Saturday, January 30, 2016

ORODHA YA VYUO VIKUU BORA TANZANIA 2015

STELLA MARIS MTWARA UNIVERSITY COLLEGE - IN THE CITY OF NATURAL GAS
This ranking is based on research publications and citations from the last five years (2010 to 2014) as well as visibility on the internet.
RankInstitutionTotal Influence Factor
1University of Dar Es Salaam28.10
2Sokoine University of Agriculture19.83
3Muhimbili University of Health and Allied Sciences15.22
4Open University of Tanzania10.72
5University of Dodoma9.02
6Tumaini University8.27
7Mzumbe University8.15
8Ardhi University7.50
9St Augustine University of Tanzania5.05
10Kilimanjaro Christian Medical College4.89
11Dar Es Salaam Institute of Technology4.43
12Nelson Mandela African Institute of Science and Technology4.18
13Catholic University of Health and Allied Sciences4.02
14Institute of Finance Management3.96
15Dar es Salaam University College of Education3.83
16Hubert Kairuki Memorial University3.49
17State University of Zanzibar3.24
18University College of Education2.94
19Kilimanjaro Christian Medical University College2.85
20Zanzibar Universitye2.67
21Mkwawa University College of Education2.44
22Weill Bugando University College of Health Sciences2.38
23University of Arusha2.34
24College of Business Education2.33
25Institute of Accountancy2.28
26Ruaha University College2.24
27Jordan University College2.14
28St John's University of Tanzania1.98
29Moshi University College of Cooperative and Business Studies1.85
30Mount Meru University1.79
31Mbeya University of Science and Technology1.77
32Arusha Technical College1.72
33Muslim University of Morogoro1.71
34Teofilo Kisanji University1.68
35St Joseph University in Tanzania1.66
36University of Iringa1.58
37Mwalimu Nyerere Memorial Academy1.53
38Makumira University College1.52
39International Medical and Technological University1.42
40University of Bagamoyo1.28
41Kampala International University Dar es Salaam College1.27
42Sebastian Kolowa Memorial University1.26
43Mwenge University College of Education1.18
44Stefano Moshi Memorial University College0.90
45Stella Maris Mtwara University College0.86
46Eckernforde Tanga University0.84
47Tanzanian Training Centre for International Health0.73
48Tanzania International University0.73
49Josiah Kibira University College0.67
50St Francis University College of Health and Allied Sciences0.63
51Archbishop Mihayo University College of Tabora0.62
52United African University of Tanzania0.56
53Katavi University of Agriculture0.12
54St Joseph's Theological Institute0.05
http://ranking.journalsconsortium.org/unirankings/country/Tanzania/2015

ORODHA YA VYUO BORA NIGERIA 2015


VYUO BORA NCHINI NIGERIA
1 University of Lagos Lagos
2 Obafemi Awolowo University Ile-Ife
3 University of Ibadan Ibadan
4 University of Ilorin Ilorin
5 Covenant University Ota
6 Federal University of Technology, Minna Minna
7 University of Nigeria Nsukka
8 University of Benin Ugbowo
9 University of Port Harcourt Port Harcourt
10 Ahmadu Bello University Zaria
11 University of Agriculture, Abeokuta
12 Landmark University Omu-Aran
13 Rivers State University of Science and Technology Port Harcourt
14 Federal University of Technology, Akur, Akure
15 University of Jos Jos
16 Nnamdi Azikiwe University Awka
17 Lagos State University Ojo
18 Redeemer’s University Mowe
19 Bayero University Kano Kano
20 University of Maiduguri Maiduguri
21 Ladoke Akintola University Of Technology Ogbomoso
22 Federal University, Dutsin-Ma Dutsin-Ma
23 Federal University of Technology, Owerri Owerri
24 Federal University, Oye-Ekiti Oye
25 Afe Babalola University Ado-Ekiti
26 Osun State University Oshogbo
27 Paul University Awka
28 Ekiti State University, Ado Ekiti Ado-Ekiti
29 Adekunle Ajasin University Akungba Akoko
30 Federal University, Dutse Dutse
31 University of Uyo Uyo
32 University of Agriculture, Makurdi, Makurdi
33 University of Abuja, Abuja
34 Ebonyi State University Abakaliki
35 Veritas University Abuja
36 Madonna University Okija
37 University of Calabar Calabar
38 Nasarawa State University Keffi
39 Pan African University Lagos
40 Ambrose Alli University Ekpoma
41 Lead City University Ibadan
42 Abubakar Tafawa Balewa University Bauchi
43 Kwara State University Ilorin
44 Delta State University, AbrakaAbraka
45 Baze University Abuja
46 Bingham University Auta Balifi
47 Bells University of Technology Ota
48 Umaru Musa Yar’Adua University Katsina
49 Babcock University Ilishan-Remo
50 Federal University of Petroleum Resources Effurun
51 Benue State University Makurdi
52 Enugu State University of Science and Technology Enugu
53 Joseph Ayo Babalola University Ikeji-Arakeji
54 Niger Delta University Wilberforce Island Yenagoa
55 African University of Science and Technology Abuja
56 Kaduna State University Kaduna
57 Federal University, Lokoja Lokoja
58 Igbinedion University Okada Okada
59 Ibrahim Badamasi Babangida University Lapai
60 Fountain University Oshogbo
61 American University of Nigeria Yola
62 Achievers University, Owo Owo
63 Ondo State University of Science & Technology Okitipupa
64 Obong University Obong Ntak
65 Crawford University Faith City
66 Federal University, Otuoke Otuoke
67 Anambra State University Uli
68 Olabisi Onabanjo University Ago Iwoye
69 Tai Solarin University Of Education Ijebu-Ode
70 Modibbo Adama University Of Technology Yola
71 Ajayi Crowther University Oyo Town
72 Imo State University Owerri
73 Caleb University Imota
74 Federal University, Ndufu-Alike Ndufu-Alike
75 University of Mkar Mkar
76 Nigerian Turkish Nile University Abuja
77 Novena University Ogume
78 Adeleke University Ede
79 Renaissance University Enugu
80 Al-Hikmah University Ilorin
81 Caritas University Enugu
82 Usmanu Danfodio University Sokoto
83 Kebbi State University Of Science and Technology Aliero
84 Benson Idahosa University Benin City
85 Oduduwa University Ile Ife
86 Michael Okpara University Of Agriculture Umuahia
87 Bowen University Iwo
88 Adamawa State University Mubi
89 Crescent University Abeokuta
90 Cross River University Of Science & Technology Calabar
91 Gombe State University Gombe
92 Elizade University Ilara-Mokin
93 Abia State University Uturu
94 Wellspring University Benin City
95 Yobe State University Damaturu
96 Western Delta University Oghara
97 Federal University, Lafia Lafia
98 Wesley University Of Science and Technology Ondo City
99 Bauchi State University Gadau
100 Federal University, Kashere Kashere
101 Federal University, Wukari Wukari
102 Samuel Adegboyega University Ogwa
103 Taraba State University Jalingo
104 Sokoto State University Sokoto
105 Kwararafa University Wukari Wukari
106 Tansian University Umunya
107 Akwa Ibom State University Uyo
108 Godfrey Okoye University Ugwuomu-Nike
109 Salem University Lokoja
110 Plateau State University Bokkos
111 Katsina University Katsina
112 Kogi State University Anyigba
113 Rhema University Aba

