Monday, April 16, 2012

MANENO MAKALI HAYAVUNJI MFUPA

The image by the courtesy of Google
                                   
"The smallest deed is better than the greatest intention." John Burrough.
Maneno Makali hayavunji mfupa!

Wazo hili nimelipata katika mtandao wa advance Africa. Mtandao ambao siku zote hutoa kwa wahitaji fursa za masomo na kazi zaidi . Mtandao huu ni nyenzo nzuri wa vijana walio masomoni na wanaotarajia kumaliza masomo yao na kujiunga na ulimwengu wa kazi.

Mtandao huu huonyesha fursa za kazi kwenye nchi mabalimbali ikiwa ni pamoja na ughaibuni. Kwanza nieleweke vyema kuwa jambo muhimu kwa mwenye kuweza kulifanyia kazi, ni mtu binafsi kujiajiri ni vyema akafanya hivyo japokuwa si vibaya kama atafanya kazi sehemu nyingine kwanza ili apate mtaji wa kuanzisha shughuli zake binafsi. Kwa wale wanaopenda kufanya kazi za kuajiriwa, wanaweza pia kufikiria kazi za hapa nchini na pia zile za kimataifa. Vijana wetu wafahamu kuwa kazi hizo zipo pia kwaajili yao si tu kwa watu wa mataifa mengine. Hata hivyo ili kuweza kupata fursa hizo ni vyema kuzingatia masuala kadhaa yenye umuhimu usio kifani. Weledi, uaminifu, kujiamini na kujituma, ujuzi wa lugha za kigeni, utayari kuishi katika tamaduni mchanganyiko na kadhalika.

Weledi ni kigezo cha uhakika kwa mtu kufanya kazi popote apendapo. Weledi ni msamiati ulioibuka hivi karibuni ukimaanisha ujuzi na uwezo wa kufanya kazi. Wanachuo ama mtu yeyote anayetaka kufanya kazi ni vyema awe na ujuzi wa kile anachotaka kufanya hii ni muhimu hasa. Hapa linaibuka swali la mtu anapata vipi uwezo na ujuzi wa kazi ili hali ndo kwanza anatoka masoni? Swali hili lafaa kujibiwa na fursa za kujitolea; vijana wanafunzi, wanavyuo tujenge utamaduni wa kujitolea kufanya kazi katika makampuni, mashirika na hata kati taasisi za kidini ili mradi kuwe na fursa ya kujijenga katika utendaji kazi na hapo hakutakuwa na ukosefu wa ujuzi.

Uaminifu; ni moja ya mahitaji muhimu katika ulimwengu wa kazi na ujasiriamali. Katika ulimwengu wa mtaji jamii "social capital" uaminifu ni suala la lazima katika mafanikio, ili ufanikiwe ni lazima uwe na mtandao mkubwa na mpana, huwezi kupata mtandao mkubwa vile kama wewe si mwaminifu. Kwa hivi basi ni lazima kujifunza kuwa mwaminifu. Tunu ya uaminifu ni moja kati ya zawadi amabazo watu wengi hujifunza toka katika familia zetu; huwatazama wazazi wetu jinsi wanavyoishi na hii hurithi toka kwao. Hata hivyo kulingana na uwezo mkubwa wa ubongo wa binadamu; unaweza kujifunza kila kitu mradi tu upatiwe mazingira na kuwe na nia na ulazima wa kufanya hivyo.

Kujiamini na kujituma; hivi ni vigezo muhimu katika mafanikio. Ili uweze kufanya jambo fulani ni lazima kwanza wewe mwenyewe ujiamini kuwa unaweza kulifanya, lakini kujiamini peke yake haitoshi ni lazima kujituma katika kile unachonuia kukifanya. Tunu hivi mbili ukiziweka pamoja basi una uhakika wa kufanikiwa. Msemo wa Kiswahili Penye nia pana njia unafaa uwe kielelezo na mwongozo katika malengo yako maishani.

Ujuzi wa lugha za kigeni; hiki ni kitendea kazi muhimu hasa hususani katika zama zetu za utandawazi. Katika nyakati hizi watu wengi zaidi husafiri, kufanya hivyo kuna walazimu kujifunza lugha kadhaa. Wewe huna sababu ya kutojifunza lugha muhimu za maitaifa mengine hasa zile zenye ushawishi kwa mataifa mengi. Unaweza kujifunza na kutawala vyema zaidi Kiingereza, Kifaransa, Kispanyola, na sasa kwa sababu za kiuchumi, watu wanajifunza kichina. Ujuzi wa lugha nyingi utakufanya uwe mshindani mkubwa na kujitofautisha na hata wale waliofanya kazi siku nyingi.

Utayari kuishi katika tamaduni mchanganyiko; binadamu sisi ni wamoja kwa namna zote muhimu. Binadamu ana undwa kwa chembe hai ndogo ndogo ambazo ni sawa kwa kila binadamu, ana mifumo kadhaa ambayo hufanya kazi sawa sawa na kadhalika. Hata hivyo tamaduni, mazingira, makuzi n.k huleta tofauti tulizonazo katika jamii za binadamu zilizosambaa katika uso wa sayari ya dunia. Tofauti hizi muhimu ndo hutufanya tufanikiwe kwani hutujengea ushindani mioyoni mwetu. Sasa kama unataka kufanikiwa ni lazima ujifunze kuishi na watu wa jamii zingine; kupitia wao utajifunza taaluma na tekinolojia za watu wengine. Ukipata fursa hiyo; itumie vyema kwani unaweza kuibadilisha dunia toka duniani kote!

Kwa wanaotafuta nafasi za kazi na masomo nje ya nchi tafuta kwa kubonyeza hapa


No comments:

Post a Comment