Tuesday, December 31, 2013

SIKU YA MWISHO YA MWAKA - UJUMBE KWA VIJANA

Hatimaye ni hakika sasa kila binadamu hai duniani na pia wafu wameongeza mwaka mmoja toka kuzaliwa. Binadamu wote ila tu waliozaliwa tarehe 29 Feburuari. Ni hao tu ndo wenye miadi na siku yao ya kuzaliwa kila baada ya miaka minne. Robo nne zinapotengeneza kitu kimoja kizima. (Mwaka mfupi una siku mia tatu sitini na tano na robo {365¼} na mwaka mrefu siku mia tatu sitini na sita {366})

Ukweli huu wa maisha unawakilisha mambo yote duniani kila jambo limepata fursa ya kukamilika; miezi yote imepata mzunguko wake, nyakati zote zimefikiwa, majuma yote yamekamilika, saa zote, dakika zote, sekunde zote na kila jambo lenye kutegemea mzunguko wa mwaka leo linakamilika.

Kupitia mzunguko na kukamilika kwa mwaka ni jambo la kujiuliza pia sisi wenyewe. Binadamu pia ana mabadiliko yake; yale ya kibaiolojia, seli mpya kuzaliwa na kuukuu kupotea, kutumia / kutumika sawa sawa kwa ubongo: kujenga fikra mpya n.k. Kumbe siku hii ya mwisho ni siku ya tathmini kwa yaliojiri maisha mwetu. Mimi Martin, Amina,  nimefanya jambo lipi la maana kwa maisha yangu na binadamu wenzangu? Nimepanda miti? Nimegundua jambo jipya muhimu kwa binadamu? Nimeandika kitabu cha maarifa na manufaa kwa wanadamu wenzangu? Nimefanya jambo lenye kulinda uhai wa binadamu? Nimefanya nini kwa nchi yangu, kwa dunia yetu? Naam ni lazima kujiuliza maswali haya, kila mmoja ajiulize kwa namna yake mwenyewe. Kila mmoja wetu afanye kile mwafalsa wa Ugiriki ya kale Socrates anavyopendekeza “maisha yasiyo na tathmini hayana tija” {tafsiri yangu isiyo rasmi}. Tathmini hizi zinatuhusu binadamu wote, viongozi wan chi duniani wahusika kwa kiasi kikubwa.

Wanasiasa wana jukumu kubwa la kuongoza nchi zao. Wanasiasa wazuri wanaongoza vyema wanasiasa wabovu wanaongoza hovyo. Watu hawa wana wajibu mkubwa zaidi kwa wananchi wenzao. Wana wajibu wa kuongoza nchi zao na kuhakikisha wananchi walio wengi wananufaika na mali asilia nchini mwao. Rais wa Marekani, mmoja kati ya mifano mizuri mwaka huu, amepigania kuboresha maisha ya Wamarekani wengi wa kawaida kwa kuboresha huduma zao za afya; moja kati ya mahitaji na haki muhimu ya binadamu. Kufanikisha jambo hilo kulihitaji ujasiri mkuu. Kwenye mlolongo huo wa siasa kuna mengi yamefanyika kote duniani; masuala anuwai mazuri kwa mabaya. Nchi nyingi hususani barani Afrika zimekumbwa na shida za kisiasa.