http://nigerianuniversityscholarships.com/list-best-universities-nigeria-2015-nuc-share/

Friday, January 29, 2016

JE AFRIKA TUNAWEZA KUMUDU ELIMU BORA NA BURE?


JE, AFRIKA INAWEZA KUMUDU ELIMU BURE?
imepakuliwa hapa: https://www.youtube.com/watch?v=D6zlTJ9xUp4

Mjadala umeendelea kote barani Afrika kupitia mtandao wa Bbc. Swali hili ni muhimu kwa Tanzania pia. Je, tunaweza kumudu elimu bure? Elimu hiyo ya bure inafaa iendane na ubora pia si tu elimu bure lakini yenye ubora bure pia.

Kwenye picha iliyochukuliwa mtandao wa bbc wanaonekana watoto wakiwa kwenye darasa la chini ya mti, wakiwa wamekalia mawe ili hali wapita njia wakiendelea na shughuli zao. Ama kwa hakika hapa ni ngumu mno kupata elimu bora hata kama itakuwa bure...
http://www.bbc.co.uk/programmes/p03g5pbx

Wednesday, January 20, 2016

SABABU ZA UGUMU WA MAISHA MTWARA ZATAJWA...


Mkoa wa Mtwara ni moja kati ya mikoa 26 ya Tanzania. Mkoa huu una sifa lukuki moja ya sifa hizo ni ugumu wa maisha; mkoa huu unasifika kwa bei kubwa za bidhaa ikilinganishwa na mikoa mingine ya nchi. Kwenye moja ya vipindi vyake maarufu vya jioni kituo cha redio PRIDE FM kilichopo mkoani humo siku ya Jumanne tarehe 19 Januari 2016 iliendesha kipindi ambacho pamoja na mambo mengine kilihoji kwanini maisha bidhaa mbalimbali katika mkoa huo ukilinganisha na mikoa mingine ni aghali zaidi?

Washiriki waliopiga simu walikuwa na majibu anuwai; mmoja kati ya wapiga simu hao alisema ni kweli kwamba maisha ni magumu Mtwara ikilinganishwa na mikoa mingine na sababu hasa ni uvivu wa wakazi wa mkoani humo. Wakazi wengi wanaojishughulisha na kilimo hulima eneo dogo tu la shamba na kutaka kuendesha maisha yao kupitia shamba hilo. Jambo hilo huwalazimu wakulima hao kupanga bei kubwa za mazao yao pindi wakati wa kupeleka bidhaa sokoni unapofika.

Mchangia mada mwingine alisema sababu hasa ni zile za kihistoria kwamba bidhaa zilizotoka mikoa ya jirani zilipangiwa bei kubwa kwa kuwa barabara kwenda mkoani humo zilikuwa mbovu mno na hivyo kufanya gharama za usafirishaji kuwa kubwa jambo liliongeza bei ya bidhaa.

Wito umetolewa kwa serikali kulitazama upya suala la bei za bidhaa mkoani humo kwa kuwa barabara imejengwa kwa kiwango cha lami na hivyo hakuna tena sababu ya gharama kubwa za usafirishaji.


Imepakuliwa hapa https://www.youtube.com/watch?v=-Wc0bwtAONY

Sunday, January 17, 2016

JIMBO KATOLIKI MTWARA LAPATA ASKOFU


Titus Joseph Mdoe, amesimikwa rasmi hivi leo kuwa askofu wa tano wa jimbo katoliki Mtwara. Askofu Mdoe aliteuliwa mwaka 2015 na Papa Fransisko kuliongoza jimbo hilo kufuatia kustaafu kwa aliyekuwa askofu wa jimbo hilo Gabriel Mmole. Askofu Mmole ambaye amelitumikia jimbo la Mtwara kwa miaka 31 anastaafu kisheria kwa mujibu wa kanuni za kanisa.

