Wednesday, September 14, 2011

Clouds Fm hongereni lakini...


Hiki ni kivuko kinachotoka Mtwara kwenda Msanga Mkuu.
Picha inaonekana kwa mbali kiasi; vitu unavyoona vya rangi ya pinki vikipepea ni maboya ya kuokoa maisha. Unaonaje yavaliwe wakati gani?

Kituo cha redio (Mawingu) Clouds Fm cha jijini Dar es Salaam, kimeanzisha mkakati wa kuchangia ununuzi wa maboya ya kuoa maisha-mkakati huo umepewa jina la "OKOA MAISHA"  Maboya hayo "life jackets" hutumika kuokoa maisha ya abiria endapo ajali ya majini itatokea. Maboya hayo huvaliwa na abiria kwenye ndege-ili kwamba chombo hicho kikiangukia majini, husaidia kuoa maisha ya abiria, vazi hilo hutakiwa kuwepo pia kwa chombo chenye kusafirisha abiria majini. Clounds wanapiga la mgambo ili kusaidia wasafiri majini. Kwa hili binafsi nawapongeza sana. Hata hivyo kuna mambo mawili hapa ya kutafakari si tu wa mpiga mwano huu bali ni kwa watanzania wote.

Mosi, binafsi natambua kuwa kwenye ndege maboya hayo, kwa kawaida, huwatosha abiria wote; kila abiria anakuwa na life jacket chini ya kitivchake. Na hivyo kikitokea kile ambacho katu hakitamaniki, bali kila abiria hupata kutumia boya lake. Nimesafiri mara mbili kwa maji toka Dar es Salaam kwenda Zanzibar, binafsi sikumbuki “boya langu” lilikuwa wapi. Kwa kusema hivi sina uhakika je, kila abiria kwenye vyombo vya maji hapa Tanzania, ana uhakika wa kupata boya lake ama, je idadi ya maboya inalingana na idadi ya abiria chomboni?

Swala la pili ni juu ya muda wa kuvaa boya hilo. Nilipokuwa mwanafunzi kule Uganda, nilipata nafasi ya kutembelea wafungwa kwenye gereza lililo kisiwani katika mji wa Jinja. Kwenda gerezani, chuo nilichosoma kiliweka utaratibu wa kila mwanafunzi kuvaa boya lake pale anapokuwa chomboni. Hi ili wanafunzi wasafiri kwa usalama na uhakika zaidi. Tunaweza kuanzisha utaratibu kama huo pia, kila abiria avae boya “life jacket” pale tu anapoingia chomboni. Najua utaratibu huu utazua hofu kwa abiria na wamiliki wa chombo.

Abiria, akivaa boya la kuokoa maisha, atajihisi kama anaingia kwenye ajali moja kwa moja na ataona kama anajiombea dua baya kwa kufanya hivyo. Mmiliki wa chombo atahisi kuwa abiria wataondoka ya maboya yake na safari inayofuata hakutakuwa na boya hata moja. Tukitaka kufanikiwa lazima tubadilishe tamaduni zinazobadilika.

Tuvae maboya mara tunapoanza safari majini; kwa kufanya hivyo ndo tutakuwa tunajali maisha hofu za kimazingaombwe kamwe haziwezi kutusaidia. Mmiliki wa chombo majini, aweke utaratibu wa kukusanya maboya mwisho wa safari; kila aingiaye chomboni apate boya na kila anapotelemka akabidhi, kama hana alipe gharama ya boya hilo hata kama hakuvaa. Kuokoa maisha ni lazima tuwe wabunifu, makini lakini pia wakali kwenye utekelezaji. Utaratibu huu kwa kiasi fulani unafanyika pale kituo cha mabasi, Ubungo, Dar es Salaam.(Kukagua abiria kama wamefunga mikanda)

Mandalu

Uzembe ukipungua ajali pia zitapungua !

Google Image
                                          Inapakiwa hapa https://www.youtube.com/watch?v=MpzE7flW9_A
Wakati tukiendelea na tafakari juu ya ajali ya meli kule Nungwi ni wasaa mwafaka kwa watanzania na wanadamu wote kwa ujumla na hasa wenye kutumia vyombo mbalimbali kusafirisha binadamu wennzao, iwe ni vya ardhini, majini ama angani, kuwa waangalifu zaidi. Ajali ya meli ya abiria LCT Spice Islanders, iliyokuwa ikitoka Unguja kwenda Pemba, imesababisha vifo vya ndugu zetu wengi. Ni msiba mkubwa kuona watu wengi wenye afya njema na ambao ni  nguvu kazi muhimu kwa ujenzi wa Taifa, wakiaga dunia.Tunamwomba Mwenyezi Mungu kwa huruma yake awapokee ndugu hawa kwenye makazi ya kudumu, na wafiwa na wajeruhi wote wapate faraja na kupona haraka! Kutokana na tukio hili serikali na wananchi wote kwa ujumla wetu tunapenda kuona wamiliki vyombo vya kusafirishia abiria, mamlaka za kudhibiti vyombo vya usafiri na wasafiri wenyewe wakiongeza umakini...

Tuesday, September 13, 2011

Vijana na Mabadiliko

Makala ya Mwandishi Ahmed Rajab; Vijana wa Afrika wanawaperemba tu viongozi... imejaa mambo anuai ambayo yana manufaa mengi kwa kijana mwenye malengo ya kuchangia katika jamii yake.

Mwandishi anaongelea mwamko mpya wa vijana barani Afrika katika kudai haki za jamii zao, aidha anatoa picha ya jinsi viongozi wabadhilifu wanavyo tumia vibaya mali za umma kwa manufaa binafsi.

Monday, September 12, 2011

Tandahimba Pia


















Sekondari ya Milongodi ilikuwa na walimu wetu pia. Hapa mkuu msaidizi wa shule hiyo akitushirikisha jambo kuhusu sekondari hiyo ambayo ingali ikikuwa kabisa.

Katika shule hii kidato kimoja kina wanafunzi wa kiume tu bila binti hata mmoja, Zaidi ya hayo walimu, kama ilivyo katika shule nyingine nyingi, ni wachache mno. Kwahiyo, walimu mafunzoni ilikuwa ni ukombozi mkubwa kwa shule nyingi za wilayani Newaala na Tandahimba, mkoani Mtwara. Pengine muda wa mazoezi uongezwe, ili huduma hiyo iendelee kwa muda mrefu zaidi? Tutawauliza walimu hawa mafunzoni.

Walimu mafunzoni

Nilipata fursa ya kukutana na walimu-mafunzo
sekondari ya kutwa Newala mjini

Alaa kumbe ni NEWALA !














Hapa nikijiandaa kuanza safari asubuhi na mapema- mjini Newala! Picha na Eric Wamalwa

Nipo wilayani Newala. Hii ndo wilaya ya kwanza kuandikishwa hapa Tanzania, ni moja ya wilaya tano za mkoa wa Mtwara. Wilaya hii, kama jinsi ilivyo kwa maeneo mengine, ina mahitaji ya kiuchumi, kijamii na kisiasa. Kuna makundi yote ya lazima katika jamii; watu wazima, vijana, na watoto.

Kijamii; maji ni shida (jamii imejenga utamaduni wa kuvuna maji ya mvua: karibu kila familia ina mikingio maji kwaajili hiyo – huu ni utamaduni wa kuigwa hasa na sehemu zenye mvua za kutosha. Maji hayo ya akiba yaweza kuwa na matumizi kedekede. Mfano kumwagilia bustani za mboga mboga, kuanzisha mabwawa ya samaki n.k )

Elimu: wilaya ina shule kadha wa kadha; karibu kila kata ina shule yake. Hili ni moja ya mambo mazuri ya serikali iliyopo madarakani. Ni vyema kuwa na shule za kuweza kuandikisha wanafunzi wengi iwezekanavyo. Vijana wengi wakiandikishwa shule za sekondari ndo hasa mwanzo mzuri na wa uhakika wa kupiga vita umasikini kwa vitendo. Hata hivyo mtaala wa elimu uzingatie mfumo wenye vitendo zaidi kuliko nadharia kama ilivyo hivi sasa. Vijana wetu wengi wakimalima masomo yao, kwa mfumo tulio nao hivi sasa, hulazimika kusubiri ajira. Mfumo unaofaa ni ule wa kumuandaa kijana ili aweze kujiajiri; hilo hasa ndo liwe lengo la elimu yetu. Tukirejea mada yetu; shule nyingi huko Newala zina watenda kazi wachache sana.

