:


ii. Kijamii na

iii. Kiuchumi

Watanzania wana uhuru mkubwa kuliko wananchi wa nchi nyingi jirani barani. Hata hivyo changamoto ya uhuru huu ni kwamba uhuru huo unahitaji kwenda sambamba na haki; kuwe na haki kwa wananchi.

Imeelezwa kwamba, wasomi wetu wenyewe ndo hasa wanaididimiza nchi. Wasomi hao wanasaini mikataba mibovu inayoleta kipato duni kwa nchi na wananchi wengi.

Mwalimu JKNyerere aliwaambia wananchi waende vyuoni ili waisaidie nchi na wananchi lakini leo wasomi hao nd’o wasaliti wa taifa. Hawainufaishi nchi katu; wanatumia kalamu zao kuwaibia watanzania wa kawaida.

Wakati Tanganyika ikipata uhuru kulikuwa na lengo kuu la kuwashinda maadui wakuu watatu:

i. Ujinga,

ii. Maradhi na

iii. Umasikini

Wanachuo wamejiuliza tumepiga hatua kiasi gani kushinda vita ya adui hawa watatu?

Leo, twaambiwa watanzania ni wajinga zaidi kuliko wakati tulipopata uhuru; - wasomi wanasaini mikataba mibovu inayoiweka nchi katika hali ngumu kiuchumi ilihali mharibifu husika aendelea kutembea huru tu; hivyo watanzania bado tu wajinga.

Leo hii watanzania bado tu wagonjwa; tunakimbilia kwa waganga wa kienyeji kupunga mapepo na kunyweshwa dawa ya kikombe, kijiko, kibuyu… n.k

Wananchi wengi vijijini wanaendelea kuishi katika umaskini. Hawa masoko ya uhakika wala uhuru wa kuuza mazao yao ili kujipatia mahitaji yao. Wengine wanazalisha kiashi cha kutosheleza kwa miezi kadhaa tu.

Sunday, December 4, 2011

TUMETHUBUTU, TUMEWEZA NA TUNASONGA MBELE!

Miaka 50 ya Uhuru wa Tanganyika - Tanzania Bara












































Miaka 50 ya Uhuru. Siku ya Uhuru Mwalimu Julius Kambarage alibeba bango lililoandikwa
"Tanganyika 1961 Complete Independence." Leo miaka hamsini baadaye watanzania wajiuliza je, ni kweli kuwa tu huru?

Nchi imefanikiwa katika mengi, lakini pia kuna changamoto za kutosha ambazo bado zi mbele yetu watanzania...

Heri ya Siku ya Uhuru Watanzania wote...
Tuangalie mazuri tuliyofanikiwa na yatutie nguvu kusonga mbele zaidi...

Makosa tuliyofanya yawe kweli vyanzo vizuri vya kupiga hatua mbele zaidi


Siku ya Uhuru wa Ghana rais Kwame Nkrumah wa nchi hiyo alisema " Ghana you are free for ever" Haya ndo maneno ambayo napenda tuyaseme kwa taifa letu tukufu la Tanzania.  "TANZANIA YOU ARE FREE FOR EVER!"

               TANZANIA HAPPY GOLDEN JUBILEE - GOD BLESS YOU MY DEAR  TANZANIA

Miundo Mbinu wakati wa Mvua Dar!

Maeneo ya Mbagala wakati wa mvua







Thursday, December 1, 2011

UKIMWI DUNIANI : Attention Na SIDA wa François Luambo Makiadi



Picha kwa hisani ya google













Upungufu wa Kinga Mwilini (UKIMWI) ni hali ambayo imezigusa familia nyingi duniani kote lakini bara Afrika likiguswa zaidi kuliko sehemu nyingine za sayari hii ya dunia. Tarehe mosi Desemba huwa ni rasmi kwa shughuli za kuangalia tuliko toka.Wakati dunia ikitafakari hatua ambazo jamii imechukua kuhakikisha maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi yanapungua na pia kuwakumbuka na kuwaombea ndugu zetu walioaga dunia, ni fursa ya kupitia nyaraka na mambo rasmi yanayoweza kutupatia ujumbe rasmi.

