Saturday, August 30, 2014

NYAMA CHOMA NA UCHUMI WA TANZANIA



President John Magufuli
PICHA KWA HISANI YA BLOGU WAANDAA TAMASHA
Nyama choma ni chakula cha kitamaduni kwa baadhi ya jamii nyingi barani Afrika na hata duniani. Historia inaonyesha kuwa jamii ama makabila mengi hapo kale ziliishi/yaliishi kwa uwindaji wa wanyama pori. Hivyo nyama choma imekuwa ikiliwa toka enzi za kale barani ila katika baadhi ya jamii tu. Jamii nyingine ziliishi kwa kula mizizi na matunda pori. Wanahistoria wanaweza kutusaidia katika hili, kuibuka kwa shughuli kuu na maalumu kwa jamii mbalimbali zama za hivi karibuni ama nyuma kidogo, kulisababishwa na shughuli zale za uwindaji naukusanyaji mizizi na matunda pori.

Baadhi ya makabila yakawekeza nguvu na muda wao katika uwindaji na baadaye kuwa wafugaji, na mengine katika ukusanyaji mizizi na matunda pori na kisha kuwa wakulima.Na kulikuwa na wavuvi halikadhalika na leo waendelea pia. Kwa hivi basi wawindaji na baadaye wafugaji bila shaka hawa walikuja kuwa wala nyama ila hali wakusanya mizizi na matunda pori baadaye wakawa wakulima wa mazao mbali mbali. Mambo haya yalitokea zama za kale za mawe na chuma. Mawe na baadaye chuma kilikuwa chombo cha kuwindia wanyama na pia zana ya kutifua ardhi na kulimia mashamba. Hayo yalifanyika enzi hizo; hivi leo mambo haya yamebadilika. Siku hizi kila mtu anakula nyama na tena kuna matamasha ya nyama choma. Ila kabla ya matamasha ya nyama choma ya kisasa tuangalie nyama choma za sehemu chache nilizozifahamu miaka ya tisini.

Miaka hiyo nilikuwa mwanafunzi mkoani Iringa. Nilisafiri kwa treni ya kati toka Shinyanga, mara nyingine toka Mwanza hadi Dar es Salaam na mara nyingine nilishukia Dodoma. Toka Dar es Salaam nilipanda basi hadi Iringa, ama nilipanda treni ya Tazara mpaka Makambako na kisha kwenda mjini Mafinga, ambako palikuwa nyumbani kwangu kwa miaka mitano. Safari kwa treni ya Tazara ilikuwa ya kitalii na ya kuvutia, kwani nilipata fursa kuwaona wanyama wengi: swala, twiga, tembo n.k. Ama niliposhuka Dodoma nilikwenda Iringa kwa njia ya “Ny’ang’oro” barabara iliyokuwa na kona nyingi za kutisha na tena njia hiyo ilikuwa ni ya hatari, kwani mara nyingine magogo yaliwekwa njiani na majambazi na kisha abiria kunyang’anywa mali zao baaada ya basi kusimama. Namshukuru Mungu sikuwahi kukutana na dhahama hiyo. Njia hii pamoja na kadhia zake ilinifurahisha kwani nilikuwa na uhakika wa kula samaki watamu pale Mtera. Sijui mambo yanakwendaje huko siku hizi kwani sijafuatilia taarifa za huko na sijapita huko tena miaka mingi sasa.

Toka kanda ya ziwa kwa treni watu wengi tulifurahia ujuzi wa wenyeji wa Saranda wa kuandaa “nyama choma.” Kile kituo cha treni Saranda wengine hupaita “Kilimanjaro Hotel”. Kila zama na kitabu chake, enzi hizo Kilimanjaro Hotel ilikuwa ndiyo Hotel pekee? ya hadhi ya juu zaidi jijini Dar es Salaam na wageni wengi maarufu walifikia pale. Saranda, moja ya vituo vya treni ya kati kilichopo mkoani Singida, ni maarufu mno kwa uuzaji wa kuku wa kienyeji. Hivyo hapo tulikula nyama choma, sikumbuki bei ya kuku wale wasioisha, iwe masika iwe kiangazi bado utawapata. Bei ya kuku wale abiria wengi daraja la tatu tuliimudu, sifahamu abiria waliokuwa mabehewa ya daraja la kwanza na la pili kama wao pia walikula nyama choma ile. Kwa daraja la tatu, sina shaka, naelewa vyema kwani nilishuhudia abiria wengi wakila “nyama choma” ya Saranda. 

Kutoka Iringa Mjini kwenda Mafinga, unapita maeneo mengi kadhaa moja muhimu huwezi kulisahau ni Tanangozi; maarufu kwa nyama choma ya aina yake. Hapa sikupata nafasi ya kula nyama choma ila nafahamu huduma hiyo ilikuwepo. Mjini Dodoma, kule Mnadani kulikuwa na nyama choma za uhakika, sijui siku hizi, tena bei yake ilikuwa rafiki kwani wananchi wa kipato cha kawaida waliimudu. Naambiwa baadhi ya ndugu wabunge walifika kule kupata nyama choma pia. Najua kuna maeneo mengine mengi yaliyokuwa yakitoa huduma hii kwa wahitaji tena kwa bei maridhawa.