Askofu Mdoe amesimikwa rasmi mbele ya umati mkuu wa maaskofu toka pande zote za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, viongozi wa ngazi mbalimbali za serikali na halaiki kuu ya waumini na watu wenye mapenzi mema mkoani Mtwara.
imepakuliwa hapa...https://www.youtube.com/watch?v=PX8-nyXfnPg

Tuesday, January 12, 2016

MAPINDUZI DAIMA

Picha na mtandao
Imepakuliwa hapa: https://www.youtube.com/watch?v=-sMDkCSC_5g

Leo 12 Januari 2016 ni kumbukumbu ya 52 ya  siku ya mapinduzi yaliyofanyika visiwani Zanzibar mwaka 1964. Mapinduzi hayo yalifanyika ili kufanikisha utawala wa wengi dhidi ya utawala wa wachache. Mapinduzi hayo yalifanyika kuuong'oa utawala wa Sultan wa kiArabu aliyekuwa amepata uhuru toka mikononi mwa Waingereza. Waarabu walikuwa wachache lakini wakapewa mamlaka na Waingereza, Wazinzibar wenyeji na wenye asili ya Afrika wakafanya mapinduzi hayo kuchukua haki yao.

Mapinduzi Daima ndiyo hasa salaam rasmi kwa siku hii na hii inakubaliana na maneno ya Heraclitus mwanafalsafa wa kale wa Kigiriki aliyekuwa wa mwanzo kusema hakuna kinachodumu ila mabadiliko, ama mapinduzi hivyo ni hakika na sahihi kusema mapinduzi daima.

Tunawapongeza wananchi wote waZanzibar na Tanzania kwa ujumla wao. Aidha maadhimisho haya yawe ni chachu ya kutanzua mgogoro wa kisiasa unaoendelea visiwani humo ili nchi indelee kuwa ya amani na salama.
Mungu ibariki Tanzania na watu wake...

Thursday, January 7, 2016

DHANA YA KUTUMBUA MAJIPU IMETOKA WAPI?

Picha kwa hisani ya mtandao
imepakuliwa hapa:https://www.youtube.com/watch?v=xCjZLhxsOcA
Wakati wengi wetu tukiendelea kumpongeza Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania ndugu JPMagufuli kwa kushughulikia vilivyo matatizo yanayoisibu nchi, wachache tu kati yetu tumejiuliza kwanini kaamua kutumia dhana hiyo aliyoichagua kutatua matatizo yanayoikumba nchi Dr JPM ameamua kutumia dhana ya kutumbua majipu kama kiwakilishi cha utatuzi wa matatizo mazito, sugu na yaliyo kero kubwa kwa wananchi wa Tanzania. Wengi wetu tuliisikia kauli na dhana hiyo siku alipoongea na wabunge wa bunge wa la Jamhuri ya Muungano siku ya uzinduzi wa bunge.

Kupata jibu kwanini aliamua kutumia dhana hiyo, kuna njia kuu mbili; ya kwanza ni kumuuliza yeye mwenyewe ndugu JPM na ya pili ni kuutumikisha ubongo kufanya shughuli hiyo. Njia ya kwanza japokuwa ni fupi, nyepesi na inatoa jibu sahihi, si njia tunayoitamani. Hatuitaki njia hiyo kwakuwa haijengi uwezo wa kufikiria kwa namna sahihi. Ila hali njia ya pili ni ndefu, inashughulisha, inaimarisha uwezo wa ubongo, inakomaza uwezo wa ubunifu na kadhalika. Zaidi njia hii ya pili inachosha lakini hasa ndiyo tunapaswa kuifuata kwa kuwa inazalisha faida nyingi zaidi mbali ya jibu ambalo huenda lisiwe sahihi licha ya kutumia muda mrefu kulipata. Hiyo ndiyo hasa kazi ya falsafa; kujenga uwezo kuuliza maswali sahihi na kupitia njia sahihi za tafakari kujenga fikra sahihi ili hali ikiwa ni kutafuta UKWELI.

Tukirejea kwenye swali letu la msingi je kwanini JPM ametumia dhana ya kutumbua majipu? Ama ametoa wapi dhana hii? Katika falsafa na jinsi ninavyoamini pia kila kitu tumekipata maishani, ama tumekiishi sisi wenyewe, ama tumeona kwa wengine, ama tumesikia, ama kuhisi toka kwa wengine, ama kwa ufupisho huyapata mambo haya kupitia milango yetu ya fahamu za hisia (kuona, kusikia, kunusa, kuhisi na kuonja) haya ndiyo mafundisho ya wanafalsafa kadhaa wakiongozwa na Aristotle. Kwa upande wa wale wanaoongozwa na Plato; mwalimu wa Aristotle na mwanafunzi wa Socrates, wao wanaamini kuwa tuliishi sehemu nyingine kabla ya kuja hapa duniani na hivyo tulifahamu mambo yote huko tulikoishi. Hivyo mambo yote tunayofanya hivi sasa ikiwa ni pamoja na elimu ni juhudi tu za kujikumbusha tuliyoyaishi hapo kabla katika ukamilifu wa maisha. Unaweza kutumia mtazamo wowote kati ya hii miwili kupata jibu. Kwa Makala hii/haya twatumia mtazamo wa kiAristotle kupata jibu na hivyo ndugu JPM katumia dhana ya kutumbua majipu toka kwenye Hasina ya kumbukumbuu zake.
google image

