Saturday, December 17, 2011

Unamfahamu mwanaAfrika huyu?



Thomas Sankara( Desemba 21, 1949 – Oktoba 15, 1987), Che Guevara wa Burkina Faso
Mwana Afrika halisi, mtu mnyofu, mwadilifu, mkweli na mzalendo wa kweli!
Mwanamapinzuzi na rais wa zamani wa Burkina Faso Thomas Isidore Sankara ( 1949 -1987) wiki moja kabla ya kifo chake alisema: “ Wakati wanamapinduzi kama watu binafsi wanaweza kuuwawa, kamwe huwezi kuziua fikra zao za kimapinduzi.”

Thomas Sankara ndiye mtu aliyebadilisha jina la nchi yake; hapo kabla ilijulikana kwa jina la Upper Volta; yeye alibadilisha na kuiita nchi yake Burkina Faso yaani NCHI YA WATU WAADILIFU – Pays des hommes integre” ama land of the upright people” hujulikana pia kama Che Guevara wa Burkina Faso


Kaburi la kawaida kabisa la MwanaAfrika huyo
likiwa limezungukwa na makaburi ya walinzi wake












 Thomas Noel Isidore Sankara alizaliwa Desemba 21, 1949. Alikuwa rais Agost 4, 1983 na huyu ndio hasa kiongozi wa kwanza aliyetambulika kwa kuwa na upendo dhahiri wa nchi yake na ambaye alihimiza kuindeleza nchi yake, kukuza na kuzitambulisha tunu za nchi hiyo na kufanya zifahamike kwa wananchi na kwa mataifa ya nje.

Sankara alipitia mafunzo mbalimbali ya kijeshi. Mwaka 1970 alikwenda Madagaska, 1978 alikwenda Moroko. Alishiriki katika vita ya Mali na Burkina Faso mwaka 1974.


Katika siasa alikuwa na mafanikio; 1981 alikuwa waziri wa habari, waziri mkuu mwaka 1982. Na kati ya 1981 na 82 alifungwa kwa tuhuma za rushwa. Na mwisho katika wigo wa kisiasa aliongoza Chama Kidemokrasia na cha Kimapinduzi hadi alipofanya mapinduzi maarufu ya Agosti 4

Kitu muhimu sana ambacho Sankara alipenda kufanya baada ya kuwa rais ni kuwataka watu wote wawe waadilifu. Alitaka serikali yake ifanye hivyo ili kutoa mfano mzuri kwa vijana na vizazi. Rushwa ilipigwa vita kwa nguvu zote. Mpango huo ulianza rasmi pale alipobadalisha jina la nchi yake. Zaidi alibadilisha pia motto, nembo ya taifa na kuwa " Nchi yetu ama kifo, Tutashinda" wananchi walihimizwa kuwa wazalendo kwa kuungana, kuilinda na kuipenda nchi yao. 
Sankara alikuwa karibu na wananchi alipiga gitaa, alicheza mpira, aliendesha baisikeli na kufanya mambo mengi ambayo yalimuweka karibu na wananchi. Kuhusu uchumi aliwapatia wananchi ardhi wapate maeneo ya kulima, aliondoa mambo kadhaa ya kuwapendelea viongozi; alifanya viongozi wawe kweli watumishi wa wananchi.
















Alifanya mambo mengi sana mazuri; hata hivyo kama wasemavyo waswahili, kizuri hakidumu. Thomas Sankara aliuwawa miaka minne baadaye. Ndani ya miaka minne aliweza kuleta mabadiliko makubwa kuliko ya miongo kadhaa. Vijana wengi barani Afrika walilia hadharani kwa kuwa waliona kuwa ile ndoto ya kuwa na mabadiliko barani Afrika iliondolewa. Wazo muhimu hapa ni je, wewe kijana unachangia nini kuleta maendeleo ya kweli kwa familia yako, jamii yako na kwa upana zaidi kwa nchi yako? Unaweza kusoma zaidi hapa











No comments:

Post a Comment