Thursday, September 15, 2011

Chanzo cha Mapato kwa Wananchi

Hii ni sehemu ya soko la Samaki mkoani Mtwara.
Hapa ni sehemu samaki wanapochuuzwa mara  baada ya kuvuliwa.



Biashara ya samaki ni moja kati ya maeno yenye kutoa ajira kwa wananchi wengi wa kawaida hususan kina mama. Hii ni shughuli ambayo huwapatia wananchi wengi pesa za kuweza kuendesha maisha yao na pia huweza kuchangia pato la taifa kwa kulipa kodi hata kama ni kiasi kidogo.

Hivi karibuni nilitembelea soko hilo kujionea jinsi lilivyo na kuangalia uwezekano wa kujipatia kitowewo. Hali niliyoikuta sokoni hapo si ya kuridhisha sana. Soko la bidhaa hiyo muhimu kwa afya ya binadamu si nzuri kiafya. Hata hivyo nilipouliza kidogo wachuuzi sokoni hapo niliambiwa kuwa kuna mikakati na ujenzi wa soko la kisasa tayari umekwishaanza. Hivyo kuna matumaini ya kupata sehemu nzuri zaidi siku za usoni.

Hii ni sehemu ya muendelezo wa soko letu la samaki mjini Mtwara, wahusika wameliona na hivyo wanaendelea kuliboresha...



Bila shaka mazingira safi ni muhimu kwa akili safi... ni muhimu marekebisho yafanyike haraka... bila shaka tutahitaji soko la kisasa kama pale Magogoni...

No comments:

Post a Comment