Showing posts with label Maisha ni nini? What is life?. Show all posts
Showing posts with label Maisha ni nini? What is life?. Show all posts

Friday, October 5, 2018

WHO WILL CRY WHEN YOU DIE - NANI ATAKULILIA SIKU UKIFA?


Tafakuri ya uchambuzi wa kitabu kiitwacho: WHO WILL CRY WHEN YOU DIE (Nani atakulilia siku ukifa?),Na Robin Sharma.

Habari mpenzi msomaji makala hizi,ninatumai u mzima na unaendelea vyema na majukumu yako ya kila siku,leo nimekuja na uchambuzi wa kitabu cha mwandishi Robin Sharma(WHO WILL CRY WHEN YOU DIE)  nakukaribisha nawe usome uchambuzi huu naamini kuna mengi utaenda kujifunza.

Kwanza kabisa katika maisha haya tunayoishi lazima tukumbe kuwa ipo siku yana ukomo wake,hakuna ambaye ataishi milele.Sasa je ulishawahi kujiuliza nani atakulilia siku ukifa?,mwandishi Robin Sharma anaeleza mambo 101 katika kitabu hiki lakini embu twende kuona haya machache na siku baada ya siku tutazidi kujifunza mengine.Karibu,

1.Chunguza na ujue wito wako ni upi? yaani uliletwa duniani ili uje kufanya nini? ukikaa na kupata jawabu,anza kuishi kwa lile kusudi uliloitiwa kuja kulifanya duniani ili uache alama yenye kukumbukwa na kila mtu hata siku ukiwa haupo tena duniani.

2.Jifunze kuwa na shukrani kwa watu,jijengee tabia ya kushukuru hata kama ulichopewa ni kidogo ila ukiweza kuthamini kilicho kidogo basi utaweza kuthamini hata kilicho kikubwa pia.

3.Simamia mitazamo yako,ili utimize lile kusudi ulilolipanga kulitekeleza.

4.Jifunze kuwa na nidhamu binafsi(self discipline),hii itakusaidia kuwa na nidhamu katika utendaji wa mambo yako bila ya kuyumbishwa tena utayatimiza kwa wakati muafaka.

5.Weka kumbukumbu ya yale uyafanyayo kila siku,andika katika notibuku yako ili uweke kumbukumbu na upate tathimini ni wapi pa kujirekebisha.

6.Jijengee tabia ya kuwa muaminifu.Unapotoa ahadi na ukashindwa kuitekeleza jua kwamba uaminifu wako unapotea kwa watu na mwisho wa siku utajikuta ukiangukia katika mahusiano mabaya na watu.Kaa chini kisha jitafakari ni mambo mangapi uliyoahidi ndani ya wiki na hujayatekeleza? ukipata jibu tafuta njia ya kujiboresha ili usirudie makosa.

7.Anza siku yako vizuri.Asubuhi ukiamka tenga japo dakika 30 za kujipanga kwa siku yako ujue kuwa itakwendaje na angalia tathimini ya siku yako iliyopita ila leo ufanye mambo kwa uzuri zaidi.

8.Jifunze kusema hapana.Hapa ipo shida kwa wengi,watu wanashindwa kujizuia kufanya mambo hata ambayo hayana faida yoyote kwao,embu jijengee tabia ya kusema hapana sio kila kitu ukiambiwa utende basi unakuwa mwepesi kutenda,ukifanya hivi itakusaidia kuokoa muda wako na kufanya mambo kwa uzuri zaidi.

9.Tenga siku yako ya mapumziko,jiwekee muda wako hata kama si siku nzima ila tenga masaa utakayopumzika na kupumzisha akili,ikiwa ni pamoja na kukaa na familia ama ndugu kisha ujipange kwa mwanzo mpya wa juma linalofuata.

Machache haya yanaweza kukusaidia endapo utachukua hatua ya utendaji,nami nikutakie kila heri katika hatua unayoenda kuchukua ya kufanya maamuzi ya kutenda.

Na mwanafunzi wa kudumu wa shule ya maisha,mshairi na mchambuzi wa vitabu;
Marko Kinyafu
+255 714 129 520
Kinyafumarcos@gmail.com.

AMKA HAPO ULIPOKAA KUNA MAVUMBI,SIMAMA UJIFUTE NA UANZE KUSONGA MBELE.

Thursday, October 4, 2018

THE POWER OF READING USEFUL BOOKS - KUSOMA VITABU VIFAAVYO HUONGEZA MAARIFA!


Ndugu msomaji wa blogu ya Wajenga Dunia,

Habari za siku nyingi? Bila shaka u mzima wa afya tele. Napenda kukukaribisha kwa mara nyingine katika ukurasa huu ili uendelee kujipatia maarifa yafaayo maishani.

Kuanzia sasa nakufahamisha kuwa tutakuwa tukifanya tafakari ya vitabu mbalimbali vyenye kukupatia maarifa na ujuzi wa mambo anuwai. Karibu sana. Kwa kila tafakari kutakuwa na mawasiliano ya mwandishi wa makala ama tafakari husika ili kama ukitaka kuwasiliana naye basi ufanye hiyo.

Martin Mandalu
+255 767 864 379

Monday, May 2, 2016

Les Sapeurs Congolais

De Caunes Sapeur
La société des ambianceurs et des personnes élégantes, ou SAPE, est une mode vestimentaire populaire née après les indépendances au Congo-Brazzaville pour ensuite se propager au Congo-Kinshasa chez les jeunes. Ce courant est dans la filiation du dandysme et ses adeptes, appelés les sapeurs s'habillent ainsi chez les grands couturiers, et pratiquent la sapologie.
......

Les dix commandements de la sapelogie

La philosophie de la sape s’accompagne de dix commandements fondamentaux, qui régissent leur comportement et résument leurs valeurs.
Premier commandement : Tu saperas sur terre avec les humains et au ciel avec ton Dieu créateur.
Deuxième commandement : Tu materas les ngayas (non connaisseurs), les nbéndés (ignorants), les tindongos (les parleurs sans but) sur terre, sous terre, en mer et dans les cieux.
Troisième commandement : Tu honoreras la sapelogie en tout lieu.
Quatrième commandement : Les voies de la sapelogie sont impénétrables à tout sapelogue ne connaissant pas la règle de trois, la trilogie des couleurs achevées et inachevées.
Cinquième commandement : Tu ne cèderas pas.
Sixième commandement : Tu adopteras une hygiène vestimentaire et corporelle très rigoureuse.
Septième commandement : Tu ne seras ni tribaliste, ni nationaliste, ni raciste, ni discriminatoire.
Huitième commandement : Tu ne seras pas violent, ni insolent.
Neuvième commandement : Tu obéiras aux préceptes de civilité des sapelogues et au respect des anciens.
Dixième commandement : De par ta prière et tes 10 commandements, toi sapelogue, tu coloniseras les peuples sapephobes.
https://fr.wikipedia.org/wiki/Soci%C3%A9t%C3%A9_des_ambianceurs_et_des_personnes_%C3%A9l%C3%A9gantes

Saturday, November 15, 2014

MAISHA NI NINI? - What is Life? - Qu'est-ce que la vie?



Image by google

Hivi karibuni nimesikia kutoka radio Maria Tanzania kuwa wana mpango wa kuanzisha kipindi kipya juu ya maisha. Nimesikia wanauliza maisha ni nini? Swali hilo limenivutia kufanya tafakari. Kisha tafakari hiyo nikaona vyema kuwashirikisha watakaopata fursa ya kutembelea ukurasa huu.

Maisha ni nini? Ni swali linalohitaji kufikiria ili kulijibu na hakika mtu hawezi kutoa jibu la maana kama atafanya hivyo bila tafakari. Swali hili lahitaji maelezo ya utangulizi kabla ya kueleza maana ya maisha. Maisha yanahusu viumbe hai, swali letu linamlega hasa binadamu nami nitamuelezea binadamu bila kwenda kwenye falsafa ya ndani ya binadamu - philosophical anthropology, nitamuelezea binadamu kwa lugha nyepesi kabisa ili kila msomaji aelewe. Hivyo basi kwa kuanza na kiumbe huyu, binadamu ni kiumbe mwenye akili na utashi zaidi kuliko viumbe wengine. 

Kiumbe huyu huanza safari ya maisha baada ya mtu mume na mtu mke kushiriki tendo la ndoa na kutungwa mimba. Kisha kutungwa mimba kiumbe kipya kinaanza kuishi ndani ya mji wa uzazi wa mwanamke. Kuishi kwa kiumbe ndani ya mwanamke kunatupatia fursa ya kurudi kwenye swali letu la msingi la maisha, yaani maisha ni nini hasa?

