Saturday, November 14, 2015

What a Talent! Andrea Bocelli

Pourqoui Paris, Why Paris, Kwanini Paris?

Crowds in Paris
Picha kwa hisani ya BBC
Mwezi Januari mwaka huu 2015, dunia ishuhudia mauji ya wafanyakazi wa jarida la Charlie Hebdo jjijni Paris. Ufaransa na nchi nyingi za magharibi waliyaita mashambulizi hayo kama ni mbinu kuzuia uhuru wa kujieleza. Msingi ambao nchi nyingi zilizoendelea zinaona ni haki muhimu mno kwa binadamu na ambayo katu hakuna taifa lililostaarabika litakubali kuiacha haki hiyo ipotee. Hivyo nchi hizo hujinasibu kuwa zipo tayari kutumia gharama kubwa kutetea haki hiyo; ila tusisahau kuwa haki inafaa iendane na wajibu pia. Watu wengi tuliunga mkono wa wale ndugu wa lile jarida kwa maneno ya kifaransa #jesuisCharlie" kuwa mi ni Charlie ama nawaunga mkono wafanyakazi wa Charlie Hebdo.

Wakati Ufaransa na dunia kwa ujumla inaanza kusahau habari za mauji ya wafanyakazi wa Charlie Hebdo. Jiji lile lile la Paris linakutana na mashambulizi mauaji makubwa na ya kutisha mno ndani ya miezi kumi tu toka tukio la mwisho, ukiachia majaribio ya mashambulizi yaliyozimwa kwenye treni miezi ya hivi karibuni. Mashambulizi haya yameacha zaidi ya watu 120 waliopoteza maisha na mamia wengine wengi waliojeruhiwa.

media
Picha kwa hisani ya RFI
Ni dhahiri kuwa mauaji haya yanaacha maswali mengi kuliko majibu kwa sasa. Uchunguzi ukikamilika bila shaka tutafahamu vyema kuhusiana na mauaji hayo. Moja ya maswali yanayojitokeza ni kwanini ushambuliwe mji wa Paris? Kwanini Paris? Itafaa siku za usoni tuangalie watu na mfumo wa maisha ya Paris; linalosemekana kuwa moja kati ya majiji ya starehe zaidi duniani. Bila shaka Ufaransa itatumia uwezo na rasilimali zinazohitajika kupata kufahamu mengi zaidi juu ya hili na kuimarisha usalama duniani.

Kwa sasa tunasema poleni sana wakazi wa Paris na nchi ya ufaransa kwa ujumla. roho za marehemu waliofariki dunia wapumzike kwa amani, amina.

Saturday, November 7, 2015

Jina la Uwaridi - The Name of The Rose - Le Nom de la Rose






The Name of The Rose (Kiingereza), ll Nome Della Rosa(Kiitaliana), Der Name der Rose(Kijerumani), Le Nom de la Rose (Kifaransa) Jina la Waridi : Filamu nzuri mno. Filamu iliyoandaliwa toka kwenye kitabu tajwa hapo juu kilichoandikwa na mwandishi muitaliana Umberto Eco. Kitabu chake kinaeleza mambo anuwai ikiwa ni pamoja na namna ya kufumbua tatizo lililoigubika monastery moja ya wafransikani. Ndugu mdogo William wa Baskerville akisadia na mnovisi wake Christian Slater anasaidia kutoa ufumbuzi wa tatizo hilo kitaaluma, kiteolojia, kifalsafa. Anatumia mbinu za Aristotle, mafundisho ya kiteolojia ya Thomas wa Akwino na uwezo wake wa kiakili. Kwa hakika ni filamu nzuri mno. Wakati watengeneza filamu wetu wanaendelea kufanya kazi mbali mbali na kuandaa filamu wajifunze toka kwenye filamu nzuri kama hii. 



The Land of Riches and Opportunities


Image by google

Tanzania is a land of riches and indeed many opportunities and yet the country is counted among poor countries of the world. Tanzania is the home of the roof of the continent; mount Kilimanjaro, the country houses one of the world's natural wonders of Serengeti, Ngorongoro Crater, the beautiful islands of Zanzibar to mention but just a few... and Knud Vilby in his book  'Independent? Tanzania's challenges since Uhuru' writes on...

