Showing posts with label Dodoma. Show all posts
Showing posts with label Dodoma. Show all posts

Sunday, November 5, 2017

SI MJAMAA, SI BEPARI JE, VIWANDANI TWAENDAJE?


Kila nchi huongozwa na falsafa fulani ili kufikia malengo iliyojiwekea. Tanzania ina dira ya miaka 25 kupitia maono yake ambapo nchi inajielekeza kwenye kundi la nchi zenye uchumi wa kati. Ili kufikia uchumi huo wa kati Tanzania imejiwekea mikakati kadhaa; mmoja kati ya mingi iliyopo ni ule wa ushirikiano baina ya serikali na sekta binafsi. Mwongozo unasema sekta binafsi ndiyo hasa itachukua nafasi kubwa katika kujenga uchumi wa kati; hayo yanapatikana katika Tanzania Development Vision  (TDV) 2025. Naam ni jambo muhimu kwa serikali kushirikiana na sekta binafsi kwani inafaa kuweka nguvu kubwa zaidi ili wananchi wengi waingie katika kundi hili kuzalisha ajira nyingi zaidi.

Hata hivyo ukisoma katiba ya nchi yetu ya mwaka 1977, 3.-(1) inasema nchi yetu ni Jamhuri ya Muungano na ni nchi ya kidemokrasia na ya kijamaa....,. Katiba katika nchi ndiyo hasa sheria kuu kuliko zote. Sasa basi kwa mantiki hiyo Tanzania ni nchi ya kijamaa! Je, kweli Tanzania kwa matendo yake, kwa jinsi inavyofanya mambo yake, kwa jinsi viongozi wake wanavyoishi na kutenda, ni nchi ya kijamaa kweli?

Swali hili na mengi mengine yanajadiliwa kwa undani ndani ya THE HIDDEN WEALTH OF TANZANIA. Kitabu kimeandikwa kwa lungha ya Kiingereza. Hata hivyo kimeandikwa kwa Kiingereza chepesi ambacho kijana aliyemaliza kidato cha nne atamudu kukielewa vyema kabisa. Kitabu kwa kiasi kikubwa kinawalenga wanavyuo, wakufunzi, wanataaluma na mtu yeyote anayependa kujua vyema mambo anuwai juu ya Tanzania. Kitabu hiki kinalenga hasa kuibua mijadala kutokana na hoja zilizomo ndani yake. 

Kwa sasa kitabu hiki kinapatikana katika maduka mbalimbali yaliyopo mitandaoni na pia katika mtandao wa Amazon. Hapo baadaye tutafanya utaratibu kuleta nakala hizo hapa nyumbani Tanzania.
http://www.amazon.com/dp/1978203284
http://www.amazon.co.uk/dp/1978203284
http://www.amazon.de/dp/1978203284
http://www.amazon.es/dp/1978203284
http://www.amazon.fr/dp/1978203284
http://www.amazon.it/dp/1978203284

Monday, August 6, 2012

Wabunge ‘wala’ rushwa marufuku kuingia China

Bunge la Tanzania Mjini Dodoma















Tumeambiwa na tunafahamu siku zote kuwa rushwa ni adui wa haki, na ni ya wananchi, ya binadamu, ama ya viumbe vilivyo hai walau kulingana  na miongozo na makubaliano yetu. Moja ya makubaliano hayo, kwa Tanzania ni kuwa rushwa ni adui wa haki, na kwenye kanuni/ ahadi za mwanaTANU (chama kilichopigania uhuru wa Tanganyika) kulikuwa na ahadi ya kutotoa na kutopokea rushwa kwani hupinga ama huzuia watu wengine kupata haki zao.

