Sunday, November 5, 2017

SI MJAMAA, SI BEPARI JE, VIWANDANI TWAENDAJE?


Kila nchi huongozwa na falsafa fulani ili kufikia malengo iliyojiwekea. Tanzania ina dira ya miaka 25 kupitia maono yake ambapo nchi inajielekeza kwenye kundi la nchi zenye uchumi wa kati. Ili kufikia uchumi huo wa kati Tanzania imejiwekea mikakati kadhaa; mmoja kati ya mingi iliyopo ni ule wa ushirikiano baina ya serikali na sekta binafsi. Mwongozo unasema sekta binafsi ndiyo hasa itachukua nafasi kubwa katika kujenga uchumi wa kati; hayo yanapatikana katika Tanzania Development Vision  (TDV) 2025. Naam ni jambo muhimu kwa serikali kushirikiana na sekta binafsi kwani inafaa kuweka nguvu kubwa zaidi ili wananchi wengi waingie katika kundi hili kuzalisha ajira nyingi zaidi.

Hata hivyo ukisoma katiba ya nchi yetu ya mwaka 1977, 3.-(1) inasema nchi yetu ni Jamhuri ya Muungano na ni nchi ya kidemokrasia na ya kijamaa....,. Katiba katika nchi ndiyo hasa sheria kuu kuliko zote. Sasa basi kwa mantiki hiyo Tanzania ni nchi ya kijamaa! Je, kweli Tanzania kwa matendo yake, kwa jinsi inavyofanya mambo yake, kwa jinsi viongozi wake wanavyoishi na kutenda, ni nchi ya kijamaa kweli?

Swali hili na mengi mengine yanajadiliwa kwa undani ndani ya THE HIDDEN WEALTH OF TANZANIA. Kitabu kimeandikwa kwa lungha ya Kiingereza. Hata hivyo kimeandikwa kwa Kiingereza chepesi ambacho kijana aliyemaliza kidato cha nne atamudu kukielewa vyema kabisa. Kitabu kwa kiasi kikubwa kinawalenga wanavyuo, wakufunzi, wanataaluma na mtu yeyote anayependa kujua vyema mambo anuwai juu ya Tanzania. Kitabu hiki kinalenga hasa kuibua mijadala kutokana na hoja zilizomo ndani yake. 

Kwa sasa kitabu hiki kinapatikana katika maduka mbalimbali yaliyopo mitandaoni na pia katika mtandao wa Amazon. Hapo baadaye tutafanya utaratibu kuleta nakala hizo hapa nyumbani Tanzania.
http://www.amazon.com/dp/1978203284
http://www.amazon.co.uk/dp/1978203284
http://www.amazon.de/dp/1978203284
http://www.amazon.es/dp/1978203284
http://www.amazon.fr/dp/1978203284
http://www.amazon.it/dp/1978203284

No comments:

Post a Comment