Thursday, December 1, 2011

UKIMWI DUNIANI : Attention Na SIDA wa François Luambo Makiadi



Picha kwa hisani ya google













Upungufu wa Kinga Mwilini (UKIMWI) ni hali ambayo imezigusa familia nyingi duniani kote lakini bara Afrika likiguswa zaidi kuliko sehemu nyingine za sayari hii ya dunia. Tarehe mosi Desemba huwa ni rasmi kwa shughuli za kuangalia tuliko toka.Wakati dunia ikitafakari hatua ambazo jamii imechukua kuhakikisha maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi yanapungua na pia kuwakumbuka na kuwaombea ndugu zetu walioaga dunia, ni fursa ya kupitia nyaraka na mambo rasmi yanayoweza kutupatia ujumbe rasmi.

Maneno yaliyomo kwenye wimbo maarufu wa Attention Na SIDA wa gwiji la muziki Kongo - Kinshasa na Afrika kwa ujumla François Luambo Makiadi (6 July 1938 - 12 October 1989), ni ujumbe mzuri mno wenye kumgusa kila binadamu kwa kumhadharisha na kumkumbusha wajibu wake. Hebu na tupitie ujumbe huu japo u katika lugha ya kiingereza.

Here is the text of Attention Na SIDA By Greame Ewens

Attention na Sida
Oh, Aids. This terrible sickness
Oh, Aids. A disease which does not pardon
A disease which spares nobody
Aids is a plague
Which leaves doctors impotent

Look after your body, and I'll look after mine
Protect your own body, I'll protect mine
Aids is taking the country
Aids does not discriminate against race
Aids does not discriminate against age
You mothers, beware
You fathers, beware

What can I say, mama? Aids is dividing peoples
Aids has broken marriages, Aids has divided families
Those who used to eat and drink with me, Have started to ignore me
They say I have got the Aids sickness, All my friends are cutting me off
Who can I complain to?


Aids is ravaging all peoples; they are frightened
Europe and the USA accuse Africa of being, The source of Aids
Recently Asia and USA were invaded by the sickness
Today every country is under attack, Aids is not stopping its sinister course
All selections of society are victims of Aids, Babies, children, youths, adults, the old,
Workers, bureaucrats, managers, Men, women and even doctors.
Aids can attack anybody. It can kill, It will kill all who do not protect themselves
You, brothers and sisters who already carry the virus
Do not behave in a way that contaminates others


Aids has made us forget all other illness, If a person is sick, they say it is Aids
If a person has a fever, they say it is Aids, If a person becomes thin, they say it is Aids
If a person dies, they say it is Aids, But why do we forget the other illnesses
Oh God, oh God, Oh God. Only you...,Sickness, Oh where are you coming from?
We forget other illness and talk of Aids

You pregnant women, you can carry the virus, You can transmit it to your babies
They may be infected, although you do not know, Ladies, avoid getting pregnant
If you know you have the virus. It is bad to ignore this, as your child could die young
Youths, beware, Aids can attack you, You are the life force of society
If you let it kill you, who will lead the people?
Avoid dangerous sex. Students beware unknown partners.
Be careful who you take money from, it could get you in deeper trouble.
Avoid occasional partners, Youths, beware of drugs. If you inject drugs with needles
You can become infected, Don´t take drugs. It is very bad for your health

It will bring you out in spots, It will give you diarrhoea.
Avoid picking up just anybody, Think before you make love
Even if you desire someone, be careful. Think first

You gentlemen, citizens, Beware of prostitutes
Avoid multiple partners, And you, ladies, citizens
Take measures for your own protection
Workers, in workshops, factories and offices
When you are talking together, Do not neglect the subject
Time passes quickly, and every day, Death takes the victims of Aids
The best way to avoid death is to protect yourself, Oh God, we pray to you

Priests at mass, pastors in churches, rabbis in synagogues,
Imams in the mosque, you each have an obligation
A great obligation to society. Use your office to help
Preach what society must know about Aids
Do not hold back. It is your duty to tell the people that
Aids is a punishment from God; it resembles
Soddom and Gomorrah in ancient times
Ask God to deliver us from this sickness
Use your prayers to ask God the way to salvation
All my family have run away from me
Because I have Aids. I am left with only my mother,
Who has to suffer again all the sickness of my childhood

Teachers, instructors, professors, At school, in class, at home
If you have a free moment discuss it,It is part of your scholarly obligation
Teachers at school, college and in universities
The parents count on you tp educate their children.
Parents, don´t be shy, tell your children and the youth
All you can about Aids,Tell the whole world, tell everybody to beware
It is for you to fight against Aids
We are waiting for a vaccine. We wait for medicine, It will take a long time to come,
Maybe five, seven or ten years. Change your behaviour
Time is pressing, the sickness spreads fast

Doctors, be like Pasteur, Flemming, Curie and other
Geniusses of the last century, Now is your turn to conquer this plague which
Terrifies humanity and defies medicine,Don't waste time finding the medicine, wherever it is
Get this plague out of the human body, Doctors you know well how Aids is caught
Do not show the disease that you are afraid, Do not discourage the sick by your behaviour
The medical profession looks to you to find courage, To conquer this sickness
Doctors beware, the patient's file is secret, It concerns only the patient and close family
Don't talk su much that you create panic
Your duty is always sacred. Your profession is sacred, Your duty is to find a medicine
If there is a miracle it will come from you, Doctors be careful with needles,
Always wear gloves when you touch blood

Governments of rich countries, help the poor countries
Lead the way in the struggle against Aids, Don't sell them arms to kill,
But provide arms for the War against Aids
Brothers and sisters of the United Nations,
Between yourselves combine experience and, Spread understanding
Political authorities, use the radio, television and the press
To inform the people of the dangers of Aids
Tell us how to protect against and combat Aids,
We must all be mobilised against Aids

Kwa rejea na habari hii soma hapa
This sickness o, this sickness, Can make you go bald

Wednesday, November 30, 2011

Vijana watanzania: Wamachinga wa China!

Picha kwa hisani ya mtandao

Ukosefu wa ajira za kutosha kwa vijana ndo hasa tatizo kuu linaloipasua kichwa serikali ya Tanzania. Hakuna ajira za kutosha kuwapatia fursa vijana wote wanaomaliza vyuo hapa nchini. Hivi karibuni tumesikia idadi ya wahitimu toka vyuo mbalimbali; kati yao wapo walio na ajira na wasio na ajira; kundi la pili likiwa kubwa zaidi. Wahitimu hao kwa baadhi ya vyuo ilikuwa kama ifuatavyo: Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine, SUA, walihitimu zaidi ya 1000, Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agostino, Mwanza, zaidi ya wahitimu 2000, Chuo Kikuu cha Dodoma wahitimu lukuki, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wahitimu lukuki pia. na kadhalika. Utaona ya kwamba kila uchao Vyuo vingi zaidi vinazidi kuongeza idadi ya wahitimu na hili ni jambo jema.