Shule kadhaa zina walimu wawili, watano, sita, nyingi zina idadi isiyozidi walimu kumi. Hii ni changamoto kuu na kubwa mno katika sekta ya elimu. Wanafunzi wanapokuwa na walimu wa kutosha ndo inawarahisishia kujifunza kwa ufanisi zaidi. Kwa walimu wakiwa na wanafunzi kiasi, kwao inakuwa ni vyema zaidi katika utendaji kazi wao.

Ukosefu nyumba za walimu; shule nyingi za kata zipo vijijini hasa, ni sawa kwani huko ndiko wanapoishi wananchi na watanzania wengi zaidi. na vijiji vyetu vingi havina huduma kwa wageni hususani nyumba za kulala wageni. Ukosefu nyumba za kulala wageni vijijini unakwamisha hata wakaguzi na wataalamu wa kada zingine kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi. Shule nyingi hizi za kata ama hazina nyumba za kutosha kwa walimu ama hazina kabisa nyumba hizo. Ni kweli walimu waliopo katika shule hizo ni wachache pengine inajieleza sawa pia kutokuwa na nyumba kwa walimu. Kuwa na nyumba za ziada kwa walimu inaweza kuwa ni fursa ya kuwavutia walimu wageni, ambao wengi wafikapo kujitambulisha na kuona mazingira ya shule hugoma kurejea shuleni huko.

Kisiasa: Newala ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa hivyo huko pia kuna mfumo wa vyama vingi vya kisiasa lakini wakazi wa huko wanaishi kwa amani na undugu. Hata hivyo hii ni tathmini yangu ya juma moja tu.

Kiuchumi: zao la korosho ni uti wa mgogo wa uchumi wa wilaya hiyo; wakazi wengi hujihusisha na kilimo cha zao hilo la msimu na lenye kuhitaji matunzo ya karibu hasa. Kwa wananchi wanaoweza kufuata vyema maelekezo ya wataalamu wa kilimo hujipatia mavuno na pesa nzuri kutokana na kilimo cha zao hilo. Hata hivyo mkulima siku zote huchukua tu bei inayopangwa sokoni na watu wengine; yeye hufanya kazi ngumu ya kutunza shamba na kufuatilia ukuazi wa korosho hadi kuwa tayari na kisha hapo watu wengine wenye “utu” zaidi ya mkulima hukaa meza na kupanga bei ya zao hilo kama ilivyo kwa mazao mengine ya wakulima wetu maskini hapa Tanzania na sehemu nyingi nyingine barani Afrika. Siku moja tufikie hatua ya kupanga bei ya mazao yetu wenye kwenye hilo soko la dunia; hii ni mantiki zaidi kwa kuwa wakulima wetu ndio wanafahamu haswa gharama za kilimo.

Ajira za vijana: Vijana kundi lenye nguvu na msukumo mkubwa wa maendeleo ya wakati uliopo na ujao katika jamii. Nikiongea na vijana kadhaa wa mjini Newala niligundua kuwa kuna idadi kubwa ya vijana wa kitanzania wanofanya shughuli za kiuchumi, hususan biashara nchini Msumbiji. Newala ni wilaya ya mpakani kabisa na Msumbiji. Upande wa kaskazini ya Msumbiji haujapiga hatua kubwa kimaendeleo na hivyo kutoa fursa nyingi kwa watafuta mali: hivyo vijana wetu hupitia huko na kufanya biashara za bidhaa anuwai. Vijana niliongea nao, wanijuza kuwa vijana hao wa kitanzania huko, hususani wale wenye bidii ya shughuli zao, ni wenye mafanikio makubwa.

Nyumba za kulala wageni chache: wilaya hii ina nyumba chache za kulala wageni. Upungufu huo hivyo unatoa fursa za kiuchumi kwa wananchi kujiimarisha kiuchumi na hivyo kujiongezea pato na pia kuongeza pato la taifa kwa ujumla.Kuna changamoto lakini pia fursa anuwi za kujiimarisha kiuchumi, kujiondoa kwenye umasikini na kuchangia kwa pato jumla la taifa.



Tuesday, August 23, 2011


Baadhi ya wadau wa Vijana tukisimama kwa picha ya pamoja

Wadu wa Vijana

Hapa ni Moro nikiwa na wadau wa vijana.
Hawa ni wadau toka mikoa mbalimbali waliokutana kujadili masuala ya afya ya uzazi na maendeleo ya vijana kwa ujumla.

Picha kwa hisani ya kiongozi wa mradi wa masuala ya vijana wa fhi









Saturday, August 20, 2011

Vijana Maji Moto

Picha kwa Hisani ya mtandao
Hivi karibuni tumeshuhudia harakati kubwa za vijana sehemu mbalimbali duniani. Harakati hizo zimekuwa na dhima na vyanzo tofauti tofauti. Harakati za vijana mashariki ya kati na Afrika kaskazini zilisababishwa na kukosa mahitaji yao muhimu hususani kukosa nafasi za kazi na kutokuwa na uhakika wa mustakabali wa maisha yao. Giza hilo kwa mustakabali wa maisha ya vijana ulisababishwa na ubinafsi wa viongozi wa nchi hizo. Kiongozi wa Tunisia, Ben Ali amekuwa madarakani kwa muda mrefu na amejikusanyia mali nyingi mno na hivyo kuharibu matumaini ya vijana na wananchi wake kwa ujumla. Hali kadhalika, Misri, Libya, Yemen na kwingineko mashariki ya kati.

Vijana wa Uingereza wao nao walisababisha fujo ama varangati (Kiswahili cha kizamani) lakini wao sababu ilikuwa tofauti. Makala ya mwandishi kutoka London Macha, inatoa sababu ambazo zinawapambanua vijana wa Uingereza na wale wa Mashariki ya kati. Wachambuzi wengine husema kuwa vijana wa dola hiyo kuu zamani, wanafundishwa tu/ ama zaidi juu ya haki zao, hawafahamu kuhusu wajibu wao kwa jamii. Hili ni tatizo kubwa. Vijana wanapokua ni vyema tukawajuza haki zao, lakini muhimu kabisa watambue pia namna ya kuwajibika kwa jamii zao. Hili ni jambo la kila mahali Tanzania na nchi nyingine zote duniani, na tena muhimu kwa wananchi na pia serikali kutoa mchango wo kwa maendeleo ya vijana.

Tanzania kuna asasi zisizo za kiserikali (AZAKI) lukuki zinazojihusisha na masuala ya vijana. AZAKI hizo zimeanzishwa na wananchi kwa malengo lukuki, ikiwa ni pamoja na kuwahudumia vijana. Hili ni jambo jema kwani vijana ni moja ya makundi yaliyo muhimu kwa maendeleo ya jamii ya wanadamu. Hata hivyo katika siku za nyuma kidogo kulizuka AZAKI nyingi ambazo hazikujali masilahi ya walengwa husika bali waanzilishi kujijaza mapesa.

Serikali yetu Tanzania, imepiga hatua kubwa hasa kwa kuwa na utashi muhimu wa kisiasa na kuazisha shule za sekondari kila kata. Bila ubishi hii ni hatua kubwa sana ya kuelekea maendeleo ya kweli. Elimu mwanzo wa ustaarabu wote duniani; elimu kwa upana wake si tu ile ya darasani. Hata hivyo changamoto kubwa kwa serikali ya Tanzania na wananchi wake kwa ujumla wao ni kuziboresha shule hizo lukuki za kata. Ni muhimu kufanya hivyo kinyume na hapo tunapata taifa la watu walioelimika nusu nusu. Hii elimu nusu ni hatari sana, pengine afadhali asiyeipata kabisa; mwenye elimu nusu hatokubalika katika kundi la wajinga kabisa kwani ana maarifa kiasi na hivyo kuwa tofauti na wasiosoma kabisa, lakini hawezi changamana pia na walioiva vilivyo kielimu kwake itakuwa ni kujinyanyapaa – “kujichora” (maarufu kwa vijana) mbele ya wasomi. Ni hatari kama nusu wasomi hawa watakuwa wengi; watadai haki kwa njia zisizokubalika kwani elimu yao yawatuma hivyo.

Hivyo AZAKI zilenge kuwasaidia vijana wapate stahili yao. Wananchi wote kwa ujumla na serikali kwa maana ya dola tujipange kuziboresha shule hizi haraka iwezekanavyo kama inavyoelezewa kwenye MKUKUTA II ili kuepukana na nusu wasomi na matatizo mengi toka kwa vijana wetu siku zijazo.

Wednesday, August 3, 2011

Familia Inafaa - Families Matter Program! FMP

Hapa nikiwa na mratibu wa Mradi wa Familia Inafaa huko mkoa wa Ruvuma. Wanakikundi ni wadau wa Familia Inafaa katika mkoa wa mashujaa wa kingoni, nyumbani kwa simba wa vita 



Hapa nikiwa na raia wa siku nyingi hapa Tanzania. Mzee huyu ananipatia somo juu ya malezi kulingana na uzoefu wake wa siku nyingi duniani hapa- asante mzee! 



