Showing posts with label KIMATAIFA. Show all posts
Showing posts with label KIMATAIFA. Show all posts

Sunday, November 5, 2017

SI MJAMAA, SI BEPARI JE, VIWANDANI TWAENDAJE?


Kila nchi huongozwa na falsafa fulani ili kufikia malengo iliyojiwekea. Tanzania ina dira ya miaka 25 kupitia maono yake ambapo nchi inajielekeza kwenye kundi la nchi zenye uchumi wa kati. Ili kufikia uchumi huo wa kati Tanzania imejiwekea mikakati kadhaa; mmoja kati ya mingi iliyopo ni ule wa ushirikiano baina ya serikali na sekta binafsi. Mwongozo unasema sekta binafsi ndiyo hasa itachukua nafasi kubwa katika kujenga uchumi wa kati; hayo yanapatikana katika Tanzania Development Vision  (TDV) 2025. Naam ni jambo muhimu kwa serikali kushirikiana na sekta binafsi kwani inafaa kuweka nguvu kubwa zaidi ili wananchi wengi waingie katika kundi hili kuzalisha ajira nyingi zaidi.

Hata hivyo ukisoma katiba ya nchi yetu ya mwaka 1977, 3.-(1) inasema nchi yetu ni Jamhuri ya Muungano na ni nchi ya kidemokrasia na ya kijamaa....,. Katiba katika nchi ndiyo hasa sheria kuu kuliko zote. Sasa basi kwa mantiki hiyo Tanzania ni nchi ya kijamaa! Je, kweli Tanzania kwa matendo yake, kwa jinsi inavyofanya mambo yake, kwa jinsi viongozi wake wanavyoishi na kutenda, ni nchi ya kijamaa kweli?

Swali hili na mengi mengine yanajadiliwa kwa undani ndani ya THE HIDDEN WEALTH OF TANZANIA. Kitabu kimeandikwa kwa lungha ya Kiingereza. Hata hivyo kimeandikwa kwa Kiingereza chepesi ambacho kijana aliyemaliza kidato cha nne atamudu kukielewa vyema kabisa. Kitabu kwa kiasi kikubwa kinawalenga wanavyuo, wakufunzi, wanataaluma na mtu yeyote anayependa kujua vyema mambo anuwai juu ya Tanzania. Kitabu hiki kinalenga hasa kuibua mijadala kutokana na hoja zilizomo ndani yake. 

Kwa sasa kitabu hiki kinapatikana katika maduka mbalimbali yaliyopo mitandaoni na pia katika mtandao wa Amazon. Hapo baadaye tutafanya utaratibu kuleta nakala hizo hapa nyumbani Tanzania.
http://www.amazon.com/dp/1978203284
http://www.amazon.co.uk/dp/1978203284
http://www.amazon.de/dp/1978203284
http://www.amazon.es/dp/1978203284
http://www.amazon.fr/dp/1978203284
http://www.amazon.it/dp/1978203284

Sunday, February 5, 2017

AZIMIO LA ARUSHA LINAPOFIKISHA MIAKA 50 : NINI KILISABABISHA KUZALIWA KWAKE?


Hivi leo Azimio la Arusha (AA) limefikisha miaka 50 ama nusu karne tangu kutangazwa kwake.... Tarehe 05.02.1977 ambayo ni miaka hamsini ama nusu karne iliyopita, lilitolewa tamko ama tangazo la kihistoria katika mji wa Arusha. Azimio hilo linaendelea kujulikana kama Azimio la Arusha hata hivi leo.



Lengo la Azimio la Arusha
Kimsingi lilikuwa ni kuboresha maisha ya Watanganyika wanyonge. Azimio la Arusha lililenga kuboresha nyanja zote za maisha ya wananchi wa kawaida lakini hasa ililenga kuboresha nguvu yao kiuchumi na kisiasa. 

