Sunday, November 27, 2011

Huu ndo uzuri wa akili ya binadamu...

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndugu Jakaya Kikwete akiongea na Ujumbe wa Chama cha CHADEMA

Ni busara sana kwa kiongozi wa nchi kukubali kukutana na viongozi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo.

Ni busara hali kadhalika kwa CHADEMA kutoka na wazo la kuomba fursa ya kukutana na kiongozi wa juu wa nchi ili kujadili suala hili la msingi kabisa.

Nini viongozi hao wataafikiana ni suala la kusubiri na kujua. Moja ambalo ni dhahiri kwa hakika itakuwa ni fursa nzuri kabisa ya kuweza kufikia muafaka wa mtiririko sahihi wa utaratibu upi utumike kupata chombo cha kukusanya kuratibu, kujumlisha na kutoa majibu ya mawazo na maoni ya watanzania. Kumbe kuna njia lukuki za kusikilizwa kama sehemu moja inashindikana basi unajaribu njia nyingine. Ni vyema sana kuwa viongozi wa CHADEMA wameamua kufanya hivyo. Muhimu kuliko vyote ni amani ya kweli; amani ya kweli ni utulivu unaoendana na haki, hivyo wananchi tunahitaji utulivu lakini pia na hasa haki na usawa katika masuala yanayohusu maliasili za nchi yetu na maendeleo ya watu wake. Tanzania ni muhimu kuliko chama chochote cha kisiasa, Tanzania itakuwepo tu na si vyama vya siasa.  

No comments:

Post a Comment