      
                                                                                                                                                               Hapa nikiwa na wadau wa Familia Inafaa mkoani Mtwara; hapa ni kijiji cha Nanguruwe Mtwara Vijijini!


Familia Inafaa – Families Matter Program! (FMP)













Huu ni mradi unaongozwa na Kampuni ya T-MARC. Mradi huu unawalenga wazazi, walezi na wadau wa malezi ya watoto ambao bado hawajabalehe kwa wavulana na hawajavunja ungo kwa mabinti. Familia Inafaa! Ni mradi ambao tayari umeshaanza kutoa huduma kwa wazazi na walezi wa mikoa ya Mtwara na Ruvuma.
• Lengo la msingi kabisa la FMP ni kuwatia shime wazazi katika juhudi zao za kuwalea watoto wao ili wakue katika afya njema.

• FMP ni program mahususi kwa ajili ya wazazi. Imeandaliwa katika namna ambayo inawasaidia wazazi kutumia mbinu ambazo zinaweza kuwalinda watoto wao dhidi ya tabia hatarishi za afya ya jinsia, hivi sasa na wakati ujao pia.

• FMP inaamini kuwa wazazi wana nafasi yenye ushawishi mkubwa wa kujenga, katika namna chanya tabia za kiafya za watoto wao.

• Lakini hata hivyo ushawishi huo ni lazima ushindane na ujumbe wanaoupata watoto wao toka kwenye vyombo vya habari, vijana wenzao, na jamii yote kwa ujumla.

• Mawasiliano ya wazazi yanaweza kuwalinda watoto, kujenga uwezo wa kufanya maamuzi yafaayo, na kufikisha ujumbe sahihi.

• FMP inataka kuwasaidia wazazi “kuongeza ujuzi wao” kwa kuwapatia vifaa na mbinu mahususi kabisa ili waweze kuwa na mtindo bora wa afya katika familia zao.

Saturday, July 23, 2011

Tunu bora ni Msingi wa Maendeleo ya Watu:Je, Za Afrika ni zipi?

Mlima Kilimanjaro - TANZANIA, paa la Afrika, na Twiga, ambao hupatikana kwa wingi nchini Tanzania.
 Bila shaka hizi ni alama muhimu zinazoitambulisha TANZANIA na bara Afrika.
Hivi tunu za Afrika ya leo ni zipi hasa? Tunu za Afrika ya kina Julius Nyerere, Kwame Nkrumah, Patrice Lumumba, Kenneth Kaunda, Houphouët-Boigny, Frantz Fanon, Nelson Mandela, n.k zilikuwa za umoja, kuungana, kushirikiana, uzalendo kwa bara letu, na kufanya kazi kwa bidii. Tunu za leo ni kuhakikisha kuwa kiongozi anashinda uchanguzi kwa mbinu zozote zile halali ama haramu, mashindano ya kujilimbikizia mali kwa wingi iwezekanavyo. Kwa majumuisho ni ushindani wa ubinafsi. Viongozi na raia wanajenga ubinafsi kwa gharama yoyote ile ikiwa ni pamoja na kuzifanya nchi zetu kuwa vyama wanavyoweza kuvitawala kwa mihula mingi wapendayo wenyewe na mashwahiba wao. Nchi zetu nyingi hatujui hasa nini tunataka kukifanya; tuna maandishi, vielelezo na miongozo mingi mizuri lakini isivyofuatwa katu. Jambo tunalopaswa kujiuliza hapa ni je, kwa tunu hizi za kibinafsi bara Afrika linaweza kweli kuwa mshirika wa maendeleo ya dunia?


Afrika, nyumbani kwa watu zaidi ya milioni 900. Bara hili ni mama ya nchi zaidi ya hamsini. Wenyeji wa bara hilo huitwa Waafrika. Waafrika hawa wana asili mbalimbali; waafrika weusi, waafrika wenye asili ya bara asia, waafrika wa asili bara ulaya. Uanuwai huu unalifanya bara kuwa na utajiri wa tamaduni na hivyo kumiliki tunu kedekede. Kufuatia bahari hiyo ya tofauti, utaona kuwa kuna nafasi ya kupata tunu zilizo bora kabisa mithili ya mbegu za kisasa zenye kufanyiwa tafiti katika maabara na mashamba darasa ya wataalam wa kilimo.


Bara Afrika, kisayansi – daktari Leaky, lasemekana kuwa ndio nyumbani kwa binadamu wa mwanzo hapa duniani. Kwa mantiki hiyo bara hili ilifaa liwe limepiga hatua kubwa zaidi kimaendeleo katika nyanja mbalimbali kama vile (kv) kisayansi, kijamii, na kadhalika kuliko ilivyo hivi sasa. Barani Afrika nyanja iliyopiga hatua kubwa zaidi ni ile ya kijamii. Nyanja nyingine zingali nyuma mno. Sayansi na teknolojia, elimu bora kwa ujumla wake vingali nyuma mno.


Uwanda wa masuala ya kijamii umepiga hatua kubwa barani humo. Ni hulka ya wanyama wote, wawe wa mwituni ama binadamu mwenyewe, kuwalea na kuwatunza watoto wao na pia kuishi katika jamii. Utaona kuwa kwenye eneo hili Afrika imepiga hatua kubwa hasa. Jamii nyingi katika Afrika bado huishi pamoja watu, familia kadhaa zinazotengeneza ukoo bado huishi pamoja. Ni jambo la kawaida kwenye familia za Kiafrika kuona ndugu wa mbali kabisa ama msaidizi akiishi na kutendewa vyema kama mtoto wa familia mwenyeji. Ni barani humo ndo kijana wa miaka hata thelathini huendelea kuishi kwa baba na mama akiwa tegemezi kabisa. Tamaduni za sehemu nyingine duniani humtaka kijana wa miaka kumi na nane aanze kujitegemea; ajitenge na aanze kujenga maisha yake mwenyewe. Ndugu wa mbali katu hathubutu kuishi na familia ya mbali naye. Tamaduni zote hizi zina mazuri na mapungufu yake, hata hivyo hii si mada ya leo. Kwa leo tuendelee na suala la sayansi na teknolojia hapa barani.


Kwenye uwanja wa sayansi na teknolojia bara Afrika linashika nafasi mbili muhimu, ya mwanzo na ya mwisho kabisa; hakuna mkaganyiko, nitaelezea:

Kwenye ubunifu, ufikirivu; utengenezaji na matumizi ya bidhaa za kiteknolojia bara hilo li nyuma kuliko mabara yote.

Kwenye matumizi ya bidhaa za kiteknolojia na kwa kuwa jaa la bidhaa duni, dhaifu, mbovu, zenye  kukaribia kuisha muda wake na ambazo hutengenezwa ughaibuni, bara letu laongoza. Umeona, hakuna mkanganyiko wowote bali ni ukweli tupu ila tu wenye kuumiza.

Hivyo katika uwanda huu bara Afrika chini ya viongozi na waafrika wote kwa pamoja tunawajibika kujenga uzalendo wa kulipenda bara hili ili kuleta ustawi na maendeleo ya kweli kwa Waafrika na hivyo kutoa mchango kwa maendeleo ya dunia yetu. Kwenye moja ya mada zilizotangulia tuliona kuwa maendeleo huchangiwa kwa kiasi kikubwa na tunu zilizo mahali husika. Kwa mtiririko huo wa kimawazo basi, tujiulize je, hapa barani Afrika tunu zetu ni zipi hasa?

Aina ya maisha na jinsi mtu anavyoishi, ikiwa ni pamoja na nyanja za kijamii, sayansi na teknolojia, husaidia katika kumuainisha binadamu husika. Waafrika kwa asili yao ni wakarimu, marafiki, wenye uteremeshi, na wenye tabasamu la kweli lililo karibu mno takribani muda wote. Furaha, bashasha juu ya binadamu wengine ni tunu zilizojaa pomoni maishani mwa mwafrika. Kwenye sayansi na teknolojia ili mmoja aweze kupiga hatua kubwa kwenda mbele ni wajibu kuwa na tunu za kujali muda zaidi, kujituma na hata kuwa mtumwa wa muda kwa kupangilia kila jambo linalotakiwa kufanyika, mtu kujali na kupenda kazi aifanyayo na kubwa zaidi uzalendo kwa nchi, na bara lake. Tunu hizi na nyingine zenye kuleta tija kwa kazi ni muhimu hasa kwa kufikia malengo mahususi ya maendeleo. Tunu hizi zipo pia barani Afrika lakini zimefichwa mno mithili ya vinasaba dhaifu visivyo na athari yoyote katika maisha ya binadamu. Kisha maelezo hayo basi ni muhimu mno kuimarisha tunu zinazoweza kuchochea maendeleo ya kweli.

