Thursday, December 1, 2011

UKIMWI DUNIANI : Attention Na SIDA wa François Luambo Makiadi



Picha kwa hisani ya google













Upungufu wa Kinga Mwilini (UKIMWI) ni hali ambayo imezigusa familia nyingi duniani kote lakini bara Afrika likiguswa zaidi kuliko sehemu nyingine za sayari hii ya dunia. Tarehe mosi Desemba huwa ni rasmi kwa shughuli za kuangalia tuliko toka.Wakati dunia ikitafakari hatua ambazo jamii imechukua kuhakikisha maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi yanapungua na pia kuwakumbuka na kuwaombea ndugu zetu walioaga dunia, ni fursa ya kupitia nyaraka na mambo rasmi yanayoweza kutupatia ujumbe rasmi.

Maneno yaliyomo kwenye wimbo maarufu wa Attention Na SIDA wa gwiji la muziki Kongo - Kinshasa na Afrika kwa ujumla François Luambo Makiadi (6 July 1938 - 12 October 1989), ni ujumbe mzuri mno wenye kumgusa kila binadamu kwa kumhadharisha na kumkumbusha wajibu wake. Hebu na tupitie ujumbe huu japo u katika lugha ya kiingereza.

Here is the text of Attention Na SIDA By Greame Ewens

Attention na Sida
Oh, Aids. This terrible sickness
Oh, Aids. A disease which does not pardon
A disease which spares nobody
Aids is a plague
Which leaves doctors impotent

Look after your body, and I'll look after mine
Protect your own body, I'll protect mine
Aids is taking the country
Aids does not discriminate against race
Aids does not discriminate against age
You mothers, beware
You fathers, beware

What can I say, mama? Aids is dividing peoples
Aids has broken marriages, Aids has divided families
Those who used to eat and drink with me, Have started to ignore me
They say I have got the Aids sickness, All my friends are cutting me off
Who can I complain to?


Aids is ravaging all peoples; they are frightened
Europe and the USA accuse Africa of being, The source of Aids
Recently Asia and USA were invaded by the sickness
Today every country is under attack, Aids is not stopping its sinister course
All selections of society are victims of Aids, Babies, children, youths, adults, the old,
Workers, bureaucrats, managers, Men, women and even doctors.
Aids can attack anybody. It can kill, It will kill all who do not protect themselves
You, brothers and sisters who already carry the virus
Do not behave in a way that contaminates others


Aids has made us forget all other illness, If a person is sick, they say it is Aids
If a person has a fever, they say it is Aids, If a person becomes thin, they say it is Aids
If a person dies, they say it is Aids, But why do we forget the other illnesses
Oh God, oh God, Oh God. Only you...,Sickness, Oh where are you coming from?
We forget other illness and talk of Aids

You pregnant women, you can carry the virus, You can transmit it to your babies
They may be infected, although you do not know, Ladies, avoid getting pregnant
If you know you have the virus. It is bad to ignore this, as your child could die young
Youths, beware, Aids can attack you, You are the life force of society
If you let it kill you, who will lead the people?
Avoid dangerous sex. Students beware unknown partners.
Be careful who you take money from, it could get you in deeper trouble.
Avoid occasional partners, Youths, beware of drugs. If you inject drugs with needles
You can become infected, Don´t take drugs. It is very bad for your health

It will bring you out in spots, It will give you diarrhoea.
Avoid picking up just anybody, Think before you make love
Even if you desire someone, be careful. Think first

You gentlemen, citizens, Beware of prostitutes
Avoid multiple partners, And you, ladies, citizens
Take measures for your own protection
Workers, in workshops, factories and offices
When you are talking together, Do not neglect the subject
Time passes quickly, and every day, Death takes the victims of Aids
The best way to avoid death is to protect yourself, Oh God, we pray to you

Priests at mass, pastors in churches, rabbis in synagogues,
Imams in the mosque, you each have an obligation
A great obligation to society. Use your office to help
Preach what society must know about Aids
Do not hold back. It is your duty to tell the people that
Aids is a punishment from God; it resembles
Soddom and Gomorrah in ancient times
Ask God to deliver us from this sickness
Use your prayers to ask God the way to salvation
All my family have run away from me
Because I have Aids. I am left with only my mother,
Who has to suffer again all the sickness of my childhood

