Thursday, December 10, 2015

10 things Zuma can learn from Tanzania’s new president

He’s been office for all of three weeks and already Magufuli has earned a reputation for rocking the boat, with his no-bullshit attitude and corruption-busting plan of action.
Sure he’s the son of a farmer, but this guy’s far from simple; his first real job was a school teacher, thereafter he educated himself as an industrial chemist and eventually became Tanzania’s minister of public works. The latter position saw Magufuli tackle some of the country’s largest construction projects without even a whisper of corruption or maladministration. In fact, he’s well-known for being a-corrupt, seriously.
So what is it that makes John Magufuli so great? Well, unlike so many of his counterparts, he’s relentless in his assault on corruption, laziness, and overspending; something that no doubt has already made him very unpopular among his own political comrades as well as leaders like Zuma and Mugabe. Let’s face it; the man makes almost every other leader look like a thief.
Three weeks in office and we’ve already got at least 10 major changes to report, imagine what the man can get done in five years.
Have a look at some of this legend’s highlights so far:
He cancelled Independence Day celebrations, saying that it’s “shameful” to celebrate while people are dying of cholera. Instead, the money that would have been used has now been set aside for street and public area cleaning.
After visiting the Muhimbili Hospital for the first time and seeing the dire state of affairs, the president ordered that more than 200 million Shillings earmarked for parliamentary parties be used to upgrade the hospital facilities. Less than a week later the hospital had 300 extra beds. He then fired the entire hospital board and had broken equipment repaired.
Magufuli cut his inauguration party budget from $100 000 to just $7 000 and gave the difference to the very same hospital mentioned above.
In his first week he ordered a ban on all international travel by government officials; adding that they need to focus on the rural areas of Tanzania and the poor, while commissioners and ambassadors who are already overseas can fulfil any foreign obligations.
All first and business class flights are off limits for government officials; except the president, vice president and prime minister.
Government workshops will no longer be held at hotels and function halls. Instead, they will be held at government-owned chambers so as to use what has already been paid for.
He fired Tanzania’s chief of revenue after 350 containers listed in his books disappeared from Dar es Salaam harbour. The prime minister is currently heading up that investigation.
He appointed the country’s very first female vice president.
When he had to travel 600km from Dar to Dodoma to open parliament; he chose to drive himself rather than have government organise a jet.
Magufuli went on record in the national assembly saying that, now that he’s president “it will not be business as usual.”
Pretty f*cking cool right? Well, here’s one more thing you might like to know about “The Bulldozer;” yeah, that’s what they’re calling him.
His tagline for his presidential campaign was “Work, nothing else.”
*Drops the mic

Wednesday, December 9, 2015

UHURU NA KAZI: KAZI YA TANU - KAZI YA MAGUFULI - KAZI YA WATANZANIA

Taken from Ndomi's Page
                                          Inapatikana hapa https://www.youtube.com/watch?v=b0Roj3MFrE4
Uhuru na kazi - Kazi ya Tanu. Maneno haya ama yanayofanana na haya yalikuwa ni moja ya salaam ambazo wananchi wa Tanganyika waliitumia kusabahiana mara baada ya uhuru. Bila shaka salaam hii ilitumika kutokana na umuhimu wa wananchi kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo ya haraka.

Ni utamaduni mzuri kukumbushana masuala ya msingi ili kuweza kufanikisha jambo ama mambo muhimu katika jamii. Kauli mbiu ya ndugu John Pombe Magufuli (JPM), Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati wa kampeni zake za uchaguzi mkuu  mwaka huu alitumia kauli mbiu ya HAPA KAZI TU! Kwa jinsi mambo yanavyoonekana kauli mbiu hiyo inaendelea kutumika wakati huu wa utendaji kazi zake za urais.

Kiongozi ni mtu ambaye huonyesha njia kwa kutenda. Na tena kiongozi mzuri huwa mbunifu na mweledi ili hali akitenda kwa mujibu wa sheria mama ya nchi yake. Hivi karibuni ndugu JPM alitoa agizo la maadhimisho ya siku ya uhuru wa Tanganyika kwa namna ya tofauti kabisa na miaka mingine iliyotangulia. Kwa kawaida nchini Tanzania maadhimisho haya hufanyika kwa gwaride la ukakamavu toka majeshi ya ulinzi na usalama, halaiki, ngoma mbalimbali na matumbuizo anuwai. Lakini agizo la JPM mwaka huu limekuwa kwamba maadhimisho ya sikukuu ya uhuru wa Tanganyika mwaka huu yafanyike kwa kufanya usafi maeneo mbalimbali zitolewapo huduma za kijamii.

