Thursday, September 29, 2011

Vijana wa CCM na CHADEMA


Picha kwa hisani ya mmiliki-Mtwara















Hawa ni vijana na wanafunzi; wataalamu wa leo na baadaye. Wana uwezo na nguvu nyingi zinazo hitaji kuelekwezwa sehemu sahihi kinyume na hapo ni maafa. Vijana kwa asili yao ni watu motomoto. Wana nguvu na hazina nyingi miilini na akilini mwao ambayo wanahitaji kuvifanyia kazi ili nguvu hizo ziwe na manufaa kwa jamii ya wanadamu.

Ili waweze kufanikiwa kuzitumia nguvu zao vyema ni lazima wapatiwe mafunzo ili watambue namna ya kuzigundua na kuzitumia vyema nguvu hizo; leo hii kuna AZAKI nyingi zinazotoa STADI ZA MAISHA kwa vijana.


Hilo ni jambo jema kwani bila kufanya hivyo huweza kuzitumia nguvu hizo vibaya. Wakitokea waharibifu wachache wenye kutambua vyema nguvu nyingi walizonazo vijana, huweza kuwaharibia kabisa  malengo yao ya maisha bila huruma. Hivi leo hapa Tanzania kwa sababu kadha wa kadha, baadhi ya vijana wanaingia kwenye Siasa kwa malengo ya kusaka ajira; siasa kwao ni ajira. Siasa, na hasa Siasa Safi (JK.Nyerere) ni muhimu na lazima kwa maendeleo ya watu. Lakini siasa isipokuwa safi ndipo hapo utasikia vijana wamefanya vurugu zilizohamasishwa na itikadi za kisiasa. Bila kuvurugwa na makundi ya wabinafsi wachache wenye kulenga kujinufaisha kupitia nguvu kazi na akili ya vijana, kundi la vijana ni hazina kuu kwa taifa lolote duniani, na halina haja ya fujo.Hayo yamedhihirishwa na makala hii ya Habari Leo: Vijana Chadema, CCM hawataki vurugu Igunga


No comments:

Post a Comment