Kwahiyo basi dhana ya kutumbua majipu ndugu JPM ama ameiishi yeye mwenyewe, ama kaishuhudia kwa mtu mwingine, ama alipata kusimuliwa juu ya dhana hiyo na mtu mwingine. Pengine kabla ya kuendelea tujiulize kwanza jipu ni nini? Kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili Sanifu ya Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili Dar es Salaam (TUKI), jipu ni uvimbe mkubwa unaotunga usaha. Na usaha ni ute wa rangi y manjano iliyopauka unaotunga aghalbu katika vidonda na majipu. Kamusi hii inaeleza tu maana ya jjipu na usaha. Lakini katika uhalisia wa maisha jipu ni adha inayousumbua mwili na kuufanya ufanye kazi zake kwa taabu. Zaidi uvimbe huu mara nyingi, bila shaka kuna sababu za kitabibu, huvimba maeneo yenye kumkosesha Amani na kumpatia binadamu usumbufu uliokithiri. Unaweza kukuta jipu limempata mtu kwenye makalio, mgongoni, sehemu zake za siri na kadhalika. Fikiria mtu mwenye kazi ya inayomlazimu kuketi muda mwingi, apatwe na jipu kwenye makalio…bila shaka unapata picha ya adha kubwa ndugu huyo atakayoipata.

google
Mtu huyo anahitaji matibabu ya haraka ili aendelee na kazi zake ili kutumia vipawa vyake,  kuitegemeza familia, jamaa zake, na taifa lake, kinyume na hapo familia jipu litamhangaisha na familia yake itaathirika, nchi itakosa mchango wake wa kimaendeleo. Kuepuka yote hayo mgonjwa anakwena hospitali kutumbuliwa jipu hilo. Kutumbua jipu hilo ni moja ya njia za kutibu uvimbe huo, nyingine inaweza kuwa vidonge vya kupunguza uvimbe na hatimaye kuisha. Kati ya njia hizi mbili, madaktari wanaweza kutujuza kama zipo njia nyinge murua zaidi yaa hizi mbili, ile ya kutumbua jipu ni bora zaidi kwa kuwa njia hii huasaidia kuondoa pia kiini cha jipu na hivyo kuzuia jipu hilo kuhamia sehemu nyingine ya mwili.

Hivyo basi utaona kuwa dhana ya Rais Magufuli ya kutumbua majipu imejengwa toka katika uhalisisa wa maisha yanayofahamika kwa watu wengi. Hivyo umithirishaji wa matatizo yanayoikumba jamii ya watanzania na tatizo la majipu mwilini ni dhana inayoeleweka kwa urahishi na hivyo inaweza kuimarisha na kuhamasisha uungwaji mkono na ushiriki wa watanzania wengi zaidi katika jitihada za kutumbua majipu (juhudi za kutatua matatizo yanayowaumiza wananchi na kubana fursa zao za kujiletea maendeleo). Kwa hiyo basi ndugu JPMagufuli huenda akawa anatumia dhana hiyo kwa kuwa anafahamu kero za majipu mwilini na jinsi ambavyo huwa kero kubwa na kubana fursa za mhanga kufanya shughuli zake za kila siku. 


Mandalu

Monday, December 28, 2015

MAISHA NI MALENGO




                                              Imepakuliwa hapa:https://www.youtube.com/watch?v=G23nC6i5jl8
Leo ni mwanzo wa juma jipya, mwezi mpya, mwanzo wa miezi mipya kumi na mbili ama maarufu zaidi mwaka mpya.

Mwanzoni mwa mwaka ni kipindi kizuri kufanya tathmini ya kile tulichokuwa tukikifanya kama hatukufanya hivyo mwishoni mwa mwaka. Ama yaweza kuwa fursa ya kuweka malengo mapya ama kuyapitia yaliyotangulia kwaajili ya muda mpya unaoanza mbele yetu.

Kufanya tathmini ama kujiwekea malengo katika maisha ni suala la msingi mno kama tunataka kuishi katika namna inayoeleweka na yenye tija na mchango katika dunia yetu. Lengo la maisha kwa kila binadamu awe anafahamu ama la ni kuwa na furaha maishani. Aristotle, mwanafalsafa wa kale anasema hivyo pia; ili mtu awe na furaha basi hana budi kujiwekea malengo. Malengo huwekwa na watu wa kila kada.

Mwalimu shuleni hujiwekea malengo yake, mwanafunzi, mwanasiasa, mwanamichezo, mwanasanaa, mwanauchumi, msomi, mwanazuoni, mwanasheria, mkufunzi, mfanyabiashara, mkulima, mchungaji kanisani, shehe msikitini, imamu sinagogini, na kadhalika…watu wote makini wa kada zote hujiwekea malengo maishani. Kutokuwa na malengo maishani ni mithili ya muuza duka bila daftari, ambapo twajua mali bila daftari hupotea bila habari. Maisha bila malengo hupotea bila taarifa.

Kujiwekea malengo ni utamaduni ambao inafaa watu wote tuwe nao. Kwa kusema hivyo nafahamu fika kuwa kuna ndugu wasio na mazoea ya kufanya hivyo; watu hao mara nyingine hufananishwa na bendera fuata upepo hufuata chochote kitakachokuwa mbele yao. Bila ubishi si utaratibu mzuri wa maisha. Kwa wasio na utaratibu huo ni wakati sawia kuuanzisha.

Dini nyingi hutueleza kuwa hapa duniani ni sehemu tu ya mpito - twapita tu na kwamba makao yetu halisi yapo kwa muumba wetu. Hivyo wakati tukiandika malengo yetu ya maisha ni vyema tukamshirikisha huyo muumbaji kwa kuwa sisi hatujui siku wala saa ya kuyahama makazi ya hapa duniani, japokuwa hatutakiwi kuogopa kifo.