Kwa upande mmoja hili ni suala jema sana kwa nchi yetu, kwamba tunapata wasomi wengi zaidi. Lakini jambo hili halifariji sana pale unapoona kwamba wasomi wote ama wengi kati yao wanasubiri tu kuajiriwa. Hapa ndipo penye changamoto kubwa kwa mitaala ya elimu tunayoitumia toka shule zetu za msingi hadi sekondari. Wengi wa vijana wetu kulingana na mitaala tunayotumia ni tegemezi mno kiuchumi, kimsingi elimu wanayoipata haiwakwamui kiuchumi; pamoja na kumaliza kidato cha sita kijana wa kitanzania bado anaomba pesa kwa wazazi ama walezi kwaajili ya matumizi yake ya kawaida kama kununua nguo n.k; hii ni aibu. Mfumo wa elimu inafaa uweze kumfunza kijana kujitegemea, kuweza kuzalisha mali kwa kiwango fulani hata kama ni dhaifu lakini mtaala huo umsaidie kuwa na uthubutu; kijana awe na moyo wa kujaribu kufanya shughuli fulani halali kwa lengo la kuzalisha mali hata kama ni kidogo tu.

STEMMUCO/SAUT MTWARA
Vijana wanaojiunga na vyuo vikuu wengi ni wale ambao wamepitia mfumo wa kuulizwa maswali, kuyajibu na kupatiwa alama basi. Hakuna nafasi ya kutosha ama hakuna tu kabisa fursa kwa wanafunzi kufikiri ama kujifunza kufikiri vya kutosha. Hii ni hatari sana kwa mustakabali wa nchi na ulimwengu, kama taifa tunawajibika kuwapatia wanafunzi wetu fursa nyingi zaidi za kufikiri na kutafakari mambo, wasiyajibu tu kwa mazoea na kupata alama kubwa za juu ilhali hawafahamu masuala hayo kiundani. Na kukosekana moyo wa kujaribu /na kufanya mambo huwafanya hata wanaojaribu waonekane tofauti na jamii kubwa. Mambo haya yanajitokeza pia kwenye maisha yetu ya kila siku. Hapa naangalia shughuli ya biashara ndogondogo na hata zile za kati zinazofanywa na wananchi wengi hususani katika miji mikubwa nchini.

Vijana wengi wa kitanzania wanafanya shughuli za umachinga; naambiwa machinga moja ya tafsiri zake ni ile ya “marching guys” jamaa watembeao (tafsiri si rasmi). Kwa mtazamo wangu hiki ni kitu muhimu kabisa vijana na ndugu wengine wanaofanya shughuli hizo ni kielelezo tosha kabisa cha ulazima wa kuwa na mitaala ya kufunza ujasiriamali (ujasiri wa kutafuta mali kihalali – tafsiri yangu mwenyewe). Ujuzi wa ujasiriamali na hamu ya kufanya majaribio katika masomo uguse aina zote za masomo yaani ya sayansi, sanaa na kadhalika. Kwa kufanya hivyo utaona kwamba hata machinga wetu watafanya mambo kizalendo tofauti na ilivyo hivi sasa.

Bidhaa za Wajasiriamali - twahitaji kuongeza tu
ubora katika bidhaa zetu na mambo yatakuwa
safi. Picha kwa hisani ya blogu la marchingguys

Wengi wa machinga wa Tanzania kwa hakika ni vibarua wa nchi ya Uchina na nchi nyingi zilizoendelea. Wafanyabiashara wengi wanafanya biashara ya bidhaa zinazotoka nje ya Tanzania. Mfumo wetu wa uchumi, kwa kujua ama kwa kutokujua, umetufanya kuwa soko zuri sana la bidhaa za watu wengine. Fikiri kuhusu vitu ulivyonunua juma hili, bidhaa kumi; pengine sita hadi saba zimetoka nje ya Tanzania, japokuwa zinauzwa na wamachinga wetu ambao kimsingi ni vibarua wa uchina, Afrika Kusini n.k. Serikali ina nia njema sana ya kuwasaidia vijana, ndio maana ikaamua kujenga Machinga Complex pale Ilala. Nimesikia kuna mpango wa kujenga Machinga Complex kadhaa katika mikoa mingine kwa lengo lilelile la kuwakwamua vijana na kina mama. Ukiachia mbali kuhusu ufanisi wa jengo hilo, angalia bidhaa zinazouzwa ndani ya jengo hilo, asilimia kubwa zinatoka Jamhuri ya watu wa Uchina, mita chache toka pale Machinga Complex unakutana na iliyogeuzwa kuwa Dubai ya Tanzania Kariakoo, chunguza bidhaa zinazotoka, Dar es Salaam, Tanga, Iringa, Mwanza, Mbeya, Tabora, Arusha, Kilimanjaro, Mtwara n.k; ni chache mno. Hii ni changamoto kubwa kwa nchi yetu; hizi “Machinga Complexes” zinazowalenga vijana wetu inatakiwa ziuze bidhaa zitokazo Kigoma, Iringa, Ruvuma, Manyara, Mwanza, Shinyanga, Rukwa, Njombe n.k - bidhaa za Tanzania. Tazama hata sekta zingine; usafirishaji: foleni za motokaa kwenye majiji hapa nchini; Dar es Salaam, Mwanza na kwingineko pamoja na magari mengi vile, sina hakika kama kuna moja lililotengenezwa pale Kibaha. Tazama baadhi ya miji yetu ilivyojaa na kuwa jaa la pikipiki, bajaji, baiskeli, hakuna zinazotoka Tanzania, lakini wamachinga na wajasiriamali ni wengi kupindukia, huoni kuwa sisi ni wamachinga wa wachina tu!

Sunday, November 27, 2011

Huu ndo uzuri wa akili ya binadamu...

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndugu Jakaya Kikwete akiongea na Ujumbe wa Chama cha CHADEMA

Ni busara sana kwa kiongozi wa nchi kukubali kukutana na viongozi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo.

Ni busara hali kadhalika kwa CHADEMA kutoka na wazo la kuomba fursa ya kukutana na kiongozi wa juu wa nchi ili kujadili suala hili la msingi kabisa.

Nini viongozi hao wataafikiana ni suala la kusubiri na kujua. Moja ambalo ni dhahiri kwa hakika itakuwa ni fursa nzuri kabisa ya kuweza kufikia muafaka wa mtiririko sahihi wa utaratibu upi utumike kupata chombo cha kukusanya kuratibu, kujumlisha na kutoa majibu ya mawazo na maoni ya watanzania. Kumbe kuna njia lukuki za kusikilizwa kama sehemu moja inashindikana basi unajaribu njia nyingine. Ni vyema sana kuwa viongozi wa CHADEMA wameamua kufanya hivyo. Muhimu kuliko vyote ni amani ya kweli; amani ya kweli ni utulivu unaoendana na haki, hivyo wananchi tunahitaji utulivu lakini pia na hasa haki na usawa katika masuala yanayohusu maliasili za nchi yetu na maendeleo ya watu wake. Tanzania ni muhimu kuliko chama chochote cha kisiasa, Tanzania itakuwepo tu na si vyama vya siasa.  

