Tuesday, December 15, 2015

MAGUFULI APASUA VICHWA WASOMI


WAKATI wananchi wengi wakipongeza hatua ya Rais Dk. John Magufuli kuelekeza pesa zilizochangwa kwa hafla ya kuzindua Bunge kununua vitanda katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, wapinzani wake wanaeleza huo ni mwanzo wa kushindwa katika vita dhidi ya ufisadi.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Profesa Mwesiga Baregu amesema hatua ya Rais Magufuli kupokea pesa hizo bila kuhoji malengo na msingi wa Mhimili huo wa kutunga sheria kuchangiwa fedha ni ishara ya wazi kuwa ameingia kwenye mtego wa ufisadi wa kimfumo.

“Bunge ni taasisi nyeti sana kuruhusu kuchagiwa pesa na watu ambao linapaswa kuwasimamia, hizi taasisi za fedha zilizochangia zinaweza kujikuta zinatakiwa kuchunguzwa na Bunge, credibility yake itakuwa wapi. Angeuliza kwanza kwanini wamechangisha pesa hizo, nani anawajibika nazo?

“Kama anasimamia uadilifu hakupaswa kuchukua tu hela ambazo zimechangwa bila kujua dhamira za wachangiaji, huko tunakokwenda tunahitaji miswada ya kusimamia sekta ya fedha, sheria za kodi wanapolipia dhifa ya kwanza ya kufungua Bunge, huu ni mtego, kwani Bunge haliwezi kupewa uwezo wa kuchukua hazina kiasi kidogo hata kama ni shilingi milioni tano kufanya mambo yake, dignity (heshima) yetu iko wapi kama tuna Bunge omba omba na hatujui dhamira za wachangiaji?” alihoji Profesa Baregu.
Aliongeza kwamba huo ndiyo ufisadi wa kimfumo unaoitesa Tanzania, huku akiweka wazi kuwa anazofanya sasa Rais ni mbio za sakafuni kwa kuwa hawezi akadumu na hali hiyo.
“Mkapa (Benjamin, Rais wa awamu ya tatu) alianza na kasi kuliko hata hii, pamoja na juhudi kubwa za Mwalimu Nyerere, kumtangaza kuwa Mr. Clean, kuunda Tume ya Warioba kuhusu rushwa na kuwa na baraza aliloiita la askari wa miavuli, ameishia wapi, katika kipindi chake ndiyo kashfa nyingi za ufisadi zimeibuka. Simuoni kama atakuwa tofauti na watangulizi wake,” alisema.
Ni kama Nyerere
Wakati Profesa Baregu anayatazama mambo kwa jicho hilo mchambuzi wa masuala ya siasa nchini Dk. Charles Kitima ameliambia Raia Mwema kuwa Rais Magufuli, amejipambanua kuwa ni aina ya kiongozi anayeweza kutekeleza anayoyasema kutokana na rekodi yake ya utendaji.
Amemweleza Rais Magufuli kuwa ni kiongozi wa kipekee ambaye hotuba yake ya kuzindua Bunge imeonyesha ni jinsi gani anaweza kuunganika na wananchi masikini wa ngazi ya chini.
“Hotuba yake imegusa watu wa kawaida kabisa, kama zilivyokuwa hotuba za Mwalimu Nyerere, anasema kwa lugha inayotoka moyoni, pengine ni kwa sababu ameishi maisha ya kawaida, ndiyo maana ameweza kuwavutia wengi,” alisema Dk. Kitima.
Aliongeza kwamba ingawa hotuba za mwanzo za viongozi ni kujaribu kuwaaminisha wananchi kwamba atatekeleza ahadi zake alizoahidi wakati wa kampeni, utekelezaji wa ahadi hizo hutegemea aina ya kiongozi husika.

Katika hotuba yake ya ufunguzi wa Bunge pamoja na mambo mengine aliwekea umuhimu suala la kubana matumizi ya serikali ili fedha zinazookolewa zielekezwe kwenye huduma za jamii.

