Thursday, October 29, 2015

AHADI ZA MTANZANIA


Google image

Chama cha TANU kilifanya kazi muhimu ya kuikomboa nchi yetu toka mikononi mwa wakoloni wa kiingereza. Haya yaliwezekana kutokana na uongozi thabiti wa kina J.K Nyerere, R.M Kawawa na viongozi wengine wazalendo, wenye utu na mapenzi makubwa kwa nchi na bara lao.

Malengo makubwa ya TANU ilikuwa ni kuleta uhuru wa waTanganyika na kushiriki katika ukombozi wa bara zima. Hapa tunakumbushana ahadi kumi za mwanaTANU ambazo zinafaa kuwa mwangaza kwa waTanzania wote bila kujali itikadi ya vyama vyetu na imani ya dini zetu. Na kwa nafasi ya kipekee ziwe mwangaza kwa viongozi popote walipo...

1. Binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja.

2. Nitaitumikia nchi yangu na watu wake wote

3. Nitajitolea nafsi yangu kuondoa umaskini, ujinga, magonjwa na dhuluma.

4. Rushwa ni adui wa haki. Sitapokea wala kutoa rushwa.

5. Cheo ni dhamana. Sitakitumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu.

6. Nitajielimisha kwa kadiri ya uwezo wangu na kutumia elimu yangu kwa faida ya wote.

7. Nitashirikiana na wenzangu wote kuijenga nchi yetu.

8. Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko.

9. Nitakuwa mwanachama mwaminifu wa TANU na raia mwema wa Tanganyika na Afrika.

10. Nitakuwa mtiifu na mwaminifu kwa Rais wa Serikali ya Tanganyika.


Chanzo:http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/97717-ahadi-kumi-10-za-mwana-tanu-na-tanzania-yetu-ya-sasa.html

No comments:

Post a Comment