Bara Afrika kongwe kwenye tunu za ukarimu, upendo, undugu, n.k limeishangaza dunia baada ya kutumbukia katika lindi la kuporomoka kwa utu na upendo barani humo. Kwa miaka kadhaa kumekuwa na vita pande nyingi barani humo. Vita nyingi barani humo zimechochewa na sababu nyingi za kibinafsi; uroho wa mali nyingi kupindukia, uchu wa mamlaka, na hata hamu ya utukufu binafsi. Jamii ambazo zilitazamwa kama zenye wema, upendo na utu wa hali ya juu ziliingia kwenye janga la mauaji na kusababisha ulemavu wa kudumu kwa watu wao. Kumekuwa na vita pande zote; kaskazini, kusini, magharibi na mashariki hali kadhalika. Wakati jamii nyingi duniani kote zinaungana, baadhi ya jamii za kiafrika zinatengana, zinawindana na kudhoofishana badala ya kusaidiana kuleta maendeleo kwa watu wao.Tumeona kuwa watu hutambulika na kuainishwa kupitia tunu zao.

Hivi tunu za Afrika ya leo ni zipi hasa? Tunu za Afrika ya kina Julius Nyerere, Kwame Nkrumah, Patrice Lumumba, Kenneth Kaunda, Houphouët-Boigny, Fanon, Nelson Mandela, n.k zilikuwa za umoja, kuungana, kushirikiana, uzalendo kwa bara letu, na kufanya kazi kwa bidii. Tunu za leo ni kuhakikisha kuwa kiongozi anashinda uchanguzi kwa mbinu zozote zile halali ama haramu, mashindano ya kujilimbikizia mali kwa wingi iwezekanavyo. Kwa majumuisho ni ushindani wa ubinafsi. Viongozi na raia wanajenga ubinafsi kwa gharama yoyote ile ikiwa ni pamoja na kuzifanya nchi zetu kuwa vyama wanavyoweza kuvitawala kwa mihula mingi wapendayo wenyewe na mashwahiba wao. Nchi zetu nyingi hatujui hasa nini tunataka kukifanya; tuna maandishi, vielelezo na miongozo mingi mizuri lakini isivyofuatwa katu. Jambo tunalopaswa kujiuliza hapa ni je, kwa tunu hizi za kibinafsi bara Afrika linaweza kweli kuwa mshirika wa maendeleo ya dunia?

Monday, July 18, 2011

Siku ya Nelson Rolihlahla Mandela

Leo Jumatatu, 18 Julai ni kumbukumbu ya kuzaliwa Mzee Nelson Mandela, rais wa kwanza wa Afrika Kusini ya Kidemokrasia (18.07.1918). Kadri ya kumbukumbu zangu huyu ndiye mtu pekee ambaye Umoja wa Mataifa umemtengea siku katika mwaka mahususu kwa heshima yake. Hivi leo anatimiza miaka 93 toka azaliwe; ni mmoja kati ya viongozi wachache wa Afrika ambao wameishi kwa muda mrefu.

Nelson Mandela ni mtu anayepewa heshima kubwa duniani kote kwa wanaomfahamu na hata wasiomfahamu. Watu wengi hasa nje ya Afrika hususani katika jamii zinazopenda kusoma vitabu wamfahamu kupitia kitabu chake cha "Long Walk to Freedom". Hiki ni kitabu kinachoelezea historia ya maisha yake kwa kina kabisa. Sehemu kubwa ya kitabu hicho ameiandika yeye mwenyewe na tena akiwa gerezani. Hili ni moja ya mambo ya kujifunza toka kwa mzee huyu-maktaba kubwa duniani kote. Tujipange tuandike historia zetu sahihi ili kuiachia jamii na dunia kwa ujumla utajiri wa mawazo kama alivyofanya mzee Mandela. Wengine tulimfahamu mzee Madiba toka enzi za utoto; tukiwa shule ya msingi tuliimba nyimbo za kutaka Mandela achiwe huru na serikali ya makaburu. Utawala wa makabulu ulitawala Afrika Kusini kwa mabavu na kwa misingi ya kibaguzi ya rangi za binadamu; ni udhalimu wa aina yake kwa ustawi wa wanadamu.

Kwanini mzee huyu ni maarufu vile?

Saturday, July 16, 2011

Uhuru wa wahadhiri kimawazo

Makala ya Profesa Mbele juu ya uhuru wa kimawazo wa wahadhiri, kwa hakika, imenitia hamu kubwa kuendelea kuijadili. Nadhani ni suala la msingi kabisa kulitazama hasa hivi leo ambapo kuna vyuo vikuu lukuki hapa nchini. Ni muhimu kuupongeza uongozi wa nchi kwa kuruhusu kuanzishwa kwa vyuo vikuu vingi hapa nchini. Vyuo vikuu vingi moja kwa moja vinamaanisha kukua kwa wigo wa fikra nchini. Kuongezeka kwa fikra ni mwanzo wa ugunduzi na kichocheo kikuu cha maendeleo.

Moja ya masuala makuu katika kipindi cha " Scholarsticism" karne ya 12 na 13 ilikuwa ni kuibuka kwa wingi kwa vyuo vikuu vilivyotoa maarifa ya aina mbalimbali. Kipindi hicho Kanisa lilikuwa na mamlaka makubwa hata juu ya kilichofunzwa vyuo vikuu. Matokeo yake kazi za mwanafalsa Aristotle (384—322 BCE) zilikataliwa, hata hivyo kukataliwa huko kulikuwa kwa muda mfupi tu kwani baadaye kazi za gwiji huyo zilianza kufundishwa katika vyuo vikuu na kuboresha zaidi mawazo kwa wanavyuo na wanazuoni.

Kwahiyo basi ni vyema kwa viongozi wa nchi yetu kulitambua hilo na kuwaacha huru wahadhiri wafanye kazi yao, ambayo kimsingi hulenga kujenga wananchi wenye ukomavu wa kujenga hoja na kuzisimamia ili kuendeleza nchi yao na dunia kwa ujumla.

Kupata mawazo zaidi ya Profesa Mbele soma makala hiyo murua kabisa hapa








.

Tuesday, July 12, 2011

MITUME WA BWANA KATIKA MAZIWA MAKUU


Hiki ni kitabu kinachoelezea safari za mwanzo kabisa za wamisionari wa shirika la wamisionari wa Afrika. Shirika hilo la dini lilianzishwa na Kadinali wa Algiers Charles-Martial Allemand Lavigerie wa Ufaransa.

Kwa hivi wengi wa wamisionari hao walitoka Ufaransa na kuja kutangaza neno la Mungu. Hawa walifika eneo la maziwa makuu hasa Afrika ya Mashariki ya leo; hivyo kitabu hiki kinaelezea historia nzuri ya ndugu hao waliofika kwa mara ya kwanza mwaka 1878. Mbali na kutangaza neno la Mungu, kitabu kinatoa pia historia ya Tanzania toka Bagamoyo hadi Kagera.

Maelezo zaidi juu ya historia ya eneo na habari hizo inapatikana hapa:  http://www.africamission-mafr.org/bagamoyo.htm

Thursday, July 7, 2011

KAZI YA TANU NA TANZANIA YA LEO


Viongozi wa TANU
Flag of TANU.svg
Bendera ya TANU
Tarehe 7 mwezi Julai, 1954 (7.7.1954) ni siku ya kuzaliwa kwa chama cha kisiasa kilichosaidia kudai uhuru wa Tanganyika. Tanganyika National Union (TANU) kilikuwa Chama cha kisiasa kilichowaunganisha wananchi wengi wa kawaida wa Tanganyika na kuwa na nguvu ya pamoja kupigania uhuru wao.

Chama hicho kilikuwa na imani na ahadi za mwanachama. Nazipenda hasa ahadi za mwanaTanu. Ahadi hizo kwa hakika inafaa ziwe ndo TUNU za taifa letu la jamuhuri ya muungano wa tanganyika na Zanzibar- Tanzania. Ahadi za TANU ambazo zimeasiriwa na Chama cha Mapinduzi, (CCM), ni mali ya watanzania wote kwa sababu zililenga kuikomboa nchi na wananchi wote kwa pamoja bila kujali itikadi zao za kisiasa, rangi, dini, wala kabila. Chama cha TANU na pia CCM ndani ya mfumo wa chama kimoja kilikuwa ni mali ya waTanzania wote na hivyo basi ahadi hizo za mwanaTANU ni mali ya waTanzania wote.