Thursday, November 24, 2011

UTANZANIA HALISI

Bendera za vyama kadhaa vya siasa zikipepea nje
ya jengo la Nyumba ya Demokrasia - huko Buguruni Dsm


















Tanzania ni nchi ya kipekee sana hapa duniani. Ndani ya nchi hiyo kuna zaidi ya makabila 120, watanzania hao wana dini nyingi na tofauti tofauti mithili ya nyuki mzingani, itikadi za kisiasa anuwai, kuna vyama vya
kisiasa zaidi ya kumi. Pamoja na mambo yote hayo hulka ya watanzania ni kuishi pamoja bila kujali tofauti zao. Hili ni jambo la msingi na maana zaidi. Utanzania ni muhimu zaidi kuliko dini zetu, itikadi zetu za kisiasa, tofauti zetu za rangi, misimamo yetu ya kitaaluma na kadhalika. Kama jinsi ilivyo kwa Mungu, yeye ni muhimu zaidi kuliko dini ama madhehebu yetu, Mungu hana dini, analojia hiyo tunaweza kuitumia pia kwa Tanzania. Nchi yetu ni muhimu kuliko tofauti zetu zote kama jinsi ilivyo katika vitambaa hivi vyenye rangi tofauti tofauti lakini vyote vinawakilisha watu wa taifa moja la Tanzania. Mungu Bariki Umoja na amani yetu!

Wednesday, November 23, 2011

Nyumbani kwa utajiri na ubinafsi mkubwa?


Nyumbani kwa utajiri mkuu na ubinafsi kupindukia?
Picha kwa hisani ya google


Fikra za watu na tafsiri zao!



Hivi mawingu huko angani hutoa ramani za sehemu mbalimbali
ama hutokea tu yakawa jinzi yalivyo kwa bahati tu? Wataalaam
wa Jiografia tafadhali tunaomba maelekezo ama tafiti kujielimisha zaidi  
Hivi karibuni nimesikia mtu aliyetoa tafsiri ya kuwa barani Afrika kumejaa migogoro inayochelewa kutatuliwa na mingine iliyodumu kwa miongo kadhaa sasa kwa sababu ya umbile la bara hilo. Ndugu huyo amedai kuwa bara la Afrika lina umbile la silaha aina ya bastola. Kwamba umbile hilo linalisababishia bara letu kukosa amani ya kudumu.

Bila shaka huu ni mtazamo wa mtu mmoja. Inafaa kuongelea kitu ambacho mtu amekifanyia tafiti ili kuepukana na taarifa  ambazo hazina ukweli wowote ila tu kuipotosha jamii ya wanadamu. Tujenge utamaduni wa kufanya tafiti za kina na si kwenda kwa sangoma kwa mambo ambayo tunaweza kuyapatia suluhu. Bila kufanya tafiti na kuwaelewesha watoto wetu kwa uhakika mambo tuliyoyatafiti tutajijengea hofu na kuendelea kuwa jamii ya hofu na kuogopana.
  
Wingu hili linaonyesha ramani ya wapi na nini tafsiri yake?

Tuesday, November 22, 2011

Sheria ya Mazingira inaishia wapi...?






Plastiki na chupa za maji zikiwa zimetupwa huku na huko na abiria waliochoka
 kutoka na adha ya usumbufu unaoletwa na ubovu wa eneo lisilo na lami.


Barabara kwa Maendeleo

 

Abiria wa Mtwara - Dar es Salaam wakimbilia mabasi yao
baada ya kukwamulia toka tope lililotamalaki barabarani
Usafiri wa uhakika ni moja ya viashiria vya kimaendeleo. Njia za usafirishaji zikiwa nzuri hurahisisha maisha ya watu na kuharakisha maendeleo ya jamii husika na taifa kwa ujumla. Mtwara ni moja kati ya mikoa ambayo imekiwa kisiwa kutokana na miundo mbinu mibovu kwa muda mrefu. Mtwara inafikika kwa njia mbalimbali; kwa ndege, kwa meli, na kwa barabara. Watu wengi zaidi nchini Tanzania husafiri kwa barabara, japokuwa njia hii ya usafiri imejaa damu. Kujegwa daraja la Mkapa ulikuwa ni ukombozi mkuu kwa ukanda wa kusini. Serikali ya Tanzania imeendelea na juhudi kubwa kuijenga barabara ya Dar es Salaam – Mtwara, zaidi ya kilometa 500 kwa kiwango cha lami.

Matembezi ya hiari yaendelea
Ni kipande kidogo kisicho na lami ndo kinaendelea kuwatesa na kuwanyanyasa wananchi wa ukanda huu maarufu kwa zao la korosho na sasa gesi asilia. Kukamilika kwa ujenzi wa barabara hiyo kutaboresha maisha ya wakazi wa mkoa huo ambao ni tegemezi kiasi kikubwa kwa jiji la Dar es Salaam.

Wednesday, November 16, 2011

UDHAIFU CHAMA CHA WASANII TATIZO KWA MAENDELEO YAO

Na Mwanndishi wa BASATA
Mhadhiri Msaidizi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agostino Martin Mandalu akifafanua jambo wakati akiwaeleza wadau wa Jukwaa la Sanaa juu ya utafiti alioufanya kwenye Muziki wa kizazi kipya. Kulia ni  Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo na Habari, BASATA, Godfrey Mungereza.







Utafiti uliofanywa kwenye muziki wa kizazi kipya ukilenga kubaini changamoto na mafanikio yake umebainisha kuwa, kukosekana kwa umoja miongoni mwa Wasanii ni moja ya sababu kubwa ya kudumaa kwa maendeleo yao.

Sababu zingine zilizotajwa ni pamoja na Wasanii kutokuzingatia mikataba kwenye kazi zao, utengenezaji wa kazi za sanaa zenye ubora hafifu, usimamizi dhaifu wa kazi zao, kukosekana kwa viongozi thabiti katika tasnia ya muziki na sababu zingine.

Katibu Mtendaji wa BASATA, Ghonche Materego akionesha kitabu kilichoandaliwa na Mhadhiri Msaidizi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agostino, Martin Mandalu kinachohusu Tasnia ya Muziki Mkombozi Kwa Vijana kwenye Jukwa la Sanaa wiki hii. Kulia ni mtunzi huyo, Bw. Mandalu.