Tanganyika ilijipatia uhuru wake wa kisiasa 09.12.1961 bila kufahamu kuwa uhuru wa kiuchumi uliendelea kuwa mikononi mwa wakoloni. Tanganyika ilirithi uchumi wa kibepari, tena ubapari wa kikoloni. Kwa mantiki hiyo utaona kuwa "sisi" tulikuwa na uhuru kisiasa ilihali "wao" walikuwa na uhuru wa kiuchumi.

Uchumi huo wa kibepari wa kikoloni ambao ulikuwa ukiongozwa kwa sheria za soko, ulikuwa kandamizi kwa wananchi wa kawaida. Wananchi waliofanya kazi kwa matajiri wa kigeni na kupangiwa mishahara kwa matakwa ya matajiri hao kabla ya uhuru waliendelea kufanya kazi kwa namna ile ile kama walivyofanya hata kabla ya uhuru wa kisiasa. Wakulima hali kadhalika walijikuta katika mazingira yale yale wakiuza mazao yao kwa mabwana wale wale na kwa bei zile zile za kabla ya uhuru.

Kutoka na uchumi ule wa kibepari, serikali haikuwa na uwezo wa kuingilia masuala ya uchumi huo na hivyo haikuwa rahisi kuwawezesha wananchi kuonja ama kushiriki katika furaha ya matunda ya uhuru. Hivyo basi kama ilitakiwa wananchi waonje ladha ya matunda ya uhuru wao basi ilikuwa lazima kwa TANU kudai ama kuchukua pia uhuru wa kiuchumi na mabadiliko hayo yalikuwa lazima.

Ili kusikiliza kusikiliza wananchi na kuhakikisha kuwa wanahisi faida za uhuru katika nchi yao, ndipo hapo chama cha Tanganyika African National Union kilipofanya maamuzi ya kihistoria.

Chama cha TANU kilitangaza za na historia mpya kabisa katika taifa changa la Tanganyika. Mnamo tarehe tano Februari mwaka elfu moja mia tisa sitini na saba pale mjini Arusha chama kilitangaza rasmi kuwa kuanzia siku hiyo nchi ya Tanganyika ilikuwa inaanza na inaingia katika siasa za ujamaa na kujitegemea.

Siasa ya ujamaa na kujitegemea ilijengwa juu ya nguzo mbili za (i) Utaifishaji wa njia zote kuu za uzalishaji mali na (ii) Vijiji vya ujamaa na kujitegemea kama nguzo muhimu kufikisha maendeleo kwa wananchi wengi.

Nini kilifanyika ndani ya siasa za ujamaa na kujitegemea? Hii ni mada ya wakati mwingine; kwa leo itoshe tu kuona kilichofanyika.