Maneno yaliyomo kwenye wimbo maarufu wa Attention Na SIDA wa gwiji la muziki Kongo - Kinshasa na Afrika kwa ujumla François Luambo Makiadi (6 July 1938 - 12 October 1989), ni ujumbe mzuri mno wenye kumgusa kila binadamu kwa kumhadharisha na kumkumbusha wajibu wake. Hebu na tupitie ujumbe huu japo u katika lugha ya kiingereza.

Here is the text of Attention Na SIDA By Greame Ewens

Attention na Sida
Oh, Aids. This terrible sickness
Oh, Aids. A disease which does not pardon
A disease which spares nobody
Aids is a plague
Which leaves doctors impotent

Look after your body, and I'll look after mine
Protect your own body, I'll protect mine
Aids is taking the country
Aids does not discriminate against race
Aids does not discriminate against age
You mothers, beware
You fathers, beware

What can I say, mama? Aids is dividing peoples
Aids has broken marriages, Aids has divided families
Those who used to eat and drink with me, Have started to ignore me
They say I have got the Aids sickness, All my friends are cutting me off
Who can I complain to?


Aids is ravaging all peoples; they are frightened
Europe and the USA accuse Africa of being, The source of Aids
Recently Asia and USA were invaded by the sickness
Today every country is under attack, Aids is not stopping its sinister course
All selections of society are victims of Aids, Babies, children, youths, adults, the old,
Workers, bureaucrats, managers, Men, women and even doctors.
Aids can attack anybody. It can kill, It will kill all who do not protect themselves
You, brothers and sisters who already carry the virus
Do not behave in a way that contaminates others


Aids has made us forget all other illness, If a person is sick, they say it is Aids
If a person has a fever, they say it is Aids, If a person becomes thin, they say it is Aids
If a person dies, they say it is Aids, But why do we forget the other illnesses
Oh God, oh God, Oh God. Only you...,Sickness, Oh where are you coming from?
We forget other illness and talk of Aids

You pregnant women, you can carry the virus, You can transmit it to your babies
They may be infected, although you do not know, Ladies, avoid getting pregnant
If you know you have the virus. It is bad to ignore this, as your child could die young
Youths, beware, Aids can attack you, You are the life force of society
If you let it kill you, who will lead the people?
Avoid dangerous sex. Students beware unknown partners.
Be careful who you take money from, it could get you in deeper trouble.
Avoid occasional partners, Youths, beware of drugs. If you inject drugs with needles
You can become infected, Don´t take drugs. It is very bad for your health

It will bring you out in spots, It will give you diarrhoea.
Avoid picking up just anybody, Think before you make love
Even if you desire someone, be careful. Think first

You gentlemen, citizens, Beware of prostitutes
Avoid multiple partners, And you, ladies, citizens
Take measures for your own protection
Workers, in workshops, factories and offices
When you are talking together, Do not neglect the subject
Time passes quickly, and every day, Death takes the victims of Aids
The best way to avoid death is to protect yourself, Oh God, we pray to you

Priests at mass, pastors in churches, rabbis in synagogues,
Imams in the mosque, you each have an obligation
A great obligation to society. Use your office to help
Preach what society must know about Aids
Do not hold back. It is your duty to tell the people that
Aids is a punishment from God; it resembles
Soddom and Gomorrah in ancient times
Ask God to deliver us from this sickness
Use your prayers to ask God the way to salvation
All my family have run away from me
Because I have Aids. I am left with only my mother,
Who has to suffer again all the sickness of my childhood

Teachers, instructors, professors, At school, in class, at home
If you have a free moment discuss it,It is part of your scholarly obligation
Teachers at school, college and in universities
The parents count on you tp educate their children.
Parents, don´t be shy, tell your children and the youth
All you can about Aids,Tell the whole world, tell everybody to beware
It is for you to fight against Aids
We are waiting for a vaccine. We wait for medicine, It will take a long time to come,
Maybe five, seven or ten years. Change your behaviour
Time is pressing, the sickness spreads fast