Unapoandaa malengo fanya hivi:

Kwa wanandoa, ama watarajiwa, wawashirikishe wenzi wao. Malengo haya si yako peke yako. Kwa hiyo nafsi ya kwanza ni Mwenyezi Mungu na pili ni mwenzi wako wa maisha; mkeo, mumeo ama mchumba wako. Muombe(ni) Mungu ili awaangazie kufanya malengo ya kweli.

Hatua ya pili ni kuwa mkweli na hali yako halisi; weka malengo ambayo yana uhalisia wa maisha yako. Mfano haina maana kwako mwanafunzi wa Tanzania kuwa na lengo la kuwa rais wa Pakstani miaka mitano ijayo. Weka malengo ambayo kwa kiasi fulani una nafasi ya kuyatekeleza. Mfano kusoma kozi ya Kifaransa kwa undani mara baada ya kumaliza masomo yako mwezi wa Juni.

Weka malengo yenye kukujenga na yatakayohitaji juhudi zako kuyatimiza.

Usiogope kuwa na malengo mengi bora tu ni muhimu katika makuzi na utu wako, mwisho wa muda wa kuyatimiza utakapowadia utakuwa na wasaa wa kujitathmini na kujua wapi ulihitaji ama utahitaji juhudi zaidi. Mara nyingine tukiwa na malengo mengi na yenye kudai juhudi zetu zaidi ndipo ambapo huwa na mafanikio zaidi maishani.

Usiwe mtu wa kujihurumia; kuona kuwa malengo haya ni mengi na magumu mno siwezi kuyatimiza. Usishindwe kujaribu, jaribu kutenda na ukishindwa wakati ukitenda ni tofauti kabisa na ukishindwa kujaribu kufanya chochote.

Jiamini na usijilaumu. Fanya utakachoweza kwa juhudi zako na mambo yakienda kombo, bila shaka utapata fursa nyingine ya kutenda tena!



Kila la heri na Mungu akubariki!

Mandalu
01/01/2012

Tuesday, December 15, 2015

MAGUFULI APASUA VICHWA WASOMI


WAKATI wananchi wengi wakipongeza hatua ya Rais Dk. John Magufuli kuelekeza pesa zilizochangwa kwa hafla ya kuzindua Bunge kununua vitanda katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, wapinzani wake wanaeleza huo ni mwanzo wa kushindwa katika vita dhidi ya ufisadi.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Profesa Mwesiga Baregu amesema hatua ya Rais Magufuli kupokea pesa hizo bila kuhoji malengo na msingi wa Mhimili huo wa kutunga sheria kuchangiwa fedha ni ishara ya wazi kuwa ameingia kwenye mtego wa ufisadi wa kimfumo.

“Bunge ni taasisi nyeti sana kuruhusu kuchagiwa pesa na watu ambao linapaswa kuwasimamia, hizi taasisi za fedha zilizochangia zinaweza kujikuta zinatakiwa kuchunguzwa na Bunge, credibility yake itakuwa wapi. Angeuliza kwanza kwanini wamechangisha pesa hizo, nani anawajibika nazo?

“Kama anasimamia uadilifu hakupaswa kuchukua tu hela ambazo zimechangwa bila kujua dhamira za wachangiaji, huko tunakokwenda tunahitaji miswada ya kusimamia sekta ya fedha, sheria za kodi wanapolipia dhifa ya kwanza ya kufungua Bunge, huu ni mtego, kwani Bunge haliwezi kupewa uwezo wa kuchukua hazina kiasi kidogo hata kama ni shilingi milioni tano kufanya mambo yake, dignity (heshima) yetu iko wapi kama tuna Bunge omba omba na hatujui dhamira za wachangiaji?” alihoji Profesa Baregu.
Aliongeza kwamba huo ndiyo ufisadi wa kimfumo unaoitesa Tanzania, huku akiweka wazi kuwa anazofanya sasa Rais ni mbio za sakafuni kwa kuwa hawezi akadumu na hali hiyo.
“Mkapa (Benjamin, Rais wa awamu ya tatu) alianza na kasi kuliko hata hii, pamoja na juhudi kubwa za Mwalimu Nyerere, kumtangaza kuwa Mr. Clean, kuunda Tume ya Warioba kuhusu rushwa na kuwa na baraza aliloiita la askari wa miavuli, ameishia wapi, katika kipindi chake ndiyo kashfa nyingi za ufisadi zimeibuka. Simuoni kama atakuwa tofauti na watangulizi wake,” alisema.
Ni kama Nyerere
Wakati Profesa Baregu anayatazama mambo kwa jicho hilo mchambuzi wa masuala ya siasa nchini Dk. Charles Kitima ameliambia Raia Mwema kuwa Rais Magufuli, amejipambanua kuwa ni aina ya kiongozi anayeweza kutekeleza anayoyasema kutokana na rekodi yake ya utendaji.
Amemweleza Rais Magufuli kuwa ni kiongozi wa kipekee ambaye hotuba yake ya kuzindua Bunge imeonyesha ni jinsi gani anaweza kuunganika na wananchi masikini wa ngazi ya chini.
“Hotuba yake imegusa watu wa kawaida kabisa, kama zilivyokuwa hotuba za Mwalimu Nyerere, anasema kwa lugha inayotoka moyoni, pengine ni kwa sababu ameishi maisha ya kawaida, ndiyo maana ameweza kuwavutia wengi,” alisema Dk. Kitima.
Aliongeza kwamba ingawa hotuba za mwanzo za viongozi ni kujaribu kuwaaminisha wananchi kwamba atatekeleza ahadi zake alizoahidi wakati wa kampeni, utekelezaji wa ahadi hizo hutegemea aina ya kiongozi husika.

