Saturday, January 30, 2016

ORODHA YA VYUO VIKUU BORA TANZANIA 2015

STELLA MARIS MTWARA UNIVERSITY COLLEGE - IN THE CITY OF NATURAL GAS
This ranking is based on research publications and citations from the last five years (2010 to 2014) as well as visibility on the internet.
RankInstitutionTotal Influence Factor
1University of Dar Es Salaam28.10
2Sokoine University of Agriculture19.83
3Muhimbili University of Health and Allied Sciences15.22
4Open University of Tanzania10.72
5University of Dodoma9.02
6Tumaini University8.27
7Mzumbe University8.15
8Ardhi University7.50
9St Augustine University of Tanzania5.05
10Kilimanjaro Christian Medical College4.89
11Dar Es Salaam Institute of Technology4.43
12Nelson Mandela African Institute of Science and Technology4.18
13Catholic University of Health and Allied Sciences4.02
14Institute of Finance Management3.96
15Dar es Salaam University College of Education3.83
16Hubert Kairuki Memorial University3.49
17State University of Zanzibar3.24
18University College of Education2.94
19Kilimanjaro Christian Medical University College2.85
20Zanzibar Universitye2.67
21Mkwawa University College of Education2.44
22Weill Bugando University College of Health Sciences2.38
23University of Arusha2.34
24College of Business Education2.33
25Institute of Accountancy2.28
26Ruaha University College2.24
27Jordan University College2.14
28St John's University of Tanzania1.98
29Moshi University College of Cooperative and Business Studies1.85
30Mount Meru University1.79
31Mbeya University of Science and Technology1.77
32Arusha Technical College1.72
33Muslim University of Morogoro1.71
34Teofilo Kisanji University1.68
35St Joseph University in Tanzania1.66
36University of Iringa1.58
37Mwalimu Nyerere Memorial Academy1.53
38Makumira University College1.52
39International Medical and Technological University1.42
40University of Bagamoyo1.28
41Kampala International University Dar es Salaam College1.27
42Sebastian Kolowa Memorial University1.26
43Mwenge University College of Education1.18
44Stefano Moshi Memorial University College0.90
45Stella Maris Mtwara University College0.86
46Eckernforde Tanga University0.84
47Tanzanian Training Centre for International Health0.73
48Tanzania International University0.73
49Josiah Kibira University College0.67
50St Francis University College of Health and Allied Sciences0.63
51Archbishop Mihayo University College of Tabora0.62
52United African University of Tanzania0.56
53Katavi University of Agriculture0.12
54St Joseph's Theological Institute0.05
http://ranking.journalsconsortium.org/unirankings/country/Tanzania/2015

