Monday, May 13, 2013

JUHUDI KAZINI?














KAZI NI MOJA TU SASA



Wanazuoni wa mwaka wa tatu chuoni STEMMUCO kwa juma la pili sasa wamekuwa wakitetea tafiti zao walizofanya kwa mieza kadhaa. Tafiti hizo, ambazo ni sehemu ya wajibu wao ili kupata sifa ya kupata shahada yao ya kwanza, (degree ya kwanza) zilikuwa na mada tofauti tofauti kama jinsi walivyo watu na miguso yao.

Baadhi ya kazi zilihusu mchango wa Chuo Kikuu cha STEMMUCO kwa maisha ya watu wa Mtwara kwa ujumla wake, zingine na nyingi hasa zilihusu masuala kadhaa ya elimu. Kwanini shule za Mtwara ubora wake wa elimu ni hafifu, kwanini shule za serikali ubora wake mbele ya zile za binafsi ni dhaifu n.k. Zingine zilihusu shughuli za kiuchumi mkoani Mtwara; uzalishaji chumvi na athari zake, mchango wa bandari Mtwara kwa wananchi. Kazi za wanazuoni wengine zilitazama masuala ya kijamii; kuongezeka kwa watoto wa mitaani, Unyago, jando na faida, hasara na changamoto zake. Mazingira pia hayakuachwa nyuma; tafiti kadhaa zimegusia suala hilo. Uhalifu ni moja ya mada zilizojadiliwa hali kadhalika.

Zoezi hili lilifanywa kwa lugha ya kiigereza; vijana wengi walijipanga na kutafuta misamiati stahiki kuelezea kazi zao; wapo waliofanya vyema sana, waliojitahidi sana na wanaohitaji kuongeza bidii zaidi. Kwa ujumla wanazuoni hawa ni hazina kubwa kwa taifa na wito kwao ni kuendelea na moyo wa kitafiti ili kuvumbua vyanzo vya matatizo na kuyafanyia kazi.



 



WASOMI WAKITETEA KAZI ZAO ZA TAALUMA

Baadhi ya wanachuo wa STEMMUCO wakijiandaa kutetea kazi zao za kitaaluma

Saturday, April 27, 2013

SIKU YA MUUNGANO STEMMUCO

Viongozi waasisi wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
Mwl. Julius Nyerere na Mzee Abeid Karume wakitia saini makubaliano
Picha kwa hisani ya blogu ya Michuzi   
Siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulikumbukwa kianazuoni zaidi. Siku hii ya leo ambayo ni kumbukizi ya Muungano baina ya sehemu mbili tajwa hapo juu za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; iliadhimishwa kwa namna yake. Kulikuwa na mada nne ambazo ziliwasilishwa na kujadiliwa na wadau mbalimbali ambapo dhima kuu ilikuwa ile ile ya umoja, haki, amani na mshikamano kwa watanzania ili kufikia malengo ya kuungana.



                                  
                                                 Mwalimu Julius K. Nyerere akichanganya udogo wa Tanganyika na Zanzibar
                                                ishara ya muungano huo. Hii kwa hakika ishara yenye nguvu sana.
                                                            Picha kwa hisani ya blogu ya Michuzi

Muungano pamoja na malengo mengine, kwa vyoyote vile ulikuwa na lengo la kufikia maendeleo ya binadamu; maendeleo ya kweli ya Mtanzania na kutoa mfano halisi wa Umoja ama muungano wa bara Afrika.

Mada zilizotolewa pale STEMMUCO zilikuwa pamoja na Muungano na MKUKUTA, Muungano na Uzalendo, Mali asili na Muungano Afrika Mashariki  

Friday, February 8, 2013

MITIHANI INAENDELEA STEMMUCO


WATAALAMU WA BAADAYE WAKIONYESHA UJUZI WA
MAJUMA 16 KATIKA SAA TATU

WANACHUO STEMMUCO WAKIENDELEA
NA MITIHANI MJINI MTWARA



WALIMU WAJIPIMA UJUZI WAO KABLA YA KWENDA KUFUNZA
WENGINE - MITIHANI