Tuesday, November 24, 2015

MAGUFULI KURUDISHA "KATIBA YA WARIOBA?"


Ndugu John Pombe Magufuli
 Majuma machache tu toka kupata mkataba toka kwa wananchi wa Tanzania kuiongoza nchi hiyo kwa kipindi cha miaka mitano, na ikiwa ni muda mfupi tu kisha kuapishwa kwake kuwatumikia wananchi, ndugu John Pombe Joseph Magufuli amefanya mambo kadhaa tofauti na ilivyokuwa imezoeleka huko nyuma.

Alichofanya ndugu JPJ Magufuli hakikinzani na katiba ya Jamhuri ya Muungano, na zaidi si kinyume na asili ya ubinadamu na kanuni za kimaumbile kwani hata Heraclitus mwanafalsafa wa kale wa Ugiriki anasema hakuna jambo la kudumu ila mabadiliko. Kwahiyo alichofanya kinaendena na kanuni za kifalsafa, ubinadamu na kanuni za kimaumbile; kila binadamu ni tofauti na wa kipekee mno na hivyo kila binadamu ana uwezo wa kufanya mambo ya kipekee na tofauti na wengine wote, hiyo ndiyo hulka sahihi ya binadamu anapokuwa na nafasi ya kujitawala.

Pamoja na mambo mengine aliyoyafanya ndugu rais, hapa hatulengi kuyaorodhesha, kusitisha safari ambazo hazina ulazima wala faida kubwa kwa taifa kwa viongozi wa serikali, kufanya mabadiliko ya matumizi ya pesa iliyokuwa imetengwa kwa sherehe za kuwapongeza wabunge na kwa kuzinduliwa rasmi kwa bunge la Tanzania. Mambo yote haya yanalenga kuongeza nidhamu ya matumizi ya pesa; hii ni stadi muhimu ambayo kila mmoja wetu inafaa ajifunze. Aidha kusitisha shamrashamra zilizozoeleka za 09/12 na badala yake kusheherekea siku hiyo ya uhuru wa Tanganyika kwa kushiriki kufanya usafi maeneo mbali mbali tunayoishi na kufanyia kazi ni jambo jema hasa. Ni dhahiri kuwa kipindu pindu hakitakwisha kwa usafi huo wa siku moja lakini agizo hilo limelenga mbali zaidi. Agizo hilo la ndugu rais linalenga mabadiliko ya tabia: jambo muhimu kwa mafanikio maishani.

Kasi ya utendaji kazi aliyoanza nayo rais Magufuli inapendeza na bila shaka tutarajie mabadiliko zaidi. Hata hivyo analazimika kuwa makini zaidi atakapokuwa “akifanya usajiri wa baraza lake la mawaziri” kwa lugha ya kisoka zaidi timu yake inafaa kuwa na wachezaji wenye viwango vya juu na wenye sifa mithili ya wachezaji wa kulipwa kama ilivyo kwa Samatta na Ulimwengu kwa TP Mazembe, Maguli kwa Stand Utd, Bocco kwa Azam, Martial, Roney kwa Man Utd, Ronaldo kwa Real Madrid, Messi, Neymar na Suarez kwa Barcelona na kadhalika na kadhalika.