Akiwasilisha utafiti wake alioukamilisha Mwaka huu kwenye Jukwaa la Sanaa la Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) mapema wiki hii , Mhadhiri Msaidizi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agostino, Martin Mandalu alisema kuwa, bila wasanii kuzifanyia kazi changamoto hizo bado kutakuwa na safari ndefu katika kuyafikia mafanikio ya kweli.

Wadau wa Jukwaa la Sanaa wakimsikiliza mmoja wa Wasanii aliyekuwa akihoji sababu hasa zinazowafanya Wasanii wasiwe kwenye umoja pamoja na juhudi zinazofanywa  za kuunda umoja wao.

“Asilimia 80 ya Wasanii waliohojiwa kwenye utafiti huu hawakuwa na taarifa ya uwepo wa umoja unaowaunganisha. Hii ni hatari kwa sababu nilipofika katika vyombo rasmi nilipata taarifa za uwepo wa vyama na mashirikisho ya wasanii. Hii ina maana wasanii hawatambui uwepo wa umoja huo” alisema Mandalu.

Kwa mujibu wa utafiti huo, Wasanii wengi waliohojiwa walikiri kuwa, wamekuwa wakipata mapato kidogo ikilinganishwa na kazi wanazofanya lakini hili likielezwa kuwa linasababishwa na kutozingatia mikataba, kukosekana kwa ushirikiano miongoni mwao na Wasani kutaka kufanya kila kitu yaani utunzi wa nyimbo, usambazaji na hata umeneja.

“Wasanii wengi waliohojiwa walionekana kukosa uongozi na usimamizi thabiti. Walionekana kufanya kila kitu kuanzia utunzi wa nyimbo, kuzifanyia matangazao, kutafuta kazi za maonyesho na umeneja kwa ujumla” alisisitiza Mandalu wakati akifafanua utafiti wake.

Kuhusu utayari wa Wasanii kutoa taarifa au kufika maeneo wanayohitajika, Mhadhiri huyo msaidizi alisema kuwa, ni tatizo kubwa kwani wasanii wengi wamekuwa wazito katika hilo na hata kutokutoa ushirikiano wa kutosha katika masuala yanayowahusu.

“Wengi wa wasanii niliokuwa napanga kukutana nao, walikuwa hawaoneshi ushirikiano. Anaweza kukwambia tukutane saa tano lakini ukifika muda huo anakwambia ana kazi nyingine kwa hiyo haitawezekana” alisema Mhadhiri huyo wakati akieleza changamoto alizokumbana nazo.

Utafiti huo ambao umechapishwa kwenye Kitabu cha Tasnia ya Muziki Mkombozi kwa Vijana umefanywa na Mhadhiri huyo kama sehemu ya kupata shahada yake ya uzamili katika stadi za Maendeleo.

Friday, November 11, 2011

Vimbwanga vya 11.11.11


Bila ubishi hii ni moja ya tarehe za aina yake ambapo kukutana nayo tena katika maisha ya hapa duniani unahitaji kupingana na uzoefu uliopo duniani mpaka hivi sasa. 11.11.11 inatazamwa kwa namna tofauti tofauti na watu tofauti tofauti soma hapa kupata mtazamo wa wanahisabati wanasema nini juu yake.

Vazi la kitaifa na miaka 50 ya Uhuru Tanzania

 Mwanamitindo maarufu nchini Tanzania, Asia Idarous akipita jukwaani na mwanamitindo kuonyesha ubunifu wake katika ufunguzi wa Swahili Fashion week.

Picha kwa hisani ya blogu la michuzi








Umri wa miaka hamsini kwa binadamu si umri haba. Katika umri huo kwa hakika binadamu anaanza kuhesabu mengi aliyoyafanya; lugha yake inaanza kuwa ya wakati uliopita. Utamsikia nilipokuwa fulani, nilipokuwa na kina fulani, nilipokuwa sehemu fulani, nilifanya hivi, nilikuwa hivi... hata hivyo hiyo ni lugha hiyo ni watu tu wa sehemu fulani tu. Kuna wengine ambao husema miaka hamsini ndo kwanza maisha yanaanza na hivyo lugha zao ni zile za wakati ujao, nitafanya hiki, nitakuwa fulani... nita... nita... nita...

 Hata hivyo muhimu zaidi kwa Tanzani hivi sasa ni kuwa baada ya miaka 50 ya Uhuru wa taifa hili ambalo ni nyumbani kwa Serengeti,mlima Kilimanjarokreta ya Ngorongoro, nyumba kwa visiwa vya karafuu Zanzibar bado haina VAZI RASMI la kitaifa. Huu ni wakati kwa wanamitindo na wanasanaa kutumia ujuzi wao kutoa kinachoweza kuwa vazi la taifa na hivyo kuwasaidia watanzania kuwa na vazi lao la kujivunia lenye kubeba na kuheshimu tamaduni zetu. 




Thursday, November 3, 2011

KUMBE KWELI SISI SHAMBA LA BIBI...

Picha kwa hisani ya google
Moja ya makala za HabariLeo katika chapisho lake la leo, imetoa habari inayotufanya nchi yetu kuonekana kama shamba la bibi lisilo na mmiliki...

Bibi ni mama mzazi wa baba ama mama; ni mtu muhimu kwani, huyu pamoja na mumewe ama mwanaume flani ambaye tutamuita babu, ameshiriki moja kwa moja kuwaleta duniani wazazi wetu. Mtu huyu ki-umri amekula chumvi nyingi, na kitamaduni sehemu nyingi barani ni mahiri katika mambo mengi. Ujuzi na busara ya mambo ipo katika uzoefu wa siku nyingi.

Bibi ndiye aliyewalea baba na mama (kila mmoja na mzazi wake - wote waitwa bibi ); hivi basi kwa jinsi wazazi wetu walivyo na nidhamu na utaratibu wa maisha, sehemu flani wamevipata toka kwa bibi. Ni yeye hasa ndio aliyewalea na kupata watoto wenye maadili mema na staha kama tuwajuavyo wazazi wetu. Ni kweli kuwa hupata ujuzi mwingine kwenye mazingira waliokulia, mafunzo sehemu mbalimbali lakini nafasi ya bibi kwa maana ya mzazi na mlezi ni kubwa hasa. Hata hivyo kuna jambo jingine ambalo hushangaza sana toka kwa bibi.

