Sunday, February 19, 2012

Binadamu hujiumba

A man, as a general rule, owes very little to what he is born with - a man is what he makes of himself.










































Kanuni ya maisha ni kwamba, binadamu hutegemea kwa kiasi kidogo mno kile anachozaliwa nacho, kimsingi binadamu anaamua yeye mwenyewe kuwa anavyotaka yeye mwenyewe.

Alexander Graham Bell.

Mwenyezi Mungu anatuumba mara moja na kutupatia pumzi ya uhai. Pumzi hiyo ya uhai nd'o has maisha yenyewe; hiyo ndo hasa sayansi bado haiwezi kuelezea ni nini hasa. Tunapozaliwa tunakuwa tumekamilika idara zote za miili yetu. Hata hivyo maamuzi ya binadamu awe nani ni suala na maamuzi binafsi lakini muhimu hasa kama tunapenda maisha yetu yawe na maana na kuleta furaha na maana kwa maisha ya watu wengine.
 
Kuvumbua, kuibua, kuja na wazo jipya na kadhalika ndo hasa mambo amabayo tunatakiwa tuyafanye ili kweli maisha yetu yawe na maana kabisa. Kutafuta na kukusanya mali kwa bidii zote (hili ndilo jambo ambalo wengi wetu hulifanya) ni muhimu na vyema kabisa ili kuupiga vita umaskini na uhohehahe lakini pesa isiwe ndio lengo letu kuu; pesa itumike tu kuboresha maisha ya jamii ya wanadamu kote duniani.
 
Hivi leo vijana wengi hapa Tanzania hatufahamu hasa nini maana ya maisha yetu tunadhani lengo la maisha ni kusaka pesa tu "mkwanja" hasa tukikutana na maneno na ushawishi wa vijana wa Marekani ama bara Ulaya, "Jitahidi kupata mali maishani ama kufani". Kamwe hili si lengo la maisha, jambo muhimu tukumbuke kila mwanadamu ana nafasi ya kujiumba na kuwa anavyotaka awe! 

No comments:

Post a Comment