Thursday, November 24, 2011

UTANZANIA HALISI

Bendera za vyama kadhaa vya siasa zikipepea nje
ya jengo la Nyumba ya Demokrasia - huko Buguruni Dsm


















Tanzania ni nchi ya kipekee sana hapa duniani. Ndani ya nchi hiyo kuna zaidi ya makabila 120, watanzania hao wana dini nyingi na tofauti tofauti mithili ya nyuki mzingani, itikadi za kisiasa anuwai, kuna vyama vya
kisiasa zaidi ya kumi. Pamoja na mambo yote hayo hulka ya watanzania ni kuishi pamoja bila kujali tofauti zao. Hili ni jambo la msingi na maana zaidi. Utanzania ni muhimu zaidi kuliko dini zetu, itikadi zetu za kisiasa, tofauti zetu za rangi, misimamo yetu ya kitaaluma na kadhalika. Kama jinsi ilivyo kwa Mungu, yeye ni muhimu zaidi kuliko dini ama madhehebu yetu, Mungu hana dini, analojia hiyo tunaweza kuitumia pia kwa Tanzania. Nchi yetu ni muhimu kuliko tofauti zetu zote kama jinsi ilivyo katika vitambaa hivi vyenye rangi tofauti tofauti lakini vyote vinawakilisha watu wa taifa moja la Tanzania. Mungu Bariki Umoja na amani yetu!

No comments:

Post a Comment