Sunday, January 17, 2016

JIMBO KATOLIKI MTWARA LAPATA ASKOFU


Titus Joseph Mdoe, amesimikwa rasmi hivi leo kuwa askofu wa tano wa jimbo katoliki Mtwara. Askofu Mdoe aliteuliwa mwaka 2015 na Papa Fransisko kuliongoza jimbo hilo kufuatia kustaafu kwa aliyekuwa askofu wa jimbo hilo Gabriel Mmole. Askofu Mmole ambaye amelitumikia jimbo la Mtwara kwa miaka 31 anastaafu kisheria kwa mujibu wa kanuni za kanisa.

Askofu Mdoe amesimikwa rasmi mbele ya umati mkuu wa maaskofu toka pande zote za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, viongozi wa ngazi mbalimbali za serikali na halaiki kuu ya waumini na watu wenye mapenzi mema mkoani Mtwara.
imepakuliwa hapa...https://www.youtube.com/watch?v=PX8-nyXfnPg

No comments:

Post a Comment