Katika hotuba yake ya ufunguzi wa Bunge pamoja na mambo mengine aliwekea umuhimu suala la kubana matumizi ya serikali ili fedha zinazookolewa zielekezwe kwenye huduma za jamii.

Ili kuonyesha alivyodhamiria kulitekeleza hilo, juzi Jumatatu, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, alisema Rais Magufuli ameagiza kufutwa kwa sherehe za uhuru ili watu watumie siku hiyo kufanya kazi ya usafi.
“Hatuwezi kusherehekea miaka 54 ya Uhuru huku tukiendelea kusumbuliwa na ugonjwa wa kipindupindu unaoweza kuzuilika kwa kufanya usafi tu. Hii ni kejeli kwa taifa huru kwa zaidi ya miaka 50.

“Wakuu wa Mikoa, Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri wameagizwa kununua vifaa vya kufanyia usafi ili siku hiyo tuiadhimishe kwa utaratibu maalumu wa kupambana na kipindupindu,” alisema Balozi Sefue.
Akizunngumzia hotuba hiyo, aliyekuwa mtia nia ya kuwania urais kupitia CCM, Williamu Ngereja alisema hotuba hiyo ya Rais Magufuli ni mwanzo mpya kwa taifa.
“Hotuba ya Rais Magufuli ni mwongozo sahihi kwa taifa letu kufikia malengo ya kuwa na uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025. Kama wananchi wanataka mabadiliko ya kweli, kama walivyoonyesha kwenye kampeni, kila mtu anapaswa kumuunga mkono,” alisema Ngeleja. - 

CHANZO CHA HABARI HII :http://www.raiamwema.co.tz/magufuli-apasua-vichwa-wasomi

Thursday, December 10, 2015

10 things Zuma can learn from Tanzania’s new president

He’s been office for all of three weeks and already Magufuli has earned a reputation for rocking the boat, with his no-bullshit attitude and corruption-busting plan of action.
Sure he’s the son of a farmer, but this guy’s far from simple; his first real job was a school teacher, thereafter he educated himself as an industrial chemist and eventually became Tanzania’s minister of public works. The latter position saw Magufuli tackle some of the country’s largest construction projects without even a whisper of corruption or maladministration. In fact, he’s well-known for being a-corrupt, seriously.
So what is it that makes John Magufuli so great? Well, unlike so many of his counterparts, he’s relentless in his assault on corruption, laziness, and overspending; something that no doubt has already made him very unpopular among his own political comrades as well as leaders like Zuma and Mugabe. Let’s face it; the man makes almost every other leader look like a thief.
Three weeks in office and we’ve already got at least 10 major changes to report, imagine what the man can get done in five years.
Have a look at some of this legend’s highlights so far:
He cancelled Independence Day celebrations, saying that it’s “shameful” to celebrate while people are dying of cholera. Instead, the money that would have been used has now been set aside for street and public area cleaning.
After visiting the Muhimbili Hospital for the first time and seeing the dire state of affairs, the president ordered that more than 200 million Shillings earmarked for parliamentary parties be used to upgrade the hospital facilities. Less than a week later the hospital had 300 extra beds. He then fired the entire hospital board and had broken equipment repaired.
Magufuli cut his inauguration party budget from $100 000 to just $7 000 and gave the difference to the very same hospital mentioned above.
In his first week he ordered a ban on all international travel by government officials; adding that they need to focus on the rural areas of Tanzania and the poor, while commissioners and ambassadors who are already overseas can fulfil any foreign obligations.
All first and business class flights are off limits for government officials; except the president, vice president and prime minister.
Government workshops will no longer be held at hotels and function halls. Instead, they will be held at government-owned chambers so as to use what has already been paid for.
He fired Tanzania’s chief of revenue after 350 containers listed in his books disappeared from Dar es Salaam harbour. The prime minister is currently heading up that investigation.
He appointed the country’s very first female vice president.
When he had to travel 600km from Dar to Dodoma to open parliament; he chose to drive himself rather than have government organise a jet.
Magufuli went on record in the national assembly saying that, now that he’s president “it will not be business as usual.”
Pretty f*cking cool right? Well, here’s one more thing you might like to know about “The Bulldozer;” yeah, that’s what they’re calling him.
His tagline for his presidential campaign was “Work, nothing else.”
*Drops the mic

Wednesday, December 9, 2015

UHURU NA KAZI: KAZI YA TANU - KAZI YA MAGUFULI - KAZI YA WATANZANIA

Taken from Ndomi's Page
                                          Inapatikana hapa https://www.youtube.com/watch?v=b0Roj3MFrE4
Uhuru na kazi - Kazi ya Tanu. Maneno haya ama yanayofanana na haya yalikuwa ni moja ya salaam ambazo wananchi wa Tanganyika waliitumia kusabahiana mara baada ya uhuru. Bila shaka salaam hii ilitumika kutokana na umuhimu wa wananchi kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo ya haraka.

Ni utamaduni mzuri kukumbushana masuala ya msingi ili kuweza kufanikisha jambo ama mambo muhimu katika jamii. Kauli mbiu ya ndugu John Pombe Magufuli (JPM), Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati wa kampeni zake za uchaguzi mkuu  mwaka huu alitumia kauli mbiu ya HAPA KAZI TU! Kwa jinsi mambo yanavyoonekana kauli mbiu hiyo inaendelea kutumika wakati huu wa utendaji kazi zake za urais.