ORODHA YA VYUO BORA NIGERIA 2015


VYUO BORA NCHINI NIGERIA
1 University of Lagos Lagos
2 Obafemi Awolowo University Ile-Ife
3 University of Ibadan Ibadan
4 University of Ilorin Ilorin
5 Covenant University Ota
6 Federal University of Technology, Minna Minna
7 University of Nigeria Nsukka
8 University of Benin Ugbowo
9 University of Port Harcourt Port Harcourt
10 Ahmadu Bello University Zaria
11 University of Agriculture, Abeokuta
12 Landmark University Omu-Aran
13 Rivers State University of Science and Technology Port Harcourt
14 Federal University of Technology, Akur, Akure
15 University of Jos Jos
16 Nnamdi Azikiwe University Awka
17 Lagos State University Ojo
18 Redeemer’s University Mowe
19 Bayero University Kano Kano
20 University of Maiduguri Maiduguri
21 Ladoke Akintola University Of Technology Ogbomoso
22 Federal University, Dutsin-Ma Dutsin-Ma
23 Federal University of Technology, Owerri Owerri
24 Federal University, Oye-Ekiti Oye
25 Afe Babalola University Ado-Ekiti
26 Osun State University Oshogbo
27 Paul University Awka
28 Ekiti State University, Ado Ekiti Ado-Ekiti
29 Adekunle Ajasin University Akungba Akoko
30 Federal University, Dutse Dutse
31 University of Uyo Uyo
32 University of Agriculture, Makurdi, Makurdi
33 University of Abuja, Abuja
34 Ebonyi State University Abakaliki
35 Veritas University Abuja
36 Madonna University Okija
37 University of Calabar Calabar
38 Nasarawa State University Keffi
39 Pan African University Lagos
40 Ambrose Alli University Ekpoma
41 Lead City University Ibadan
42 Abubakar Tafawa Balewa University Bauchi
43 Kwara State University Ilorin
44 Delta State University, AbrakaAbraka
45 Baze University Abuja
46 Bingham University Auta Balifi
47 Bells University of Technology Ota
48 Umaru Musa Yar’Adua University Katsina
49 Babcock University Ilishan-Remo
50 Federal University of Petroleum Resources Effurun
51 Benue State University Makurdi
52 Enugu State University of Science and Technology Enugu
53 Joseph Ayo Babalola University Ikeji-Arakeji
54 Niger Delta University Wilberforce Island Yenagoa
55 African University of Science and Technology Abuja
56 Kaduna State University Kaduna
57 Federal University, Lokoja Lokoja
58 Igbinedion University Okada Okada
59 Ibrahim Badamasi Babangida University Lapai
60 Fountain University Oshogbo
61 American University of Nigeria Yola
62 Achievers University, Owo Owo
63 Ondo State University of Science & Technology Okitipupa
64 Obong University Obong Ntak
65 Crawford University Faith City
66 Federal University, Otuoke Otuoke
67 Anambra State University Uli
68 Olabisi Onabanjo University Ago Iwoye
69 Tai Solarin University Of Education Ijebu-Ode
70 Modibbo Adama University Of Technology Yola
71 Ajayi Crowther University Oyo Town
72 Imo State University Owerri
73 Caleb University Imota
74 Federal University, Ndufu-Alike Ndufu-Alike
75 University of Mkar Mkar
76 Nigerian Turkish Nile University Abuja
77 Novena University Ogume
78 Adeleke University Ede
79 Renaissance University Enugu
80 Al-Hikmah University Ilorin
81 Caritas University Enugu
82 Usmanu Danfodio University Sokoto
83 Kebbi State University Of Science and Technology Aliero
84 Benson Idahosa University Benin City
85 Oduduwa University Ile Ife
86 Michael Okpara University Of Agriculture Umuahia
87 Bowen University Iwo
88 Adamawa State University Mubi
89 Crescent University Abeokuta
90 Cross River University Of Science & Technology Calabar
91 Gombe State University Gombe
92 Elizade University Ilara-Mokin
93 Abia State University Uturu
94 Wellspring University Benin City
95 Yobe State University Damaturu
96 Western Delta University Oghara
97 Federal University, Lafia Lafia
98 Wesley University Of Science and Technology Ondo City
99 Bauchi State University Gadau
100 Federal University, Kashere Kashere
101 Federal University, Wukari Wukari
102 Samuel Adegboyega University Ogwa
103 Taraba State University Jalingo
104 Sokoto State University Sokoto
105 Kwararafa University Wukari Wukari
106 Tansian University Umunya
107 Akwa Ibom State University Uyo
108 Godfrey Okoye University Ugwuomu-Nike
109 Salem University Lokoja
110 Plateau State University Bokkos
111 Katsina University Katsina
112 Kogi State University Anyigba
113 Rhema University Aba

http://nigerianuniversityscholarships.com/list-best-universities-nigeria-2015-nuc-share/

Friday, January 29, 2016

JE AFRIKA TUNAWEZA KUMUDU ELIMU BORA NA BURE?


JE, AFRIKA INAWEZA KUMUDU ELIMU BURE?
imepakuliwa hapa: https://www.youtube.com/watch?v=D6zlTJ9xUp4

Mjadala umeendelea kote barani Afrika kupitia mtandao wa Bbc. Swali hili ni muhimu kwa Tanzania pia. Je, tunaweza kumudu elimu bure? Elimu hiyo ya bure inafaa iendane na ubora pia si tu elimu bure lakini yenye ubora bure pia.