Wednesday, February 3, 2016

THE LIST OF BEST UNIVERSITIES AND COLLEGES IN TANZANIA 2015

STELLA MARIS MTWARA UNIVERSITY COLLEGE - IN THE CITY OF NATURAL GAS
This ranking is based on research publications and citations from the last five years (2010 to 2014) as well as visibility on the internet.
RankInstitutionTotal Influence Factor
1University of Dar Es Salaam28.10
2Sokoine University of Agriculture19.83
3Muhimbili University of Health and Allied Sciences15.22
4Open University of Tanzania10.72
5University of Dodoma9.02
6Tumaini University8.27
7Mzumbe University8.15
8Ardhi University7.50
9St Augustine University of Tanzania5.05
10Kilimanjaro Christian Medical College4.89
11Dar Es Salaam Institute of Technology4.43
12Nelson Mandela African Institute of Science and Technology4.18
13Catholic University of Health and Allied Sciences4.02
14Institute of Finance Management3.96
15Dar es Salaam University College of Education3.83
16Hubert Kairuki Memorial University3.49
17State University of Zanzibar3.24
18University College of Education2.94
19Kilimanjaro Christian Medical University College2.85
20Zanzibar Universitye2.67
21Mkwawa University College of Education2.44
22Weill Bugando University College of Health Sciences2.38
23University of Arusha2.34
24College of Business Education2.33
25Institute of Accountancy2.28
26Ruaha University College2.24
27Jordan University College2.14
28St John's University of Tanzania1.98
29Moshi University College of Cooperative and Business Studies1.85
30Mount Meru University1.79
31Mbeya University of Science and Technology1.77
32Arusha Technical College1.72
33Muslim University of Morogoro1.71
34Teofilo Kisanji University1.68
35St Joseph University in Tanzania1.66
36University of Iringa1.58
37Mwalimu Nyerere Memorial Academy1.53
38Makumira University College1.52
39International Medical and Technological University1.42
40University of Bagamoyo1.28
41Kampala International University Dar es Salaam College1.27
42Sebastian Kolowa Memorial University1.26
43Mwenge University College of Education1.18
44Stefano Moshi Memorial University College0.90
45Stella Maris Mtwara University College0.86
46Eckernforde Tanga University0.84
47Tanzanian Training Centre for International Health0.73
48Tanzania International University0.73
49Josiah Kibira University College0.67
50St Francis University College of Health and Allied Sciences0.63
51Archbishop Mihayo University College of Tabora0.62
52United African University of Tanzania0.56
53Katavi University of Agriculture0.12
54St Joseph's Theological Institute0.05
http://ranking.journalsconsortium.org/unirankings/country/Tanzania/2015

UGANDA WAPIGA HATUA NYINGE ZAIDI...

Basi linalotumia umeme wa nguvu za jua ambalo limedaiwa na watengezaji wake nchini Uganda kuwa la kwanza barani Afrika limeendeshwa hadharani.
Basi hilo la kielektroniki aina ya Kayoola linalomilikiwa na kampuni ya Kiira Motors lilionyeshwa katika uwanja wa Uganda mjini Kampala.
Mojawapo ya betri zake zinaweza kuwekwa chaji na vibamba vya umeme wa jua katika paa la nyumba ambavyo huongeza kasi ya gari hilo hadi kilomita 80 kwa saa.
Watengezaji wake sasa wanalenga kuwavutia wateja wataolitengeza basi hilo ili kuvutia soko kubwa la magari duniani.
Mkurugenzi mkuu wa Kiira Motors Paul Isaac Musasizi ameiambia BBC kwamba amefurahishwa na jaribio la gari hilo lilipoendeshwa.
Raia wamefurahishwa na wazo kwamba Uganda ina uwezo wa kutengeza mfano kama huu na bw. Musasizi anasema kwamba angependelea kulisaidia taifa hilo kushindana na kampuni nyengine za magari katika eneo hili.
Pia anatumai kwamba hatua hiyo itabuni ajira zifikiazo 7000 kufikia mwaka 2018.Hatahivyo mradi huo hauwezi kuanza bila ya usaidizi wa kampuni zinazotengeza vifaa vya magari.
Image captionBasi linalotumia umeme wa jua
Lengo ni kwamba kufikia 2039,kampuni hiyo itakuwa na uwezo wa kutengeza vifaa vya magari na kuviunganisha nchini Uganda bila kutegemea kampuni nyengine .
Basi hilo lenye viti 35 linalenga kufanya kazi katika miji midogo badala ya mji mkuu kutokana na masharti ya umbali linakoweza kusafiri.
Iwapo mabasi hayo yatazalishwa kwa wingi,kila basi litagharimu kiasi cha dola 58,000 ambacho bw,Musaizi anasema ni bei nzuri katika soko lenye ushindani mkubwa.
Kampuni ya Kiira Motors ilianzishwa kutokana na mradi uliofanyika katika chuo kikuu cha Makerere,ambacho ni mmoja wa mmiliki wa hisa katika kampuni hiyo na pia kimenufaika na ufadhili kutoka kwa hazina ya fedha ya serikali.