Katika nchi nyingi duniani, Tanzania ikiwa mojawapo, kuna utaratibu wa kuwa na chombo cha kutolea mawazo, kuihoji serikali iliyo madarakani, kutunga sheria n.k. Chombo hicho kinafanya kazi kwa uwakilishi; si rahisi kwa mwananchi mmoja mmoja kuingia katika chombo hiko kutetea, kudai haki yake ama/ na kufanya shughuli zingine za chombo hicho ambazo kwetu kinajulikana kwa jina la BUNGE. Kwa kuwa si rahisi wote kuingia basi tumelazimika kuwa na wawakilishi wachache ili wawe SAUTI zetu na waseme na kutenda kwa niaba yetu. Hivi karibuni tumesikia habari ya kushangaza juu ya hawa wawakilishi wetu. Tumesoma na kusikia vyombo vya habari vikielezea juu ya baadhi ya wawakilishi wetu hawa wakifanya kile tulichofundishwa kuwa ni adui wa haki, sio lengo la makala hii kuongelea suala hilo bali tu kuiwasilisha makala iliyo katika gazeti la MTANZANIA inayoeleza juu ya kicha habari.   

Mwalimu JKNyerere aliwahi kusema IKULU ni patakatifu nadhani BUGENI halikadhalika ni vivyo hivyo. Je, kama kweli kuna wabunge wameenda kinyume na utakatifu inafaa kweli waendelee kuwepo patakatifu?

Na Arodia Peter .

TUHUMA za rushwa zinazoendelea kuwaandama wabunge, zimechukua sura mpya, baada ya Serikali ya China kujiandaa kupiga marufuku wabunge wote wanaotuhumiwa kujihusisha na rushwa kuingia nchini humo.

Habari za uhakika ambazo MTANZANIA imezipata kutoka ubalozi wa China hapa nchini, zinasema umepokea taarifa rasmi kutoka kwa viongozi wakuu wa China, wafuatilie kwa karibu wabunge wote wanaotuhumiwa kwa rushwa, kisha watume taarifa ili wakibainika wasiingie kwenye nchi hiyo.
“Tumeletewa taarifa na viongozi wetu wa ngazi za juu, kuwa tufuatilie kwa kina wabunge wote ambao wanatuhumiwa na wakibainika majina yao yatumwe China, ili wazuiliwe kuingia kule,

…unajua taifa letu ni taifa ambao halina mchezo na mtu anayepokea rushwa ovyo ovyo na ni kosa la jina. kwa kiongozi kama hawa wabunge kujihusisha na siasa,

“Kwa kipindi chote hiki, kama wabunge hawa wangekuwa China leo hii, tungekuwa tunazungumza mambo mengine, wangekuwa wamechukuliwa hatua kali,

“Tunashangaa kuona kwa nini hapa kwenu, bado wanaendelea kuruhusiwa kuingia bungeni… au wanasubiri majibu ya kamati ndogo iliyoundwa kuchunguza tuhuma hizi,” kilihoji chanzo chetu.

Chanzo hicho, kilisema ubalozi wa China hapa nchini, umetuma maofisa wake mjini Dodoma kwa ajili ya kupata mwenendo wa wabunge wote wanatuhumiwa.

“Hivi sasa hapa Dodoma kuna maofisa wa ubalozi wa China, wanaendesha uchunguzi kuhusu tuhuma hizi, ikibainika ni za kweli baada ya majina ya wabunge ‘wala rushwa’ kutajwa, watachukua picha zao kwa ajili ya kuzituma China, ambako hawataruhusiwa kukanyaga kwa sababu kwao rushwa ni kosa la jinai,” kilisema chanzo chetu.

Naye Mratibu wa maombi yanayoendeshwa na Umoja wa Makanisa ya Kikristo Tanzania, mjini Dodoma Mchungaji William Mwamalanga alisema kwa kauli moja viongozi wa dini, wamesikitishwa na tuhuma hizo.

Alisema viongozi wa dini ambao wamepiga kambi mkoani Dodoma, kwa ajili ya kuliombea taifa, wamewataka wabunge wote waliotajwa wajiuzulu mara moja.

“Viongozi wa madhehebu mbalimbali tupo hapa Dodoma, kwa ajili ya kuliombea taifa, lakini moja ya jambo kubwa ambalo tumekubaliana kupita katika majimbo yao, kueleza waumini wetu matatizo haya ya rushwa… tunataka wajiuzulu kwa ajili ya kulinda heshima zao,