Kina bibi wengi wanaelezewa kama watu wenye kuwadekeza kupindukia watoto wa watoto wao; wajukuu. Kiasi cha kuwadekeza huko, huwashangaza watoto wao yaani baba na mama zetu, ambao mara nyingine hulazimika hutoa simulizi za namna ambavyo bibi alivyokuwa mkali enzi za malezi yake kwao. Kuna sababu kadhaa zinazoeleza kwanini bibi anakuwa mpole na rafiki mno kwa wajukuu zake. Moja ya sababu hizo ni uzee, uchovu na upweke wa utu uzima. Bibi anawahitaji watoto wa watoto wake ambao kwake ni marafiki; ili kuwapata mara nyingi huweza kutumia rasilimali alizonazo kuwaweka kwenye himaya yake. Ni kupitia mwanya huo basi mali za bibi huweza kutumika vibaya; kuharibiwa, kuhujumiwa, kila mmoja akachukua anachotaka na tena kwa nafasi yake. Katika hili bibi hajali mali yake inaharibiwa kiasi gani, muhimu kwake ni kujenga mahusiano na wajukuu wake wakiharibu ama wasiharibu hilo si muhimu kwake muhimu ni kwamba uhusiano wa kirafiki na wajukuu unakuwa bora zaidi na zaidi. Ni kutokana na masuala hayo ndo analojia ya shamba la bibi ikazuka.

Habari Leo hivi leo wametoa taarifa yenye kufanana na analojia ya shamba la bibi. Hapa nchini, katikati ya kitovu cha uchumi wa nchi, Dar es Salaam kumekuwa na shule ikiendeshwa kinyume na sheria kwa miaka kumi na miwili. Hii inaweza kuwa kipande cha pande kubwa la “jabari” la barafu baharini. Si ajabu kuna mengi ambayo hayajagunduliwa na tena yenye madhara makubwa kwa taifa.  Nchi ina mali asili nyingi tena za kila namna; je ni namna gani rasilimali hizo zinaendeshwa katika namna inayowanufaisha wananchi walio wengi na taifa kwa ujumla wake.

Tanzania ina mbuga lukuki za wanyama pori, je shughuli za kiuchumi za wanyama pori zinafanyika kwa jinsi inayotakikana? Je, taifa linapata pato stahiki? Tanzania ina bahari, maziwa, mito na mabonde yenye uwezo wa kunufaisha taifa kwa namna anuwai; je watu waliokabidhiwa madaraka kuendesha vyanzo hivyo vya mapato wanaitendea haki jamii na taifa kwa ujumla? Je, shughuli hizo zinaendeshwa katika namna endelevu? Ili kwamba wajukukuu wa wajukuu wetu wakute mali hizo ama faida zake na wao pia wamudu kuendesha maisha yao kwa furaha? Tunaweza kuorodhesha utajiri na zawadi nyingi zilizopo nchini  hata hivyo si nia yangu kufanya hivyo lengo ni kukumbushana juu ya taifa letu na mustakabali wake.

Kuhitimisha tunasema kuwa kila mmoja wetu awajibike kizalendo ili kulinda na kutetea maslahi ya taifa letu la Tanzania, na kuboresha maisha ya jamii ya wanadamu wanaoishi sasa na wale watakao kuja baadaye kwa taratibu na sheria zinazokubalika.

Monday, October 31, 2011

KIBANGA AMPIGA MKOLONI

Na. Maisha na Mafanikio
Zamani za ukoloni, palitokea Mzungu mmoja. Mzungu huyo hakuwa mtu mwema. Alikuwa mkali na mkatili sana. Kwa ajili ya ukatili wake watu walimwita mkoloni. Wanancgi wote walimchukia sana popote pale alipokwenda.


Mzungu huyo alikuwa Bwana Shamba. Alikuwa na bakora iliyokuwa imetengenezwa kwa mkwaju. Kila alipokwenda kukagua mashamba, alikuwa na bakora hiyo mkononi. Alipendelea sana kuitwa "Bwana Mkubwa". Mkolono huyo alifurahia sana kupiga watu. Aliwapiga watu waliposhindwa kupalilia mashamba. Aliwapiga pamba yao ilipokuwa chafu. Aliwapa taabu sana.

Friday, October 28, 2011

Mtwara by Night

Mmoja wa mitaa ya mji wa Mtwara ukiwa ndani ya giza licha ya umeme wa uhakika mkoani humo- mipango miji wako wapi?

















Mkoa wa Mtwara ni moja kati ya mikoa michache nchini Tanzania isiyofahamu kadhia ya mgawo wa umeme. Mkoa haujaunganishwa kwenye mfumo mmoja wa taifa, hapa ni kwa faida ya wakazi wa Mtwara. Kwani hakuna maana kuwa chanzo cha umeme na usiupate umeme huo. Kwa Mtwara ni tofauti na maeneo yenye utajiri mkubwa ilihali watu wake hohehahe wa kutupwa.

Mkoani Mtwara kuna umeme utokanao na gesi asilia; gesi hii asilia inapatikana mkoni humu na hii inajidhihirisha kwa wakazi wa mkoani humo kwani hakuna mgao. Nafahamu kuwa hii ni hali ambayo wakazi wa mikoa mingi wangependa kuiishi. Na katika hali ya kawaida, ungetarajia kukutana na mitaa yenye kumulikwa vyema na taa nzuri za barabarani nyakati za usiku, lakini hali si hiyo. Nyakati za usiku mjini Mtwara kuna giza kubwa sawa sawa na mikoa yenye mgao wa nishati hiyo muhimu kwa maendeleo ya binadamu. Wazo kwa wahusika wakuu hususani wapanga maendeleo ya mji, wajipange na kuweka taa za barabarani katika mitaa ya mji huo wa kusini mwa nchi yetu ili kuupendezesha mji huo, kuongeza usalama wa mji na hivyo kuvutia wawekezaji wengi zaidi mjini humo.

Elimu kwa Maendeleo

Wanafunzi wa Stella Maris Mtwara University Collegge wakijisomea katika maktaba mpya ya chuo hicho.

Tuesday, October 18, 2011

WASANII WATOA ELIMU

Msanii wa Kundi la Orijino Komedi, Lucas Mhavile ‘Joti’ akisisitza jambo wakati akizungumzia Changamoto anazokumbana nazo kwenye Sanaa ya Vichekesho anayoifanya.


 
 
Picha na maelezo kwa hisani ya BASATA

BASATA NA HAKI ZA WASANII

Meneja Mzalishaji wa Kundi la Vichekesho la Orijino Komedi, Sekion David ‘Seki’ (aliyesimama) akiongea na wadau wa Jukwaa la Sanaa wiki kwenye Ukumbi wa BASATA.Wengine kutoka kulia ni Kaimu Mratibu wa Jukwaa hilo, Aristide Kwizela, Msanii Lucas Mhavile ‘Joti’ na Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo na Habari, BASATA Godfrey Mungereza.

Picha zote na maelezo kwa hisani ya mwandishi wa BASATA

BASATA YAWATAKA WASANII KUJITAMBUA

Na Mwandishi  BASATA
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limewataka wasanii kujitambua kwa kuwa na mipango ya muda mfupi na mrefu katika kazi zao na kutambua thamani yao.