Hivi leo tunapokuwa katika mfumo wa vyama vyingi ni dhahiri kuwa vyama vya kisiasa vina katiba, imani na miongozo mbalimbali ya kisiasa, hiyo ni vyema kwa ushindani wa kisiasa. Tanzania kama nchi, pmoja na kwamba ina mwongozo mama-Katiba, inafaa iwe na TUNU ambazo zitafuatwa na wananchi wote bila kujali itikadi zao za kisiasa. Ahadi za mwanaTANU zinaweza kutufaa sana.

AHADI ZA MWANATANU

(1)Binadamu wote in ndugu zangu na Afrika ni moja

(2) Nitaitumikia nchi yangu na watu wake wote

(3) Nitajitolea nafsi yangu kuondosha umaskini, ujinga, magonjwa na dhuluma.
(4) Rushwa ni adui wa haki, sitapokea wala kutoa rushwa.
(5) Cheo ni dhamana, sitatumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu.
(6) Nitajielimisha kwa kadri ya uwezo wangu na kuitumia elimu yangu kwa faida ya wote.
(7) Nitashirikiana na wenzangu wote kujenga nchi yetu.
(8) Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko.
(9) Nitakuwa mwanachama mwaminifu wa TANU na raia mwema wa Tanzania na Afrika.


Tuesday, July 5, 2011

SIKU YA JUMUIYA SAUT - Mtwara

Sehemu ya kwaya ikiongoza maandamano ili kuanza ibada. Naam waimbaji walipendeza hasa! 

SIKU YA JUMUIYA SAUT - Mtwara

Sehemu ya wanajumuiya wakifuatilia matukio ya siku yao kadri yalivyokuwa yakitokea

SIKU YA JUMUIYA SAUT - Mtwara

Jumuiya za watu duniani zinajenga utamaduni wa kukutana kwa malengo mbalimbali. Kuimarisha umoja wao, kujenga uzalendo kwa jumuiya na kadhalika. SAUT Mtwara ni jumuiya ya wasomi; watu wanaoandaliwa kuwa wajenzi wa dunia. Kwa kuwa jumuiya ya aina hiyo ina jukumu kubwa la kujielimisha zaidi ili kuondoa ujinga binafsi na kuisaidia jamii yake, basi inafaa mara mojamoja kupata nafasi ya kujipumzisha. Tarehe 4 Juni, 2011 ilikuwa ni siku ya jumuiya hiyo.

Kulikuwa na shughuli kadha wa kadha kuishi siku hiyo; ikiwa ni pamoja na hotuba anuwai za kitaaluma na maonyesho toka idara za hapo chuoni.

Sehemu ya wanajumuiya ya Saut wakianza sherehe za siku yao kwa maandamano.

Monday, June 27, 2011

UTANDAWAZI NA MALEZI

Na. Mdee Mwanahiza

Picha kwa hisani ya mtandao

Kamusi ya Kiswahili sanifu toleo la pili (2010) imeelezea maana ya utandawazi kua ni mfumo wa uhisiano wa kimataifa katika nyanja mbalimbali kama vile biashara, uchumi au siasa uliowezeshwa na maendeleo ya teknolojia ya habari yanayofanya mataifa kuwasiliana kiurahisi


Malezi ni njia ya ukuzaji wa mtoto kwa kutarajiwa kufuata tabia na mwenendo unaostahiki, makuzi na mafunzo.kwa watoto na vijana wanaokua katika jamii husika. Kwa ujumla utandawazi ni hali ya mabadiliko katika nyanja mbalimbali za kimaisha ya mwanadamu kama vile Uchumi, Siasa Jamii na Utamaduni na kuwa katika hali ya mfanano mmoja duniani kote. Mabadiliko haya yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na kukua na kuenea kwa sayansi na teknolojia ambayo imesambaa kwa kiasi kikubwa sana na kugusa karibu kila sekta ya maisha ya mwanadamu.

1:1 CHANGAMOTO KATIKA MALEZI

Kutokana na kukua na kuenea kwa utandawazi kumeathiri suala zima la malezi na kupelekea watu hasa watoto na vijana kukosa mwelekeo bora wa kimaisha kutokana na kulega kwa wakala wa malezi.

1:2 WAKALA WA MALEZI

Wakala wa malezi ni vyombo vinavyofanya kazi kwa niaba ya jamii husika katika kuhakikisha kwamba watoto na vijana wanapata malezi na mafunzo mema yanayoendana na jamii hiyo kama vile heshima, nidhamu, staidi mbalimbali za kimaisha ili waweze kujiandaa na maisha yao ya baadae na kuweza kushiriki katika shughuli mbalimbali za uzalishaji bila kupotoka na mambo mabaya yasiyostahiki katika jamii.

Hapo awali wakala wa malezi walikua ni familia, shule na dini pamoja na jamii yote kwa ujumla. Lakini kutokana na jamii kuzidi kukua na kuongezeka katika masuala ya uzalishaji, biashara na kupelekea kukua kwa miji kumesababisha kuongezeka kwa wakala wengine wa malezi kama vile vyombo vya habari hasa runinga, tovuti na simu za mkononi, magazeti na majarida mbalimbali. Makundi rika ambayo yanatokana na kukua na kuenea kwa sayansi na teknologia nayo yamekua ni miongoni mwa wakala wa malezi.. Hivyo kwa pamoja tunaweza kusema kisosholojia kwamba kuna wakala watano wa malezi ambao ni Familia,Dini ,Shule, Vyombo vya habari pamoja na makundi rika.

Wakala hawa wa malezi kila mmoja ana nafasi yake katika suala zima la kutoa malezi kwa vijana na watoto wa jamii husika. Kutokana na kipaumbele cha jamii hiyo kwa vijana na watoto.

1:3 FAMILIA

Kisosholojia familia ni muunganiko wa Baba, Mama na Watoto pamoja na ndugu wengine wa karibu. Kimsingi familia ndiyo muhimili mkubwa katika jamii yoyote ile. Mtoto anapozaliwa huanza kupata malezi kutoka kwa Baba na Mama yake pamoja na ndugu wengine wanaoizunguka jamii hiyo ili aweze kukua kwa kufuata mila na desturi za kimaisha katika jamii yake. Mtoto hufunzwa mambo muhimu kama vile heshima,Utii, adabu na nidhamu mbele ya wazazi wake na watu wengine nje ya familia yake pia hufundishwa stadi mbalimbali za Kimaisha na kujiingiza katika shughuli mbalimbali za uzalishaji mali ndani na nje ya familia.

Takribani miongo mitatu imepita tangu tulipopata mafanikio ya sayansi na teknologia ambayo yamekua ni chachu ya mageuzi katika familia zetu na maisha ya jamii nzima kwa ujumla. Mageuzi haya yameziathiri sana familia zetu katika suala zima la malezi, hi imesababisha baba na mama kuwaacha watoto wao wadogo na kwenda kufanya kazi za Ofisini mbali na nyumbani kwa siku nzima na kuwaacha watoto na walezi wengine..Hapo awali mwanamke ndiye aliyekua mlezi mkubwa wa familia wakati baba alikua anatoka nyumbani na kumuacha mama na kwenda kutafuta riziki kwa ajili ya familia yote. Mabadiliko haya ya baba na mama wote kwenda kutafuta riziki mbali na familia yao yameleta mmomonyoko wa maadili kwa watoto kwa kiasi kikubwa na kupelekea familia nyingi kusambaratika. wazazi wenyewe kwa wenyewe kulaumiana mwishowe tunaona wazazi wanaanza kupeana talaka.

Wazazi kuachana imekua ni jambo la kawaida katika karne hii ya utandawazi ambako kumepelekea athari mbalimbali katika familia kama vile.

i) Watoto kukosa malezi ya wazazi sahihi

ii) Ongezeko la familia za mzazi mmoja

iii) Ndoa za mikataba

iv) Kuongezeka kwa Umasikini katika ngazi ya kaya na Taifa kwa ujumla.

Kutokana na huu utandawazi tumeona wazazi hawawanyonyeshi watoto wao kwa wakati muafaka unaoshauriwa na wataalamu wa afya ili aweze kuendelea na majukumu yake ya kazini alipoajiriwa au kujiajiri. Hii inapelekea watoto na vijana kupoteza uwezo wao wa kufikiri na kushuka kwa kinga na hivyo kupelekea kupatwa na maradhi ya mara kwa mara na kushindwa kuwa wabunifu wanapokua wakubwa.

