Thursday, November 15, 2012

MHADHARA WA NJIA YA UFUNZAJI VYUO VIKUU - SAUT MTWARA (STEMMUCO)

Sehemu ya Chuo Kikuu Aalborg
Chuo Kikuu Kishiriki Cha Stella Maris Mtwara (Cha Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agostino Tanzania) kilikuwa mwenyeji wa wanazuoni toka chuo kikuu cha Aalborg cha nchini Denmark.

Pamoja na kubadilishana mawazo wanazuoni wawili toka chuo hicho kikuu Profesa Jens Muller(PhD) na Profesa Mona Dahms waliotoa mada ambazo zilijadiliwa na wanazuoni wa Stemmuco ndugu Festo Gabriel na Profesa Eginald Mihanjo(PhD). Kisha mada hizo zilijadiliwa na wanachuo na wanataaluma waliohudhuria mhadhara huo.
Sehemu ya Chuo Kikuu Kishiriki Stella Maris Mtwara
Jens Muller, amebobea katika sayansi ya uhandisi, katika mada yake aliongelea suala la teknolojia mahalia na ulazima wa kuikuza teknolojia hiyo ili iwe na mchango kwa teknolojia ya dunia.

Gabriel Festo, akijadili mada hiyo alisisitiza kuwa jamii zetu nyingi za kale zimekuwa na teknolojia yake na wajibu wetu leo ni kuziendeleza na kujichochea jamii hizo kuziibua zaidi teknolojia hizo ili ziinufaishe jamii kubwa zaidi.

Mona Dahms aliongelea juu ya namna ya ufundishaji katika vyuo vikuu; alieza kuwa chuo chake kimekuwa kikifuata mfumo wa utatuzi wa matatizo katika ufundishaji. Alisema, tafiti zinaonyesha kuwa vijana wanaofundishwa kwa utaratibu huo wanaonekana kufanya vyema wanapokuwa kazi.

Eginald Mihanjo, mtaalam wa historia, aliwapongeza wanazuoni wa Aalborg kwa njia yao hiyo ya ufundishaji. Aliongeza kuwa huo ni mfumo mzuri ambao Tanzania iliutumia kupitia falsafa ya elimu ya Julius K.Nyerere aliyefuata na kusisitiza kuwa elimu iwe kwaajili ya kujitegemea. Mfumo huo haupo tena na hii ni hatari kwani vyuo vyetu vinaweza kutoa wahitimu wasio na ujuzi hitajika katika jamii.

No comments:

Post a Comment