Thursday, August 6, 2015

Kwanini KIFO?

Life is a great surprise
Kwanini Kifo? Hili ni moja ya maswali ya lazima na ya mwanzo kabisa ambayo binadamu alianza kujiuliza toka zama za kale kabisa huko Ugiriki karne kadhaa kabla kuzaliwa Yesu Kristo. Swali hili lilikuwa lazima na muhimu enzi hizo na linaendelea kuwa hivyo leo pia.

Kabla ya kujibu kwanini kifo ni lazima kwanza kueleza kifo ni nini? Kifo kinaweza kuelezewa kwa mitazamo anuwai. kwa uchache tunaweza kutazama kile ambacho kinasema katika dini, biolojia kwa maana ya sayansi na falsafa. Sehemu ya maelezo ya dini juu ya kifo inapata ushawishi toka falasafa.

Dini mbalimbali zina mitazamo fulani juu ya kifo. Wayahudi, Wakristo, Waislamu, na Wahindu wanaamini katika maisha baada ya kifo. Na wanaamini kwamba mwili una sehemu mbili: mwili na roho. Katika muunganiko huo, binadamu anapofariki dunia, roho na mwili vinatengana. Dini nyingi zinaamini kuwa roho haifi bali inabadili mfumo wa maisha bila kuambatana na mwili.

Katika falsafa, binadamu ni muunganiko wa mwili na roho. Katika muunganiko huu roho ni mashuhuri na muhimu zaidi kuliko mwili. Roho haiathiriki na utengano wa mwili na roho. Pamoja na mitazamo tofauti katika falsafa toka kwa wanafikra mbalimbali juu ya kifo, kwa ujumla na kwa muhtasari katika falsafa, KIFO ni utengano wa mwili na roho. Hata hivyo wanafalsafa mbalimbali wana mitazamo tofauti tofauti si lengo la makala haya kupitia moni ya wanafalsafa hao.

Katika sayansi; kibaiolojia kifo ni mwisho wa shughuli zote za kibaiolojia mwilini. Hii inatokana na moyo kushindwa kuendelea kusukuma damu mwilini na hivyo ubongo kutopata oksijeni.

Sasa kwanini KIFO? Kwanza tukubaliane kuwa katika hali ya kawaida hili ni jambo la majonzi sana. Binadamu hupatwa na majonzi makubwa tunapopoteza wapendwa na ndugu zetu. Hii ni kwa sababu mara wanapofariki, basi katika maisha yetu yaliyobakia hapa duniani, kwa wingi wake kabisa pengine miaka mia moja, kamwe hatuwezi  kukutana nao tena. Wataalamu wa saikolojia hususani juu ya mambo ya kifo, wanasema kila kiumbe kinapofariki basi kilikuwa kimekomaa tayari kwa kifo. Sasa kwanini kuwe na kifo?

Wanafalsafa wanamitazamo mbalimbali yenye kutofautiana juu ya kifo. Epicurus yeye anasema kifo si chochote...Heraclitus yeye anasema kifo ni lazima kwaajili ya uhai wa ulimwengu. Anadai ili ulimwengu uendelee kuwepo basi ni lazima kuzaliwa na kufa kwa viumbe hai kuendelee kuwepo. Socrates hana hakika kwanini kuna kifo hata hivyo anatoa mapendekezo mawili. Mosi, kama ilivyo kwa Epicurus anaona kifo si chochote ila sawa na usingizi wa daima, ambapo mtu alala vizuri bila kusumbuliwa na chochote. Pili anaona kifo kama fursa ya mabadiliko toka katika hali tuliyonayo, ambayo anaona kuwa ni duni, kwenda kwenye hali iliyo bora zaidi. Plato yeye anakitazama kifo kama fursa muhimu ambapo hatimaye roho inapata fursa ya kujikomboa toka katika gereza la mwili. Mtazamo wa Plato ni kwamba binadamu ni mwili na roho na kwamba roho ina hadhi ya juu zaidi na tena haikumbwi na mauti, haifi na wala haiozi kama ilivyo kwa mwili.

