Tuesday, November 22, 2011

Barabara kwa Maendeleo

 

Abiria wa Mtwara - Dar es Salaam wakimbilia mabasi yao
baada ya kukwamulia toka tope lililotamalaki barabarani
Usafiri wa uhakika ni moja ya viashiria vya kimaendeleo. Njia za usafirishaji zikiwa nzuri hurahisisha maisha ya watu na kuharakisha maendeleo ya jamii husika na taifa kwa ujumla. Mtwara ni moja kati ya mikoa ambayo imekiwa kisiwa kutokana na miundo mbinu mibovu kwa muda mrefu. Mtwara inafikika kwa njia mbalimbali; kwa ndege, kwa meli, na kwa barabara. Watu wengi zaidi nchini Tanzania husafiri kwa barabara, japokuwa njia hii ya usafiri imejaa damu. Kujegwa daraja la Mkapa ulikuwa ni ukombozi mkuu kwa ukanda wa kusini. Serikali ya Tanzania imeendelea na juhudi kubwa kuijenga barabara ya Dar es Salaam – Mtwara, zaidi ya kilometa 500 kwa kiwango cha lami.

Matembezi ya hiari yaendelea
Ni kipande kidogo kisicho na lami ndo kinaendelea kuwatesa na kuwanyanyasa wananchi wa ukanda huu maarufu kwa zao la korosho na sasa gesi asilia. Kukamilika kwa ujenzi wa barabara hiyo kutaboresha maisha ya wakazi wa mkoa huo ambao ni tegemezi kiasi kikubwa kwa jiji la Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment