Tuesday, November 13, 2012

KONGAMANO LA KIMATAIFA KUZUIA UHALIFU KWA VIJANA


Baadhi ya washiriki wa mhadhara wa kimataifa wa kuzuia uhalifu wa vijana katika jamii
White Sands Dsm 6-8 Nov 2012
Hivi karibuni Tanzania ilipewa uenyeji na taasisi ya haki na uzuiaji wa uhalifu ya Afrika Kusini (CJCP), kuendesha mhadhara (kongamano) wa kuzuia uhalifu kwa vijana. Mhadhara huo ilijumuisha wadau wa kada kadhaa: wanawake, vijana, watoto na yote ambayo yanalenga kuzuia uhalifu katika jamii. Mkutano huu ulifanyika hoteli ya White Sands (tarehe 6 - 8 Novemba 2012), Dar es Salaam.

Ndugu Msangi akitoa mada juu ya sera za jeshi la Polisi Tz















Mhadhara huu ulikuwa na mada anuwai zilizofanyiwa kazi. Malezi mema kwa watoto wangali wadogo kabisa, Njia mbadala za kuzuia uhalifu katika jamii, Polisi jamaa na vijana, Njia mbadala na fursa za kazi kwa vijana na kadhalika.

Ndugu Mandalu akitoa mada juu ya njia mbadala kupunguza
uhalifu miongoni mwa vijana















Wanamhadhara walitoka zaidi ya nchi ishirini na tano za mabara karibu yote ya dunia. Kwa hakika ilikuwa ni fursa nzuri kusikia wadau wa haki na amani wanavyofanya kazi kufanya dunia kuwa sehemu njema na ya kufaa kuishi sisi sote. Wanataaluma hawakuachwa kando pia, waliwasilisha tafiti zao zenye kutoa maelekezo na mwongozo wa namna ya kupunguza uhalifu katika jamii, wakati huo huo vijana, ambao ni wahanga wa fujo na wanawezeshwa kuondokana na adha hiyo. Inafahamika vyema kuwa wadau wakuu wa ujenzi wa dunia ni vijana, kwa kuwa ni kundi la watu wenye uwezo na nguvu kazi kubwa; kwahiyo basi ni muhimu kuwalea vyema wadau hao.   
Ndugu Muchunguzi akiwasilisha mada juu ya malezi

Monday, October 29, 2012

Mhadhara wa Katiba CHUONI STEMMUCO

Nchi ya Tanzania,  inaendelea na mchakato wake wa kuandika katiba mpya yenye mguso wa moja kwa moja toka kwa WaTanzania walio wengi. Katika juhudi hizo wadau mabalimbali ikiwa ni pamoja na taasisi, watu binafsi na kadhalika wanafanya juhudi kuwaelimisha wananchi walio wengi na wasio na ujuzi na uelewa wa katiba inayotumika nchini hivi sasa. STEMMUCO kwa nafasi yake imefanya kazi hiyo ya kuwaelimisha wanachuo juu ya katiba inayoiongoza Tanzania kwa sasa. Idara ya sheria, chuoni hapo imeongoza mhadhara wa wazi kwa wote waliopenda ili kuielezea katiba hiyo.








Thursday, October 25, 2012

MCHWA NA MAENDELEO MTWARA

Nguzo yenye kusambaza nishati ya umeme ikisaidiwa kazi hiyo na mti jirani
Manispaa ya Mtwara - Mikindani ina utajiri mkubwa wa kila namna. Kwa uchache utajiri huo unajumuisha, ujuzi wa uchongaji vinyago, ngoma za aina yake, mazao ya kibiashara; korosho, karanga na kadhalika, mali asili lukuki, kina bandari asilia, gesia asilia na kadhalika na kadhalika.





Mchwa ni moja ya utajiri mkubwa wa Mtwara, wataalamu wa masuala ya viumbe hai tunawaomba wafanye tafiti zinazowalenga mchwa kuona ni namna gani Mtwara -Mikindani na taifa kwa ujumla linaweza kunufaika na viumbe hawa. Wapo karibu kila sehemu na hushamiri zaidi kipindi cha ukame, huvamia karibu kila kitu kikavu kilicho mbele yao.





Sehemu ya nguzo iliyooza kwa karibu inavyoonekana


Hii nd'o nguzo iliyooza vibaya kwenye picha ndogo hapo juu

Katika pitapita zangu nimekuta mji kati kabisa wakiwa wamekula nguzo zisambazazo nishati ya umeme na sikuona juhudi za maana zikichukuliwa kunusuru linaweza kuwa tishio la maisha mjini humo.

Thursday, September 27, 2012

SIKU YA UTALII TANZANIA NA DUNIANI

Kazi ya Sanaa Mji mkongwe MIKINDANI
Wanayama wakivuka mto huko Serengeti - Tanzania



Sanaa MIKINDANI - MTWARA

Faru weusi huko Ngorongoro - Tanzania





















Leo ni siku ya UTALII TANZANIA NA DUNIANI: Utalii ni moja kati ya vyanzo vikubwa vya uchumi duniani. Kuna nchi kadhaa ambazo hutegemea tu uchumi kujiendesha na kuendelea kuwepo. Kikubwa ni uwekezaji wa makusudi na lazima katika sekta hiyo yenye uwezo wa kuzalisha ajira lukuki. Tanzania ina mali asili nyingi mno ambazo ni vivutio tosha vya utalii; moja ya mambo yanayoturudisha nyuma katika hili ni uwekezaji hafifu kwa watu wetu.

 Uwekezaji huu utazame kwa makini hasa aina ya elimu tuitoayo kwa wanafunzi wetu; kwa kuwa tuna vivutio vingi vya utalii basi tuwe na mitaala yenye kulenga utalii toka shule ya msingi. Shule zetu ziwe na michepuo yenye kuendana na mahitaji ya karne ya ishirini na moja. Kuwe na shule zenye kuangazia masomo ya sayansi na teknolojia yenye kujibu mahitaji ya moja kwa moja ya watu wetu. Tukirudi kwenye utaliii, shule na mitaala yenye kufunza huo utalii zianze mapema kufunza yaliyo ya lazima; uaminifu, ukarimu, lugha za kigeni, na mengine muhimu hiyo itasaidia kutumia vyema rasilimali na utajiri mkubwa tuliopatiwa na Mwenyezi Mungu, kinyume na hivyo tutaendelea kuwalaumu majirani waliojipanga kunufaisha jamii zao na hiyo nd'o hasa jukumu la serikali.    


Friday, September 21, 2012

Mashindano ya Hisabati, kemia, Fizikia, Jiografia n.k

Msaani Akitoa burudani kwa umma- Mashindano ya mavazi, mavazi sahihi- picha kwa hisani ya google?
Hapa duniani kila jamii ina aina fulani ya burudani na hiyo muhimu kwa maisha ya binadamu. Hata hivyo maisha ya nchi na watu wake ili yaweze kwenda mbele na nchi kupiga hatua za kimaendeleo ni muhimu ikawekeza kwa kiasi kikubwa zaidi katika elimu. Elimu kama tuambiawavyo nd'o ufunguo wa maisha. Elimu ndio inaweza kuwaweka sawa, kwa kiasi fulani, watoto wa tajiri na wamasikini. Ni kupitia hiyo elimu ndo mambo mengi iwe ni burudani; muziki, mpira, urembo, sana ya mavazi, iwe ni mawasiliano, sheria, tiba, taja tasnia zote; zinahitaji elimu ili kufanya vyema zaidi.

Nchini Tanzania, nchi yangu hii, kwa maoni yangu naona elimu hatuipatii fursa ya kutosha; ni kweli Serikali na wadau wengine wengi wanajitahidi kwa kiasi kikubwa kutoa huduma hiyo muhimu kwa jamii. Hata hivyo juhudi mara dufu bado yahitajika. Kuna njia na mbinu nyingi elimu inaweza kuiga toka kwenye kada nyingine hapa nchini.

Kwenye Muziki, filamu na sekta nyingine, wadau kadhaa wameanzisha tamasha maalumu kutafuta vijana wenye vipaji, na tamasha hizo zinafanywa kwa mbwembwe,ubunifu na bila shaka udhamini mkubwa na wenye gharama kubwa tu. Jambo hili ni jema sana kwani shughuli hizi zinachangia kuwakwamua vijana toka kwenye kukosa ajira na kuweza kupata kipato ambacho bila shughuli hizo wasingekipata.  Hata hivyo wazo na wito wangu: kuibuke wadau wengine watakao fanya mashindano ya vijana kwenye hisabati, fizikia, baiolojia, jiografia, kiswahili... wazunguke mkoa mmoja hadi mwingine kupata wataalamu wa hisabati, na kadhalika. Kufanya hivyo kutatuwezesha kupata teknolojia na kujenga hamu ya kubobea na kujikita zaidi  katika ulimwengu wa sayansi na teknolojia.   

Monday, August 27, 2012

Wasanii watakiwa kujiendeleza kitaaluma


Na Mwandishi BASATA

Mkufunzi wa masuala ya uandaaji wa Filamu Ngalimecha
 Ngahyoma akizumza jambo na wadau wa sanaa
ukumbi wa Basata

Wasanii wa nchini wametakiwa kujiimarisha katika masuala ya taaaluma ili waweze kufanya kazi zenye ubora na zinazokidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchini.

Akizungumza katika Jukwaa la Sanaa jana, mkufunzi wa masuala ya uandaaji wa filamu hapa nchini Ngalimecha Ngahyoma amesema kumekuwa na matatizo mengi katika uandaaji wa kazi za filamu hapa nchini kutokana na wasanii kutokuelewa misingi ya uandaaji wa filamu.

“Kuna maeneo ya msingi ambayo yanahitaji watu kubobea ili kuyafanya kwa utimilifu, na hakuna njia ya mkato ni lazima kuyapata shuleni kwa maana lazima mtu ufundishwe. Wasanii wengi wanatumia vipaji vyao, lakini matokeo ya kufanya mambo kwa vipaji ndiyo haya ambayo yanatupa filamu zenye matatizo katika maeneo mbalimbali,” alisema.

Tuesday, August 7, 2012

BASATA LAKERWA NA WASANII KUNG’ANG’ANIA FILAMU NA MUZIKI PEKEE

BASATA LAKERWA NA WASANII KUNG’ANG’ANIA FILAMU NA MUZIKI PEKEE


Na Mwandishi wa BASATA

Sehemu ya wadau waliohudhuria kwenye Jukwaa la Sanaa
wiki hii wakifuatilia kwa makini programu
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limeeleza kusikitishwa na hali iliyopo sasa ya wasanii kuzipa kisogo Sanaa zingine na kung’ang’ania filamu na muziki pekee hali inayowafanya wengi wao kubaki wakihangaika na kulalama.

Akizungumza wiki hii kwenye programu ya Jukwaa la Sanaa inayofanyika makao makuu ya Basata, Katibu Mtendaji wa BASATA Ghonche Materego alisema kuwa, ni jambo la kushangaza kuona wasanii wakifunga milango yote katika sekta ya Sanaa na kubaki wakihangaika na madirisha mawili tu ya filamu na muziki.

“Ndugu zangu hebu tujiulize tu, Sanaa ni pana sana na ina fursa nyingi katika kutupa ajira na kuzalisha kipato kwa vijana wengi lakini kwa nini wote tunang’ang’ana na filamu na muziki pekee? Fursa nyingine tunamwachia nani? Alihoji Materego.

Monday, August 6, 2012

Wabunge ‘wala’ rushwa marufuku kuingia China

Bunge la Tanzania Mjini Dodoma















Tumeambiwa na tunafahamu siku zote kuwa rushwa ni adui wa haki, na ni ya wananchi, ya binadamu, ama ya viumbe vilivyo hai walau kulingana  na miongozo na makubaliano yetu. Moja ya makubaliano hayo, kwa Tanzania ni kuwa rushwa ni adui wa haki, na kwenye kanuni/ ahadi za mwanaTANU (chama kilichopigania uhuru wa Tanganyika) kulikuwa na ahadi ya kutotoa na kutopokea rushwa kwani hupinga ama huzuia watu wengine kupata haki zao.

Katika nchi nyingi duniani, Tanzania ikiwa mojawapo, kuna utaratibu wa kuwa na chombo cha kutolea mawazo, kuihoji serikali iliyo madarakani, kutunga sheria n.k. Chombo hicho kinafanya kazi kwa uwakilishi; si rahisi kwa mwananchi mmoja mmoja kuingia katika chombo hiko kutetea, kudai haki yake ama/ na kufanya shughuli zingine za chombo hicho ambazo kwetu kinajulikana kwa jina la BUNGE. Kwa kuwa si rahisi wote kuingia basi tumelazimika kuwa na wawakilishi wachache ili wawe SAUTI zetu na waseme na kutenda kwa niaba yetu. Hivi karibuni tumesikia habari ya kushangaza juu ya hawa wawakilishi wetu. Tumesoma na kusikia vyombo vya habari vikielezea juu ya baadhi ya wawakilishi wetu hawa wakifanya kile tulichofundishwa kuwa ni adui wa haki, sio lengo la makala hii kuongelea suala hilo bali tu kuiwasilisha makala iliyo katika gazeti la MTANZANIA inayoeleza juu ya kicha habari.   

Mwalimu JKNyerere aliwahi kusema IKULU ni patakatifu nadhani BUGENI halikadhalika ni vivyo hivyo. Je, kama kweli kuna wabunge wameenda kinyume na utakatifu inafaa kweli waendelee kuwepo patakatifu?

Na Arodia Peter .

TUHUMA za rushwa zinazoendelea kuwaandama wabunge, zimechukua sura mpya, baada ya Serikali ya China kujiandaa kupiga marufuku wabunge wote wanaotuhumiwa kujihusisha na rushwa kuingia nchini humo.

Habari za uhakika ambazo MTANZANIA imezipata kutoka ubalozi wa China hapa nchini, zinasema umepokea taarifa rasmi kutoka kwa viongozi wakuu wa China, wafuatilie kwa karibu wabunge wote wanaotuhumiwa kwa rushwa, kisha watume taarifa ili wakibainika wasiingie kwenye nchi hiyo.
“Tumeletewa taarifa na viongozi wetu wa ngazi za juu, kuwa tufuatilie kwa kina wabunge wote ambao wanatuhumiwa na wakibainika majina yao yatumwe China, ili wazuiliwe kuingia kule,

…unajua taifa letu ni taifa ambao halina mchezo na mtu anayepokea rushwa ovyo ovyo na ni kosa la jina. kwa kiongozi kama hawa wabunge kujihusisha na siasa,

“Kwa kipindi chote hiki, kama wabunge hawa wangekuwa China leo hii, tungekuwa tunazungumza mambo mengine, wangekuwa wamechukuliwa hatua kali,

“Tunashangaa kuona kwa nini hapa kwenu, bado wanaendelea kuruhusiwa kuingia bungeni… au wanasubiri majibu ya kamati ndogo iliyoundwa kuchunguza tuhuma hizi,” kilihoji chanzo chetu.

Chanzo hicho, kilisema ubalozi wa China hapa nchini, umetuma maofisa wake mjini Dodoma kwa ajili ya kupata mwenendo wa wabunge wote wanatuhumiwa.

“Hivi sasa hapa Dodoma kuna maofisa wa ubalozi wa China, wanaendesha uchunguzi kuhusu tuhuma hizi, ikibainika ni za kweli baada ya majina ya wabunge ‘wala rushwa’ kutajwa, watachukua picha zao kwa ajili ya kuzituma China, ambako hawataruhusiwa kukanyaga kwa sababu kwao rushwa ni kosa la jinai,” kilisema chanzo chetu.

Naye Mratibu wa maombi yanayoendeshwa na Umoja wa Makanisa ya Kikristo Tanzania, mjini Dodoma Mchungaji William Mwamalanga alisema kwa kauli moja viongozi wa dini, wamesikitishwa na tuhuma hizo.

Alisema viongozi wa dini ambao wamepiga kambi mkoani Dodoma, kwa ajili ya kuliombea taifa, wamewataka wabunge wote waliotajwa wajiuzulu mara moja.

“Viongozi wa madhehebu mbalimbali tupo hapa Dodoma, kwa ajili ya kuliombea taifa, lakini moja ya jambo kubwa ambalo tumekubaliana kupita katika majimbo yao, kueleza waumini wetu matatizo haya ya rushwa… tunataka wajiuzulu kwa ajili ya kulinda heshima zao,  

Saturday, July 28, 2012

TAARIFA YA SERIKALI KUHUSU KUSUDIO LA WALIMU KUGOMA


SERIKALI kupitia Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi leo, Ijumaa, Julai 27, 2012 majira ya saa tisa alasiri, imepokea notisi ya saa arobaini na nane (48) ya kusudio la walimu wanachama wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kugoma kuanzia Jumatatu tarehe 30 Julai 2012 saa moja na nusu asubuhi.

Kabla ya notisi hii kutolewa, Serikali imekuwa ikifanya jitihada nyingi za kujadiliana na viongozi wa CWT kuhusu jinsi ya kuboresha maslahi ya walimu kwa nia ya kumaliza suala hili kwa maelewano kwa kutumia vyombo na ngazi mbali mbali za kisheria.

