Wednesday, April 25, 2012

Siku ya Malaria Duniani

Ugonjwa wa malaria ambao ni wakitropiki, unaendelea kuuwa watu wengi duniani na hasa barani Afrika hususani kusini mwa jangwa la Sahara. Ungonjwa huu ambao inasemekana umekuwa ukimsumbua binadamu kwa zaidi ya miaka 50'000 ni tishio kwa afya za Waafrika wengi.

Malaria huuwa zaidi kina mama na watoto
picha hii kwa hisani ya blogu hili
Asilimia 90% ya vifo vyote vya malaria hutokea barani mwetu, ambapo asilimia sitini ya vifo vyote huwa ni watoto wadogo chini ya miaka mitano. Mara nyingi malaria huambatanishwa na umasikini, na huenda ukawa moja ya vyanzo vya umasikini barani. Kuhusiswa huko na umasikini ni kutokana familia nyingi barani kushindwa kumudu manunuzi ya dawa za kuzuia maambukizi lakini pia mara nyingine kukosa uelewa wa namna ya kujikinga hususani vijijini na mijini kwenye familia zenye elimu na kipato cha kadri ama chini .
Chandarua chaweza kuzuia maambukizi
Ugonjwa huu unaweza kuzuiwa kwa kutumia chandarua kilichotiwa dawa ya kuua mbu na wadudu wengine, kusafisha vyema mazingira ya maeneo tunayoishi ili kuharibu mazalia ya mbu, kukausha na kuondoa maji yote yaliyotuama. na kadhalika.

Ugonjwa wa malaria unazuilika na inawezekana kufanya hivyo kama usemavyo ujumbe wa kataa Malaria. Na ukweli huu umedhihirika huko Zanzibar na Zambia ambapo katika ripoti za hivi karibuni, ugonjwa huo umedhibitiwa kwa asilimia zaidi ya hamsini.

Kwa kumbukumbu ya siku hii tujihadhari zaidi na kuhadharisha wenzetu wawe makini na ugonjwa huu unaoendelea kuuwa binadamu wengi zaidi mithiri ya vita.  

Taarifa za Malaria zaidi zinaweza kupatikana katika blogu hii pia. na katika blogu la unicef, who nk




No comments:

Post a Comment