Tuesday, January 12, 2016

MAPINDUZI DAIMA

Picha na mtandao
Imepakuliwa hapa: https://www.youtube.com/watch?v=-sMDkCSC_5g

Leo 12 Januari 2016 ni kumbukumbu ya 52 ya  siku ya mapinduzi yaliyofanyika visiwani Zanzibar mwaka 1964. Mapinduzi hayo yalifanyika ili kufanikisha utawala wa wengi dhidi ya utawala wa wachache. Mapinduzi hayo yalifanyika kuuong'oa utawala wa Sultan wa kiArabu aliyekuwa amepata uhuru toka mikononi mwa Waingereza. Waarabu walikuwa wachache lakini wakapewa mamlaka na Waingereza, Wazinzibar wenyeji na wenye asili ya Afrika wakafanya mapinduzi hayo kuchukua haki yao.

Mapinduzi Daima ndiyo hasa salaam rasmi kwa siku hii na hii inakubaliana na maneno ya Heraclitus mwanafalsafa wa kale wa Kigiriki aliyekuwa wa mwanzo kusema hakuna kinachodumu ila mabadiliko, ama mapinduzi hivyo ni hakika na sahihi kusema mapinduzi daima.

Tunawapongeza wananchi wote waZanzibar na Tanzania kwa ujumla wao. Aidha maadhimisho haya yawe ni chachu ya kutanzua mgogoro wa kisiasa unaoendelea visiwani humo ili nchi indelee kuwa ya amani na salama.
Mungu ibariki Tanzania na watu wake...

No comments:

Post a Comment