Kiongozi ni mtu ambaye huonyesha njia kwa kutenda. Na tena kiongozi mzuri huwa mbunifu na mweledi ili hali akitenda kwa mujibu wa sheria mama ya nchi yake. Hivi karibuni ndugu JPM alitoa agizo la maadhimisho ya siku ya uhuru wa Tanganyika kwa namna ya tofauti kabisa na miaka mingine iliyotangulia. Kwa kawaida nchini Tanzania maadhimisho haya hufanyika kwa gwaride la ukakamavu toka majeshi ya ulinzi na usalama, halaiki, ngoma mbalimbali na matumbuizo anuwai. Lakini agizo la JPM mwaka huu limekuwa kwamba maadhimisho ya sikukuu ya uhuru wa Tanganyika mwaka huu yafanyike kwa kufanya usafi maeneo mbalimbali zitolewapo huduma za kijamii.

Tumeshuhudia mwitikio mkubwa toka kwa wananchi waliojitokeza kufanya usafi katika maeneo mbalimbali. Ni jambo zuri wananchi kuitikia agizo hili ambalo pia limelenga kusaidia kupambana na ugonjwa wa kipindupindu. Moja ya sifa za kiogozi mzuri tuliona kwa ufupi ni kuonyesha njia kwa mfano; pichani hapo juu JPM anaonekana akishiriki kwa dhati kabisa katika kufanya usafi. Usafi huu ni muendelezo wa kauli mbiu ya HAPA KAZI TU!

HAPA KAZI TU! ni kauli mbiu nzuri inayofaa kutumika vyema na kwa undani zaidi kuliko ilivyo hivi sasa. Wakati kauli mbiu hii inahamasisha watu kutenda kazi, kuna watu wengine wengi hawana kazi na hivi kauli mbiu hii inakosa mantiki kwao. Hata hivyo kauli mbiu hii kama tulivyosema inatuhusu mno watanzania kwa kuwa nchi yetu bado ina uchumi duni. Hivi karibuni wadau wa HAKI ELIMU wametoa ripoti inayoelezea jinsi sekta ya elimu ilivyotenda ndani ya miaka kumi ya uongozi wa awamu ya nne.

Ripoti ya HakiElimu inasema awamu ya nne ilifanikiwa kwenye kuongeza idadi ya vitendea kazi katika sekta hiyo ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya shule za msingi na pia za sekondari, vyumba vya madarasa, mtundu ya vyoo, maabara na kadhalika. Hata hivyo ubora wa elimu katika miaka hiyo kumi imekuwa duni. Kuna wanafunzi wamemaliza masomo pasi ya kuwa na uwezo wa kusoma na kuandika. Hivyo ripoti hiyo inaisihi serikali ya awamu ya tano kuwekeza zaidi katika ubora wa elimu. Katika taarifa ya ripoti hiyo watoa mada walisema serikali ya awamu ya kwanza ilifanikiwa kwenye ubora wa elimu kwa kuwa waliweka falsafa ya kutolea elimu. Falsafa iliyotumika kipindi hicho ilikuwa ni elimu ya ujamaa na kujitegemea. Kupitia elimu hiyo wanafunzi walipata mafunzo anuwai wakati wakiwa shuleni. Mwanafunzi alipohitimu masomo yake aliondoka shuleni akiwa pia na ujuzi fulani ambao ungemwezesha kujiajiri ama kufanya kazi ndogo ndogo nyumbani kwao kulingana na fani aliyojifunza na hata aliposhindwa kuendelea na masomo tayari alikuwa na fani ya kuanzia maisha.
Makamu wa Rais aikishiriki zoezi la usafi katika eneo analoishi
Serikali ya awamu ya tano inayo nafasi pia ya kuboresha elimu kwa kauli mbiu ya hapa kazi tu. Kwa mantiki hii elimu yetu inafaa ibebe kauli mbiu hii ya kazi ambapo anaweza kufuata mbinu zilizotumika awamu ya kwanza. Hivi leo elimu yetu iwajengee wanafunzi wetu moyo wa kufanya kazi, iwapatie maarifa yanayohitajika na ambayo anaweza kuyatumia maarifa hayo ama kujiajiri, kuajiri wengine ama ayatumie atakapoajiriwa. Zaidi elimu yetu iwajengee vijana wetu uthubutu wa kutenda mambo, iwajengee uwezo wa kujiamini, iwasaidie kuibua na kuvifanyia kazi vipaji vyao ili wawe na uwezo wa kushindana katika soko la ajira. Ukitazama vizuri nchini mwetu utagundua kuwa kuna watu wengi toka nchi jirani katika nafasi zenye kulipa vizuri katika sekta binafsi kadhaa, sababu ya wageni kupata fursa hizo ni uwezo wa kujieleza kwa ufasaha katika lugha za kigeni hususani kiingereza. 
Waziri Mkuu akishiriki zoezi la usafi wa mazingira
Hivyo, wakati mjadala wa lugha ya kufundishia ukiendelea, wataalamu wa mitaala watazame mbinu za kuwezesha ufundishaji lugha mbali mbali kwa ufanisi. Ushahidi unaonyesha kuwa mwanafunzi anaweza kusoma vizuri na kumudu vyema kabisa lugha zaidi ya mbili. Ni dhahiri kuwa inatengemea pia kipaji cha mtu mmoja hadi mwingine lakini uwezo huo upo kwa binadamu na upo kwa mtanzania pia. Hivyo basi hapa kazi tu, Uhuru na kazi, kazi ya Magufuli, Kazii ya Mtanzania itakuwa na maana zaidi pale itakapowekwa katika falsafa ya kuongoza elimu yetu.

Mandalu Martin


Tuesday, November 24, 2015

MAGUFULI KURUDISHA "KATIBA YA WARIOBA?"