Kwenye picha iliyochukuliwa mtandao wa bbc wanaonekana watoto wakiwa kwenye darasa la chini ya mti, wakiwa wamekalia mawe ili hali wapita njia wakiendelea na shughuli zao. Ama kwa hakika hapa ni ngumu mno kupata elimu bora hata kama itakuwa bure...
http://www.bbc.co.uk/programmes/p03g5pbx

Wednesday, January 20, 2016

SABABU ZA UGUMU WA MAISHA MTWARA ZATAJWA...


Mkoa wa Mtwara ni moja kati ya mikoa 26 ya Tanzania. Mkoa huu una sifa lukuki moja ya sifa hizo ni ugumu wa maisha; mkoa huu unasifika kwa bei kubwa za bidhaa ikilinganishwa na mikoa mingine ya nchi. Kwenye moja ya vipindi vyake maarufu vya jioni kituo cha redio PRIDE FM kilichopo mkoani humo siku ya Jumanne tarehe 19 Januari 2016 iliendesha kipindi ambacho pamoja na mambo mengine kilihoji kwanini maisha bidhaa mbalimbali katika mkoa huo ukilinganisha na mikoa mingine ni aghali zaidi?

Washiriki waliopiga simu walikuwa na majibu anuwai; mmoja kati ya wapiga simu hao alisema ni kweli kwamba maisha ni magumu Mtwara ikilinganishwa na mikoa mingine na sababu hasa ni uvivu wa wakazi wa mkoani humo. Wakazi wengi wanaojishughulisha na kilimo hulima eneo dogo tu la shamba na kutaka kuendesha maisha yao kupitia shamba hilo. Jambo hilo huwalazimu wakulima hao kupanga bei kubwa za mazao yao pindi wakati wa kupeleka bidhaa sokoni unapofika.

Mchangia mada mwingine alisema sababu hasa ni zile za kihistoria kwamba bidhaa zilizotoka mikoa ya jirani zilipangiwa bei kubwa kwa kuwa barabara kwenda mkoani humo zilikuwa mbovu mno na hivyo kufanya gharama za usafirishaji kuwa kubwa jambo liliongeza bei ya bidhaa.

Wito umetolewa kwa serikali kulitazama upya suala la bei za bidhaa mkoani humo kwa kuwa barabara imejengwa kwa kiwango cha lami na hivyo hakuna tena sababu ya gharama kubwa za usafirishaji.


Imepakuliwa hapa https://www.youtube.com/watch?v=-Wc0bwtAONY

Sunday, January 17, 2016

JIMBO KATOLIKI MTWARA LAPATA ASKOFU


Titus Joseph Mdoe, amesimikwa rasmi hivi leo kuwa askofu wa tano wa jimbo katoliki Mtwara. Askofu Mdoe aliteuliwa mwaka 2015 na Papa Fransisko kuliongoza jimbo hilo kufuatia kustaafu kwa aliyekuwa askofu wa jimbo hilo Gabriel Mmole. Askofu Mmole ambaye amelitumikia jimbo la Mtwara kwa miaka 31 anastaafu kisheria kwa mujibu wa kanuni za kanisa.

Askofu Mdoe amesimikwa rasmi mbele ya umati mkuu wa maaskofu toka pande zote za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, viongozi wa ngazi mbalimbali za serikali na halaiki kuu ya waumini na watu wenye mapenzi mema mkoani Mtwara.
imepakuliwa hapa...https://www.youtube.com/watch?v=PX8-nyXfnPg

Tuesday, January 12, 2016

MAPINDUZI DAIMA

Picha na mtandao
Imepakuliwa hapa: https://www.youtube.com/watch?v=-sMDkCSC_5g

Leo 12 Januari 2016 ni kumbukumbu ya 52 ya  siku ya mapinduzi yaliyofanyika visiwani Zanzibar mwaka 1964. Mapinduzi hayo yalifanyika ili kufanikisha utawala wa wengi dhidi ya utawala wa wachache. Mapinduzi hayo yalifanyika kuuong'oa utawala wa Sultan wa kiArabu aliyekuwa amepata uhuru toka mikononi mwa Waingereza. Waarabu walikuwa wachache lakini wakapewa mamlaka na Waingereza, Wazinzibar wenyeji na wenye asili ya Afrika wakafanya mapinduzi hayo kuchukua haki yao.