Maisha ni jumla ya shughuli zote azifanyazo binadamu toka kutungwa mimba hadi pale moyo (kiungo chenye kazi ya kusukuma damu mwilini sehemu zote za mwili na hivyo kuurutubisha mwili kwani damu ndiyo njia kuu ya usafirishaji mwilini) utakapokoma kufanya kazi yake.

Katika maisha ya kila binadamu kuna shughuli zinazofanana kwa viumbe wote na kuna shughuli zinazotofautiana toka binadamu mmoja hadi mwingine. Kwa kawaidaa shughuli zote za kimaumbile za binadamu hufanana. Shughuli hizo ni pamoja na zile zifanyikazo ndani ya mwili wa binadamu; ndani ya mwili wa binadamu kuna mifumo zaidi ya kumi inayoshirikiana kati yao na pia ikipata ushirikiano na idara kadhaa mwilini. Baadhi ya mifumo iliyo mwilini kwa binadamu ni pamoja na mfumo wa usafirishaji ambapo moyo na mishipa mwilini husafirisha damu na vyakula sehemu zote za mwili. Upumuaji ni mfumo unaotumia idara za pua, mapafu na kadhalika kuwezesha upumuaji wa mwili. Utoaji taka mwilini huhusisha idara kadhaa na hata mifumo mingine kufanya kazi hiyo...

Pamoja na shughuli zinazofanana kwa binadamu wote kuna mahitaji ya lazima ambayo ni muhimu kwa viumbe wote hao bila kuzingatia nafasi zao kijamii, kiuchumi na kadhalika. Chakula, hewa safi, na hifadhi ya namna fulani ni kati ya mahitaji ya lazima kwa binadamu wote.

Ili aweze kuishi vyema na mwili wake ufanye kazi, binadamu analazimika kula; lazima apate chakula katika kipindi fulani ili mwili wake uendelee kupata mahitaji na virutubisho vinavyouwezesha mwili kuendelea kuishi, hali kadhalika kwa hewa safi. Ili mwili uendelee na kazi zake lazima upate hewa safi ili kubadilishana kwa hewa safi (Okisijeni O2)  na hewa chafu (Kaboni diokisaidi CO2) kuendelee kufanyika. Binadamu wote huhitaji hifadhi ya namna fulani; toka kwenye mavazi hadi nyumba ya kujihifadhi, ni ubora tu ndiyo hutofautiana toka mmoja hadi mwingine.

Tunapojiuliza maisha ni nini kuna jambo la lazima kuligusa pia. Nini lengo la maisha? LENGO KUU LA MAISHA NI KUTAFUTA FURAHA. Kwenye dini tunaambiwa lengo kuu la maisha ni kumtumikia Mungu kupitia huduma kwa binadamu wenzetu na mwisho turudi kwa Mungu. Kwahiyo, kwa mara nyingine, kwa binadamu wote lengo kuu la maisha ni kutafuta furaha. Binadamu wote shughuli zetu zote, ama kwa kujua ama kwa kutokufahamu, ni harakati za kutafuta furaha na hivyo basi maisha ni jumla ya shughuli zote binadamu anazozifanya katika harakati za kusaka furaha.

Binadamu wote bila kasoro, lengo la maisha yetu ni kusaka furaha. Tuliona mwanzoni kuwa binadamu ni kiumbe mwenye akili na utashi mkubwa kuliko viumbe wengine wote. Utashi na akili nyingi aliyonayo binadamu humpatia fursa ya kuitafuta furaha kwa namna ya kipekee kwa jinsi ya maumbile na muundo wake unaotokana na mpangilio wa 'genes' zake, ushawishi wa mazingira aliyolelewa na pia aina na ubora wa chakula alacho hasa toka utotoni. Ndiyo maana kuna wenye hutafuta furaha kwa kufanya kazi halali kwa bidii, wengine kwa kufanya kazi haramu kwa bidii (kazi haramu huleta furaha ya muda tu kwa kuwa huwadhuru binadamu wengine), wengine kwa namna yao kulingana na vipaji vyao na wengine kwa namna zao kwa namna namna.

Hivyo basi maisha ni jumla ya shughuli zote azifanyazo binadamu katika harakati za kusaka furaha katika kipindi chote ambapo moyo unafanya kazi ya kusukuma damu mwilini!

Martin Mandalu
Alice, Eastern Cape
15/11/2014