Nchini Mali kulitokea uasi ambao ulivuruga maisha na ustaarabu wa siku nyingi wa moja kati nchi zenye historia yenye kubeba bara lenye nchi nyingi zaidi duniani. Afrika ya Kati maisha bado hayajarejea hali ya kawaida kufuatia uroho wa mamlaka na dhambi ya ubaguzi inayoendelea kuwatafuna wanasiasa wa nchi hiyo yenye kubeba sawia jina lake na mahali ilipo. Misri, nchi yenye utajiri wa historia na kumbukumbu mahususi za maendeleo ya kale haikubaki salama na bado kunaendelea kuwa na chokochoko baina ya makundi hasimu. Jamhuri ya kidemokrasiaya Kongo iliendelea kuwa kwenye hali ya sitofahamu hususani mashariki mwa nchi hiyo tajiri kwa maliasili na ukubwa wa eneo barani. Ni dhahiri kuwa kila nchi ilikumbana na masuala anuwai ya kupendeza na yasiyo ya kuvutia, changamoto na fursa za kimaendeleo. Nchi kadhaa zimeendelea kusheherekea jubilei za miaka hamsini na zaidi. Tanzania na watanzania kwa mara ya kwanza walipata fursa ya kuchangia mchakato wa kuandaa sheria mama za nchi yao ama nzuri zaidi makabrasha ambayo ni mali ya wananchi, mkataba baina ya wananchi wa viongozi. Mkataba huo maarufu zaidi  katiba ni muongozo wa namna viongozi: watu ambao hutoka miongoni mwa wananchi na hukabidhiwa mamlaka ya/ na wananchi, ili waufahamu na waelewe ni namna ipi inawapasa kuwatumikia wananchi. Zoezi la kuandaa mkataba huo kwa mara ya kwanza nchini Tanzania, lilishirikisha/ linashirikisha wananchi wote ama moja kwa moja ama kwa njia ya uwakilishi, ni jambo jema. Wafaransa, waanzilishi wa Jamhuri, kupitia mapinduzi yao maarufu, wana msemo: “hucheka vyema zaidi anayecheka mwishoni” Tunawaombea watanzania wapate mkataba/ katiba yenye uzalendo hasa wa watu hao. Mwishoni AfrikaKusini, bara Afrika na dunia iliondokewa na Nelson Mandela.

Nelson Mandela: mtu ambaye alipata umaarufu mkubwa kupitia mambo kadha wa kadha: kifungo chake kwa kuipinga serikali ya ubaguzi rangi nchini mwake, kung’atuka madarakani kisha muhula mmoja wa uongozi, kufanya maridhiano badala ya kulipa kisasi nchini mwake, kupata nishani ya Nobel, kutambuliwa mno na vyombo habari vya magharibi n.k. Kifo, heshima ya kitaifa na kisha mazishi  ya kitaifa ya Nelson Mandela al maarufu Madiba ilikuwa ni tukio kubwa la kidunia. Viongozi mashuhuri walifika kwenye kumuaga ndugu huyo ambaye ni sehemu ya wanaAfrika waliotoa mchango mkubwa wa kizalendo kwa bara hili: Mwalimu JK.Nyerere, Dr.Kwame Nkrumah, Dr. KenethKaunda, na wengine lukuki. Kwa Madiba pengine maneno ya Sauli ama Paulo kwa Warumi 5: 3-5 yanaweza kufaa sana hapa. Kwa sasa tuishie hapa. Lakini kwa ujumbe kwa vijana.


Mwaka unapokwisha si kitu cha ajabu sana kwa maana ya kuja kwa jambo jipya kabisa ni mzunguko ule ule wa Jumatatu, Jumanne, Jumatano, Alhamisi, Ijumaa, Jumamosi na Jumapili. Kwa kuwa mzunguko ni ule ule nawaalika vijana kutafakari juu ya malengo ya maisha yenu/ yetu. Nini hasa unataka kufanya duniani: kukusanya mali za dunia yote, “itakufaidia nini kupata mali zote na kisha kupoteza nafsi yako” Maneno ya Mmisionari mmoja. Maneno na tafakari hii ni muhimu kwa vijana kwani mwaka huu tumesikia lukuki (hatuna takwimu hapa) wakikamatwa na dawa za kulevya…Kukusanya mali na tena kuvumbua njia nyingi iwezekanavyo za kukusanya mali lakini kwa njia halali ni muhimu vyema lakini tusisahau pia kuwa mwili ni mmoja lakini wenye mahitaji ya kiroho pia...

Wasalaaam,

Thursday, December 26, 2013

SIKU YA KUFUNGUA MAKASHA YA ZAWADI




                                                                                                                           
IMEPAKULIWA HAPA : https://www.youtube.com/watch?v=L99hWdZGelI

Siku moja baada ya Noeli imekuwa, kimapokeo, ni siku ya kufungua makasha ya zawadi. Soma hii taarifa inaonyesha kuwa kazi ya kupokea makasha ya zawadi ni ya wafanyakazi nyumbani, Makasha ya zawadi hupokelewa kabla ya siku husika na leo kazi inakuwa moja tu ya kuyafungua makasha hayo kutaka kujua kuna nini humo ndani. Utamaduni wa kupeana zawadi siku za matukio maalumu ni jambo na utamaduni mzuri.

