Friday, January 29, 2016

JE AFRIKA TUNAWEZA KUMUDU ELIMU BORA NA BURE?


JE, AFRIKA INAWEZA KUMUDU ELIMU BURE?
imepakuliwa hapa: https://www.youtube.com/watch?v=D6zlTJ9xUp4

Mjadala umeendelea kote barani Afrika kupitia mtandao wa Bbc. Swali hili ni muhimu kwa Tanzania pia. Je, tunaweza kumudu elimu bure? Elimu hiyo ya bure inafaa iendane na ubora pia si tu elimu bure lakini yenye ubora bure pia.

Kwenye picha iliyochukuliwa mtandao wa bbc wanaonekana watoto wakiwa kwenye darasa la chini ya mti, wakiwa wamekalia mawe ili hali wapita njia wakiendelea na shughuli zao. Ama kwa hakika hapa ni ngumu mno kupata elimu bora hata kama itakuwa bure...
http://www.bbc.co.uk/programmes/p03g5pbx

Wednesday, January 20, 2016

SABABU ZA UGUMU WA MAISHA MTWARA ZATAJWA...


Mkoa wa Mtwara ni moja kati ya mikoa 26 ya Tanzania. Mkoa huu una sifa lukuki moja ya sifa hizo ni ugumu wa maisha; mkoa huu unasifika kwa bei kubwa za bidhaa ikilinganishwa na mikoa mingine ya nchi. Kwenye moja ya vipindi vyake maarufu vya jioni kituo cha redio PRIDE FM kilichopo mkoani humo siku ya Jumanne tarehe 19 Januari 2016 iliendesha kipindi ambacho pamoja na mambo mengine kilihoji kwanini maisha bidhaa mbalimbali katika mkoa huo ukilinganisha na mikoa mingine ni aghali zaidi?

Washiriki waliopiga simu walikuwa na majibu anuwai; mmoja kati ya wapiga simu hao alisema ni kweli kwamba maisha ni magumu Mtwara ikilinganishwa na mikoa mingine na sababu hasa ni uvivu wa wakazi wa mkoani humo. Wakazi wengi wanaojishughulisha na kilimo hulima eneo dogo tu la shamba na kutaka kuendesha maisha yao kupitia shamba hilo. Jambo hilo huwalazimu wakulima hao kupanga bei kubwa za mazao yao pindi wakati wa kupeleka bidhaa sokoni unapofika.

Mchangia mada mwingine alisema sababu hasa ni zile za kihistoria kwamba bidhaa zilizotoka mikoa ya jirani zilipangiwa bei kubwa kwa kuwa barabara kwenda mkoani humo zilikuwa mbovu mno na hivyo kufanya gharama za usafirishaji kuwa kubwa jambo liliongeza bei ya bidhaa.

Wito umetolewa kwa serikali kulitazama upya suala la bei za bidhaa mkoani humo kwa kuwa barabara imejengwa kwa kiwango cha lami na hivyo hakuna tena sababu ya gharama kubwa za usafirishaji.


Imepakuliwa hapa https://www.youtube.com/watch?v=-Wc0bwtAONY

Sunday, January 17, 2016

JIMBO KATOLIKI MTWARA LAPATA ASKOFU


Titus Joseph Mdoe, amesimikwa rasmi hivi leo kuwa askofu wa tano wa jimbo katoliki Mtwara. Askofu Mdoe aliteuliwa mwaka 2015 na Papa Fransisko kuliongoza jimbo hilo kufuatia kustaafu kwa aliyekuwa askofu wa jimbo hilo Gabriel Mmole. Askofu Mmole ambaye amelitumikia jimbo la Mtwara kwa miaka 31 anastaafu kisheria kwa mujibu wa kanuni za kanisa.

Askofu Mdoe amesimikwa rasmi mbele ya umati mkuu wa maaskofu toka pande zote za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, viongozi wa ngazi mbalimbali za serikali na halaiki kuu ya waumini na watu wenye mapenzi mema mkoani Mtwara.
imepakuliwa hapa...https://www.youtube.com/watch?v=PX8-nyXfnPg