Tuesday, January 31, 2012

Mgomo wa madaktari Tanzania

Baadhi ya matabibu na wauguzi wa hospitali ya
Muhimbili wakijadiliana mambo kadhaa picha kwa
hisani ya rfi Kiswahili

















Tunawapa pole wote wanaoathiriwa na mgomo huu!

Binadamu, kulingana na biolojia tunayoifahamu sisi wanadamu hivi leo, ndio mnyama mwenye ubongo mkubwa na wenye kufanya kazi vyema zaidi kuliko wanyama wengine. Bila shaka ukweli huu upo kwa lengo mahususi na si kwa bahati mbaya.

Binadamu mara tu anapozaliwa ana jukumu muhimu kwa dunia hii, hiyo ni moja kati ya sababu nyeti za uwepo wake hapa duniani - la raison d'être. Hali hiyo ni lazima kwa kila kilicho!

Hivyo basi, lazima tujiulize hivi nini hasa sababu ya uwepo na wajibu wa serikali kwa wananchi wake, ikiwa ni pamoja na madaktari? Nini sababu ya uwepo na wajibu wa madaktari hapa duniani?

Bila shaka kwa kutumia ubongo wenye uwezo mkubwa wa kupambanua magumu, tunaweza kupata suluhu ya tatizo hili...  

No comments:

Post a Comment