Jambo hili ni sehemu ya tamaduni za jamii nyingi duniani, na kama si sehemu ya tamaduni zetu basi ni jambo la kuiga na ni vyema tukafanya hivyo kwa wale tusio na utamaduni huo. Kufanya hivyo kunaendeleza na kujenga udugu, umoja, upendo n.k katika jamii. 


Kupitia utamaduni wa kupeana zawadi tujifunzie hapo hapo pia kutoa misaada kwa wahitaji bila kujali mahusiano yetu ya kindugu. Kwa asili binadamu wote tu ndugu wamoja. Asili, chimbuko letu wote; kidini, kibaiolojia/kisanyansi ni moja. Hivyo tunawajibika kusaidiana. Kwa wale wenye makasha mengi ya zawadi tuwakumbuke wahitaji wasio na msaada wa karibu; yatima, wajane, wagonjwa na wengine wote wenye kuhitaji katika jamii.   

Thursday, October 31, 2013

Maonyesho Mtwara katika Picha


Vikapu vya kiwango cha juu kabisa katika maonyesho ya Mtwara




Sehemu ya Maonyesho ya wajasiriamali




Mawasiliano ya baadhi ya vikundi vya wajasiriamali toka sehemu mbalimbali








Maonesho ya WajasiriaMali Mtwara




















Maonesho ya bidhaa mbalimbali za wajasiria mali kutoka pande mbalimbali za nchi na  nchi jirani yamenza mjini Mtwara. Maonesho hayo yaliyoandaliwa na SIDO na wadau wenzi, yanalenga kuonesha bidhaa anuwai zitengenezwazo na wabunifu na pia kutafuta masoko toka kwa wadau. Mkoa wa Mtwara, ambao umesikika masikioni mwa wadau wengi hivi karibu kufuatia kugunduliwa kwa gesi asilia, unaanza kuwa moja ya masoko makubwa tarajiwa ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Maonesho haya ambayo yamefunguliwa rasmi na ndugu mwenye dhamana ya viwanda vya Tanzania, ni fursa nzuri ya kuweza kuonesha bidhaa na mwanzo mzuri ya viwanda vyetu wenyewe kuanzia hatua za mwanzo kabisa. Kupitia wadau hawa wa bidhaa hizo ndogo, Taifa linaweza siku za usoni, kama tutaweka mkazo wa kutosha, kuwa na viwanda vyake lenyewe. Ili tuweze kufikia ndoto na lengo hilo ni muhimu kutengeneza mazingira ya kuwawezesha wajarisiliamali wetu kutengeneza bidhaa zao kwa gharama nafuu. Gharama za uzalishaji ikiwa ni pamoja na mali ghafi zikiwa  na bei ya chini, itawezesha wadau wengi kujiajiri na bidhaa zao zitakuwa na bei ya chini.

















Nasema hivyo kwa kuwa baadhi ya bidhaa nilizoziona zinauzwa kwa bei kumbwa mno ukilinganisha na ubora wake. Bidhaa  nyingi ni za asili kabisa na hivyo kuwa imara ukilinganisha na zitangenezwazo na makanjanja mjini, japokuwa ubora wake unahitaji kuongezwa zaidi ili zivutie wanunuzi wengi zaidi. Nilipohoji juu ya bei mmoja wabunifu wa bidhaa alisema: "nalazimika kuuza kwa bei ya juu kwa sababu nalipia kodi na  ushuru mbalimbali na pia kwa kuwa hakuna watazamaji wengi nauza bei ya juu ili kupitia mauzo haya nijikimu hapa mjini". Baadhi ya wadau hawa wa bidhaa asilia waliomba waandalizi wa maonesho haya wafikilie kuwalipia baadhi ya gharama ili kumudu vyema zaidi maonesho hayo. (Mwandishi hakupata fursa kuongea na timu ya maandalizi juu ya suala hili)

















Wakazi wa mjini Mtwara, hawajahamasika vya kutosha kutembelea maonesho hayo, jambo ambalo lingewezesha wajasiriamali kuuza bidhaa zao na kumudu kujikimu kupitia mauzo hayo. Hata hivyo ni fursa kwa wenyeji wa mkoa huo kujifunza mbinu mbalimbali za kukabiliana na maisha na utawala wa mazingira ya binadamu.