Akizungumza wiki hii kwenye Jukwaa la Sanaa linalofanyika makao makuu ya BASATA, Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo na Habari, Godfrey Mungereza alisema kuwa, kujitambua kwa msanii ni mwanzo wa kuipa kazi yake thamani kubwa kuliko ilivyo sasa ambapo wasanii wamekuwa wakikubali kulipwa malipo kidogo.

“Sanaa ni kazi, sanaa inalipa, ni lazima wasanii wawe na mipango ya muda mfupi na mrefu. Muhimu ni kwa wasanii kutambua thamani yao na kazi wanazozifanya. Ifike mahali wasanii watambue thamani yao ni nini” alieleza Mungereza...

Friday, October 14, 2011

Julius Kambarage NYERERE (1922-1999)







Huko Tanzania, Oktoba 14 ya kila mwaka imetangazwa kuwa siku mahususi ya kumkumbuka na kumuenzi Julius Kambarage Nyerere, maarufu zaidi, Mwalimu Nyerere, ni siku aliyofariki huko Uingereza mwaka 1999. Rais wa kwanza wa nchi hiyo, MwanaAfrika na mjengadunia halisi; mpigania uhuru wa nchi nyingi barani humo, mwanafalsafa, mwandishi, mzalendo, mcha Mungu na binadamu mwadilifu.

Mwalimu ni mmoja kati ya viongozi wachache wa kiafrika aliyekuwa kwenye mamlaka kwa muda mrefu. Alikuwa waziri mkuu wa kwanza wa Tanganyika mara tu baada ya kupata uhuru 1961  (1962 -1985) bila kujilimbikizia mali kama wafanyavyo viongozi wengi barani humo, mwalimu hakuwa mbinafsi. Alijitahidi kuishi vyema na kufuata misingi ya fikra za ujamaa na kujitegemea alizoziasisi.




Mwalimu pamoja na wenzake aliasisi Azimio la Arusha ambalo lilitoa maelekezo ya kuliongoza taifa ikiwa ni pamoja na maadili ya viongozi. Hii ilisaidia kuongoza nchi kwa uadilifu na ubadhilifu ulidhibitiwa kwa umakini, “Awamu ya kwanza rushwa ilikuwepo, lakini mtoa na mpokea rushwa wote walitiwa msukosuko mkubwa,… aliyebainika kupokea rushwa alicharazwa viboko 24, kumi na viwili kabla ya kwenda gerezani na kumi na viwili akimaliza kifungo chake ili akamwonyeshe mke wake…”

Julius Nyerere alikuwa na fikra binafsi ambazo aliziasisi, moja ya fikra hizo ni ile ya Ujamaa na kujitegemea. Katika nadharia hii Mwalimu alilenga kujenga taifa lenye uwezo wa kujipatia mahitaji yake lenyewe bila kutegemea sana mataifa ya ng’ambo. Mwalimu alijaribu kusimamia nadharia hiyo kwa mfano hata kama haikufanikiwa kama ambavyo angependa.

Zaidi Mwalimu aliwaunganisha watanzania wenye makabila zaidi ya miamoja na ishirini; wakati Tanganyika ikipata uhuru, kulikuwa na vijitaifa vingi, hivyo kazi aliyoifanya Mwalimu na viongozi wenzake ilikuwa ni kuunganisha mataifa hayo madogo madogo kuwa taifa moja kubwa. Kazi hiyo nzuri ilisaidia kuliepusha taifa hili la Tanganyika, na kisha muungano wa Tanganyika na Zanzibar 26. 04. 1964, Tanzania, toka kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe ambazo zimesambaa kote barani Afrika.

J.K Nyerere aliasisi mbio za Mwenge kwa tukio lenye hisia, kumbukumbu, na ujumbe mzuri hasa. Mwenge huo wa uhuru ulisimikwa kileleni mwa mlima mrefu kuliko yote barani Afrika; Kilimanjaro. Ni kapteni Alex Nyirenda wa jeshi la wananchi wa Tanganyika ndiye aliyefanya kazi hiyo nzuri. Akihutubia mjumuiko wa Umoja wa mataifa Mwalimu Nyerere alisema sisi tumeamua kuuwasha mwenge na kuuweka juu ya Mlima Kilimanjaro ili umulike hata nje ya mipaka yetu, ulete tumaini pale walipokata tama, heshima palipojaa dharau (si maneno halisi)…………Ni dhahiri kuwa makala hii ni fupi mno kumuelezea mmoja wa waasisi wa taifa tukufu la Tanzania. Hata hivyo jambo la msingi ni je, tunamuenzi  kwa kiasi gani Mwalimu Julius Nyerere?

Miaka kadhaa baada ya kifo cha Mwalimu, Tanzania inaendelea kumuenzi mzee huyu aliyefanya mambo mengi makubwa kwa taifa hili la Afrika Mashariki, lenye utajiri mkubwa japokuwa utajiri wake hauwafikii wote kwa usawa. Taifa linaendelea kumuenzi sana Mwalimu kwa sifa na sherehe zenye mbwembwe nyingi kote nchini. Lakini hatumuenzi Mwalimu kwa mambo ambayo yeye mwenyewe aliyataja kama muhimu kufikia maendeleo ya kweli ya watu. Kwani lengo kuu la kuongoza nchi ni kuleta maendeleo kwa wananchi; mwalimu alisema ili tuendelee tunahitaji mambo manne;

1. Watu,

2. Ardhi,

3. Siasa safi na

4. Uongozi bora

Ili nchi zetu ziweze kuendelea tunawahitaji watu wenye elimu nzuri, afya njema, chakula cha kutosha na mahitaji yao muhimu ya kila siku ili kushiriki katika ujenzi wa taifa lao, jamii ya wanadamu na dunia kwa ujumla wake. Lakini hivi leo watu wengi wa nchi hiyo bado hawana huduma za lazima kufikia wanapotaka kufika.
















Ardhi, ni chanzo cha vyakula vingi anavyotumia binadamu na ni sehemu ambapo shughuli za kijamii na kimaendeleo za binadamu hufanyikia. Hii leo hiyo yenye utajiri, rutuba na mengine muhimu wanapatiwa wananchi wachache wenye pesa nyingi na wageni wenye mapesa na ushawishi mkubwa.

Siasa safi na uongozi bora ni tunu muhimu na za lazima kwa maendeleo ya watu…tunu hizo zimepiga hatua kubwa kwa malengo nia ile ile ya kuleta maendeleo kwa watanzania. Hata hivyo bado kuna mapungufu katika nyanja hiyo ya siasa safi na uongozi bora; kwa hivi kuna haja ya kuendelea kufanya marekebisho kwenye suala hili la uongozi. Hivi leo huko Tanzania, siasa inaonekana kama ni ajira yenye kuleta kipato kikubwa kwa haraka, matokeo yake watu wengi wenye kutaka utajiri wa haraka haraka, ikiwa ni wasomi, wafanyabiashara, wakulima hukimbilia siasa hata kama hawana wito huo. Viongozi wengi hivi leo hawana maadili sahihi ya uongozi, wameingia siasa kwa malengo mbalimbali; wengine wameingia kulinda biashara zao, wengine kujiongezea heshima tu na kulinda malengo yao binafsi. Azimio la Arusha lilitoa mwongozo namna gani kiongozi aongoze watu wake. Siasa safi na uongozi bora ni muhimu mno kwa maendeleo ya kweli ya WATANZANIA WOTE! Hivyo lazima kuwe na namna flani ya Azimio la Kujenga maadili ya viongozi nchini!