Ili kuonyesha alivyodhamiria kulitekeleza hilo, juzi Jumatatu, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, alisema Rais Magufuli ameagiza kufutwa kwa sherehe za uhuru ili watu watumie siku hiyo kufanya kazi ya usafi.
“Hatuwezi kusherehekea miaka 54 ya Uhuru huku tukiendelea kusumbuliwa na ugonjwa wa kipindupindu unaoweza kuzuilika kwa kufanya usafi tu. Hii ni kejeli kwa taifa huru kwa zaidi ya miaka 50.

“Wakuu wa Mikoa, Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri wameagizwa kununua vifaa vya kufanyia usafi ili siku hiyo tuiadhimishe kwa utaratibu maalumu wa kupambana na kipindupindu,” alisema Balozi Sefue.
Akizunngumzia hotuba hiyo, aliyekuwa mtia nia ya kuwania urais kupitia CCM, Williamu Ngereja alisema hotuba hiyo ya Rais Magufuli ni mwanzo mpya kwa taifa.
“Hotuba ya Rais Magufuli ni mwongozo sahihi kwa taifa letu kufikia malengo ya kuwa na uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025. Kama wananchi wanataka mabadiliko ya kweli, kama walivyoonyesha kwenye kampeni, kila mtu anapaswa kumuunga mkono,” alisema Ngeleja. - 

CHANZO CHA HABARI HII :http://www.raiamwema.co.tz/magufuli-apasua-vichwa-wasomi

Thursday, December 10, 2015

10 things Zuma can learn from Tanzania’s new president

He’s been office for all of three weeks and already Magufuli has earned a reputation for rocking the boat, with his no-bullshit attitude and corruption-busting plan of action.
Sure he’s the son of a farmer, but this guy’s far from simple; his first real job was a school teacher, thereafter he educated himself as an industrial chemist and eventually became Tanzania’s minister of public works. The latter position saw Magufuli tackle some of the country’s largest construction projects without even a whisper of corruption or maladministration. In fact, he’s well-known for being a-corrupt, seriously.
So what is it that makes John Magufuli so great? Well, unlike so many of his counterparts, he’s relentless in his assault on corruption, laziness, and overspending; something that no doubt has already made him very unpopular among his own political comrades as well as leaders like Zuma and Mugabe. Let’s face it; the man makes almost every other leader look like a thief.
Three weeks in office and we’ve already got at least 10 major changes to report, imagine what the man can get done in five years.
Have a look at some of this legend’s highlights so far:
He cancelled Independence Day celebrations, saying that it’s “shameful” to celebrate while people are dying of cholera. Instead, the money that would have been used has now been set aside for street and public area cleaning.
After visiting the Muhimbili Hospital for the first time and seeing the dire state of affairs, the president ordered that more than 200 million Shillings earmarked for parliamentary parties be used to upgrade the hospital facilities. Less than a week later the hospital had 300 extra beds. He then fired the entire hospital board and had broken equipment repaired.
Magufuli cut his inauguration party budget from $100 000 to just $7 000 and gave the difference to the very same hospital mentioned above.
In his first week he ordered a ban on all international travel by government officials; adding that they need to focus on the rural areas of Tanzania and the poor, while commissioners and ambassadors who are already overseas can fulfil any foreign obligations.
All first and business class flights are off limits for government officials; except the president, vice president and prime minister.
Government workshops will no longer be held at hotels and function halls. Instead, they will be held at government-owned chambers so as to use what has already been paid for.
He fired Tanzania’s chief of revenue after 350 containers listed in his books disappeared from Dar es Salaam harbour. The prime minister is currently heading up that investigation.
He appointed the country’s very first female vice president.
When he had to travel 600km from Dar to Dodoma to open parliament; he chose to drive himself rather than have government organise a jet.
Magufuli went on record in the national assembly saying that, now that he’s president “it will not be business as usual.”
Pretty f*cking cool right? Well, here’s one more thing you might like to know about “The Bulldozer;” yeah, that’s what they’re calling him.
His tagline for his presidential campaign was “Work, nothing else.”
*Drops the mic

Wednesday, December 9, 2015

UHURU NA KAZI: KAZI YA TANU - KAZI YA MAGUFULI - KAZI YA WATANZANIA

Taken from Ndomi's Page
                                          Inapatikana hapa https://www.youtube.com/watch?v=b0Roj3MFrE4
Uhuru na kazi - Kazi ya Tanu. Maneno haya ama yanayofanana na haya yalikuwa ni moja ya salaam ambazo wananchi wa Tanganyika waliitumia kusabahiana mara baada ya uhuru. Bila shaka salaam hii ilitumika kutokana na umuhimu wa wananchi kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo ya haraka.