Doctors, be like Pasteur, Flemming, Curie and other
Geniusses of the last century, Now is your turn to conquer this plague which
Terrifies humanity and defies medicine,Don't waste time finding the medicine, wherever it is
Get this plague out of the human body, Doctors you know well how Aids is caught
Do not show the disease that you are afraid, Do not discourage the sick by your behaviour
The medical profession looks to you to find courage, To conquer this sickness
Doctors beware, the patient's file is secret, It concerns only the patient and close family
Don't talk su much that you create panic
Your duty is always sacred. Your profession is sacred, Your duty is to find a medicine
If there is a miracle it will come from you, Doctors be careful with needles,
Always wear gloves when you touch blood

Governments of rich countries, help the poor countries
Lead the way in the struggle against Aids, Don't sell them arms to kill,
But provide arms for the War against Aids
Brothers and sisters of the United Nations,
Between yourselves combine experience and, Spread understanding
Political authorities, use the radio, television and the press
To inform the people of the dangers of Aids
Tell us how to protect against and combat Aids,
We must all be mobilised against Aids

Kwa rejea na habari hii soma hapa
This sickness o, this sickness, Can make you go bald

Wednesday, November 30, 2011

Vijana watanzania: Wamachinga wa China!

Picha kwa hisani ya mtandao

Ukosefu wa ajira za kutosha kwa vijana ndo hasa tatizo kuu linaloipasua kichwa serikali ya Tanzania. Hakuna ajira za kutosha kuwapatia fursa vijana wote wanaomaliza vyuo hapa nchini. Hivi karibuni tumesikia idadi ya wahitimu toka vyuo mbalimbali; kati yao wapo walio na ajira na wasio na ajira; kundi la pili likiwa kubwa zaidi. Wahitimu hao kwa baadhi ya vyuo ilikuwa kama ifuatavyo: Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine, SUA, walihitimu zaidi ya 1000, Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agostino, Mwanza, zaidi ya wahitimu 2000, Chuo Kikuu cha Dodoma wahitimu lukuki, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wahitimu lukuki pia. na kadhalika. Utaona ya kwamba kila uchao Vyuo vingi zaidi vinazidi kuongeza idadi ya wahitimu na hili ni jambo jema.

Kwa upande mmoja hili ni suala jema sana kwa nchi yetu, kwamba tunapata wasomi wengi zaidi. Lakini jambo hili halifariji sana pale unapoona kwamba wasomi wote ama wengi kati yao wanasubiri tu kuajiriwa. Hapa ndipo penye changamoto kubwa kwa mitaala ya elimu tunayoitumia toka shule zetu za msingi hadi sekondari. Wengi wa vijana wetu kulingana na mitaala tunayotumia ni tegemezi mno kiuchumi, kimsingi elimu wanayoipata haiwakwamui kiuchumi; pamoja na kumaliza kidato cha sita kijana wa kitanzania bado anaomba pesa kwa wazazi ama walezi kwaajili ya matumizi yake ya kawaida kama kununua nguo n.k; hii ni aibu. Mfumo wa elimu inafaa uweze kumfunza kijana kujitegemea, kuweza kuzalisha mali kwa kiwango fulani hata kama ni dhaifu lakini mtaala huo umsaidie kuwa na uthubutu; kijana awe na moyo wa kujaribu kufanya shughuli fulani halali kwa lengo la kuzalisha mali hata kama ni kidogo tu.

STEMMUCO/SAUT MTWARA
Vijana wanaojiunga na vyuo vikuu wengi ni wale ambao wamepitia mfumo wa kuulizwa maswali, kuyajibu na kupatiwa alama basi. Hakuna nafasi ya kutosha ama hakuna tu kabisa fursa kwa wanafunzi kufikiri ama kujifunza kufikiri vya kutosha. Hii ni hatari sana kwa mustakabali wa nchi na ulimwengu, kama taifa tunawajibika kuwapatia wanafunzi wetu fursa nyingi zaidi za kufikiri na kutafakari mambo, wasiyajibu tu kwa mazoea na kupata alama kubwa za juu ilhali hawafahamu masuala hayo kiundani. Na kukosekana moyo wa kujaribu /na kufanya mambo huwafanya hata wanaojaribu waonekane tofauti na jamii kubwa. Mambo haya yanajitokeza pia kwenye maisha yetu ya kila siku. Hapa naangalia shughuli ya biashara ndogondogo na hata zile za kati zinazofanywa na wananchi wengi hususani katika miji mikubwa nchini.

