Thursday, July 18, 2013

SIKU YA MZEE MADIBA


Nadhani hii ndo siku pekee ambayo binadamu mmoja amepewa heshima ya kuwa na siku yake ya kimataifa duniani. Ndugu Nelson Mandela kapewa heshima hiyo hasa kwaajili ya kumaliza kwa amani, kupitia tume ya haki na maridhiano, mvutano ambao ungejitokeza baina ya weusi wengi, na jamii nyingine za watu wasio weupe wa asili ya Ulaya kwa upande mmoja, na wazungu wa asili ya Ulaya kwa upande mwingine.

Suluhu hiyo iliyohitimisha miaka mingi ya ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini, kwa utulivu wa namna yake, ndo hasa sababu ya mzee Mandela kupewa heshima yote hiyo.

No comments:

Post a Comment