Ni utamaduni mzuri kukumbushana masuala ya msingi ili kuweza kufanikisha jambo ama mambo muhimu katika jamii. Kauli mbiu ya ndugu John Pombe Magufuli (JPM), Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati wa kampeni zake za uchaguzi mkuu  mwaka huu alitumia kauli mbiu ya HAPA KAZI TU! Kwa jinsi mambo yanavyoonekana kauli mbiu hiyo inaendelea kutumika wakati huu wa utendaji kazi zake za urais.

Kiongozi ni mtu ambaye huonyesha njia kwa kutenda. Na tena kiongozi mzuri huwa mbunifu na mweledi ili hali akitenda kwa mujibu wa sheria mama ya nchi yake. Hivi karibuni ndugu JPM alitoa agizo la maadhimisho ya siku ya uhuru wa Tanganyika kwa namna ya tofauti kabisa na miaka mingine iliyotangulia. Kwa kawaida nchini Tanzania maadhimisho haya hufanyika kwa gwaride la ukakamavu toka majeshi ya ulinzi na usalama, halaiki, ngoma mbalimbali na matumbuizo anuwai. Lakini agizo la JPM mwaka huu limekuwa kwamba maadhimisho ya sikukuu ya uhuru wa Tanganyika mwaka huu yafanyike kwa kufanya usafi maeneo mbalimbali zitolewapo huduma za kijamii.

Tumeshuhudia mwitikio mkubwa toka kwa wananchi waliojitokeza kufanya usafi katika maeneo mbalimbali. Ni jambo zuri wananchi kuitikia agizo hili ambalo pia limelenga kusaidia kupambana na ugonjwa wa kipindupindu. Moja ya sifa za kiogozi mzuri tuliona kwa ufupi ni kuonyesha njia kwa mfano; pichani hapo juu JPM anaonekana akishiriki kwa dhati kabisa katika kufanya usafi. Usafi huu ni muendelezo wa kauli mbiu ya HAPA KAZI TU!

HAPA KAZI TU! ni kauli mbiu nzuri inayofaa kutumika vyema na kwa undani zaidi kuliko ilivyo hivi sasa. Wakati kauli mbiu hii inahamasisha watu kutenda kazi, kuna watu wengine wengi hawana kazi na hivi kauli mbiu hii inakosa mantiki kwao. Hata hivyo kauli mbiu hii kama tulivyosema inatuhusu mno watanzania kwa kuwa nchi yetu bado ina uchumi duni. Hivi karibuni wadau wa HAKI ELIMU wametoa ripoti inayoelezea jinsi sekta ya elimu ilivyotenda ndani ya miaka kumi ya uongozi wa awamu ya nne.

