Tuesday, June 7, 2011

Tasnia Ya Muziki Mkombozi wa Vijana

    Tasnia ya Muziki
Mkombozi wa Vijana

Hiki ni kitabu ambacho kinatokana na utafiti uliofanywa kitaalam. Kitabu hiki kinaelezea tatizo la ajira nchini Tanzania. Ukosefu wa ajira ndo hasa tatizo linalowakabili vijana wa Tanzania.

Vijana wengi huko Tanzania wanajituma ili kuepukana na tatizo hili la ukosefu wa ajira. Vijana wa mijini huko Tanzania, wameingia katika tasnia ya Muziki, hususani katika muziki wa vijana al maarufu Bongo flava. Muziki huu unachukuliwa na vijana hao kama aina ya ajira na kwa hiyo basi ilitarajiwa kuwa kazi hii ingekuwa ni mkombozi kwao. Taarifa ambapo hazikuwa zimefanyiwa utafiti zilionyesha kuwa vijana hao hawakunufaika kama ambavyo ilifaa wanufaike. Hali hii kwa hakika ilionyesha ombwe la maelezo; ni kwa sababu ya kutaka kutoa maelezo ndo hasa utafiti ulifanyika ili kuelezea kilichojiri.

Katika ukurasa huu tutakuwa na mfululizo kukielezea kitabu ambazo kinatoa mchango wa namna ya kukabiliana na tatizo hili la ukosefu wa ajira kwa vijana wetu hapa Tanzania.

No comments:

Post a Comment