Mapinduzi Daima ndiyo hasa salaam rasmi kwa siku hii na hii inakubaliana na maneno ya Heraclitus mwanafalsafa wa kale wa Kigiriki aliyekuwa wa mwanzo kusema hakuna kinachodumu ila mabadiliko, ama mapinduzi hivyo ni hakika na sahihi kusema mapinduzi daima.

Tunawapongeza wananchi wote waZanzibar na Tanzania kwa ujumla wao. Aidha maadhimisho haya yawe ni chachu ya kutanzua mgogoro wa kisiasa unaoendelea visiwani humo ili nchi indelee kuwa ya amani na salama.
Mungu ibariki Tanzania na watu wake...

Thursday, January 7, 2016

DHANA YA KUTUMBUA MAJIPU IMETOKA WAPI?

Picha kwa hisani ya mtandao
imepakuliwa hapa:https://www.youtube.com/watch?v=xCjZLhxsOcA
Wakati wengi wetu tukiendelea kumpongeza Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania ndugu JPMagufuli kwa kushughulikia vilivyo matatizo yanayoisibu nchi, wachache tu kati yetu tumejiuliza kwanini kaamua kutumia dhana hiyo aliyoichagua kutatua matatizo yanayoikumba nchi Dr JPM ameamua kutumia dhana ya kutumbua majipu kama kiwakilishi cha utatuzi wa matatizo mazito, sugu na yaliyo kero kubwa kwa wananchi wa Tanzania. Wengi wetu tuliisikia kauli na dhana hiyo siku alipoongea na wabunge wa bunge wa la Jamhuri ya Muungano siku ya uzinduzi wa bunge.

Kupata jibu kwanini aliamua kutumia dhana hiyo, kuna njia kuu mbili; ya kwanza ni kumuuliza yeye mwenyewe ndugu JPM na ya pili ni kuutumikisha ubongo kufanya shughuli hiyo. Njia ya kwanza japokuwa ni fupi, nyepesi na inatoa jibu sahihi, si njia tunayoitamani. Hatuitaki njia hiyo kwakuwa haijengi uwezo wa kufikiria kwa namna sahihi. Ila hali njia ya pili ni ndefu, inashughulisha, inaimarisha uwezo wa ubongo, inakomaza uwezo wa ubunifu na kadhalika. Zaidi njia hii ya pili inachosha lakini hasa ndiyo tunapaswa kuifuata kwa kuwa inazalisha faida nyingi zaidi mbali ya jibu ambalo huenda lisiwe sahihi licha ya kutumia muda mrefu kulipata. Hiyo ndiyo hasa kazi ya falsafa; kujenga uwezo kuuliza maswali sahihi na kupitia njia sahihi za tafakari kujenga fikra sahihi ili hali ikiwa ni kutafuta UKWELI.