Vijana wengi wa kitanzania wanafanya shughuli za umachinga; naambiwa machinga moja ya tafsiri zake ni ile ya “marching guys” jamaa watembeao (tafsiri si rasmi). Kwa mtazamo wangu hiki ni kitu muhimu kabisa vijana na ndugu wengine wanaofanya shughuli hizo ni kielelezo tosha kabisa cha ulazima wa kuwa na mitaala ya kufunza ujasiriamali (ujasiri wa kutafuta mali kihalali – tafsiri yangu mwenyewe). Ujuzi wa ujasiriamali na hamu ya kufanya majaribio katika masomo uguse aina zote za masomo yaani ya sayansi, sanaa na kadhalika. Kwa kufanya hivyo utaona kwamba hata machinga wetu watafanya mambo kizalendo tofauti na ilivyo hivi sasa.

Bidhaa za Wajasiriamali - twahitaji kuongeza tu
ubora katika bidhaa zetu na mambo yatakuwa
safi. Picha kwa hisani ya blogu la marchingguys

Wengi wa machinga wa Tanzania kwa hakika ni vibarua wa nchi ya Uchina na nchi nyingi zilizoendelea. Wafanyabiashara wengi wanafanya biashara ya bidhaa zinazotoka nje ya Tanzania. Mfumo wetu wa uchumi, kwa kujua ama kwa kutokujua, umetufanya kuwa soko zuri sana la bidhaa za watu wengine. Fikiri kuhusu vitu ulivyonunua juma hili, bidhaa kumi; pengine sita hadi saba zimetoka nje ya Tanzania, japokuwa zinauzwa na wamachinga wetu ambao kimsingi ni vibarua wa uchina, Afrika Kusini n.k. Serikali ina nia njema sana ya kuwasaidia vijana, ndio maana ikaamua kujenga Machinga Complex pale Ilala. Nimesikia kuna mpango wa kujenga Machinga Complex kadhaa katika mikoa mingine kwa lengo lilelile la kuwakwamua vijana na kina mama. Ukiachia mbali kuhusu ufanisi wa jengo hilo, angalia bidhaa zinazouzwa ndani ya jengo hilo, asilimia kubwa zinatoka Jamhuri ya watu wa Uchina, mita chache toka pale Machinga Complex unakutana na iliyogeuzwa kuwa Dubai ya Tanzania Kariakoo, chunguza bidhaa zinazotoka, Dar es Salaam, Tanga, Iringa, Mwanza, Mbeya, Tabora, Arusha, Kilimanjaro, Mtwara n.k; ni chache mno. Hii ni changamoto kubwa kwa nchi yetu; hizi “Machinga Complexes” zinazowalenga vijana wetu inatakiwa ziuze bidhaa zitokazo Kigoma, Iringa, Ruvuma, Manyara, Mwanza, Shinyanga, Rukwa, Njombe n.k - bidhaa za Tanzania. Tazama hata sekta zingine; usafirishaji: foleni za motokaa kwenye majiji hapa nchini; Dar es Salaam, Mwanza na kwingineko pamoja na magari mengi vile, sina hakika kama kuna moja lililotengenezwa pale Kibaha. Tazama baadhi ya miji yetu ilivyojaa na kuwa jaa la pikipiki, bajaji, baiskeli, hakuna zinazotoka Tanzania, lakini wamachinga na wajasiriamali ni wengi kupindukia, huoni kuwa sisi ni wamachinga wa wachina tu!

Sunday, November 27, 2011

Huu ndo uzuri wa akili ya binadamu...

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndugu Jakaya Kikwete akiongea na Ujumbe wa Chama cha CHADEMA

Ni busara sana kwa kiongozi wa nchi kukubali kukutana na viongozi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo.

Ni busara hali kadhalika kwa CHADEMA kutoka na wazo la kuomba fursa ya kukutana na kiongozi wa juu wa nchi ili kujadili suala hili la msingi kabisa.