Kibaiolojia, kifo kinatokea kwa sababu mifumo mbalimbali mwilini inakuwa haiwezi tena kufanya majukumu yake kutoka na kuchakaa na kuishiwa uwezo wa kuzalisha viini uhai vinavyoufanya mwiili uendelee kufanya majukumu yake. Maelezo haya yanahusu mtu aliyefikia umri mkubwa mno yaani uzee. Lakini kuna sababu nyingine lukuki zinazosababisha mwili kushindwa kufanya kazi zake sawa sawa na hivyo kushindwa kwa moyo kusukuma damu mwilini. Ajali, magonjwa yasababishwayo na mfumo wa maisha tunayoishi, na kadhalika. Kisayansi kifo ni mwisho wa binadamu, japokuwa kuna wanasayansi wanaofanyia uchunguzi kuona kama kuna uwezekano wa maisha baada ya kifo.

Katika dini, kifo ni ukamilifu wa ubinadamu; kuzaliwa na kufa. kuna maisha baada ya kifo. Ni fursa ya kurejea kwa muumbaji na kutoa hesabu ya jinsi tulivyoishi maisha yetu hapa duniani. Hivyo japokuwa ni jambo lenye majonzi mengi kwetu tunaoachwa duniani, ni fursa kwa anayetuacha kwenda mbele ya muumbaji na pengine anaweza kuwa na ushawishi fulani ili tufanikiwe kuishi vyema kwa maombi yake na hasa kama yeye aliishi vizuri maisha yake hapa duniani.

Kumbe dini inatupatia matumai ambayo mimi pia nayaunga mkono kuwa wapendwa wetu tulioishi nao, tuliokula nao, tuliyoshirikiana nao mambo mengi hawaishii katika kifo na kuzikwa tu ardhini; kuna muendelezo wa maisha yao baada ya kifo. Na kwa imani yangu ya Kikristo ni kifo si mwisho wa kila kitu. Yesu Kristo alifufuka na kutupatia wanadamu matumaini mapya; maisha baada ya kifo. 

Sunday, June 14, 2015

CHEOSOMO WA DAR ES SALAAM


Image by google
Somocheo /Cheosomo wa Dar es Salaam kwa Nigeria ni Lagos, kwa namna fulani, Mombasa kwa Kenya, na tena kwa namna moja ama nyingine Johannesburg kwa Afrika Kusini. Na bila shaka orodha inaweza kuendelea kuwa ndefu ama kubwa mithili ya mpira wa thelujini.

Lakini hapa inafaa pia kujiuliza, je, Dar es Salaam ina shika nafasi ipi tunapotazama masuala ya miumdo mbinu yenye kufanikisha maendeleo ya watu na kukuza uchumi? Barabara zipo vipi? Reli, usafiri wa anga, usafiri wa majini? Nishati ya umeme na kadhalika. Lakini pia kigezo cha amani na utulivu.

Kwa maoni yangu, kwa kutazama kwa makini na kwa takwimu zilizopo, Cheosomo wengi wa Dar es Salaam niliowaorodhesha wanaicha Dar es Salaam kwa mbali sana katika maeoneo mengi. Dar es Salaam, nadhani inatawaongoza cheosomo wake kwenye eneo la amani na kujaliana kuliko kwingine kote; hii ni kutokana na mtazamo jumla wa Tanzania kama nchi.

Hapa Chini ni Kenya
Sehemu ya Miundombinu Jijini Mombasa

Hapa chini ni Nigeria
Sehemu ya miundo mbinu Jijini Lagos 


Hapa chini ni Afrika Kusini

Picha zote kwa hisania ya mtandao wa google. Unaweza kuweka picha bora zaidi ya hizi, Zilizopo hapa zimetumika kufukisha ujumbe tu kwa wasomaji