Thursday, December 8, 2011

UHURU NIGHT


















Wanachuo wa STELLA MARIS MTWARA UNIVERSITY COLLEGE wameendesha mjadala juu ya uhuru wa Tanzania bara. Ni jambo jema mno kusikiliza mawazo na malubano ya kihoja ya wanataaluma / wanazuoni.

Hapa chini kuna sehemu kidogo tu ya yaliyojiri katika mazungumzo hayo. Mijadala ndo hasa fursa za vijana kujifunza kujenga hoja na kuwa na mawazo yetu binafsi jambo hili ni muhimu sana.

Independence and Freedom of TanzaniaJe, Tanzania ipo huru?

Wanachuo wa STELLA MARIS MTWARA UNIVERSITY COLLEGE jioni ya leo wameandaa mdahalo kuadhimisha Jubilei ya dhahabu ya Uhuru wa Tanzania bara, kipindi hicho ikiitwa Tanganyika.

Tanganyika, sasa Tanzania bara, ilipata uhuru wake toka kwa waangalizi wa kiingereza. Waingereza walipatiwa mamlaka ya kuilinda Tanganyika ili itakapokuwa tayari waipatie uhuru wake… maelezo zaidi ni historia ya uhuru wa Tanzania…

Wanachuo wamejadiliana juu ya masuala mengi ya msingi kwa taifa la Tanzania. Wameangalia muda uliopita, uliopo na ujao. Wameangalia mafanikio, changamoto, kufeli kwa viongozi na taifa kwa jumla. Lakini wanachuo wameangalia nafasi na mchango wao pia katika maendeleo ya Tanzania.

Wanachuo waliuchambua uhuru kupitia nyanja kuu tatu:


ii. Kijamii na

iii. Kiuchumi

Watanzania wana uhuru mkubwa kuliko wananchi wa nchi nyingi jirani barani. Hata hivyo changamoto ya uhuru huu ni kwamba uhuru huo unahitaji kwenda sambamba na haki; kuwe na haki kwa wananchi.

Imeelezwa kwamba, wasomi wetu wenyewe ndo hasa wanaididimiza nchi. Wasomi hao wanasaini mikataba mibovu inayoleta kipato duni kwa nchi na wananchi wengi.

Mwalimu JKNyerere aliwaambia wananchi waende vyuoni ili waisaidie nchi na wananchi lakini leo wasomi hao nd’o wasaliti wa taifa. Hawainufaishi nchi katu; wanatumia kalamu zao kuwaibia watanzania wa kawaida.

Wakati Tanganyika ikipata uhuru kulikuwa na lengo kuu la kuwashinda maadui wakuu watatu:

i. Ujinga,

ii. Maradhi na

iii. Umasikini

Wanachuo wamejiuliza tumepiga hatua kiasi gani kushinda vita ya adui hawa watatu?

Leo, twaambiwa watanzania ni wajinga zaidi kuliko wakati tulipopata uhuru; - wasomi wanasaini mikataba mibovu inayoiweka nchi katika hali ngumu kiuchumi ilihali mharibifu husika aendelea kutembea huru tu; hivyo watanzania bado tu wajinga.

Leo hii watanzania bado tu wagonjwa; tunakimbilia kwa waganga wa kienyeji kupunga mapepo na kunyweshwa dawa ya kikombe, kijiko, kibuyu… n.k

Wananchi wengi vijijini wanaendelea kuishi katika umaskini. Hawa masoko ya uhakika wala uhuru wa kuuza mazao yao ili kujipatia mahitaji yao. Wengine wanazalisha kiashi cha kutosheleza kwa miezi kadhaa tu.

No comments:

Post a Comment