Thursday, December 26, 2013

SIKU YA KUFUNGUA MAKASHA YA ZAWADI




                                                                                                                           
IMEPAKULIWA HAPA : https://www.youtube.com/watch?v=L99hWdZGelI

Siku moja baada ya Noeli imekuwa, kimapokeo, ni siku ya kufungua makasha ya zawadi. Soma hii taarifa inaonyesha kuwa kazi ya kupokea makasha ya zawadi ni ya wafanyakazi nyumbani, Makasha ya zawadi hupokelewa kabla ya siku husika na leo kazi inakuwa moja tu ya kuyafungua makasha hayo kutaka kujua kuna nini humo ndani. Utamaduni wa kupeana zawadi siku za matukio maalumu ni jambo na utamaduni mzuri.

Jambo hili ni sehemu ya tamaduni za jamii nyingi duniani, na kama si sehemu ya tamaduni zetu basi ni jambo la kuiga na ni vyema tukafanya hivyo kwa wale tusio na utamaduni huo. Kufanya hivyo kunaendeleza na kujenga udugu, umoja, upendo n.k katika jamii. 


Kupitia utamaduni wa kupeana zawadi tujifunzie hapo hapo pia kutoa misaada kwa wahitaji bila kujali mahusiano yetu ya kindugu. Kwa asili binadamu wote tu ndugu wamoja. Asili, chimbuko letu wote; kidini, kibaiolojia/kisanyansi ni moja. Hivyo tunawajibika kusaidiana. Kwa wale wenye makasha mengi ya zawadi tuwakumbuke wahitaji wasio na msaada wa karibu; yatima, wajane, wagonjwa na wengine wote wenye kuhitaji katika jamii.   

No comments:

Post a Comment