Teachers, instructors, professors, At school, in class, at home
If you have a free moment discuss it,It is part of your scholarly obligation
Teachers at school, college and in universities
The parents count on you tp educate their children.
Parents, don´t be shy, tell your children and the youth
All you can about Aids,Tell the whole world, tell everybody to beware
It is for you to fight against Aids
We are waiting for a vaccine. We wait for medicine, It will take a long time to come,
Maybe five, seven or ten years. Change your behaviour
Time is pressing, the sickness spreads fast

Doctors, be like Pasteur, Flemming, Curie and other
Geniusses of the last century, Now is your turn to conquer this plague which
Terrifies humanity and defies medicine,Don't waste time finding the medicine, wherever it is
Get this plague out of the human body, Doctors you know well how Aids is caught
Do not show the disease that you are afraid, Do not discourage the sick by your behaviour
The medical profession looks to you to find courage, To conquer this sickness
Doctors beware, the patient's file is secret, It concerns only the patient and close family
Don't talk su much that you create panic
Your duty is always sacred. Your profession is sacred, Your duty is to find a medicine
If there is a miracle it will come from you, Doctors be careful with needles,
Always wear gloves when you touch blood

Governments of rich countries, help the poor countries
Lead the way in the struggle against Aids, Don't sell them arms to kill,
But provide arms for the War against Aids
Brothers and sisters of the United Nations,
Between yourselves combine experience and, Spread understanding
Political authorities, use the radio, television and the press
To inform the people of the dangers of Aids
Tell us how to protect against and combat Aids,
We must all be mobilised against Aids

Kwa rejea na habari hii soma hapa
This sickness o, this sickness, Can make you go bald

Wednesday, November 30, 2011

Vijana watanzania: Wamachinga wa China!

Picha kwa hisani ya mtandao

Ukosefu wa ajira za kutosha kwa vijana ndo hasa tatizo kuu linaloipasua kichwa serikali ya Tanzania. Hakuna ajira za kutosha kuwapatia fursa vijana wote wanaomaliza vyuo hapa nchini. Hivi karibuni tumesikia idadi ya wahitimu toka vyuo mbalimbali; kati yao wapo walio na ajira na wasio na ajira; kundi la pili likiwa kubwa zaidi. Wahitimu hao kwa baadhi ya vyuo ilikuwa kama ifuatavyo: Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine, SUA, walihitimu zaidi ya 1000, Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agostino, Mwanza, zaidi ya wahitimu 2000, Chuo Kikuu cha Dodoma wahitimu lukuki, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wahitimu lukuki pia. na kadhalika. Utaona ya kwamba kila uchao Vyuo vingi zaidi vinazidi kuongeza idadi ya wahitimu na hili ni jambo jema.

Kwa upande mmoja hili ni suala jema sana kwa nchi yetu, kwamba tunapata wasomi wengi zaidi. Lakini jambo hili halifariji sana pale unapoona kwamba wasomi wote ama wengi kati yao wanasubiri tu kuajiriwa. Hapa ndipo penye changamoto kubwa kwa mitaala ya elimu tunayoitumia toka shule zetu za msingi hadi sekondari. Wengi wa vijana wetu kulingana na mitaala tunayotumia ni tegemezi mno kiuchumi, kimsingi elimu wanayoipata haiwakwamui kiuchumi; pamoja na kumaliza kidato cha sita kijana wa kitanzania bado anaomba pesa kwa wazazi ama walezi kwaajili ya matumizi yake ya kawaida kama kununua nguo n.k; hii ni aibu. Mfumo wa elimu inafaa uweze kumfunza kijana kujitegemea, kuweza kuzalisha mali kwa kiwango fulani hata kama ni dhaifu lakini mtaala huo umsaidie kuwa na uthubutu; kijana awe na moyo wa kujaribu kufanya shughuli fulani halali kwa lengo la kuzalisha mali hata kama ni kidogo tu.