Kwa sasa, shauri hili liko Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi na leo hii siku ya Ijumaa tarehe 27 Julai, 2012 majira ya saa sita mchana pande zote mbili zilifika Mahakamani, na Mahakama ikaamuru kwamba pande zote zikamilishe maelezo yao ifikapo siku ya Jumanne tarehe 31 Julai, 2012 saa sita mchana, ili kuiwezesha Mahakama kuendelea kusikiliza shauri hilo na hatimaye kutoa uamuzi.

Kwa hiyo, Mgomo huu siyo halali kwa sababu shauri hili bado liko Mahakamani.

Kwa msingi huo hatua ya CWT kutoa notisi ya kuanza kwa mgomo kabla ya kukamilika kwa shauri hili ni kukiuka taratibu halali za Kimahakama ambazo kila mmoja anawajibika kuziheshimu.

Serikali inapenda kuwafahamisha walimu wote kuwa kujihusisha na mgomo huu ni kwenda kinyume cha Sheria, Kanuni na Taratibu za kazi. Hivyo, walimu wanapaswa kupima madhara ya mgomo huu usiokuwa halali na Serikali inawataka walimu kupuuza mgomo huo na kutokujihusisha nao. Walimu wote wanatakiwa waendelee na kazi kama kawaida.



Peniel M. Lyimo
KAIMU KATIBU MKUU KIONGOZI
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
27 Julai, 2012

Tuesday, July 17, 2012

MKUTANO WA WAKUU AFRIKA WAMALIZIKA


Viongozi wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika Jijini Addis Ababa.
Viogozi wa Afrika wakimaliza mkutano wa 19 wa kawaida wa Umoja wa bara hilo makao makuu ya Umoja huo jijini Addis Ababa. Pamoja na kumchangua kiongozi mpya mtendaji bi Nkosazana Dlamini-Zuma, ambaye anakuwa mwanamke wakwanza kuuongoza umoja huo, viongozi hao wamekubaliana pia kuangalia na kuifanyia kazi migogoro mikubwa miwili inayoendelea barani humo. Mgogoro ule wa kaskazini mwa Mali na ule wa Mashariki wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Kiongozi mpya wa Umoja wa Afrika
bi Nkosazana Dlamini Zuma picha kwa hisani ya blogu wadau

Mama Nkosazana Dlamini Zuma akifurahia jambo. Picha na wadau

 












Friday, June 22, 2012

Nafasi ya Masomo ya juu zaidi



Wanachuo wakifanya mitihani yao Picha kwa Hisani ya wadau wa blogu
Wanavyuo katika vyuo kadhaa nchini Tanzania hivi sasa wanaendelea na mitihani yao ya mwisho wa mwaka.

Tunawatakia mafanikio katika mitihani yao. Mitihani kwa maoni yangu si kipimo bora zaidi kuliko vipimo vingine, ila ndo kipimo cha uelewa kinachokubalika, inawezekana kabisa kukawa na njia nyingine bora zaidi lakini bora hazijakubalika.

Kwa kuwa mitihani ndo njia inayokubalika kupima uwezo wetu basi tuiheshimu na kuifanya kwa bidii na maarifa. Bidii na maarifa vinatakiwa kuja wakati wa maandalizi ili kuweza kumudu na kutawala somo kabla ya kuingia chumba cha mitihani. Ni m uhimu kufanya hivyo ili kujiamini katika kufanya mitihani, kuthibitisha utu na maadili yetu. Ni vyema mtu akafanya mitihani yeye mwenyewe bila kutumia vyanzo visivyoruhusiwa. Kufanya hivyo ni kipimo cha utu bora na faida kwa taifa na dunia kwa ujumla, kwani viongozi na watu wema wamo miongoni mwa wanavyuo wanaoendelea na mitihani yao hivi sasa.

Ili kujijenga zaidi kitaaluma nhapa chini kuna nafasi ya masomo ya uzamili kwa wanaopenda ila nafasi ijazwe haraka kwa kuwa muda umekwisha. Fanya haraka kupata nafasi hii:

 
MASTERS STUDIES - MPhil in African Studies
Our aim is to offer students a window into the cultural, intellectual, and political dynamism of African societies. At a time when Africa is often represented a place in need of outsiders' benevolence and direction, we hope to give students the linguistic and interpretive tools to study African societies on their own terms. The degree will provide an excellent foundation for those who wish to expand their knowledge of Africa, and particularly for students entering positions in the arts, the media, NGOs, and other professions.

The application deadline for MPhil in African Studies 2012-13 is the 30 June 2012

KWA TAARIFA ZAIDI SOMA HAPA