Ripoti ya HakiElimu inasema awamu ya nne ilifanikiwa kwenye kuongeza idadi ya vitendea kazi katika sekta hiyo ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya shule za msingi na pia za sekondari, vyumba vya madarasa, mtundu ya vyoo, maabara na kadhalika. Hata hivyo ubora wa elimu katika miaka hiyo kumi imekuwa duni. Kuna wanafunzi wamemaliza masomo pasi ya kuwa na uwezo wa kusoma na kuandika. Hivyo ripoti hiyo inaisihi serikali ya awamu ya tano kuwekeza zaidi katika ubora wa elimu. Katika taarifa ya ripoti hiyo watoa mada walisema serikali ya awamu ya kwanza ilifanikiwa kwenye ubora wa elimu kwa kuwa waliweka falsafa ya kutolea elimu. Falsafa iliyotumika kipindi hicho ilikuwa ni elimu ya ujamaa na kujitegemea. Kupitia elimu hiyo wanafunzi walipata mafunzo anuwai wakati wakiwa shuleni. Mwanafunzi alipohitimu masomo yake aliondoka shuleni akiwa pia na ujuzi fulani ambao ungemwezesha kujiajiri ama kufanya kazi ndogo ndogo nyumbani kwao kulingana na fani aliyojifunza na hata aliposhindwa kuendelea na masomo tayari alikuwa na fani ya kuanzia maisha.
Makamu wa Rais aikishiriki zoezi la usafi katika eneo analoishi
Serikali ya awamu ya tano inayo nafasi pia ya kuboresha elimu kwa kauli mbiu ya hapa kazi tu. Kwa mantiki hii elimu yetu inafaa ibebe kauli mbiu hii ya kazi ambapo anaweza kufuata mbinu zilizotumika awamu ya kwanza. Hivi leo elimu yetu iwajengee wanafunzi wetu moyo wa kufanya kazi, iwapatie maarifa yanayohitajika na ambayo anaweza kuyatumia maarifa hayo ama kujiajiri, kuajiri wengine ama ayatumie atakapoajiriwa. Zaidi elimu yetu iwajengee vijana wetu uthubutu wa kutenda mambo, iwajengee uwezo wa kujiamini, iwasaidie kuibua na kuvifanyia kazi vipaji vyao ili wawe na uwezo wa kushindana katika soko la ajira. Ukitazama vizuri nchini mwetu utagundua kuwa kuna watu wengi toka nchi jirani katika nafasi zenye kulipa vizuri katika sekta binafsi kadhaa, sababu ya wageni kupata fursa hizo ni uwezo wa kujieleza kwa ufasaha katika lugha za kigeni hususani kiingereza. 
Waziri Mkuu akishiriki zoezi la usafi wa mazingira
Hivyo, wakati mjadala wa lugha ya kufundishia ukiendelea, wataalamu wa mitaala watazame mbinu za kuwezesha ufundishaji lugha mbali mbali kwa ufanisi. Ushahidi unaonyesha kuwa mwanafunzi anaweza kusoma vizuri na kumudu vyema kabisa lugha zaidi ya mbili. Ni dhahiri kuwa inatengemea pia kipaji cha mtu mmoja hadi mwingine lakini uwezo huo upo kwa binadamu na upo kwa mtanzania pia. Hivyo basi hapa kazi tu, Uhuru na kazi, kazi ya Magufuli, Kazii ya Mtanzania itakuwa na maana zaidi pale itakapowekwa katika falsafa ya kuongoza elimu yetu.

Mandalu Martin


Tuesday, November 24, 2015

MAGUFULI KURUDISHA "KATIBA YA WARIOBA?"


Ndugu John Pombe Magufuli
 Majuma machache tu toka kupata mkataba toka kwa wananchi wa Tanzania kuiongoza nchi hiyo kwa kipindi cha miaka mitano, na ikiwa ni muda mfupi tu kisha kuapishwa kwake kuwatumikia wananchi, ndugu John Pombe Joseph Magufuli amefanya mambo kadhaa tofauti na ilivyokuwa imezoeleka huko nyuma.

Alichofanya ndugu JPJ Magufuli hakikinzani na katiba ya Jamhuri ya Muungano, na zaidi si kinyume na asili ya ubinadamu na kanuni za kimaumbile kwani hata Heraclitus mwanafalsafa wa kale wa Ugiriki anasema hakuna jambo la kudumu ila mabadiliko. Kwahiyo alichofanya kinaendena na kanuni za kifalsafa, ubinadamu na kanuni za kimaumbile; kila binadamu ni tofauti na wa kipekee mno na hivyo kila binadamu ana uwezo wa kufanya mambo ya kipekee na tofauti na wengine wote, hiyo ndiyo hulka sahihi ya binadamu anapokuwa na nafasi ya kujitawala.

