Wednesday, September 14, 2011

Clouds Fm hongereni lakini...


Hiki ni kivuko kinachotoka Mtwara kwenda Msanga Mkuu.
Picha inaonekana kwa mbali kiasi; vitu unavyoona vya rangi ya pinki vikipepea ni maboya ya kuokoa maisha. Unaonaje yavaliwe wakati gani?

Kituo cha redio (Mawingu) Clouds Fm cha jijini Dar es Salaam, kimeanzisha mkakati wa kuchangia ununuzi wa maboya ya kuoa maisha-mkakati huo umepewa jina la "OKOA MAISHA"  Maboya hayo "life jackets" hutumika kuokoa maisha ya abiria endapo ajali ya majini itatokea. Maboya hayo huvaliwa na abiria kwenye ndege-ili kwamba chombo hicho kikiangukia majini, husaidia kuoa maisha ya abiria, vazi hilo hutakiwa kuwepo pia kwa chombo chenye kusafirisha abiria majini. Clounds wanapiga la mgambo ili kusaidia wasafiri majini. Kwa hili binafsi nawapongeza sana. Hata hivyo kuna mambo mawili hapa ya kutafakari si tu wa mpiga mwano huu bali ni kwa watanzania wote.

Mosi, binafsi natambua kuwa kwenye ndege maboya hayo, kwa kawaida, huwatosha abiria wote; kila abiria anakuwa na life jacket chini ya kitivchake. Na hivyo kikitokea kile ambacho katu hakitamaniki, bali kila abiria hupata kutumia boya lake. Nimesafiri mara mbili kwa maji toka Dar es Salaam kwenda Zanzibar, binafsi sikumbuki “boya langu” lilikuwa wapi. Kwa kusema hivi sina uhakika je, kila abiria kwenye vyombo vya maji hapa Tanzania, ana uhakika wa kupata boya lake ama, je idadi ya maboya inalingana na idadi ya abiria chomboni?

Swala la pili ni juu ya muda wa kuvaa boya hilo. Nilipokuwa mwanafunzi kule Uganda, nilipata nafasi ya kutembelea wafungwa kwenye gereza lililo kisiwani katika mji wa Jinja. Kwenda gerezani, chuo nilichosoma kiliweka utaratibu wa kila mwanafunzi kuvaa boya lake pale anapokuwa chomboni. Hi ili wanafunzi wasafiri kwa usalama na uhakika zaidi. Tunaweza kuanzisha utaratibu kama huo pia, kila abiria avae boya “life jacket” pale tu anapoingia chomboni. Najua utaratibu huu utazua hofu kwa abiria na wamiliki wa chombo.

Abiria, akivaa boya la kuokoa maisha, atajihisi kama anaingia kwenye ajali moja kwa moja na ataona kama anajiombea dua baya kwa kufanya hivyo. Mmiliki wa chombo atahisi kuwa abiria wataondoka ya maboya yake na safari inayofuata hakutakuwa na boya hata moja. Tukitaka kufanikiwa lazima tubadilishe tamaduni zinazobadilika.

Tuvae maboya mara tunapoanza safari majini; kwa kufanya hivyo ndo tutakuwa tunajali maisha hofu za kimazingaombwe kamwe haziwezi kutusaidia. Mmiliki wa chombo majini, aweke utaratibu wa kukusanya maboya mwisho wa safari; kila aingiaye chomboni apate boya na kila anapotelemka akabidhi, kama hana alipe gharama ya boya hilo hata kama hakuvaa. Kuokoa maisha ni lazima tuwe wabunifu, makini lakini pia wakali kwenye utekelezaji. Utaratibu huu kwa kiasi fulani unafanyika pale kituo cha mabasi, Ubungo, Dar es Salaam.(Kukagua abiria kama wamefunga mikanda)

Mandalu

Uzembe ukipungua ajali pia zitapungua !

Google Image
                                          Inapakiwa hapa https://www.youtube.com/watch?v=MpzE7flW9_A
Wakati tukiendelea na tafakari juu ya ajali ya meli kule Nungwi ni wasaa mwafaka kwa watanzania na wanadamu wote kwa ujumla na hasa wenye kutumia vyombo mbalimbali kusafirisha binadamu wennzao, iwe ni vya ardhini, majini ama angani, kuwa waangalifu zaidi. Ajali ya meli ya abiria LCT Spice Islanders, iliyokuwa ikitoka Unguja kwenda Pemba, imesababisha vifo vya ndugu zetu wengi. Ni msiba mkubwa kuona watu wengi wenye afya njema na ambao ni  nguvu kazi muhimu kwa ujenzi wa Taifa, wakiaga dunia.Tunamwomba Mwenyezi Mungu kwa huruma yake awapokee ndugu hawa kwenye makazi ya kudumu, na wafiwa na wajeruhi wote wapate faraja na kupona haraka! Kutokana na tukio hili serikali na wananchi wote kwa ujumla wetu tunapenda kuona wamiliki vyombo vya kusafirishia abiria, mamlaka za kudhibiti vyombo vya usafiri na wasafiri wenyewe wakiongeza umakini...