Nini viongozi hao wataafikiana ni suala la kusubiri na kujua. Moja ambalo ni dhahiri kwa hakika itakuwa ni fursa nzuri kabisa ya kuweza kufikia muafaka wa mtiririko sahihi wa utaratibu upi utumike kupata chombo cha kukusanya kuratibu, kujumlisha na kutoa majibu ya mawazo na maoni ya watanzania. Kumbe kuna njia lukuki za kusikilizwa kama sehemu moja inashindikana basi unajaribu njia nyingine. Ni vyema sana kuwa viongozi wa CHADEMA wameamua kufanya hivyo. Muhimu kuliko vyote ni amani ya kweli; amani ya kweli ni utulivu unaoendana na haki, hivyo wananchi tunahitaji utulivu lakini pia na hasa haki na usawa katika masuala yanayohusu maliasili za nchi yetu na maendeleo ya watu wake. Tanzania ni muhimu kuliko chama chochote cha kisiasa, Tanzania itakuwepo tu na si vyama vya siasa.  

Thursday, November 24, 2011

UTANZANIA HALISI

Bendera za vyama kadhaa vya siasa zikipepea nje
ya jengo la Nyumba ya Demokrasia - huko Buguruni Dsm


















Tanzania ni nchi ya kipekee sana hapa duniani. Ndani ya nchi hiyo kuna zaidi ya makabila 120, watanzania hao wana dini nyingi na tofauti tofauti mithili ya nyuki mzingani, itikadi za kisiasa anuwai, kuna vyama vya
kisiasa zaidi ya kumi. Pamoja na mambo yote hayo hulka ya watanzania ni kuishi pamoja bila kujali tofauti zao. Hili ni jambo la msingi na maana zaidi. Utanzania ni muhimu zaidi kuliko dini zetu, itikadi zetu za kisiasa, tofauti zetu za rangi, misimamo yetu ya kitaaluma na kadhalika. Kama jinsi ilivyo kwa Mungu, yeye ni muhimu zaidi kuliko dini ama madhehebu yetu, Mungu hana dini, analojia hiyo tunaweza kuitumia pia kwa Tanzania. Nchi yetu ni muhimu kuliko tofauti zetu zote kama jinsi ilivyo katika vitambaa hivi vyenye rangi tofauti tofauti lakini vyote vinawakilisha watu wa taifa moja la Tanzania. Mungu Bariki Umoja na amani yetu!

Wednesday, November 23, 2011

Nyumbani kwa utajiri na ubinafsi mkubwa?


Nyumbani kwa utajiri mkuu na ubinafsi kupindukia?
Picha kwa hisani ya google


Fikra za watu na tafsiri zao!



Hivi mawingu huko angani hutoa ramani za sehemu mbalimbali
ama hutokea tu yakawa jinzi yalivyo kwa bahati tu? Wataalaam
wa Jiografia tafadhali tunaomba maelekezo ama tafiti kujielimisha zaidi  
Hivi karibuni nimesikia mtu aliyetoa tafsiri ya kuwa barani Afrika kumejaa migogoro inayochelewa kutatuliwa na mingine iliyodumu kwa miongo kadhaa sasa kwa sababu ya umbile la bara hilo. Ndugu huyo amedai kuwa bara la Afrika lina umbile la silaha aina ya bastola. Kwamba umbile hilo linalisababishia bara letu kukosa amani ya kudumu.

Bila shaka huu ni mtazamo wa mtu mmoja. Inafaa kuongelea kitu ambacho mtu amekifanyia tafiti ili kuepukana na taarifa  ambazo hazina ukweli wowote ila tu kuipotosha jamii ya wanadamu. Tujenge utamaduni wa kufanya tafiti za kina na si kwenda kwa sangoma kwa mambo ambayo tunaweza kuyapatia suluhu. Bila kufanya tafiti na kuwaelewesha watoto wetu kwa uhakika mambo tuliyoyatafiti tutajijengea hofu na kuendelea kuwa jamii ya hofu na kuogopana.
  
Wingu hili linaonyesha ramani ya wapi na nini tafsiri yake?

Tuesday, November 22, 2011

Sheria ya Mazingira inaishia wapi...?






Plastiki na chupa za maji zikiwa zimetupwa huku na huko na abiria waliochoka
 kutoka na adha ya usumbufu unaoletwa na ubovu wa eneo lisilo na lami.


