Saturday, June 1, 2013

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


National Arts Council BASATA
30/05/2013

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kwa kushirikiana na Chama cha Waandishi wa Habari za Sanaa na Utamaduni (CAJAtz) kila Jumatatu kuanzia saa 4 Asubuhi limekuwa likiendesha ‘Jukwaa la Sanaa’ kwenye ukumbi wake ulioko makao makuu ya Baraza Ilala Sharif Shamba.Katika jukwaa hilo linalohusisha wadau wote wa sanaa, hoja nzito na motomoto kuhusu tasnia ya Sanaa na Utamaduni zimekuwa zikijadiliwa na kujibiwa.

Katika kuelekea urasimishaji wa Sekta ya Filamu na Muziki ambao ulianza rasmi tarehe 1/01/2013, ifikapo tarehe 01/07/2013 hakuna kazi yoyote ya Filamu na Muziki itakayoingia sokoni bila kuwa na stamp ya TRA. Baraza la Sanaa katika Jukwaa la Tarehe 03/06/2013 litazikutanisha taasisi zote nne zinazohusika na urasmishaji ili kutoa elimu kwa Wasanii, wadau na wakuzaji sanaa kuanzia saa 4 :30 Asubuhi. Wadau wa sekta ya sanaa mnakaribishwa kuleta michango na hoja zenu ili kuleta mustakabali utakaojenga sekta ya sanaa. Taasisi zinazohusika na Urasimishaji wa sekta ya sanaa ni :

1. Bodi ya Filamu na Michezo ya Kuigiza

2. Chama cha Hakimiliki na Hakishiriki Tanzania (COSOTA)

3. Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)

4. Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA)

WOTE MNAKARIBISHWA
Godfrey Lebejo Mngereza

KAIMU KATIBU MTENDAJI, BASATA


Barua zote ziandikwe kwa Katibu Mtendaji

All correspondence to be addressed to The Executive Secretary

BASATA Arts Centre, Ilala Sharif Shamba, P.O. Box. 4779, Dar es Salaam, Tanzania.

Telephone: 2863748/2860485, Fax: 0255 - (022) - 286 0486 E-mail: info@basata.or.tz Website: basata.or.tz



No comments:

Post a Comment