Tumeshuhudia mwitikio mkubwa toka kwa wananchi waliojitokeza kufanya usafi katika maeneo mbalimbali. Ni jambo zuri wananchi kuitikia agizo hili ambalo pia limelenga kusaidia kupambana na ugonjwa wa kipindupindu. Moja ya sifa za kiogozi mzuri tuliona kwa ufupi ni kuonyesha njia kwa mfano; pichani hapo juu JPM anaonekana akishiriki kwa dhati kabisa katika kufanya usafi. Usafi huu ni muendelezo wa kauli mbiu ya HAPA KAZI TU!

HAPA KAZI TU! ni kauli mbiu nzuri inayofaa kutumika vyema na kwa undani zaidi kuliko ilivyo hivi sasa. Wakati kauli mbiu hii inahamasisha watu kutenda kazi, kuna watu wengine wengi hawana kazi na hivi kauli mbiu hii inakosa mantiki kwao. Hata hivyo kauli mbiu hii kama tulivyosema inatuhusu mno watanzania kwa kuwa nchi yetu bado ina uchumi duni. Hivi karibuni wadau wa HAKI ELIMU wametoa ripoti inayoelezea jinsi sekta ya elimu ilivyotenda ndani ya miaka kumi ya uongozi wa awamu ya nne.

Ripoti ya HakiElimu inasema awamu ya nne ilifanikiwa kwenye kuongeza idadi ya vitendea kazi katika sekta hiyo ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya shule za msingi na pia za sekondari, vyumba vya madarasa, mtundu ya vyoo, maabara na kadhalika. Hata hivyo ubora wa elimu katika miaka hiyo kumi imekuwa duni. Kuna wanafunzi wamemaliza masomo pasi ya kuwa na uwezo wa kusoma na kuandika. Hivyo ripoti hiyo inaisihi serikali ya awamu ya tano kuwekeza zaidi katika ubora wa elimu. Katika taarifa ya ripoti hiyo watoa mada walisema serikali ya awamu ya kwanza ilifanikiwa kwenye ubora wa elimu kwa kuwa waliweka falsafa ya kutolea elimu. Falsafa iliyotumika kipindi hicho ilikuwa ni elimu ya ujamaa na kujitegemea. Kupitia elimu hiyo wanafunzi walipata mafunzo anuwai wakati wakiwa shuleni. Mwanafunzi alipohitimu masomo yake aliondoka shuleni akiwa pia na ujuzi fulani ambao ungemwezesha kujiajiri ama kufanya kazi ndogo ndogo nyumbani kwao kulingana na fani aliyojifunza na hata aliposhindwa kuendelea na masomo tayari alikuwa na fani ya kuanzia maisha.
Makamu wa Rais aikishiriki zoezi la usafi katika eneo analoishi
Serikali ya awamu ya tano inayo nafasi pia ya kuboresha elimu kwa kauli mbiu ya hapa kazi tu. Kwa mantiki hii elimu yetu inafaa ibebe kauli mbiu hii ya kazi ambapo anaweza kufuata mbinu zilizotumika awamu ya kwanza. Hivi leo elimu yetu iwajengee wanafunzi wetu moyo wa kufanya kazi, iwapatie maarifa yanayohitajika na ambayo anaweza kuyatumia maarifa hayo ama kujiajiri, kuajiri wengine ama ayatumie atakapoajiriwa. Zaidi elimu yetu iwajengee vijana wetu uthubutu wa kutenda mambo, iwajengee uwezo wa kujiamini, iwasaidie kuibua na kuvifanyia kazi vipaji vyao ili wawe na uwezo wa kushindana katika soko la ajira. Ukitazama vizuri nchini mwetu utagundua kuwa kuna watu wengi toka nchi jirani katika nafasi zenye kulipa vizuri katika sekta binafsi kadhaa, sababu ya wageni kupata fursa hizo ni uwezo wa kujieleza kwa ufasaha katika lugha za kigeni hususani kiingereza. 
Waziri Mkuu akishiriki zoezi la usafi wa mazingira
Hivyo, wakati mjadala wa lugha ya kufundishia ukiendelea, wataalamu wa mitaala watazame mbinu za kuwezesha ufundishaji lugha mbali mbali kwa ufanisi. Ushahidi unaonyesha kuwa mwanafunzi anaweza kusoma vizuri na kumudu vyema kabisa lugha zaidi ya mbili. Ni dhahiri kuwa inatengemea pia kipaji cha mtu mmoja hadi mwingine lakini uwezo huo upo kwa binadamu na upo kwa mtanzania pia. Hivyo basi hapa kazi tu, Uhuru na kazi, kazi ya Magufuli, Kazii ya Mtanzania itakuwa na maana zaidi pale itakapowekwa katika falsafa ya kuongoza elimu yetu.

Mandalu Martin