STEMMUCO/SAUT MTWARA
Vijana wanaojiunga na vyuo vikuu wengi ni wale ambao wamepitia mfumo wa kuulizwa maswali, kuyajibu na kupatiwa alama basi. Hakuna nafasi ya kutosha ama hakuna tu kabisa fursa kwa wanafunzi kufikiri ama kujifunza kufikiri vya kutosha. Hii ni hatari sana kwa mustakabali wa nchi na ulimwengu, kama taifa tunawajibika kuwapatia wanafunzi wetu fursa nyingi zaidi za kufikiri na kutafakari mambo, wasiyajibu tu kwa mazoea na kupata alama kubwa za juu ilhali hawafahamu masuala hayo kiundani. Na kukosekana moyo wa kujaribu /na kufanya mambo huwafanya hata wanaojaribu waonekane tofauti na jamii kubwa. Mambo haya yanajitokeza pia kwenye maisha yetu ya kila siku. Hapa naangalia shughuli ya biashara ndogondogo na hata zile za kati zinazofanywa na wananchi wengi hususani katika miji mikubwa nchini.

Vijana wengi wa kitanzania wanafanya shughuli za umachinga; naambiwa machinga moja ya tafsiri zake ni ile ya “marching guys” jamaa watembeao (tafsiri si rasmi). Kwa mtazamo wangu hiki ni kitu muhimu kabisa vijana na ndugu wengine wanaofanya shughuli hizo ni kielelezo tosha kabisa cha ulazima wa kuwa na mitaala ya kufunza ujasiriamali (ujasiri wa kutafuta mali kihalali – tafsiri yangu mwenyewe). Ujuzi wa ujasiriamali na hamu ya kufanya majaribio katika masomo uguse aina zote za masomo yaani ya sayansi, sanaa na kadhalika. Kwa kufanya hivyo utaona kwamba hata machinga wetu watafanya mambo kizalendo tofauti na ilivyo hivi sasa.

Bidhaa za Wajasiriamali - twahitaji kuongeza tu
ubora katika bidhaa zetu na mambo yatakuwa
safi. Picha kwa hisani ya blogu la marchingguys

Wengi wa machinga wa Tanzania kwa hakika ni vibarua wa nchi ya Uchina na nchi nyingi zilizoendelea. Wafanyabiashara wengi wanafanya biashara ya bidhaa zinazotoka nje ya Tanzania. Mfumo wetu wa uchumi, kwa kujua ama kwa kutokujua, umetufanya kuwa soko zuri sana la bidhaa za watu wengine. Fikiri kuhusu vitu ulivyonunua juma hili, bidhaa kumi; pengine sita hadi saba zimetoka nje ya Tanzania, japokuwa zinauzwa na wamachinga wetu ambao kimsingi ni vibarua wa uchina, Afrika Kusini n.k. Serikali ina nia njema sana ya kuwasaidia vijana, ndio maana ikaamua kujenga Machinga Complex pale Ilala. Nimesikia kuna mpango wa kujenga Machinga Complex kadhaa katika mikoa mingine kwa lengo lilelile la kuwakwamua vijana na kina mama. Ukiachia mbali kuhusu ufanisi wa jengo hilo, angalia bidhaa zinazouzwa ndani ya jengo hilo, asilimia kubwa zinatoka Jamhuri ya watu wa Uchina, mita chache toka pale Machinga Complex unakutana na iliyogeuzwa kuwa Dubai ya Tanzania Kariakoo, chunguza bidhaa zinazotoka, Dar es Salaam, Tanga, Iringa, Mwanza, Mbeya, Tabora, Arusha, Kilimanjaro, Mtwara n.k; ni chache mno. Hii ni changamoto kubwa kwa nchi yetu; hizi “Machinga Complexes” zinazowalenga vijana wetu inatakiwa ziuze bidhaa zitokazo Kigoma, Iringa, Ruvuma, Manyara, Mwanza, Shinyanga, Rukwa, Njombe n.k - bidhaa za Tanzania. Tazama hata sekta zingine; usafirishaji: foleni za motokaa kwenye majiji hapa nchini; Dar es Salaam, Mwanza na kwingineko pamoja na magari mengi vile, sina hakika kama kuna moja lililotengenezwa pale Kibaha. Tazama baadhi ya miji yetu ilivyojaa na kuwa jaa la pikipiki, bajaji, baiskeli, hakuna zinazotoka Tanzania, lakini wamachinga na wajasiriamali ni wengi kupindukia, huoni kuwa sisi ni wamachinga wa wachina tu!