Tukirejea kwenye swali letu la msingi je kwanini JPM ametumia dhana ya kutumbua majipu? Ama ametoa wapi dhana hii? Katika falsafa na jinsi ninavyoamini pia kila kitu tumekipata maishani, ama tumekiishi sisi wenyewe, ama tumeona kwa wengine, ama tumesikia, ama kuhisi toka kwa wengine, ama kwa ufupisho huyapata mambo haya kupitia milango yetu ya fahamu za hisia (kuona, kusikia, kunusa, kuhisi na kuonja) haya ndiyo mafundisho ya wanafalsafa kadhaa wakiongozwa na Aristotle. Kwa upande wa wale wanaoongozwa na Plato; mwalimu wa Aristotle na mwanafunzi wa Socrates, wao wanaamini kuwa tuliishi sehemu nyingine kabla ya kuja hapa duniani na hivyo tulifahamu mambo yote huko tulikoishi. Hivyo mambo yote tunayofanya hivi sasa ikiwa ni pamoja na elimu ni juhudi tu za kujikumbusha tuliyoyaishi hapo kabla katika ukamilifu wa maisha. Unaweza kutumia mtazamo wowote kati ya hii miwili kupata jibu. Kwa Makala hii/haya twatumia mtazamo wa kiAristotle kupata jibu na hivyo ndugu JPM katumia dhana ya kutumbua majipu toka kwenye Hasina ya kumbukumbuu zake.
google image

Kwahiyo basi dhana ya kutumbua majipu ndugu JPM ama ameiishi yeye mwenyewe, ama kaishuhudia kwa mtu mwingine, ama alipata kusimuliwa juu ya dhana hiyo na mtu mwingine. Pengine kabla ya kuendelea tujiulize kwanza jipu ni nini? Kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili Sanifu ya Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili Dar es Salaam (TUKI), jipu ni uvimbe mkubwa unaotunga usaha. Na usaha ni ute wa rangi y manjano iliyopauka unaotunga aghalbu katika vidonda na majipu. Kamusi hii inaeleza tu maana ya jjipu na usaha. Lakini katika uhalisia wa maisha jipu ni adha inayousumbua mwili na kuufanya ufanye kazi zake kwa taabu. Zaidi uvimbe huu mara nyingi, bila shaka kuna sababu za kitabibu, huvimba maeneo yenye kumkosesha Amani na kumpatia binadamu usumbufu uliokithiri. Unaweza kukuta jipu limempata mtu kwenye makalio, mgongoni, sehemu zake za siri na kadhalika. Fikiria mtu mwenye kazi ya inayomlazimu kuketi muda mwingi, apatwe na jipu kwenye makalio…bila shaka unapata picha ya adha kubwa ndugu huyo atakayoipata.

google
Mtu huyo anahitaji matibabu ya haraka ili aendelee na kazi zake ili kutumia vipawa vyake,  kuitegemeza familia, jamaa zake, na taifa lake, kinyume na hapo familia jipu litamhangaisha na familia yake itaathirika, nchi itakosa mchango wake wa kimaendeleo. Kuepuka yote hayo mgonjwa anakwena hospitali kutumbuliwa jipu hilo. Kutumbua jipu hilo ni moja ya njia za kutibu uvimbe huo, nyingine inaweza kuwa vidonge vya kupunguza uvimbe na hatimaye kuisha. Kati ya njia hizi mbili, madaktari wanaweza kutujuza kama zipo njia nyinge murua zaidi yaa hizi mbili, ile ya kutumbua jipu ni bora zaidi kwa kuwa njia hii huasaidia kuondoa pia kiini cha jipu na hivyo kuzuia jipu hilo kuhamia sehemu nyingine ya mwili.

Hivyo basi utaona kuwa dhana ya Rais Magufuli ya kutumbua majipu imejengwa toka katika uhalisisa wa maisha yanayofahamika kwa watu wengi. Hivyo umithirishaji wa matatizo yanayoikumba jamii ya watanzania na tatizo la majipu mwilini ni dhana inayoeleweka kwa urahishi na hivyo inaweza kuimarisha na kuhamasisha uungwaji mkono na ushiriki wa watanzania wengi zaidi katika jitihada za kutumbua majipu (juhudi za kutatua matatizo yanayowaumiza wananchi na kubana fursa zao za kujiletea maendeleo). Kwa hiyo basi ndugu JPMagufuli huenda akawa anatumia dhana hiyo kwa kuwa anafahamu kero za majipu mwilini na jinsi ambavyo huwa kero kubwa na kubana fursa za mhanga kufanya shughuli zake za kila siku. 


Mandalu