Na pia kutokana na huu utandawazi wazazi wanaona kua suala la kulea ni sawa na kupoteza muda wao kwani wana majukumu bora na mazuri kwao wao wenyewe na wala sio kwa watoto wao na kuona kwamba kulea ni kupoteza. bora wawe bize makazini. Hii .inachangia watoto kukosa mwongozo wa maisha yao na kushindwa kutatua matatizo yanayowakabili mbele yao na kushindwa kuendeleza vipaji vyao vya asili kwa ajili ya ;.

i) Kutokujua lugha zao za asili

ii) Kushindwa kumiliki miili yao

iii) Kutokufahamu taratibu na sheria za kijamii

iv) Kutojua mila na tamaduni zao

v) Kutokua na huruma kwa ndugu zao

vi) Uvunjifu wa maadili na kupoteza kabisa malengo ya kimaisha.

Utandawazi huu umeweza kusambaratisha familia zetu moja kwa moja ambapo hapo awali mtoto alikua ni mali ya jamiinzima, anaongozwa na kujirekebisha. Huu utandawazi umesababisha watoto kujitegemea na kujilea wenyewe pasipo kujua mwenendo mzima wa maadili ya jamii zao na matokeo yake ni kama vile.

i) Vijana kutosaidiana na kuthaminiana wao wenyewe.

ii) Kukosa umoja na mshikamano kama ndugu wa moja.

iii) Vita vya wenyewe kwa wenyewe ndani ya jamii moja.

vi) Umimi, Udini, Ukabila na Ukanda vimeyatawala maisha yetu

1:4 MAKUNDI RIKA

Rika ni watu ambao wana umri unaokaribiana na kulingana. Kundi rika anaweza kuwa rafiki ,yako jirani yako au hata mwanafunzi mwenzako. Watu wa kundirika wana uwanda mpana wa mazungumzo tofauti na mazungumzo katika familia au jamii kwa ujumla. Makundi rika ya zamani yaliongozwa na mafunzo ya jamii ya jando na unyago. Walifundishwa namna ya kuishi katika hali ya usawa, upendo, uvumilivu na maarifa mbalimbali ili waweze kukabiliana na changamoto za kimaisha pindi watakapokua na familia zao wenyewe ili nao waweze kuwalea watoto wao katika misingi hiyo hiyo yenye tija kubwa katika maisha yao. Kulingana na mabadiliko ya kimaisha yaliyoletwa na utandawazi yameharibu maana halisi ya mafunzo ya jando na unyago kwa vijana katika jamii nyingi za kiafrika ikiwemo Tanzania.

Makundi rika ya sasa hayana mafunzo yoyote ya kimaadili kwa wakubwa na wadogo zao, yametawaliwa na jaziba, hasira, chuki majivuno na dharau kutunushiana misuli mizozo isiyokua na tija kwao, fujo subira imepotea kabisa. Umaarufu ndio ngao ya maisha yao, kudai haki bila kufanya kazi, hawajui wajibu wao sio kwa wao wenyewe kwa familia zao wala kwa jamii zao. Mwelekeo potevu kwa makundi rika haya ni kutokana na utandawazi ambao umepelekea kulega na kupotea kwa mafunzo yetu ya asili ya jando na unyago na kutekwa kwa kiasi kikubwa na tamaduni za kimagharibi hivyo kujishughulisha zaidi na mambo ya kuiga na kushindwa kufanya mambo yao ya ubunifu na kusahau kabisa tamaduni zao katika suala zima la malezi na kujishughulisha na mambo ambayo hayana tija katika maisha yao.

1:5 TAASISI ZA ELIMU

Taasisi za elimu zinajishughulisha na malezi na mafunzo kwa niaba ya jamii husika. Husaidia vijana na watoto kupata mafunzo na stadi mbalimbali za maisha, taaluma na ujuzi ili waweze kukabiliana na changamoto mbalimbali za kimaisha pindi wanapohitimu mafunzo yao.

Taasisi hizi huongozwa na sera na mafunzo mbalimbali ambapo wakati mwingine hubadilika kutokana na huu utandawazi tulionao hivi sasa. Utandawazi huu kwa kiasi kikubwa umechangia kuwa na mabadiliko katika sekta ya elimu kama vile mabadiliko ya mara kwa mara katika mitaala yetu ya masomo na kusababisha kubadilika kwa mwenendo mzima wa utoaji elimu katika jamii husika. Kwa mfano hapa kwetu Tanzania kuongezeka kwa mtaala na teknolojia ya habari na mawasiliano (Teknohama) ambapo imepelekea watoto na vijana kuweza kutumia tovuti mbalimbali ambapo zingine hazina maadili kwa umri wao na hivyo kuwapelekea kuiga na kufanya vitendo ambavyo havina maadili katika jamii yetu.

Kwa upande mwingine vijana hawa ndiyo wanakua waalimu wa shule hapo baadae ambapo inapeleka ukosefu wa maadili shuleni kwani tayari wameshajifunza mambo tofauti ambayo yameathiri saikolojia zao na hivyo kuwafanya wanafunzi ambao ni watoto kuiga mienendo mibaya ya walimu wao na kupelekea utovu wa nidhamu kwa wanafunzi dhidi ya waalimu wao na kusababisha wanafunzi kutowasikiliza waalimu wao na hivyo kupelekea kuwa na matokeo mabaya katika masomo yao, kupata mimba wakiwa bado shuleni, matumizi ya simu darasani huku mwalimu akiwa anafundisha na kufuta ile dhana ya hapo awali kwamba mwanafunzi ni sawa na mtoto wa mwalimu lakini kutokana na utandawazi mwanafunzi anamwona mwalimu kama rafiki yake wa mtaani tu.

1:6 DINI

Dini ni mojawapo ya wakala wa malezi katika jamii toka jadi mpaka sasa. Dini zinatoa mafundisho mbalimbali ya kimwili na kiroho kwa watu wote hasa hasa watoto na vijana ili waweze kuwa na tabia na mienendo mema katika jamii kama vile namna kuabudu, kuheshimu wakubwa, nidhamu katika kazi na huduma nyingine za kimalezi katika jamii.

Utandawazi umeibua taasisi mbalimbali za kidini ambazo zimekua na mitazamo tofauti tofauti kuhusiana na suala zima la Kimungu na kimalezi katika jamii kama vile kuamini kuwa maombi yanaweza kumsaidia mtu awe na hali nzuri na ustawi wa kijamii katika maisha yake bila kufanya kazi. Hali hii imewafanya watu wengi kuacha kufanyakazi za kijamaa za uzalishajimali na malezi kwenye familia zao na kwenda kwenye vituo mbalimbali vya mahubiri na kukaa huko kwa muda mrefu huku wakiwa na imani kwamba watafanikiwa kimaisha kwa njia ya mahubiri na kumkemea shetani kama ndiye adui mkubwa wa hali ngumu ya maisha yao. Viongozi wa madhebu haya wameshindwa kuwafunza watu mbinu mbalimbali za kupambana na hali ngumu ya maisha kama vile kujituma bila kukata tama na kua waadilifu na waaminifu katikakazi mbalimbali za maendeleo katika jamii zao. Kwa mfano kwa sasa kuna vipindi vingi sana vya maombi na mahubiri kwa njia ya runinga kama vile Saa ya Maajabu.Tutashinda, Joshua Tv, Emanuel Tv ,ukiangalia vile vipindi kuna watu wengi wamehudhuria na sisi wengine huku nje tumekuwa watazamaji hivyo wote kwa pamoja tunaibiwa muda wetu badala ya kwenda kujishughulisha na shughuli zingine za uzalishajimali. Pia kuna baadhi makanisa yanaidhinisha kufunga ndoa za jinsia moja. Huu ni upotoshaji wa maadili kwa viongozi wa dini dhidi ya wafuasi wao wanaowaamini kama sehemu ya malezi kwao na jamii kwa ujumla.

1:7 VYOMBO VYA HABARI

Vyombo vya habari ni pamoja na runinga, tovuti ,magazeti , simu za mkononi na majarida mbalimbali. Vyombo hivyo ni sehemu mojawapo ya malezi na mafundisho kwa watu wa jamii mbalimbali, huelimisha, huburudisha na vilevile huonya kwa kupitia vipindi mbalimbali vinavyooneshwa kwenye runinga kama vile taarifa za habari vipindi vya uzalishaji mali, miradi mbalimbali vipindi vizuri vya watoto na elimu,.kwenye magazeti huandikwa habari na makala mbalimbali. Husaidia kuibua matatizo mbalimbali yanayoikabili jamii yetu kuonya na kukosoa viongozi wetu kuanzia ngazi ya kaya. hadi Taifa kwa ujumla.

