Sunday, December 11, 2011

Elimu ya kweli ni vitendo!



Elimu ikitafsiriwa kwenye matendo ndo haswa Elimu!























Chuo kikuu cha Makerere, kikishirikiana na vyuo vikuu vingine kimeshiriki katika mradi wa kutengeneza gari linalotumia nguvu ya umeme. Magari ya aina hii yatasaidia katika utunzaji wa mazingira kwani hayatoi moshi na hivyo kutunza mazingira. Changamoto ni kwa vyuo vikuu vingine hususani vile vikongwe, Afrika Mashariki vinafanya nini?

Kupata maelezo vizuri juu ya mradi huu soma hapa



Sehemu tofauti za gari hilo!


Siku za Usoni Chuo Kikuu cha Makerere kikishirikiana na vyuo vikuu vingine kitatengeneza gari la aina hii. Je, huu ni ukombozi wa kweli kwa bara letu la Afrika? 

Saturday, December 10, 2011

Sala / Swala kabla na baada ya kazi


File:Flag of Tanzania.svgTanzania ni nchi isiyo na dini ila watanzania wana imani na dini zao. Tanzania, ni nchi na si binadamu, mtanzania ni binadamu na wala si nchi. Hivyo watanzania hawa kwa kuwa wanamwamini Mungu basi katika mambo muhimu na rasmi yanayohusu nchi, watanzania hawa huyaanza kwa kumuomba na kumshukuru Mungu. Huu ni wito tosha kwetu sote pamoja na viongozi wetu kusali kabla na baada ya shughuli zetu.Changamoto mpya kwa maendeleo ya nchi yetu - Hofu ya Mungu na upendo kwa Jirani ni muhimu hasa!




WIMBO WA TAIFA WA TANZANIA


Mungu ibariki Afrika                                                   God bless Africa


Wabariki Viongozi wake                                             Bless its leaders
Hekima Umoja na Amani                                            Wisdom, unity and peace
Hizi ni ngao zetu                                                         These are our shields

Afrika na watu wake.                                                  Africa and its people

Kiitikio:                                                              Chorus

Ibariki Afrika, Ibariki Afrika                                   Bless Africa, Bless Africa

Tubariki watoto wa Afrika.                                    Bless us, the children of Africa


Mungu ibariki Tanzania                                           God bless Tanzania
Dumisha uhuru na Umoja                                        Grant eternal freedom and unity
Wake kwa Waume na Watoto                                To its women, men and children
Mungu Ibariki Tanzania na watu wake.                     God bless Tanzania and its people


Kiitikio:                                                               Chorus:
Ibariki Tanzania, Ibariki Tanzania                              Bless Tanzania, Bless Tanzania
Tubariki watoto wa Tanzania.                                   Bless us, the children of Tanzania