Pamoja na mambo mengine aliyoyafanya ndugu rais, hapa hatulengi kuyaorodhesha, kusitisha safari ambazo hazina ulazima wala faida kubwa kwa taifa kwa viongozi wa serikali, kufanya mabadiliko ya matumizi ya pesa iliyokuwa imetengwa kwa sherehe za kuwapongeza wabunge na kwa kuzinduliwa rasmi kwa bunge la Tanzania. Mambo yote haya yanalenga kuongeza nidhamu ya matumizi ya pesa; hii ni stadi muhimu ambayo kila mmoja wetu inafaa ajifunze. Aidha kusitisha shamrashamra zilizozoeleka za 09/12 na badala yake kusheherekea siku hiyo ya uhuru wa Tanganyika kwa kushiriki kufanya usafi maeneo mbali mbali tunayoishi na kufanyia kazi ni jambo jema hasa. Ni dhahiri kuwa kipindu pindu hakitakwisha kwa usafi huo wa siku moja lakini agizo hilo limelenga mbali zaidi. Agizo hilo la ndugu rais linalenga mabadiliko ya tabia: jambo muhimu kwa mafanikio maishani.

Kasi ya utendaji kazi aliyoanza nayo rais Magufuli inapendeza na bila shaka tutarajie mabadiliko zaidi. Hata hivyo analazimika kuwa makini zaidi atakapokuwa “akifanya usajiri wa baraza lake la mawaziri” kwa lugha ya kisoka zaidi timu yake inafaa kuwa na wachezaji wenye viwango vya juu na wenye sifa mithili ya wachezaji wa kulipwa kama ilivyo kwa Samatta na Ulimwengu kwa TP Mazembe, Maguli kwa Stand Utd, Bocco kwa Azam, Martial, Roney kwa Man Utd, Ronaldo kwa Real Madrid, Messi, Neymar na Suarez kwa Barcelona na kadhalika na kadhalika.

Wakati wapenda maendeleo wengi wanaendelea kufurahia hatua za uchapakazi ndugu rais na hivyo kutoa pongezi kemkem kwake, nasi pia twaungana nao kumtia shime zaidi ndugu John Magufuli aendelee kufanya vyema na tunamuombea kwa Mwenyezi Mungu amlinde na kumuongoza zaidi. Hata hivyo tufahamu kuwa ndugu rais anatimiza wajibu wake kama kiongozi mkuu wa nchi mithili ya baba anayewajibika vyema kwa familia yake. Baba anayelipa ada kuwasomesha watoto wake katika shule ya viwango vya juu, anapotoa mahitaji stahiki kwa familia yake na kadhalika hapewi sifa na wala hapaswi kujisifu kwa vile anatimiza wajibu wake impasavyo. Pengine mazoea ya kuona baba wa jirani akikosa kuwajibika impasavyo kwa familia yake ndicho kinachosababisha kuona kuwa baba mtimiza wajibu anafanya mambo yasiyokuwa ya kawaida. Hivyo tufahamu na tumpatie ushirikiano ndugu rais aendelee kutimiza wajibu wake vizuri zaidi na zaidi.
Jaji Mstaafu Warioba
Wito wetu katika Makala hii/haya kwa rais Magufuli ni juu ya ama kujenga ama kuimarisha taasisi zetu. Taasisi zetu za uongozi inafaa ziwe imara na zenye mamlaka yaliyojitosheleza, zikiwa imara basi kiongozi yeyote akipata mkataba kuongoza nchi atalazimika kufanya kazi vizuri ama kwa utashi wake ama kwa kulazimishwa na taasisi hizo. Bila kuwa na taasisi imara utendaji kazi na uongozi utategemea hisani na hulka ya kiongozi aingiaye madarakani. Kiongozi mchapakazi na mzalendo “akiukwaa” mkataba kuongoza nchi mambo yatakwenda vyema na wanachi tutaona kama tunafanyiwa hisani ila hali akiingia kiongozi mwenye uzalendo hafifu na mwenyekujipenda yeye mwenyewe zaidi basi katika nchi tutashuhudia madudu. Hivyo basi ili tuepuke kucheza bahati nasibu ya uongozi ni vyema basi tukawa na taasisi imara. Taasisi hizo imara tunaweza kuzipata kwenye mabadiliko ya katiba yenye kushirikisha na kukubaliwa na wananchi walio wengi.