Kwa wajasiria mali, napenda kuwapongeza kwa kazi nzuri wanazozifanya, ila nawashauri pia waweke vitambulisho vya nchi zao wanakotoka ili kutambulisha bidhaa zao na pia kuzitambulisha nchi zao kibiashara zaidi. Hili linajumuisha kundika kwenye bidhaa jina la nchi bidhaa ilikozalishwa, kundika anuani  ama utambulisho uliojitosheleza ili mdau husika apatikane kwa wepesi kokote duniani. Ni muhimu kufanya hivyo kwani dunia imekuwa ndogo mno kupitia mapinduzi ya mawasiliano ulimwenguni.

Thursday, September 12, 2013

MTAZAMO MAISHANI


Bodi ya Korosho Mjini Mtwara

Bodi ya Tumbaku Mjini Tabora


Mtazamo wa nafsi yako mwenyewe - Picha kwa hisani ya wadau

Thursday, July 25, 2013

SIKU YA MASHUJAA NA UZALENDO TANZANIA


Sehemu ya wanajeshi wa Tanzania wakitoa heshima kwa Amiri Jeshi mkuu wa majeshi.
Picha kwa hisani ya BBC

Tarehe ya leo imeteuliwa kuwa siku ya mashujaa Tanzania. Ni tarehe waliyopokelewa wanajeshi wetu- mashujaa waliokuwa vitani nchini Uganda. Wanajeshi wetu walikwenda kazini kumnyoosha nduli Iddi Amini. Rais huyo wa zamani wa Uganda aliyejigamba kuwa na nguvu za kuchukua sehemu ya Ardhi ya Tanzania na kuifanya kuwa sehemu ya nchi yake. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati huo Mwalimu Julius Nyerere (1922-1999), kwa kutumia vigezo vya "vita halali" just war ya St. Augustine of Hippo 354-430  alitangaza vita kwa kuzingatia sababu inayokubalika, kujilinda dhidi ya adui, na kupigana vita kwa uangalifu na kupunguza maumivu kwa wasio na hatia. Vijana wa jeshi la Tanzania na nchi yote kwa ujumla tulishinda.

Tunapokumbuka mashujaa wetu, watu wengi hufikiria tu wanajeshi na wapiganaji wengine waliolipigania Taifa letu. Hapa utakumbuka watawala kama Mkwawa, Kimweri, Mirambo, Mputa, na wengine wengi. Ni vyema sana kuwakumbuka ndugu waliokuwa tayari kulilinda Taifa letu. Muhimu katika kumbukumbu hii ni suala zima la uzalendo. Watu wote tunaowatambua kama mashujaa, kwa namna fulani walikuwa na uzalendo mioyoni mwao. Hawa ni sawa na watu tunao watambu kama watakatifu, watakatifu huitwa wadhambi waliotubu. Nawafananisha mashujaa katika nchi na watu wenye "utakatifu" unapowapima kwa vigezo vya uzalendo. Kumbe tunapowaheshimu mashujaa wetu ni lazima tujitazame na kujipima uzalendo wetu.

Mzalendo tunamtarajia kuwa mtu mwenye kuipenda kwa moyo wake wote nchi yetu ya Tanzania. Katika hili kila mmoja na hasa wenye ofisi za Umma ama zozote zenye kutoa huduma kwa umma wa wanadamu, wanaalikwa kujipima, wanajali kwa kiasi gani maslahi ya wananchi walio wengi dhidi ya maslahi binafsi. Kiongozi anapopata fursa ya uongozi anatakiwa kufanya hivyo kwa niaba ya wananchi walio wengi; na ili aongoze vyema kuna mkataba unaomwelekeza kama anavyosema mwanafalsafa Jean-Jacques Rousseau(1712-1778) kwenye kazi yake ya The Social Contract (1762), kiongozi anafanya yale anayoelekezwa na wananchi na si anayotaka yeye; viongozi wangapi hivi leo hapa nchini wanazingatia anachosema mwanafalsa huyu. Wengi hawafuati makubaliano baina yao na wananchi, na kwa hivi wanalazimika kuacha mamlaka kwa wananchi wengine ili waongoze kama anavyosema mwafalsafa mwingereza John Locke (1632-1704). Locke anasema kiongozi mzuri anatakiwa awe na kumbukumbu ya makubaliano yake na wananchi moyoni mwake, vinginevyo aachie mamlaka.