Ugumu wa maisha kipimo cha akili ama uvumbuzi mama wa maendeleo, hivi karibuni hususani jijini Dar es Salaam kumeibuka matamasha ya nyama choma. Kama tulivyoona hapo awali hili si jambo jipya na kuliona kama uvumbuzi. Upya wa nyama choma hii ni kule “kusasaishwa” ambapo kuna kuwa na eneo mahususi la kuendesha shughuli hiyo, ndani ya eneo ambamo kuna kuwa na mambo anuwai yakiendelea ikiwa ni pamoja na ajira kadhaa za muda; mama/baba lishe, biashara mbalimbali mfano uuzaji vinywaji, na bidhaa nyingine lukuki. Ili kuingia eneo hilo ni lazima kutoa kiingilio. Nimeona matangazo kiingilio mara nyingine huwa shilingi za Tanzania elfu saba 7,000/= hadi kumi elfu 10,000/=. Kiingilio hicho si tiketi ya kwenda kunufaika na kila huduma kwenye tamasha hilo, muingiaji atalazimika kuendelea kutoa pesa kwaajili ya huduma zingine. Kwa haraka haraka nyama choma hii si kama ile ya Mnadani ama Saranda, hii ni kwaajili ya watu wa tabaka maalumu.

Kwa hakika matamasha ya nyama choma ya namna hii yanawalenga watu wenye ahueni kubwa ya maisha. Ni jambo jema ama jambo baya si lengo la makala hii leo. Hapa najiuliza tu je, hizi ni dalili za kukuwa kwa uchumi wa taifa la Tanzania ambapo wananchi, baadhi yao, wanapata kipato cha matumizi ya ziada, matumizi yasiyo ya lazima? Sera ya maendeleo ya Taifa inalenga kuwa ifikiapo mwaka 2025 jamii ya Tanzania iwe na watu wenye uchumi wa kati. Hii maana yake Mtanzania mmoja anakuwa na uwezo wa kutumia kiasi cha dola za Marekani 5,960, yaani pesa ya Tanzania 9,536,000/= kwa mwaka walau kitakwimu, ama shilingi 26,126/= kwa siku. Kulingana na ripoti ya maendeleo ya binadamu ya shirika la maendeleo la Umoja wa Mataifa ya mwaka 2014 Mtanzania wa leo, kitakwimu, ana uwezo wa kutumia dola za kimarekani 1702, yaani wastani wa pesa ya milioni mbili laki saba ishirini na tatu elfu na mia mbili 2,723,200/= kwa mwaka, ama wastani wa shillingi elfu saba na mia nne na sitini 7,460/= kwa siku. Hii ni kama pato jumla la Taifa litagawanywa kwa kila mmoja wetu. Utagundua kuwa kwa uchumi tulionao hivi sasa kitakwimu yaani kila Mtanzania kuweka mfukoni mwake shillingi 7,460/= tamasha la nyama choma litakosa wateja. Kwahiyo, ni dhahiri kuwa matamasha ya nyama choma ni kwaajili ya watu mahususi. Lakini inawezekana pia kuwa wingi wa matamasha ya nyama choma na maisha ya mtindo huo ni kiashiria cha kukua kwa tabaka la kati katika uchumi wa Tanzania.

Swali hapa ni je uchumi wa Tanzania umekuwa kiasi cha kuwa na matamasha ya nyama choma mengi vile, ila hali uwanja wa mpira wa taifa unaweza kujazwa na watu wenye bahasha za kaki? Je, uchumi wetu umekuwa kiasi cha kutosheleza sherehe kila uchao wakati imani za kishirikina zimetujaa mpaka shingoni? Mauji ya albino yanaendelea kila uchao. Je, hii ni jamii ya watu tusioelimika? Uchumi mkubwa wa wala nyama choma hauwezi kumkata kiungo binadamu mwenzake kwa kisingizio cha kupata mali. Uchumi uliokuwa na kukomaa watu wake hufanya kazi halali kwa bidii zaidi, hulipa kodi, huheshimu tofauti zao na watu wengine katika jamii, hutimiza wajibu wao iwapasavyo na kisha huenda kwenye TAMASHA LA NYAMA CHOMA.


Tuesday, August 12, 2014

Friday, August 1, 2014

The Continent is not short of Heroes!

Dr Sheik Umar Khan
Dr. Sheik Umar Khan (1975-2014) - Photo by BBC

Doctor Sheik Umar Khan (1975-2014) is to Sierra Leone what Doctor Matthew Lukwiya (1957- 2000) is to Uganda

Dr. Matthew Lukwiya (1957-2000) Photo by Wikipedia
"It is our vocation to save life. It involves risk, but when we serve with love, that is when the risk does not matter so much. When we believe our mission is to save lives, we have got to do our work." Dr. Matthew Lukwiya


Dr. Lukwiya and Dr. Khan died while serving their people-treating patients of the EBOLA disease
This is indeed the spirit of "for my people and my country"- let political leaders in Africa take these two men as models and keep the social contract dear in their hearts as they serve their fellow citizens just like these two scientists.