Thursday, October 4, 2018

THE POWER OF READING BOOKS - NGUVU YA USOMAJI VITABU



Tafakuri ya  kitabu cha THE POWER OF READING BOOKS(Nguvu ya usomaji vitabu) Na. Shemeji Melayeki.

Mpendwa rafiki natumai haujambo,kwa wasaa mwingine natamani nikushirikishe mambo machache ambayo mwandishi Shemeji Melayaki ameyaelezea katika hiki kifupi kabisa chenye kurasa 14 tu,lakini kikiwa kimesheheni somo kubwa sana,basi nawe karibu twende pamoja.

Watu wakubwa waliowahi kuwapo na waliopo duniani mafanikio yao ukiwafuatilia utawakuta walikuwa ni wasomaji wakubwa wa vitabu,tabia ya usomaji vitabu imekuwa ni ngumu sana kwa watu kuiigia kutokana na uvivu mkubwa watu walionao na hali ya kupenda kuhairisha mambo na hii hujikuta kuona kama suala la usomaji wa vitabu ni la watu fulani au la watu wachache lakini hii si kweli,ila mtu yeyote atakae kufanikiwa sharti asome vitabu ili apate maarifa thabiti katika lile eneo analotaka kujinoa ikiwa ni katika kipaji,biashara,ujuzi,nk.Tabia huathiriwa na tabia hivyo tabia ya kutopenda kusoma vitabu itaathiriwa pale tu utakapo chukua uamuzi leo wa kuanza kusoma vitabu.

Description: 📚Yapo mambo mengi sana mtu hupata faida baada ya kusoma vitabu,machache miongoni mwa hayo ni kama;

-Maarifa humuongezea mtu nguvu ya kujiamini na kufanya mambo makubwa kwasababu anakuwa ana uhakika na lile alifanyalo.

-Maarifa yanamuongezea mtu nguvu ya ushawishi katika kutekeleza mambo makubwa,kwa sababu vipo vitabu vingi vinavyolezea jinsi watu walivyofanikiwa katika maisha yao mfano kitabu cha I CAN,I WILL,I MUST the keys of success kitabu hiki kinaeleza jinsi Dr Regnald Mengi alivyopitia changamoto nyingi hadi kufikia hapa alipo sasa,hivyo nawe kupitia kusoma kitabu utapata nguvu ya ushawishi wa kuona kuwa kumbe mambo makubwa yanawezekana endapo tu ukiamua kweli kuchukua hatua.

-Kitabu huyaunganisha mawazo ya msomaji na mwandishi wa kitabu kwa kupitia njia ya usomaji.

-Viongozi wote ni wasomaji vitabu(all leaders are readers),huwezi kuongoza kama hupendi kusoma vitabu.

-Maarifa ya vitabuni huunoa ujuzi wako na kukufanya uwe bora zaidi katika eneo lako unalofanyia kazi ikiwa ni biashara,kipaji,huduma n.k,Mungu mwenyewe hutumia kitabu kuweka taarifa zake,je si zaidi sana sisi wanadamu? ,Kutoka 32:33
*BWANA akamwambia Musa, Mtu ye yote aliyenitenda dhambi ndiye nitakayemfuta katika kitabu changu.*

Description: 📖MBINU ZA KUANZA KUWA MSOMAJI VITABU.

~Kwanza kabisa tafuta vitabu vya eneo ambalo unapenda kujifunza hii itakufanya uwe na hamasa ya kupenda kujifunza kila siku.

~Anza kwa kusoma kitabu kidogo kwa kuanza na kurasa chache chache mwisho utajikuta ukipiga hatua siku hadi siku kama vile wenye hekima walivyosema kuwa haba na haba mwisho hujaza kibaba.

~Soma kila siku.Usiache tabia ya kusoma japo kwa kurasa chache mwisho utajikuta hii itakuwa ni tabia yako ya kudumu.

~Fanya tafakuri ya yale uliyojifunza.Kufanya tafakuri ni sawa na mmeng'enyo wa chakula baada ya mtu kumaliza kula,nawe ukimaliza kusoma kitabu yaangalie yale uliyojifunza kwa kupiga picha na jinsi maisha yako halisi yalivyo,kisha chukua hatua ya kutendea kazi.

~Shirikisha wengine yale unayojifunza.Usiwe mchoyo wa kuwapa wenzio yale uyajauyo,kwa jinsi unavyozidi kushirikisha watu kile ukijuacho ndipo unapozidi kuwa bora zaidi(master) katika eneo hilo.

Anza leo kusoma vitabu ukianzia kwa hatua ndogondogo huku ukiweka nia ya kutamani kupiga hatua zaidi.Aonaye kununua kitabu ni gharama kubwa basi asubiri kulipa gharama kubwa zaidi atayoilipa kwa kutosoma vitabu.Mtu asiyesoma vitabu uhisi dunia ni kama sehemu ndogo ambayo unaweza kuizunguka na kuimaliza punde kama vile uzungukavyo kijiji,lakini si kweli,ila uhalisia ni kuwa dunia ina vitu vingi sana ambavyo kila siku tunatakiwa kujifunza na hatutavimaliza hadi siku tunakufa,basi anza leo nawe kuishi kiutoshelevu ili uje kufa ukiwa tupu.

Nikutakie heri wewe uendaye kuchukua hatua katika kutenda na hakika ipo siku utajishuhudia jinsi utakavyo kuwa mtu mpya siku baada ya siku katika eneo la maarifa.


Mimi Mwanafunzi wa shule ya maisha,Mchambuzi na mshairi.
Marko Kinyafu.
Description: 📞📩+255 714 129 520
Dar es salaam, Tanzania.

_Kuyatawala maisha huanza kwa kuitawala siku moja na siku yenyewe ndio leo_


No comments:

Post a Comment