Hivyo basi tunaweza kuwaenzi vizuri zaidi mashujaa wetu kwa kujitazama katika kioo na kuona kiwango cha uzalendo wetu kwa Tanzania yetu. Asanteni Mashujaa wetu na Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania!

Thursday, July 18, 2013

SIKU YA MZEE MADIBA


Nadhani hii ndo siku pekee ambayo binadamu mmoja amepewa heshima ya kuwa na siku yake ya kimataifa duniani. Ndugu Nelson Mandela kapewa heshima hiyo hasa kwaajili ya kumaliza kwa amani, kupitia tume ya haki na maridhiano, mvutano ambao ungejitokeza baina ya weusi wengi, na jamii nyingine za watu wasio weupe wa asili ya Ulaya kwa upande mmoja, na wazungu wa asili ya Ulaya kwa upande mwingine.

Suluhu hiyo iliyohitimisha miaka mingi ya ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini, kwa utulivu wa namna yake, ndo hasa sababu ya mzee Mandela kupewa heshima yote hiyo.

Saturday, June 1, 2013

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


National Arts Council BASATA
30/05/2013

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kwa kushirikiana na Chama cha Waandishi wa Habari za Sanaa na Utamaduni (CAJAtz) kila Jumatatu kuanzia saa 4 Asubuhi limekuwa likiendesha ‘Jukwaa la Sanaa’ kwenye ukumbi wake ulioko makao makuu ya Baraza Ilala Sharif Shamba.Katika jukwaa hilo linalohusisha wadau wote wa sanaa, hoja nzito na motomoto kuhusu tasnia ya Sanaa na Utamaduni zimekuwa zikijadiliwa na kujibiwa.

Katika kuelekea urasimishaji wa Sekta ya Filamu na Muziki ambao ulianza rasmi tarehe 1/01/2013, ifikapo tarehe 01/07/2013 hakuna kazi yoyote ya Filamu na Muziki itakayoingia sokoni bila kuwa na stamp ya TRA. Baraza la Sanaa katika Jukwaa la Tarehe 03/06/2013 litazikutanisha taasisi zote nne zinazohusika na urasmishaji ili kutoa elimu kwa Wasanii, wadau na wakuzaji sanaa kuanzia saa 4 :30 Asubuhi. Wadau wa sekta ya sanaa mnakaribishwa kuleta michango na hoja zenu ili kuleta mustakabali utakaojenga sekta ya sanaa. Taasisi zinazohusika na Urasimishaji wa sekta ya sanaa ni :

1. Bodi ya Filamu na Michezo ya Kuigiza

2. Chama cha Hakimiliki na Hakishiriki Tanzania (COSOTA)

3. Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)

4. Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA)

WOTE MNAKARIBISHWA
Godfrey Lebejo Mngereza

KAIMU KATIBU MTENDAJI, BASATA


Barua zote ziandikwe kwa Katibu Mtendaji

All correspondence to be addressed to The Executive Secretary

BASATA Arts Centre, Ilala Sharif Shamba, P.O. Box. 4779, Dar es Salaam, Tanzania.

Telephone: 2863748/2860485, Fax: 0255 - (022) - 286 0486 E-mail: info@basata.or.tz Website: basata.or.tz



Salaam za Rambirambi


Baraza la Sanaa la Taifa limepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za msiba wa msanii wa tasnia ya Muziki nchini Albert Mangwea a.k.a Ngwair.

“ Baraza limestushwa na kuhuzunishwa sana kutokana na taarifa ya kifo hiki cha Ngwair ambaye mchango wake unahitajika sana katika tasnia ya sanaa, pengo aliloliacha ni kubwa kwani ubunifu wao bado unahitajika katika tasnia hii.” Baraza linatoa pole kwa familia ya marehemu na wasanii wote nchini, aidha linawatakia moyo wa subira katika wakati huu wa majonzi ya kuondokewa na mpendwa wetu.

Tunaomba mwenyezi Mungu aipumzishe mahala pema peponi roho ya marehemu. Baraza liko pamoja na familia ya marehemu katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo, tutambue kuwa haya ni mapenzi ya Mungu.


Imetolewa na
Ghonche materego
Katibu Mtendaji
Baraza la Sanaa la taifa.