Kwa upande mwingine vyombo hivi vimeweza kupotosha watoto na vijana ambao hawana muongozo mzuri katika matumizi ya vyombo hivi. Kuna mambo mengine yanaoneshwa na kuandikwa katika vyombo vya habari ambavyo havina maadili mazuri katika jamii yetu. Watoto na vijana wasiokua na muongozo ndio waathirika wakubwa kwani hutumia muda wao mwingi kuangalia na kusoma mambo haya kama vile picha za ngono kwenye filamu na tovuti, kusoma majarida ya udaku na kimapenzi, kuangalia tamthilia na vichekesho mbalimbali kama vile Vichekesho vya Hinye Gwedegwede ambvyao kwa sasa imepigwa marufuku. Hali hii imechangia uvunjifu wa maadili kwa kiasi kikubwa sana kwa watoto na vijana wa Taifa letu.

Utandawazi umepelekea vijana kuiga tabia na mienendo mibaya kama vile hisia za kimapenzi na utumiaji wa madawa ya kulevya na kujiingiza katika vitendo vya uhalifu. Hii ni kutokana na kuoneshwa kwa filamu za kiuhalifu na ngumi katika runinga zetu ambayo inapunguza ubunifu na kuendeleza vitendo vya uigaji na vijana kushindwa kujiingiza kwenye shughuli za uzalishaji mali na hatimaye kuwa wahalifu na kushindwa kufanya mambo yenye manufaa katika jamii.

NINI KIFANYIKE ILI KUKABILIANA NA CHANGAMOTO HIZI

• Wazazi watambue umuhimu na wajibu wao katika suala zima la malezi kwa watoto wao kwani wao ndio walezi wa kwanza katika jamii yoyote ile.Kwani wazazi ndio muhimili mkuu katika familia na taifa kwa ujumla,hivyo waoombwa wayajue na kuyatafakari upya majukumu yao kama wazazi ili waende sambamba na mabadiliko ya kisayansi na kiteknolojia pamoja na changamoto zake katika malezi ya familia na taifa kwa ujumla.

• Walimu inawapasa kutambua kwamba wanafunzi wa sasa ni mayatima,wengine hulelewa na baba au mama tu pia wengine wanatoka katika familia zenye migogoro,hivo wanahitaji msaada wao si wa kielimu tu bali hata wa kimalezi ili nao waelewe misingi ya maisha ya jamii zao pindi wanapohitimu masomo yao.Nahii itawasaidi kupambana na hali mbaya za maisha yao ya huko majumbani mwao na kuweza kuishi kwa kufuata mila na tamaduni za jamii zao.

• Viongozi wa dini waache tabia ya kumkemea shetani kana kwamba yeye ndiye chanzo cha matatizo na migogoro katika jamii zetu bali watumie nafasi zao kuwakeme wale ambao ni wafuasi wao katika kuwafunza zaidi masuala yanayotukabili kwa sasa na mienendo mema katika jamii ili nao weweze kuwaunza wanaowategemea na kumuomba mungu awape wepesi katika katika shunguli zao za kila siku na si kumkemea tu shetani.

• Serikali itilie mkazo na isimamie uuzaji wa filamu za ngono na urushaji wa vipindi ambavyo haviendani na maadili ya jamii yetu.isiangalie tu maslahi na haki za watunzi wa tunzi wa mambo haya bali wapige vita mambo ambayo yanaipotosha jamii.Wazazi nao wawaongoze watoto wao katika vipindi vyenye manufaa kwao na kwa jamii kwa ujumla.

• Wazazi na walezi wanatakiwa kuwafahamu kwa undani marafiki wa watoto wao.,na pia wajue walipo watoto wao na wanafanya nini.vilevile watumie muda wao mwingi wa kukaa na watoto waokuliko kuwaacha watumie muda wao mwingi kucheza na marafiki.Hii itawaepushi watoto kujiingiza katika mienendo mibaya.

HITIMISHO

Wakala hawa wa malezi huweza kujenga na pia kubomoa misingi ya jamii.hivyo vinahitaji ushirikiano wangu na wako katika malezi ya jamii ili kuleta maendeleo ya familia zetu na taifa kwa ujumla.

ASANTENI KWA USIKIVU WENU

.

Tuesday, June 7, 2011

Tasnia Ya Muziki Mkombozi wa Vijana

    Tasnia ya Muziki
Mkombozi wa Vijana

Hiki ni kitabu ambacho kinatokana na utafiti uliofanywa kitaalam. Kitabu hiki kinaelezea tatizo la ajira nchini Tanzania. Ukosefu wa ajira ndo hasa tatizo linalowakabili vijana wa Tanzania.

Vijana wengi huko Tanzania wanajituma ili kuepukana na tatizo hili la ukosefu wa ajira. Vijana wa mijini huko Tanzania, wameingia katika tasnia ya Muziki, hususani katika muziki wa vijana al maarufu Bongo flava. Muziki huu unachukuliwa na vijana hao kama aina ya ajira na kwa hiyo basi ilitarajiwa kuwa kazi hii ingekuwa ni mkombozi kwao. Taarifa ambapo hazikuwa zimefanyiwa utafiti zilionyesha kuwa vijana hao hawakunufaika kama ambavyo ilifaa wanufaike. Hali hii kwa hakika ilionyesha ombwe la maelezo; ni kwa sababu ya kutaka kutoa maelezo ndo hasa utafiti ulifanyika ili kuelezea kilichojiri.

Katika ukurasa huu tutakuwa na mfululizo kukielezea kitabu ambazo kinatoa mchango wa namna ya kukabiliana na tatizo hili la ukosefu wa ajira kwa vijana wetu hapa Tanzania.

Sunday, April 24, 2011

Ufufuko

Ufufuko unamaanisha matumaini!

Kutokana na ufufuko kifo kilipoteza nguvu zake zote; hivyo basi kifo hakina tena nguvu mbele ya maisha!

Monday, August 23, 2010

Mtwara

Mtwara Mikindani: Hapa ni Mikindani katika jengo lililojengwa mwaka 1895.

Hapa ni juu kabisa ya mnara wa ulinzi. Ukiwa hapo unapata kuona eneo karibu la mji mdogo wote wa Mikindani.

Posted by Picasa

Friday, July 16, 2010

Some Useful Proverbs


The image by Google
1. Happiness is like perfume – You can not spray it on yourself without affecting the     one next to you

2. A man who has never submitted to anything will soon submit to a burial mat.

3. Judge not your beauty by the number of people who look at you but rather the number of people who smile at you

4. True happiness does not come from having everything I want but from wanting      everything I have.

5. A wound given by words is many times harder to cure than that given by the sword.

6. A fly that had nobody to advise it followed a corpse into a tomb.

7. On the day of the monkey’s death all the trees become slippery.

8. We do not only offend others by doing what is bad to them but also by our failure to      do what is good to them.

9. He who provides you with seeds is better than he who provides you with food.

10. It is those who visit the orchards who eat good fruits

11. A lost opportunity never returns

12. A short man is not a boy

13. When a stick bites your eye, it wants you to see

14. A tongue cannot pretend to be ignorant of what the teeth are chewing.

15. No matter how short you may be, you can see the sky.

Originally written by Muchunguzi Theobald in the PCJ VOICES, Volume 11, 2002
tmuchunguzi@yahoo.com

ARE HUMAN BEINGS REALLY BETTER THAN OTHER ANIMALS?

One day when I was in Tororo for my annual retreat, in one of the moments when I was meditating, I saw a cock chasing a hen for mating. It happened that one of my friends had seen the cock too. He said to me, “this cock is hopeless, it cannot even feel shy to chase the hen in front of us, it should have waited for us to go away at least” This is not only for birds (hens) but it is a habit of most animals. At Lavigerie house, I take care of animals; we have two pigs and a cat; when a she pig is in heat the male knows and they mate. When it is their proper time they do so regardless of my presence. This I guess is not an uncommon experience to many of us.

The experience that I get from birds and most irrational animals makes me, most of the time, say that we human beings are more advanced, intellectual wise, than other animals. In fact this is what even biology tells us, that man is superior to all other animals. I think this is very true and for so long this has been my conviction. But recently my conviction has been challenged so much by what I call inhuman deeds.

In our “modern world” it is an order of the day to hear about the issue of rape. I hear a lot about it and somehow many of us get used to hearing about it without doing anything to help the victims. Some may go to the extent of saying “it is normal” or “that is how life is.” And you know some even dare say that most women who are raped are responsible for that, for they “provoke” men. They provoke men? I have heard of old ladies some even of 80 being raped, and worse still , I have heard of babies of some few months being raped and yet some say that the victims provoke the “predators”?