Barabara kwa Maendeleo

 

Abiria wa Mtwara - Dar es Salaam wakimbilia mabasi yao
baada ya kukwamulia toka tope lililotamalaki barabarani
Usafiri wa uhakika ni moja ya viashiria vya kimaendeleo. Njia za usafirishaji zikiwa nzuri hurahisisha maisha ya watu na kuharakisha maendeleo ya jamii husika na taifa kwa ujumla. Mtwara ni moja kati ya mikoa ambayo imekiwa kisiwa kutokana na miundo mbinu mibovu kwa muda mrefu. Mtwara inafikika kwa njia mbalimbali; kwa ndege, kwa meli, na kwa barabara. Watu wengi zaidi nchini Tanzania husafiri kwa barabara, japokuwa njia hii ya usafiri imejaa damu. Kujegwa daraja la Mkapa ulikuwa ni ukombozi mkuu kwa ukanda wa kusini. Serikali ya Tanzania imeendelea na juhudi kubwa kuijenga barabara ya Dar es Salaam – Mtwara, zaidi ya kilometa 500 kwa kiwango cha lami.

Matembezi ya hiari yaendelea
Ni kipande kidogo kisicho na lami ndo kinaendelea kuwatesa na kuwanyanyasa wananchi wa ukanda huu maarufu kwa zao la korosho na sasa gesi asilia. Kukamilika kwa ujenzi wa barabara hiyo kutaboresha maisha ya wakazi wa mkoa huo ambao ni tegemezi kiasi kikubwa kwa jiji la Dar es Salaam.

Wednesday, November 16, 2011

UDHAIFU CHAMA CHA WASANII TATIZO KWA MAENDELEO YAO

Na Mwanndishi wa BASATA
Mhadhiri Msaidizi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agostino Martin Mandalu akifafanua jambo wakati akiwaeleza wadau wa Jukwaa la Sanaa juu ya utafiti alioufanya kwenye Muziki wa kizazi kipya. Kulia ni  Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo na Habari, BASATA, Godfrey Mungereza.







Utafiti uliofanywa kwenye muziki wa kizazi kipya ukilenga kubaini changamoto na mafanikio yake umebainisha kuwa, kukosekana kwa umoja miongoni mwa Wasanii ni moja ya sababu kubwa ya kudumaa kwa maendeleo yao.

Sababu zingine zilizotajwa ni pamoja na Wasanii kutokuzingatia mikataba kwenye kazi zao, utengenezaji wa kazi za sanaa zenye ubora hafifu, usimamizi dhaifu wa kazi zao, kukosekana kwa viongozi thabiti katika tasnia ya muziki na sababu zingine.

Katibu Mtendaji wa BASATA, Ghonche Materego akionesha kitabu kilichoandaliwa na Mhadhiri Msaidizi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agostino, Martin Mandalu kinachohusu Tasnia ya Muziki Mkombozi Kwa Vijana kwenye Jukwa la Sanaa wiki hii. Kulia ni mtunzi huyo, Bw. Mandalu.

Akiwasilisha utafiti wake alioukamilisha Mwaka huu kwenye Jukwaa la Sanaa la Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) mapema wiki hii , Mhadhiri Msaidizi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agostino, Martin Mandalu alisema kuwa, bila wasanii kuzifanyia kazi changamoto hizo bado kutakuwa na safari ndefu katika kuyafikia mafanikio ya kweli.

Wadau wa Jukwaa la Sanaa wakimsikiliza mmoja wa Wasanii aliyekuwa akihoji sababu hasa zinazowafanya Wasanii wasiwe kwenye umoja pamoja na juhudi zinazofanywa  za kuunda umoja wao.

“Asilimia 80 ya Wasanii waliohojiwa kwenye utafiti huu hawakuwa na taarifa ya uwepo wa umoja unaowaunganisha. Hii ni hatari kwa sababu nilipofika katika vyombo rasmi nilipata taarifa za uwepo wa vyama na mashirikisho ya wasanii. Hii ina maana wasanii hawatambui uwepo wa umoja huo” alisema Mandalu.

Kwa mujibu wa utafiti huo, Wasanii wengi waliohojiwa walikiri kuwa, wamekuwa wakipata mapato kidogo ikilinganishwa na kazi wanazofanya lakini hili likielezwa kuwa linasababishwa na kutozingatia mikataba, kukosekana kwa ushirikiano miongoni mwao na Wasani kutaka kufanya kila kitu yaani utunzi wa nyimbo, usambazaji na hata umeneja.

