Tuesday, July 12, 2011

MITUME WA BWANA KATIKA MAZIWA MAKUU


Hiki ni kitabu kinachoelezea safari za mwanzo kabisa za wamisionari wa shirika la wamisionari wa Afrika. Shirika hilo la dini lilianzishwa na Kadinali wa Algiers Charles-Martial Allemand Lavigerie wa Ufaransa.

Kwa hivi wengi wa wamisionari hao walitoka Ufaransa na kuja kutangaza neno la Mungu. Hawa walifika eneo la maziwa makuu hasa Afrika ya Mashariki ya leo; hivyo kitabu hiki kinaelezea historia nzuri ya ndugu hao waliofika kwa mara ya kwanza mwaka 1878. Mbali na kutangaza neno la Mungu, kitabu kinatoa pia historia ya Tanzania toka Bagamoyo hadi Kagera.

Maelezo zaidi juu ya historia ya eneo na habari hizo inapatikana hapa:  http://www.africamission-mafr.org/bagamoyo.htm

No comments:

Post a Comment