Image by the courtesy of google
"Tanzania is one of the most peaceful, stable and democratic countries in Africa. Nevertheless, the country faces almost insoluble problems. The African continent is one of a huge variety of difficulties and potentials. The problems of Tanzania tell us something about the huge challenges facing many other countries in the continent..."
e
o


Ngorongoro Crater
Part of the Zanzibar island

Nini Muhimu Zaidi Uchaguzi Mkuu?



Tunapoelekea uchaguzi mkuu wa viongozi wa nchi yetu kuna mambo ambayo inafaa wanasiasa na wapiga kura tuyazingatie. Kuna maswali tunayopaswa kujiuliza:
1. Kwanini takwimu zinaonyesha uchumi unakuwa lakini bado kuna umasikini?
2. Vyama vituambie vitatumia mfumo upi wa uzalishaji mali? Je, ni ujamaa na kujitegemea,      Ubepari, Ubepari uchwara, ama mfumo upi?
3. Kuna jitihada zipi kupunguza kwa dhati umasikini mkubwa wa vijijini? (NBS 2012) inasema zaidi ya asilimia 70 ya watu wanaishi vijijini na kuwa karibu asilimia 90 ya watu hao ni masikini.
4. Miundo mbinu mibovu inatukosesha mapato mengi
    - Barabara vijijini mbovu hivyo usafirishaji mazao kupeleka sokoni inakuwa taabu
    - Reli ziboreshwe na kusafirisha mizigo mizito ili barabara zidumu muda mrefu na kupunguza ajali
5.Bandari ziboreshwe zaidi kupata biashara za nchi jirani
6. Elimu na wazazi wote wawasaidie vijana wetu kuongeza uthubutu, waongeze moyo wa kusoma vitabu zaidi kupata maarifa, wajifunze lugha za kishindani ili kushindana na vijana wenigne kote duniani
7. Watueleze watatumia vipi rasilimali nyingi zulizonazo kuondoa kabisa umasikini nchini. Tuna watu wengi (nguvu kazi), ardhi kubwa, bahari, maziwa, mito, jua (umeme jua), madini anuwai, gesi asilia, vivutio vingi vya utalii kwa uchache tu mlima Kilimanjaro, Serengeti, Ngorongoro, Ruaha, Mikumi, etc..Visiwa vya Zamzibar...

Baadhi ya viongozi wa siasa Tanzania wakiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Dar es Salaam,
31/08/2015

Thursday, October 29, 2015

AHADI ZA MTANZANIA


Google image

Chama cha TANU kilifanya kazi muhimu ya kuikomboa nchi yetu toka mikononi mwa wakoloni wa kiingereza. Haya yaliwezekana kutokana na uongozi thabiti wa kina J.K Nyerere, R.M Kawawa na viongozi wengine wazalendo, wenye utu na mapenzi makubwa kwa nchi na bara lao.

Malengo makubwa ya TANU ilikuwa ni kuleta uhuru wa waTanganyika na kushiriki katika ukombozi wa bara zima. Hapa tunakumbushana ahadi kumi za mwanaTANU ambazo zinafaa kuwa mwangaza kwa waTanzania wote bila kujali itikadi ya vyama vyetu na imani ya dini zetu. Na kwa nafasi ya kipekee ziwe mwangaza kwa viongozi popote walipo...

1. Binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja.

2. Nitaitumikia nchi yangu na watu wake wote

3. Nitajitolea nafsi yangu kuondoa umaskini, ujinga, magonjwa na dhuluma.

4. Rushwa ni adui wa haki. Sitapokea wala kutoa rushwa.

5. Cheo ni dhamana. Sitakitumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu.

6. Nitajielimisha kwa kadiri ya uwezo wangu na kutumia elimu yangu kwa faida ya wote.

7. Nitashirikiana na wenzangu wote kuijenga nchi yetu.

8. Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko.

9. Nitakuwa mwanachama mwaminifu wa TANU na raia mwema wa Tanganyika na Afrika.

10. Nitakuwa mtiifu na mwaminifu kwa Rais wa Serikali ya Tanganyika.


Chanzo:http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/97717-ahadi-kumi-10-za-mwana-tanu-na-tanzania-yetu-ya-sasa.html