Are we really better than the Tororo cock? September the eleventh is the day which will have a long life span in the memory of many people, not only Americans but almost everybody who came to know about it, not only people of good will but by people of “evil intentions” as well. One would have expected such an event, which has captured permanence in many peoples’ memory, to be of great benefit to many people. Instead, it is just the opposite. Even though the act is terribly evil according to moral standards, it is “good” to some people. It is good, of course, to the authors. I guess they look at the act as their masterpiece. “Some gentlemen” pretending to be passengers hijack the planes having many passengers, they take control of the planes and deliberately hit the planes against the twin towers; they know that the planes have many people on board and they know that the twin towers are buildings which have the capacity of having an enormous number of people at a time. They know beyond doubt that what they are doing will cause a big loss of human life and that they too will not escape death. But still they go on and do it…

In our modern “developed” world it is strange not to hear of a considerable loss of human life almost every day, and the agent in most cases is man himself. The events of September 11th, the suicidal attacks and many other causes of deaths of the same nature were and are being planned and carried out by an animal with the most developed brain – a rational animal. I wonder if by doing all such inhuman acts, even though they are rational, for they are “well” planned and “well” carried out, we still remain better than other animals!

Originally written by Martin Mandalu in the PCJ VOICES, Volume 11, April, 2002

SO BITTER ARE SEPARATIONS!

The Photo From a Missionary site
“...but Mandalu, why shouldn’t we have known each other deeper than we have done?” That was a question from a friend of mine known by the name of Tausi.

Previous to her question I had told her; it would have been better if we had not met and known each other. But why say this to a friend? If I said so, then it is because it was motivated by something serious. Yes, indeed it was pushed by the pain of separation.

So bitter is separation, it can be witnessed through our everyday experiences. The baby experience is very typical: an “infant.” When it has to detach from its best friend and best home for the past nine months, it feels the pain so much, indeed so bitter it is. But it can’t do much to express itself instead it resolves to crying. Yes so bitter it is.

I had to leave my friends for the first time when I was about five or six. I was still young but all the same I felt the pain for leaving them behind. The separation was caused by the move that my family had to make from one region to another in Tanzania. The decision followed a piece of advice from our family doctor, for my mum’s health was so poor because of the cooler weather in that region.

My second separation, which I remember, was when I finished my primary level of education, ready to join the secondary school level. Here I had to separate with my friends and yes, it was indeed bitter, I think it was so because I knew I would never see again many of those friends, and yes, I have not met most of them again.
Kirinya prison is a place where I go for my apostolate; I work with the prisoners who have not attended their trials yet. Some stay there for two or even three years, they get so much used to the place and the other guys that they find in the prison. Somehow, that becomes their home for the period that they have to stay in the prison, they make friends. When their time to go home comes, they have to go, I suppose under normal circumstances none of them would want to stay back, and yet the pain of separation is still there. In one incident, a prisoner was telling me “Ssebo, I have been her for three years, these fellows have become my brothers, but back home I have a family, I feel like staying behind but I just can’t help”

This morning, when I was contemplating on the subject, I learned that the intensity of bitterness in my separations has been increasing in direct proportion to the increase of my age and the increase of commitments in life. In the same contemplation, there came the idea of the coming separation, separation from friends of the PCJ. At first I did not want it to come to my conscious and so I was suppressing it. But I realized that suppressing it won’t do me any good, instead I should better let it come out and learn how to deal with it.

When I think of the many friends that I have and that when I conceive the idea of separation, that is,when the time for me to leave comes I will have to separate from them, then I feel so sad. In the course of my stay at the PCJ and Uganda at large, for about three years now, I have been able to meet with many people and so make friends from both the PCJ and outside the institution. I have come across friends from Tanzania, Zambia, Uganda, Kenya, Malawi, South Africa, Cameroon, Burundi, Benin, DRC, Sudan, UK, Holland, Belgium, Ireland, USA, Italy, Spain, France, and many more. And yet I may never meet most of them again. Yes, this is what indeed makes me sense the coming pain so bitter…yes, so bitter it is. Separations are painful and yet inevitable. I know that relationships are very important for our proper growth and yet separations are so important for that proper growth as well.

When I was five, our family had to separate from many friends that we had in the first town. But it was because of “a higher good,” that is for the health of one of the family members we all had to leave behind our friends. Should we have clung to our friendship while one of the members in the family was suffering? No, we had to leave.

Should those guys in the prison remain with their friends and forget about their families back home? I do not think so. They must go and let life continue. Furthermore, separations have big benefits to us even though they are bitter. If a baby in the womb decided to remain in there (if that were possible), then it would not have developed, as it does when it comes out of the womb. The same applies to a pupil. If she or he decides to remain at the primary school level (for the sake of staying with the friends, whom I guess they too will have to move on) then the development of formal education and other disciplines would not be possible. Thanks to our faculty of memory that we can forget our past temporarily or even permanently, and so are able to live properly and make more friends again.

Indeed separations are so painful but so inevitable and important.

Originally written by Martin Mandalu in the PCJ VOICES, Volume 11, April, 2002

Tuesday, July 6, 2010

AND WHAT SHALL WE SAY?

The image is taken from the Loop of Life
Some old people die without seeing their grandchildren,
Some farmers die before harvesting the product of their hard labour,
Some students die before seating for their exams,
Others die without seeing their results.

When some mourn, others rejoice.
When some die, others are born.
When some pass their exams, others fail.
Some gain when others lose.

In fact that is how life should be…
Before having two, one should have one.
Those who have more should give those who have none.
Those who have none should look for one.

This is how life is…
If you choose celibacy then you forgo marriage,
If you opt for marriage then celibacy is left out.
If you choose to become a pilot then you might need to forget becoming a doctor.
If you choose to sleep, then you will have to forget running.

When you go for celibacy, then you automatically miss a wife or husband.
When you go for your best half, then you can be sure of having somebody at your side.
When you are married then, you are in most cases going to become daddy / mum.
When you go for celibacy, you will miss it so much but you will at least become uncle/aunt.

When a baby is born as a male, he is forced to become a man.
When a baby is born as a female, she is forced to become a woman.
Yes, you are either a woman or a man.
You are either married or unmarried.
Yes, nature has no mercy on us.


Martin Mandalu   Originally written in The PCJ VOICE, Volume 11, April, 2002

ON PAYING THE PRICE!!!

Photo taken from a mental strength website

We know that whoever is, exists and that if one is of sound mind and of good physical health then she/ he has to major a particular career in life so as to support his/ her life and even other’s lives.

Doing something is one thing and of course we know that almost everybody has to do something. But doing that thing the way it is supposed to be done correctly and with full conviction, is something else.
Many of us are good at observing things being done, and since we just observe, many of us still do not care whether they are done properly or not. All that we know is that something is being done, but how is it being done? Many of us would say it is none of my business.

Ladies and gentleman everybody who is has to live but we cannot live a “good life” without doing a substantial work in life. And we should bear in mind that we have to be responsible for the fruit that our work will produce. If we want to be happy in life and want to have a “good life” then we need to opt for an honest kind of job. Although such a type of (an endeavour ) work does not necessarily make us prosper, we can be sure of an inner peace. But we should not forget that such type of work will make us have many “enemies.”

I assume many of us want to live a happy and not necessarily a prosperous life; then if that is the case let us make sure that we are ready to pay the price for that or better we forget about it I don’t want to say that I myself know how to do or go about it. But we can learn from many of our elder brothers and sisters who knew both the importance of what they were doing and that they had to pay the price for their choice.

Socrates a Greek philosopher was teaching the youth the truth about life, he new that it was so important, for he was sent by the gods to do that work. He was free to do it or not to. He did it even though he knew it would bring him a lot of misunderstanding and confusion, but still he persevered. We know he was condemned to death for what was called impiety and misleading of the youth.

We know the story of the Archbishop Romero; he decided to speak for the poor and the voiceless; he did so even though he knew it was dangerous and of course as many people had expected he was murdered.

Nelson Mandela as a young man fought against the minority rule of the whites in South Africa, the apartheid regime. He fought for equal rights of all people in his country. He knew what it meant to take such a stand. We know what happened to him; he had to spend a good number of years in prison (paying the price for his choice of work)

There are many examples of such people who consciously decide to undertake such type of “dangerous” work. My aim is not simply to enumerate them for the sake of narrating stories but to let you know that there are many people who have been able to pay the price of their choice of work and that we are not alone or the first ones.

Martin Mandalu


Wednesday, June 30, 2010

Gazeti na uzalendo barani!!!

Gazeti hili la huko nchini Ghana hufanya uchambuzi wa mambo mengi kwa undani na hasa kwa mlengo wa kizalendo. hapa barani Afrika.

http://ghanaian-chronicle.com/

Saturday, June 12, 2010

Vijana na Ajira zenye Staha!

Katika kurasa zifuatazo tutajadili juu ya ajira zenye staha kwa vijana duniani kote. Tutaanza kufanya hivyo kuanzia na kazi za vijana wa Tanzania.