Bahati njema mabadiliko ya katiba yanayokubaliwa na wananchi tunayo kwenye chapisho la ‘katiba ya Warioba.’ Hivyo basi ndugu rais tunakuomba uturejeshee “katiba ya Warioba” ambayo itatufaa sana kwa dira ya taifa letu kwa miaka mingi ijayo.

Monday, November 23, 2015

FURSA KWA VIJANA KUSAFIRI NA KUJIFUNZA NCHINI AFRIKA KUSINI



Warsha kwa vijana wa kati ya miaka 18 - 25 itafanyika huko nchini Afrika Kusini mwezi September 2016. Ili kushiriki kijana anatakiwa kujaza fomu ya maombi mtandaoni mapema na mwisho ni tarehe 4 Desemba 2015


Calling Young Leaders in Conservation and Animal Protection: Ages 18-25

In September 2016, the first Youth Forum for People and Wildlife will take place in Johannesburg, South Africa. Twenty young leaders working in animal and conservation-related fields from around the world will connect with experts, explore solutions, and build skills that will help them better understand wildlife conservation issues from multiple perspectives and empower them to become compassionate conservationists. Travel and participation costs covered.

Friday, November 20, 2015

WANASIASA KAMA WANANDOA!!!

Image by google
Makundi haya mawili yote hula kiapo cha utii na uaminifu mbele za watu na Mungu lakini bado wanachakachua!!!

WANANDOA:
Image by google

Watu wawili kwa kawaida mtu mme na mtu mke wanapopendana na kukubaliana kuishi pamoja hulazimika kuweka wazi suala hilo mbele ya umma wa wanajamii wanaoishi nao. Kwa kawaida watu hawa hula kiapo, huwekeana ahadi kuwa watakuwa waaminifu baina yao na kawaida huomba msaada wa Mungu awawezeshe kuwa waaminifu katika kiapo chao. Hufanya hivyo na kuahidi kuwa wavumilifu katika jua na mvua, afya na ugonjwa, mali na kutokuwa na mali hadi hapo kifo kitakapowatenganisha.

Hapa hatutaki kuangalia kama watu wetu wanakuwa kweli wameandaliwa na kama wanajua nini maana ya kuishi katika ndoa. Bila shaka suala hili tutalijadili mara nyingine kwa marefu na mapana yake stahiki.

WANASIASA:

Watu waume na wake walioamua kuingia kwenye shuguli za kisiasa hulazimika, kama ilivyo kwa wanandoa, kula kiapo na kuahidi kulinda na kutumikia kwa lengo la kuboresha maisha ya watu wetu. Wanasiasa pia husikika wakisema na tena kwa kutumia vitabu vitakatifu kuwa kwa akili zao timamu watailinda katiba ya Jamhuri ya Muungano na kuwa wanaomba Mungu awasaidie katika utekelezaji huo.
Image by google

Kwa upande wa siasa nafahamu pia kuwa si wanasiasa wote wanaofahamu uzito na umuhimu wa kazi hii ya kitumishi. Kama asemavyo mwanafalsafa nguli John Locke kwamba mwanasiasa mzuri ni yule anayefahamu moyoni mwake kuwa kazi hiyo ni mkataba baina ya mwanasiasa na wananchi.

MADUDU

Pamoja na kula viapo wanandoa huvikiuka viapo vyao na kuvunja ahadi zao za ndoa na kuanzisha nyumba ndogo ambazo ni kinyume na ahadi zao za ndoa. Kama ilivyo kwa wanandoa, wanasiasa wetu wengi pia hukiuka na kuvunja ahadi na viapo vyao kwa kuchakachua rasilimali zetu na kushiriki kwenye ufisadi na wizi mkubwa mkubwa tu. Mfano wa uchakachuzi hapa ni pamoja na kushiriki katika ESCROW, EPA, RICHMOND na wizi mwingi unaowakesesha wananchi haki zao. Hivyo basi wanasiasa na wanandoa wote kwa nafasi zao hufanya madudu na kukiuka viapo vyao.