“Wasanii wengi waliohojiwa walionekana kukosa uongozi na usimamizi thabiti. Walionekana kufanya kila kitu kuanzia utunzi wa nyimbo, kuzifanyia matangazao, kutafuta kazi za maonyesho na umeneja kwa ujumla” alisisitiza Mandalu wakati akifafanua utafiti wake.

Kuhusu utayari wa Wasanii kutoa taarifa au kufika maeneo wanayohitajika, Mhadhiri huyo msaidizi alisema kuwa, ni tatizo kubwa kwani wasanii wengi wamekuwa wazito katika hilo na hata kutokutoa ushirikiano wa kutosha katika masuala yanayowahusu.

“Wengi wa wasanii niliokuwa napanga kukutana nao, walikuwa hawaoneshi ushirikiano. Anaweza kukwambia tukutane saa tano lakini ukifika muda huo anakwambia ana kazi nyingine kwa hiyo haitawezekana” alisema Mhadhiri huyo wakati akieleza changamoto alizokumbana nazo.

Utafiti huo ambao umechapishwa kwenye Kitabu cha Tasnia ya Muziki Mkombozi kwa Vijana umefanywa na Mhadhiri huyo kama sehemu ya kupata shahada yake ya uzamili katika stadi za Maendeleo.

Friday, November 11, 2011

Vimbwanga vya 11.11.11


Bila ubishi hii ni moja ya tarehe za aina yake ambapo kukutana nayo tena katika maisha ya hapa duniani unahitaji kupingana na uzoefu uliopo duniani mpaka hivi sasa. 11.11.11 inatazamwa kwa namna tofauti tofauti na watu tofauti tofauti soma hapa kupata mtazamo wa wanahisabati wanasema nini juu yake.

Vazi la kitaifa na miaka 50 ya Uhuru Tanzania

 Mwanamitindo maarufu nchini Tanzania, Asia Idarous akipita jukwaani na mwanamitindo kuonyesha ubunifu wake katika ufunguzi wa Swahili Fashion week.

Picha kwa hisani ya blogu la michuzi








Umri wa miaka hamsini kwa binadamu si umri haba. Katika umri huo kwa hakika binadamu anaanza kuhesabu mengi aliyoyafanya; lugha yake inaanza kuwa ya wakati uliopita. Utamsikia nilipokuwa fulani, nilipokuwa na kina fulani, nilipokuwa sehemu fulani, nilifanya hivi, nilikuwa hivi... hata hivyo hiyo ni lugha hiyo ni watu tu wa sehemu fulani tu. Kuna wengine ambao husema miaka hamsini ndo kwanza maisha yanaanza na hivyo lugha zao ni zile za wakati ujao, nitafanya hiki, nitakuwa fulani... nita... nita... nita...

 Hata hivyo muhimu zaidi kwa Tanzani hivi sasa ni kuwa baada ya miaka 50 ya Uhuru wa taifa hili ambalo ni nyumbani kwa Serengeti,mlima Kilimanjarokreta ya Ngorongoro, nyumba kwa visiwa vya karafuu Zanzibar bado haina VAZI RASMI la kitaifa. Huu ni wakati kwa wanamitindo na wanasanaa kutumia ujuzi wao kutoa kinachoweza kuwa vazi la taifa na hivyo kuwasaidia watanzania kuwa na vazi lao la kujivunia lenye kubeba na kuheshimu tamaduni zetu. 




Thursday, November 3, 2011

KUMBE KWELI SISI SHAMBA LA BIBI...

Picha kwa hisani ya google
Moja ya makala za HabariLeo katika chapisho lake la leo, imetoa habari inayotufanya nchi yetu kuonekana kama shamba la bibi lisilo na mmiliki...

Bibi ni mama mzazi wa baba ama mama; ni mtu muhimu kwani, huyu pamoja na mumewe ama mwanaume flani ambaye tutamuita babu, ameshiriki moja kwa moja kuwaleta duniani wazazi wetu. Mtu huyu ki-umri amekula chumvi nyingi, na kitamaduni sehemu nyingi barani ni mahiri katika mambo mengi. Ujuzi na busara ya mambo ipo katika uzoefu wa siku nyingi.