Ndugu John Pombe Magufuli
 Majuma machache tu toka kupata mkataba toka kwa wananchi wa Tanzania kuiongoza nchi hiyo kwa kipindi cha miaka mitano, na ikiwa ni muda mfupi tu kisha kuapishwa kwake kuwatumikia wananchi, ndugu John Pombe Joseph Magufuli amefanya mambo kadhaa tofauti na ilivyokuwa imezoeleka huko nyuma.

Alichofanya ndugu JPJ Magufuli hakikinzani na katiba ya Jamhuri ya Muungano, na zaidi si kinyume na asili ya ubinadamu na kanuni za kimaumbile kwani hata Heraclitus mwanafalsafa wa kale wa Ugiriki anasema hakuna jambo la kudumu ila mabadiliko. Kwahiyo alichofanya kinaendena na kanuni za kifalsafa, ubinadamu na kanuni za kimaumbile; kila binadamu ni tofauti na wa kipekee mno na hivyo kila binadamu ana uwezo wa kufanya mambo ya kipekee na tofauti na wengine wote, hiyo ndiyo hulka sahihi ya binadamu anapokuwa na nafasi ya kujitawala.

Pamoja na mambo mengine aliyoyafanya ndugu rais, hapa hatulengi kuyaorodhesha, kusitisha safari ambazo hazina ulazima wala faida kubwa kwa taifa kwa viongozi wa serikali, kufanya mabadiliko ya matumizi ya pesa iliyokuwa imetengwa kwa sherehe za kuwapongeza wabunge na kwa kuzinduliwa rasmi kwa bunge la Tanzania. Mambo yote haya yanalenga kuongeza nidhamu ya matumizi ya pesa; hii ni stadi muhimu ambayo kila mmoja wetu inafaa ajifunze. Aidha kusitisha shamrashamra zilizozoeleka za 09/12 na badala yake kusheherekea siku hiyo ya uhuru wa Tanganyika kwa kushiriki kufanya usafi maeneo mbali mbali tunayoishi na kufanyia kazi ni jambo jema hasa. Ni dhahiri kuwa kipindu pindu hakitakwisha kwa usafi huo wa siku moja lakini agizo hilo limelenga mbali zaidi. Agizo hilo la ndugu rais linalenga mabadiliko ya tabia: jambo muhimu kwa mafanikio maishani.

Kasi ya utendaji kazi aliyoanza nayo rais Magufuli inapendeza na bila shaka tutarajie mabadiliko zaidi. Hata hivyo analazimika kuwa makini zaidi atakapokuwa “akifanya usajiri wa baraza lake la mawaziri” kwa lugha ya kisoka zaidi timu yake inafaa kuwa na wachezaji wenye viwango vya juu na wenye sifa mithili ya wachezaji wa kulipwa kama ilivyo kwa Samatta na Ulimwengu kwa TP Mazembe, Maguli kwa Stand Utd, Bocco kwa Azam, Martial, Roney kwa Man Utd, Ronaldo kwa Real Madrid, Messi, Neymar na Suarez kwa Barcelona na kadhalika na kadhalika.

Wakati wapenda maendeleo wengi wanaendelea kufurahia hatua za uchapakazi ndugu rais na hivyo kutoa pongezi kemkem kwake, nasi pia twaungana nao kumtia shime zaidi ndugu John Magufuli aendelee kufanya vyema na tunamuombea kwa Mwenyezi Mungu amlinde na kumuongoza zaidi. Hata hivyo tufahamu kuwa ndugu rais anatimiza wajibu wake kama kiongozi mkuu wa nchi mithili ya baba anayewajibika vyema kwa familia yake. Baba anayelipa ada kuwasomesha watoto wake katika shule ya viwango vya juu, anapotoa mahitaji stahiki kwa familia yake na kadhalika hapewi sifa na wala hapaswi kujisifu kwa vile anatimiza wajibu wake impasavyo. Pengine mazoea ya kuona baba wa jirani akikosa kuwajibika impasavyo kwa familia yake ndicho kinachosababisha kuona kuwa baba mtimiza wajibu anafanya mambo yasiyokuwa ya kawaida. Hivyo tufahamu na tumpatie ushirikiano ndugu rais aendelee kutimiza wajibu wake vizuri zaidi na zaidi.
Jaji Mstaafu Warioba
Wito wetu katika Makala hii/haya kwa rais Magufuli ni juu ya ama kujenga ama kuimarisha taasisi zetu. Taasisi zetu za uongozi inafaa ziwe imara na zenye mamlaka yaliyojitosheleza, zikiwa imara basi kiongozi yeyote akipata mkataba kuongoza nchi atalazimika kufanya kazi vizuri ama kwa utashi wake ama kwa kulazimishwa na taasisi hizo. Bila kuwa na taasisi imara utendaji kazi na uongozi utategemea hisani na hulka ya kiongozi aingiaye madarakani. Kiongozi mchapakazi na mzalendo “akiukwaa” mkataba kuongoza nchi mambo yatakwenda vyema na wanachi tutaona kama tunafanyiwa hisani ila hali akiingia kiongozi mwenye uzalendo hafifu na mwenyekujipenda yeye mwenyewe zaidi basi katika nchi tutashuhudia madudu. Hivyo basi ili tuepuke kucheza bahati nasibu ya uongozi ni vyema basi tukawa na taasisi imara. Taasisi hizo imara tunaweza kuzipata kwenye mabadiliko ya katiba yenye kushirikisha na kukubaliwa na wananchi walio wengi.


Bahati njema mabadiliko ya katiba yanayokubaliwa na wananchi tunayo kwenye chapisho la ‘katiba ya Warioba.’ Hivyo basi ndugu rais tunakuomba uturejeshee “katiba ya Warioba” ambayo itatufaa sana kwa dira ya taifa letu kwa miaka mingi ijayo.