Thursday, November 19, 2015

German Universities Now All Free of Tuition Fees - Vyuo Vikuu Vyote Ujeruman Hakuna Ada sasa

Reichtag
Universities in Germany are now free of tuition fees for all including international students. Yesterday, Lower Saxony became the last of seven German states to abolish their tuition fees, which were already extremely low.
German universities had been charging for tuition since 2006. The measure proved unpopular, and German states began dropping them one by one. It is now all gone throughout the country, even for foreigners.
This means that now, both domestic and international undergraduate students at public universities in Germany are able to study in Germany for free, with just a small fee to cover administration– usually between €150 and €250 (US$170-280)  – and other living expenses costs per semester (food, transport, accommodation, entertainment, course materials and other necessities).
Germans barely had to pay for undergraduate study even before tuition fees were abolished. Semester fees averaged around €500 ($630). It is now gone.
Free education is a concept that is embraced in most of Europe with notable exceptions like the U.K., where the government voted to lift the cap on university fees in 2010, and tripled the tuition fees therefore. The measure has reportedly cost more money than it brought in. The Guardian reported last March that students are failing to pay back student loans.
Maybe for now, learning German might be the best financial choice an high school student can make.
Move to Germany with a student visa by using the step by step virtual assistant to the German student visa or reading about visa for international student in Germany on migreat.com.
Read more about Scholarships for Filipinos in Germany // Scholarships Para sa Mga Filipino sa Germany
Got questions about studying in Germany? Ask Migreat Communities in Germany.

TANZANIA YETU YA FURAHA - Atomic Jazz Band

Picha kwa hisani ya Google

Tanzania ni nchi ya aina yake na tuna wajibu wa kuifanya isonge mbele hasa. Atomic Jazz Band walifanya kazi hiyo vizuri kwa kutunga wimbo unaodumu daima. Wimbo wao utuhamasishe tutumie vyema vipaji vyetu ili tuijenge nchi hii.

Monday, November 16, 2015

A Nigerian Scholar Solves 156-Year-Old Mathematics Puzzle

Image courtesy of google
In what can be regarded as a rare achievement and possible entry in Guinness world of records, a Nigerian scholar, Dr Opeyemi Enoch, has successfully solved the 156 -year- old Riemann Hypothesis, the most important problem in Mathematics.
With this breakthrough, Dr Enoch, who teaches at the Federal University, Oye Ekiti (FUOYE), has become the fourth egghead to resolve one of the seven Millennium Problems in Mathematics.
The Kogi State-born mathematician had, before now, worked on mathematical models and structures for generating electricity from sound, thunder and Oceanic bodies.
A statement in Ado Ekiti, the Ekiti State capital yesterday, said Dr Enoch presentation of the Proof on November 11, 2015 during the International Conference on Mathematics and Computer Science in Vienna, Austria becomes more symbolic coming on the exact day and month 156 years after the problem was delivered by a German Mathematician in 1859.
The Riemann Zeta Hypothesis is one of the seven Millennium problems set forth by the Clay Mathematics Institute with a million Dollar reward for each solved problem for the past 16 years.
The statement reads in part, "Dr Enoch first investigated and then established the claims of Riemann. He went on to consider and to correct the misconceptions that were communicated by Mathematicians in the past generations, thus paving way for his solutions and proofs to be established.
"He also showed how other problems of this kind can be formulated and obtained the matrix that Hilbert and Poly predicted will give these undiscovered solutions. He revealed how these solutions are applicable in cryptography, quantum information science and in quantum computers."
Three of the problems had been solved and the prizes given to the winners. This makes it the fourth to be solved of all the seven problems.
Dr Enoch had previously designed a prototype of a silo for peasant farmers and also discovered a scientific technique for detecting and tracking someone on an evil mission.
Enoch has succeeded in inventing methods by which oil pipelines can be protected from vandalism and he is currently working on Mathematical approaches to Climate Change.
The home link to this story: http://allafrica.com/stories/201511160834.html?utm_campaign=trueAnthem:+Trending+Content&utm_content=564a324004d301547840c792&utm_medium=trueAnthem&utm_source=twitter