Picha kwa hisani ya tovuti ya nyerere.info

Thursday, October 13, 2011

MUDA WA KUSAKA FIKRA ZAIDI


Mtaalamu wa burudani za mafunzo akiburudisha na kuelimisha wageni waalikwa siku ya hiyo ya ufunguzi wa mwaka wa masomo.

         MJ wa Mtwara hakukosa kwenye orodha ya waelimisha jamii wa siku                                      
   



                                                                                                                                                                
Burudani hii murua ilitufunza namna ya kupokea tofauti na vipaji vyetu na kuendelea kuishi kati jumuiya moja kwa upendo na mafanikio. Burudani nyingi zilitolewa na kundi hili maarufu la SAUT TRAVELLING GROUP (STG)




MUDA WA KUSAKA FIKRA ZAIDI

Picha kwa hisani ya blogu ya mdau Muliriye

Jumatatu ya 10.10.2011 ilitumika kufungua mwaka wa masomo Chuo Kikuu Cha Mtakatifu Agostino – Mtwara. Masomo ni njia ya kumwezesha mtu kugundua vipawa vyake na kuvitumia kwa malengo yale yale ya kuweza kuitawala dunia na vilivyomo humo ilikuboresha maisha ya jamii ya wanadamu.

Elimu ya Chuo Kikuu, kwa kutumia maneno ya Mwalimu Nyerere, ni elimu hasa yenye malengo ya kumfunza mtu kuwa na fikra bayana, kuwa na uhuru wa fikra, kuchanganua, na kutatua matatizo kwa kiwango cha juu kabisa, haya ni mawazo ya Mwalimu kwa maneno yangu. Kwa hivi basi elimu ya Chuo Kikuu imjenge kijana kuwa na fikra binafsi na tena zenye nia ya kuiendeleza jamii ya wanadamu.

Kumbe elimu hiyo ya juu haina lengo la kumfanya mwanafunzi akariri, lengo kuu ni kumfanya awe na uwezo wa kujenga fikra binafsi, zenye kuweza kuijenga jamii na awe na uwezo wa kuyatetea na kuyasimamia mawazo yake, kwa kufanya hivyo ndio tunaweza kupata wagunduzi (wavumbuzi), wanasayansi na watu waliotayari kuijenga dunia.

Huko SAUT Mtwara, shughuli za kuanza mwaka wa kuendeleza ujenzi wa fikra mpya ulianza kwa kuomba msaada wa Mwenyezi Mungu na kisha kufuatiwa na shughuli mbalimbali za kijamii.



Baadhi ya wageni mashuhuri wakielekea eneo la tukio


Wageni Maarufu na mashuhuri mno walikuwepo, hapa Profesa kijana akiwa na wadau wengine wakielekea eneo la tukio katika viwanja mahususi kwa tukio la siku

Hapo chini wadau wakiimba wimbo wa Taifa kabla ya kuanza shughuli yenyewe

Tuesday, October 11, 2011

Falsafa - kiwanda cha fikra!















Muhula wa mwaka mpya wa masomo wa vyuo vikuu nchini Tanzania kwa kawaida huwa ni miezi ya Septemba na Oktoba. Hii ni kwa sababu wanaojiunga na vyuo humaliza masomo yao ya elimu ya sekondari mwezi Februari, na kisha matokeo yao kutoka hufuata utaratibu maalumu kuomba nafasi ya kujiunga na vyuo vikuu nchini ambavyo idadi yake yazidi kuongezeka. Pamoja na vyuo vikuu nchini kuongezeka, bado vyuo hivyo haviwezi kuchukua idadi ya wanafunzi wote nchini wenye sifa za kujiunga na elimu hiyo ya kiwango cha juu. Vyuo kadhaa binafsi vinasaidia kwa kiasi kikubwa kutatua tatizo hili kwa kuanzisha matawi ya vyuo hivyo sehemu mbali mbali nchini. Kwa kiasi kikubwa hii inasaidia sana kuwapatia wanafunzi wengi fursa za kuendelea na masomo katika elimu ya juu.

Katika makala hii naangazia japo kwa ufupi tu tawi la Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agostino kilichopo mjini Mtwara. Chuo hiki ambacho kilianza kama kituo cha masomo cha "Saint Augustine University of Tanzania" (SAUT) kimepiga hatua sasa na kuwa "University College" hatua ya juu kuelekea kuwa na mamlaka binafsi. Chuo hiki kinafundisha programu ambazo hakuna sehemu nyingine hapa nchini. Moja ya programu hizo ni ile ya falsafa na elimu. Falsafa ni somo geni kwa wanafunzi wengi wa nchi zinazotumia kiingereza kama moja ya lugha zake rasmi, hususani za Afrika Mashariki, kwa nchi zinazotumia kifaransa, somo hili hufunzwa hata katika elimu ya sekondari.

Falsafa ni chimbuko kuu la mawazo; humjengea mtu nafasi ya kuwa na fikra binafsi ambazo anaweza kuzisimamia na kuzielezea bayana. Kwa mtazamo wangu binafsi, nchi zetu za Afrika, kupitia viongozi wake, zina haja ya kubuni mikakati na fikra binafsi za kiafrika ili kutatua matatizo yanayotusibu hapa barani. Falsafa inawapatia wanafunzi fursa ya kukutana na mawazo ya watu mbalimbali toka bara ulaya, bara Asia, Marekani, na pia barani Afrika; inafanya hivyo kwa lengo la kumpatia kijana fursa ya kujenga fikra zake binafsi. Wakati kijana anapata fursa ya kujenga mawazo binafsi, anafaidika pia na kwa kujifunza masuala ya maadili, jambo ambalo lazitatiza nchini nyingi barani Afrika, hususani tatizo la rushwa.

Wakati vijana wanaanza safari yao ya kujenga na kunoa bongo zao ni vyema wakajipanga kwa kusoma mambo ambayo yatainufaisha jamii nzima ya wanadamu na hivyo kuwa kweli wajenzi wa dunia; kila mmoja wetu ana nafasi ya kuwa mjenzi wa dunia hii kwa namna yake mwenyewe kulingana na vipaji alivyojaaliwa; akiongeza na kipawa cha falsafa mambo yatakuwa mazuri zaidi.