Monday, May 13, 2013

FAINALI ZA MASHINDANO YA KUTETEA UHAI (PRO-LIFE)


Makamu bingwa wa kombe la kutetea Uhai timu ya STEMMUCO

Mabingwa wapya wa kombe la kutetea Uhai -
Timu ya Chuo cha Utumishi wa Umma - Mtwara

Wachezaji wa timu zilizofika fainali wakimsikiliza mgeni rasmi





Weledi?









JUHUDI KAZINI?














KAZI NI MOJA TU SASA



Wanazuoni wa mwaka wa tatu chuoni STEMMUCO kwa juma la pili sasa wamekuwa wakitetea tafiti zao walizofanya kwa mieza kadhaa. Tafiti hizo, ambazo ni sehemu ya wajibu wao ili kupata sifa ya kupata shahada yao ya kwanza, (degree ya kwanza) zilikuwa na mada tofauti tofauti kama jinsi walivyo watu na miguso yao.

Baadhi ya kazi zilihusu mchango wa Chuo Kikuu cha STEMMUCO kwa maisha ya watu wa Mtwara kwa ujumla wake, zingine na nyingi hasa zilihusu masuala kadhaa ya elimu. Kwanini shule za Mtwara ubora wake wa elimu ni hafifu, kwanini shule za serikali ubora wake mbele ya zile za binafsi ni dhaifu n.k. Zingine zilihusu shughuli za kiuchumi mkoani Mtwara; uzalishaji chumvi na athari zake, mchango wa bandari Mtwara kwa wananchi. Kazi za wanazuoni wengine zilitazama masuala ya kijamii; kuongezeka kwa watoto wa mitaani, Unyago, jando na faida, hasara na changamoto zake. Mazingira pia hayakuachwa nyuma; tafiti kadhaa zimegusia suala hilo. Uhalifu ni moja ya mada zilizojadiliwa hali kadhalika.

Zoezi hili lilifanywa kwa lugha ya kiigereza; vijana wengi walijipanga na kutafuta misamiati stahiki kuelezea kazi zao; wapo waliofanya vyema sana, waliojitahidi sana na wanaohitaji kuongeza bidii zaidi. Kwa ujumla wanazuoni hawa ni hazina kubwa kwa taifa na wito kwao ni kuendelea na moyo wa kitafiti ili kuvumbua vyanzo vya matatizo na kuyafanyia kazi.



 



WASOMI WAKITETEA KAZI ZAO ZA TAALUMA

Baadhi ya wanachuo wa STEMMUCO wakijiandaa kutetea kazi zao za kitaaluma

Saturday, April 27, 2013

SIKU YA MUUNGANO STEMMUCO

Viongozi waasisi wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
Mwl. Julius Nyerere na Mzee Abeid Karume wakitia saini makubaliano
Picha kwa hisani ya blogu ya Michuzi   
Siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulikumbukwa kianazuoni zaidi. Siku hii ya leo ambayo ni kumbukizi ya Muungano baina ya sehemu mbili tajwa hapo juu za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; iliadhimishwa kwa namna yake. Kulikuwa na mada nne ambazo ziliwasilishwa na kujadiliwa na wadau mbalimbali ambapo dhima kuu ilikuwa ile ile ya umoja, haki, amani na mshikamano kwa watanzania ili kufikia malengo ya kuungana.



                                  
                                                 Mwalimu Julius K. Nyerere akichanganya udogo wa Tanganyika na Zanzibar
                                                ishara ya muungano huo. Hii kwa hakika ishara yenye nguvu sana.
                                                            Picha kwa hisani ya blogu ya Michuzi

Muungano pamoja na malengo mengine, kwa vyoyote vile ulikuwa na lengo la kufikia maendeleo ya binadamu; maendeleo ya kweli ya Mtanzania na kutoa mfano halisi wa Umoja ama muungano wa bara Afrika.

Mada zilizotolewa pale STEMMUCO zilikuwa pamoja na Muungano na MKUKUTA, Muungano na Uzalendo, Mali asili na Muungano Afrika Mashariki  

Friday, February 8, 2013

MITIHANI INAENDELEA STEMMUCO


WATAALAMU WA BAADAYE WAKIONYESHA UJUZI WA
MAJUMA 16 KATIKA SAA TATU

WANACHUO STEMMUCO WAKIENDELEA
NA MITIHANI MJINI MTWARA



WALIMU WAJIPIMA UJUZI WAO KABLA YA KWENDA KUFUNZA
WENGINE - MITIHANI