Thursday, March 8, 2012

Siku ya Wanawake duniani katika matukio Mtwara

Vazi rasmi siku hiyo ilikuwa kitenge - Naam kina mama wanapendeza
na kuongeza staha sana kwa mwanamke pale wanapovalia mavazi ya heshima




























Hii ni siku mahususi kwa wanawake duniani. Hutumika kuwakumbusha wanawake wenyewe, watunga sera, na jamii yote kwa ujumla juu ya haki na nafasi ya mwanamke katika nyanja zote za maisha.































Tafiti nyingi hapa Tanzania zinaonyesha kuwa mwanamke hususani yule wa kijijini anafanya kazi nyingi kuliko mwananchi mwingine yeyote. Pamoja na mchango huo mkubwa wa wanawake, mara nyingi juhudi zao hazitambuliki vya kutosha na wala hawathaminiwi na jamii kwa kiasi stahiki. Hivyo kwa siku ya leo ni fursa kuikumbusha jamii na wanawake wenyewe hasa wale wa mashambani. Ni dhahiri kuwa wanawake wengi vijijini wanafanya kazi nyingi kwa kuwa tamaduni nyingi, zenye mfumo dume, zinawalazimu kufanya hivyo.





























Tunawaomba na kuwapa changamoto wanawake wa mijini, kulihamasisha kundi hili lenye mchango mkubwa kwa uchumi wa nchi yetu. Mwaka huu, kwa kutambua nafasi ya elimu kuleta mabadiliko kwa jamii, wito umeelekezwa kwa ushiriki wa mtoto wa kike katika elimu kama kichocheo kikubwa kuleta maendeleo ya jamii.

Saturday, March 3, 2012

Duh angurumapo simba mcheza nani?


Hii toka kwa kaka michuzi
Hakuna ubishi kuwa watu wengi tunapenda mchezo wa soka hapa Tanzania.

kupitia huu upenzi wa mpira kwanini tusibuni njia ya kuhamasishana kwenye elimu kupita soka ili kiwango na ubora wa elimu yetu vikue pamoja na soka hasa la kina mama; soka la kina mama Tanzania ni bora zaidi kuliko la kina baba, kwa kigezo cha matokeo. Taifa Stars imewahi kuifunga timu nyingine mabao matano?


Hii ni keki tuliyokula siku ya ufunguzi wa Simba TV. Hata hivyo TV hiyo inayorusha vipindi vyake kupitia clouds tv inaishia tu mikocheni, haifiki walipo watazamaji wa mdenga, Mtwara, Lindi, Mazoo, Shytown, Ta etc fikisheni mapema basi! 

Harakati za Ubunifu wa vazi la Taifa?




Picha zote kwa hisani ya blogu la UDADISI

Thursday, March 1, 2012

Mtazamo Chanya Humjenga Binadamu!

Maneno haya ya kiingereza juu ya rais huyu wa Marekani ni fundisho la aina yake
tujifunze kupenda tunachofanya na tukifanye kwa moyo wote matokeo yake ni furaha na amani
Ujumbe huu nimeupata toka kwenye e-mail niliyotumiwa na Edward Ezekiel, kwa hakika ni ujumbe mzuri na wa maana mno.

Huu unawafaa vijana wote ambao ni wepesi wa kukatishwa tamaa na watu wengine. Kumbuka hakuna mtu mwenye mamlaka ya kukufanya ukose furaha, ili ukose furaha, ukasirike ama uwe kwenye aina yote ya hisia ni lazima wewe mwenyewe uamue; Lincoln ni mfano mzuri mno. Maneno ya watu wengine si yenye kutubomoa.

Fundisho la pili ni kufanya kazi zetu kwa uadilifu, ubunifu, umakini na zaidi ya yote upendo. Mambo hayo husaidia kuvumbua mbinu mpya za kurahisisha maisha na kuleta maendeleo kwa watu haraka. Ndugu huyu japo si Mwafrika na atukumbushe kutenda mema!

Je Afrika imejididimiza yenyewe?

Ndugu zangu salam,
Kigoda cha Taaluma cha Mwalimu Nyerere kinawakaribisha wote kwenye , Malumbano ya Hoja baina ya Wanafunzi wa Sekondari na Chuo Kikuu, mada ni " Handira hii inaamini kwamba Afrika imejididimiza yenyewe" ikifuatiwa na filamu ya "The Last Days of Walter Rodney" hapa UDSM-katika ukumbi wa Nkrumah, tarehe 03.03.2012 siku ya Jumamosi kuanzia saa 4:00 asubuhi mpaka 8:15 mchana. Malumbano haya ya hoja yatakuwa katika lugha ya Kiswahili. Nawaombeni tusambaze tangazo hili kwenye mitandao yetu ya jamii. Karibuni sana.
Nimeambatanisha ratiba na bango bonyeza hapa.

Walter Rodney Luanda
Mwalimu Nyerere Chair-Senior Administrative Officer