Tuesday, October 9, 2018

TAKE THE STAIRS - PANDA NGAZI



Success is never owned, it is only rented and the rent is due every day". 

Kitabu rejea;TAKE THE STAIRS (7 steps to achieving true success).By Rory Vaden.

Katika maisha yetu wanadamu kila mtu huwa anapenda kufanikiwa kwenye maeneo mbalimbali ikiwa ni kwenye biashara,taaluma,ama ujuzi alionao.Ila watu wanashindwa kufahamau njia bora za kufikia mafanikio yatakayowapa raha na furaha ya kudumu.Mafanikio yoyote yanapatikana kwa hatua na si jambo lijalo kwa ghafla tu,na tatizo linalowamaliza watu ni kuishi kwa kudhani mafanikio unaweza yafikia kwa mfano wa kupanda lift ya ghorofa na punde ukajikuta umeshafika ghorofa ya tano,lakini mafanikio hayapo hivo,mtu yeyote ukitaka kufanikiwa ni lazima upande ngazi(hatua) ili uende hatua kwa hatua,labda jiulize swali dogo tu je, upandapo lift katika ghorofa mwili wako huwa unapata faida ipi? ,hebu mtazame mtu apandae ghorofa kwa kutumia ngazi,mtu huyu hupata faida nyingi ,kwanza mwili wake unapotoa jasho huujenga na kupunguza sukari isiyotakiwa mwilini  na faida nyingine kadha wa kadha.Huu ni mfano tu wa ngazi za kupanda katika jengo,basi ndivyo yalivyo na mafanikio  ya mtu huwa yanahitaji kuyaendea kwa kufuata hatua ili uweze kuwa na uchungu nayo pale ukishayapata,jitoe mapema kwenye ESCALATOR MENTALITY ili usizidi kuupoteza muda.

Mafanikio ya mtu yeyote yanajengwa kwa mtu kuwa na nidhamu kubwa na si kwa njia za mikato kama watu wadhaniavyo.Kuwa na nidhamu binafsi (self discipline) si jambo jepesi hata kidogo,uonapo watu wamefanikiwa jua kwamba walitengeneza nidhamu zao binafsi,hawakungoja kusukumwa sukumwa katika kutenda yale wapendayo kuyatenda na ndipo walijikuta wakifika kule walipotamani kufika.Mpendwa msomaji nikuambie tu wazi,utakapo amua leo kujijengea nidhamu binafsi jua si jambo ambalo utalipata kwa wakati mfupi na pia hutalipata kwa gharama ndogo,jipange kujitoa kwelikweli ili ujijengee nidhamu binafsi katika kazi yako,biashara yako,kipaji chako n.k.

Pia watu wengi hupenda na hutamani kufikia hatua kubwa za mafanikio lakini sumu kubwa inayowamaliza ni tabia ya kupenda kuhairisha mambo.Unakuta mtu anatamani kuwa mfanyabiashara mkubwa lakini kila siku husema nitaanza kesho Mwandishi mmoja alisema "successful people form the habit of doing things that failures don't like doing".Na hivi ndivyo watu wakubwa wanavyofanikiwa ni kwa sababu hawaghairishi mambo na nidhamu zao za hali ya juu ndizo zinazowasaidia kuviishi  viapo vyao.

Lakini pia watu hudhani watu waliofanikiwa walikutana utajiri wa kifedha,kuwa na biashara kubwa,ama ubobezi katika fani fulani kwa siku moja,lakini si kweli,ukirudi na kufuatilia watu wote waliofanikiwa walipita maisha ya kufanya mambo madogo madogo yaliyo na tija katika maisha yao na baadaye wakajikuta yakiwaletea matokeo makubwa(small choices yield big results),anza kujijengea nidhamu katika mambo madogo madogo nawe utajishuhudia ukipiga hatua siku baada ya siku.

Ukiwa na nidhamu maishani utaishi maisha unayoyapenda ikiwa ni katika biashara yako,katika kazi yako au ujuzi wako na maisha hayo ya furaha hayatakuwa ya muda bali  yatakuwa ni ya kudumu maishani mwako,kumbuka kuwa mafanikio hayana umiliki wa kudumu ni kama kitu kilichokodishwa tu na gharama yake ya kulipia ni nidhamu.Ikiwa unataka uwe na afya bora lazima uwe na nidhamu katika ulaji wako,ukiwa unataka mafanikio ya kibiashara ni lazima uwe na nidhamu katika biashara yako,ukiwa unataka ndoa yako iwe yenye furaha lazima uwe na nidhamu katika ndoa yako n.k.

Nenda kafanyie kazi haya machache niliyokushirisha ukilianza vyema juma hili la 41 katika mwaka wetu 2018,na nitaendelea kukushirikisha hatua 7 saba muhimu za kufikia mafanikio yoyote makubwa,njia hizi amezielezea vyema mwandishi Rory Vaden.Nikutakie heri wewe unaeenda kuchukua hatua ya kuyafanyia kazi yale ambayo umejifunza.

Na mwanafunzi wa kudumu wa shule ya maisha, Mchambuzi wa vitabu na Mshairi;
Marko Kinyafu.
+255 714 129 520.
Dar es salaam,Tanzania.

Kupata maarifa ni bure ila kulipa gharama ya ujinga ni kazi kubwa kuliko gharama unayoikimbia sasa ya kupata kile kilichobora kwa ukombozi wa fikra zako.


No comments:

Post a Comment