Bibi ndiye aliyewalea baba na mama (kila mmoja na mzazi wake - wote waitwa bibi ); hivi basi kwa jinsi wazazi wetu walivyo na nidhamu na utaratibu wa maisha, sehemu flani wamevipata toka kwa bibi. Ni yeye hasa ndio aliyewalea na kupata watoto wenye maadili mema na staha kama tuwajuavyo wazazi wetu. Ni kweli kuwa hupata ujuzi mwingine kwenye mazingira waliokulia, mafunzo sehemu mbalimbali lakini nafasi ya bibi kwa maana ya mzazi na mlezi ni kubwa hasa. Hata hivyo kuna jambo jingine ambalo hushangaza sana toka kwa bibi.

Kina bibi wengi wanaelezewa kama watu wenye kuwadekeza kupindukia watoto wa watoto wao; wajukuu. Kiasi cha kuwadekeza huko, huwashangaza watoto wao yaani baba na mama zetu, ambao mara nyingine hulazimika hutoa simulizi za namna ambavyo bibi alivyokuwa mkali enzi za malezi yake kwao. Kuna sababu kadhaa zinazoeleza kwanini bibi anakuwa mpole na rafiki mno kwa wajukuu zake. Moja ya sababu hizo ni uzee, uchovu na upweke wa utu uzima. Bibi anawahitaji watoto wa watoto wake ambao kwake ni marafiki; ili kuwapata mara nyingi huweza kutumia rasilimali alizonazo kuwaweka kwenye himaya yake. Ni kupitia mwanya huo basi mali za bibi huweza kutumika vibaya; kuharibiwa, kuhujumiwa, kila mmoja akachukua anachotaka na tena kwa nafasi yake. Katika hili bibi hajali mali yake inaharibiwa kiasi gani, muhimu kwake ni kujenga mahusiano na wajukuu wake wakiharibu ama wasiharibu hilo si muhimu kwake muhimu ni kwamba uhusiano wa kirafiki na wajukuu unakuwa bora zaidi na zaidi. Ni kutokana na masuala hayo ndo analojia ya shamba la bibi ikazuka.

Habari Leo hivi leo wametoa taarifa yenye kufanana na analojia ya shamba la bibi. Hapa nchini, katikati ya kitovu cha uchumi wa nchi, Dar es Salaam kumekuwa na shule ikiendeshwa kinyume na sheria kwa miaka kumi na miwili. Hii inaweza kuwa kipande cha pande kubwa la “jabari” la barafu baharini. Si ajabu kuna mengi ambayo hayajagunduliwa na tena yenye madhara makubwa kwa taifa.  Nchi ina mali asili nyingi tena za kila namna; je ni namna gani rasilimali hizo zinaendeshwa katika namna inayowanufaisha wananchi walio wengi na taifa kwa ujumla wake.

Tanzania ina mbuga lukuki za wanyama pori, je shughuli za kiuchumi za wanyama pori zinafanyika kwa jinsi inayotakikana? Je, taifa linapata pato stahiki? Tanzania ina bahari, maziwa, mito na mabonde yenye uwezo wa kunufaisha taifa kwa namna anuwai; je watu waliokabidhiwa madaraka kuendesha vyanzo hivyo vya mapato wanaitendea haki jamii na taifa kwa ujumla? Je, shughuli hizo zinaendeshwa katika namna endelevu? Ili kwamba wajukukuu wa wajukuu wetu wakute mali hizo ama faida zake na wao pia wamudu kuendesha maisha yao kwa furaha? Tunaweza kuorodhesha utajiri na zawadi nyingi zilizopo nchini  hata hivyo si nia yangu kufanya hivyo lengo ni kukumbushana juu ya taifa letu na mustakabali wake.

Kuhitimisha tunasema kuwa kila mmoja wetu awajibike kizalendo ili kulinda na kutetea maslahi ya taifa letu la Tanzania, na kuboresha maisha ya jamii ya wanadamu wanaoishi sasa na wale watakao kuja baadaye kwa taratibu na sheria zinazokubalika.