Picha kwa hisani ya google

Wednesday, October 5, 2011

Siku ya Walimu duniani












Picha zote katika makala hii ni kwa hisani ya google
Oktoba, 5 ni siku ya walimu duniani. Siku hii ambayo kimataifa imeanza kusheherekewa 1994, ina malengo hasa ya kuikumbusha jamii ya wanadamu kuwa walimu ni muhimu kwa maendeleo ya jamii zetu na kwa dunia kwa ujumla. Ni fursa nzuri kuwakumbuka walimu ambao wamechangia sisi wote kuwa hapa tulipo.

Walimu ndio chanzo cha mafanikio katika kila sekta, kila mtaalamu, katika hali ya kawaida, huhitaji mwalimu wa aina yoyote ile ili kujifunza, kuboresha alichonacho ama kujifunza zaidi na kuwa imara zaidi. Kwa hivi hata wale wenye vipawa maalumu bado ni lazima wapate maongozo ya namna flani. Kwahiyo kimantiki, mwalimu inatakiwa awe ni mtu mwenye uwezo mkubwa sana kiakili, uwezo mkubwa wa kuwafundisha wengine na si kinyume chake. Na zaidi tunahitaji walimu wengi ili kutoa ujuzi kwa watu wengi zaidi. Vigezo hivi muhimu vyatulazimisha watanzania kutafakari kwa kina mahitaji yetu ya walimu na ubora wao.















Kwa Tanzania, tunaungana na jamii ya kimataifa kusheherekea siku hii adhimu kwa jamii ya wanadamu. Ni muhimu kwa kuwa kila mmoja wetu ana mwalimu ama walimu wake ambao kamwe hawezi kuwasahau kwa jinsi walivyomsaidia na kumjenga kitaaluma, kiutu, kijamii na kadhalika.

Kama tulivyoona hapo juu, mwalimu ni mtu mwenye (anayepaswa kuwa na) mafunzo ama ujuzi maalumu kwaajili ya kuwafunza na kuwasaidia wengine. Mtu mwenye kufanya hizo inafaa awe na uwezo mkubwa wa kuelewa na kuwasilisha ujuzi huo kwa watu wengine. Ujuzi na uwezo wa mtu, kwa bahati mbaya sana, mpaka hivi sasa hupimwa kutumia vyeti alivyonazo. Vyeti hivyo huonesha matokeo ya mitihani mbalimbali ambayo mtu huyo alifanya; binafsi siamini njia hii ya namna ya kupima uwezo wa mtu, nakumbuka HakiElimu waliwahi kusema elimu sio cheti bali uwezo. Kurejea kwenye mada yetu, swali hapa ni je, walimu wetu Tanzania wana sifa zipi na ni namna gani huwapata?

Sina rejea sahihi kuhusiana na uwezo wa Mwalimu Julius Nyerere, ila simulizi za walimu wangu shuleni zinaonesha(hapa ni uvivu wa kufanya utafiti) kuwa alikuwa mwanafunzi hodari ndio maana akasomea ualimu. Mwalimu wangu darasani aliniambia kuwa huo ulikuwa ni utaratibu wa kikoloni kuwa wanafunzi wenye uwezo mkubwa darasani wanakwenda kusomeshwa ualimu ili wafundishe wengine. Utaratibu huu ulikuwa na mantiki na maana kubwa sana. Mtu anataka kuwa mwalimu awe ni yule aliyefaulu vyema sana katika masomo yake, kwa kutumia vyeti, tuchukue wanafunzi wenye daraja la kwanza na la pili.

Na kwa taaluma zingine, ambazo pia ni muhimu kama vile utabibu, uhandishi, sheria, wanasaikolojia n.k kuwe na utaratibu utakaofaa; wanafunzi wote wakifundishwa vyema na walimu wenye uwezo mkubwa basi madaraja yoyote kuanzia la kwanza hadi la tatu yanaweza kutoa wataalamu wenye sifa takikana kabisa. Kwa hali ilivyo hivi sasa baadhi ya watu hapa Tanzania waidharau taaluma ya ualimu, kiasi cha kushauri mwanafunzi aliyefanya vibaya mitihani kusomea ualimu. Sasa hii, si sawa, kwa kuwa mwanafunzi ambaye hana uwezo wa kutosha kuelewa inawezekana kabisa akawa na uwezo mdogo wa kuelewesha wengine. Kwa hivi basi kuna haja ya kuangalia kwa makini namna tunavyowapata walimu wetu wa baadaye ili kupata  kuwa na uhakika wa kupata wanataalamu wa fani zingine waliofunzwa na walimu wenye ujuzi na uwezo wa kufaa kuwapatia elimu hitajika. Kinyume na hapo tutapata wataalamu wasioiva sawasawa ni muhimu sana.

Ili wanafunzi wanaofanya vyema waweze kwenda kusomea ualimu na kufunza ni muhimu wakapatiwa motisha ili kuwahamasisha. Ni muhimu kufanya hivyo kuwa kila binadamu ana uhuru wa kufanya aonavyo muhimu ili mradi tu hadhuru ama haathiri haki za wengine. Kuwe na utaratibu na sheria ya namna ya kuwafanya wanafunzi waliofanya vyema zaidi kwenda kusomea ualimu. Hiyo inaweza kuwa moja ya malengo ya kimaendeleo ya taifa hasa wakati huu ambapo hapa nchini kuna shule nyingi kama zilivyo kata. Ili kuepuka kuendelea kuwa na takwimu kubwa ya shule bila ubora stahiki basi hilo tuliangalie.
Shule ya Tusiime Picha na google












Sifa stahiki za walimu zinatupeleka kwenye sifa stahiki pia kwa shule zetu. Serikali ya Tanzania imepiga hatua kubwa kwenye sekta ya elimu, japokuwa, bado kuna mengi yanatakiwa kufanyika. Kuwa na shule kila kata ni hatua nzuri mno ya kimaendeleo, lakini aina gani ya shule ni muhimu zaidi kwa kuwa shule inaweza kuwa ni ukombozi ama utumwa. Mwanafunzi aliyefunzwa vyema yeye na jamii yote ya wanadamu itakuwa imekombolewa ilhali yule asiyefunzwa barabara atakuwa mzigo mkubwa kwa jamii; kwa vile atatazamwa kama aliyekombolewa na elimu. Mtu aliepata elimu katika mazingira duni ya kitaaluma ni mtu aliyeelimika nusunusu, mtu mwenye elimu nusunusu ni hatari kweli katika jamii kwani anaweza kuutumia, ashalkumu si matusi, umbumbumbu wake kuleta madhara akidhani kuwa anatoa msaada kwa jamii. Kwa hiyo wito hapa ni kuboresha walimu na mazingira yao ili wafanye kazi kwa uzuri na hivyo kuwa chachu kwa maendeleo ya taifa lote.