Wakati wapenda maendeleo wengi wanaendelea kufurahia hatua za uchapakazi ndugu rais na hivyo kutoa pongezi kemkem kwake, nasi pia twaungana nao kumtia shime zaidi ndugu John Magufuli aendelee kufanya vyema na tunamuombea kwa Mwenyezi Mungu amlinde na kumuongoza zaidi. Hata hivyo tufahamu kuwa ndugu rais anatimiza wajibu wake kama kiongozi mkuu wa nchi mithili ya baba anayewajibika vyema kwa familia yake. Baba anayelipa ada kuwasomesha watoto wake katika shule ya viwango vya juu, anapotoa mahitaji stahiki kwa familia yake na kadhalika hapewi sifa na wala hapaswi kujisifu kwa vile anatimiza wajibu wake impasavyo. Pengine mazoea ya kuona baba wa jirani akikosa kuwajibika impasavyo kwa familia yake ndicho kinachosababisha kuona kuwa baba mtimiza wajibu anafanya mambo yasiyokuwa ya kawaida. Hivyo tufahamu na tumpatie ushirikiano ndugu rais aendelee kutimiza wajibu wake vizuri zaidi na zaidi.
Jaji Mstaafu Warioba
Wito wetu katika Makala hii/haya kwa rais Magufuli ni juu ya ama kujenga ama kuimarisha taasisi zetu. Taasisi zetu za uongozi inafaa ziwe imara na zenye mamlaka yaliyojitosheleza, zikiwa imara basi kiongozi yeyote akipata mkataba kuongoza nchi atalazimika kufanya kazi vizuri ama kwa utashi wake ama kwa kulazimishwa na taasisi hizo. Bila kuwa na taasisi imara utendaji kazi na uongozi utategemea hisani na hulka ya kiongozi aingiaye madarakani. Kiongozi mchapakazi na mzalendo “akiukwaa” mkataba kuongoza nchi mambo yatakwenda vyema na wanachi tutaona kama tunafanyiwa hisani ila hali akiingia kiongozi mwenye uzalendo hafifu na mwenyekujipenda yeye mwenyewe zaidi basi katika nchi tutashuhudia madudu. Hivyo basi ili tuepuke kucheza bahati nasibu ya uongozi ni vyema basi tukawa na taasisi imara. Taasisi hizo imara tunaweza kuzipata kwenye mabadiliko ya katiba yenye kushirikisha na kukubaliwa na wananchi walio wengi.


Bahati njema mabadiliko ya katiba yanayokubaliwa na wananchi tunayo kwenye chapisho la ‘katiba ya Warioba.’ Hivyo basi ndugu rais tunakuomba uturejeshee “katiba ya Warioba” ambayo itatufaa sana kwa dira ya taifa letu kwa miaka mingi ijayo.

Monday, November 23, 2015

FURSA KWA VIJANA KUSAFIRI NA KUJIFUNZA NCHINI AFRIKA KUSINI



Warsha kwa vijana wa kati ya miaka 18 - 25 itafanyika huko nchini Afrika Kusini mwezi September 2016. Ili kushiriki kijana anatakiwa kujaza fomu ya maombi mtandaoni mapema na mwisho ni tarehe 4 Desemba 2015


Calling Young Leaders in Conservation and Animal Protection: Ages 18-25

In September 2016, the first Youth Forum for People and Wildlife will take place in Johannesburg, South Africa. Twenty young leaders working in animal and conservation-related fields from around the world will connect with experts, explore solutions, and build skills that will help them better understand wildlife conservation issues from multiple perspectives and empower them to become compassionate conservationists. Travel and participation costs covered.

Friday, November 20, 2015

WANASIASA KAMA WANANDOA!!!

Image by google
Makundi haya mawili yote hula kiapo cha utii na uaminifu mbele za watu na Mungu lakini bado wanachakachua!!!

WANANDOA:
Image by google

Watu wawili kwa kawaida mtu mme na mtu mke wanapopendana na kukubaliana kuishi pamoja hulazimika kuweka wazi suala hilo mbele ya umma wa wanajamii wanaoishi nao. Kwa kawaida watu hawa hula kiapo, huwekeana ahadi kuwa watakuwa waaminifu baina yao na kawaida huomba msaada wa Mungu awawezeshe kuwa waaminifu katika kiapo chao. Hufanya hivyo na kuahidi kuwa wavumilifu katika jua na mvua, afya na ugonjwa, mali na kutokuwa na mali hadi hapo kifo kitakapowatenganisha.

Hapa hatutaki kuangalia kama watu wetu wanakuwa kweli wameandaliwa na kama wanajua nini maana ya kuishi katika ndoa. Bila shaka suala hili tutalijadili mara nyingine kwa marefu na mapana yake stahiki.

WANASIASA:

Watu waume na wake walioamua kuingia kwenye shuguli za kisiasa hulazimika, kama ilivyo kwa wanandoa, kula kiapo na kuahidi kulinda na kutumikia kwa lengo la kuboresha maisha ya watu wetu. Wanasiasa pia husikika wakisema na tena kwa kutumia vitabu vitakatifu kuwa kwa akili zao timamu watailinda katiba ya Jamhuri ya Muungano na kuwa wanaomba Mungu awasaidie katika utekelezaji huo.
Image by google

Kwa upande wa siasa nafahamu pia kuwa si wanasiasa wote wanaofahamu uzito na umuhimu wa kazi hii ya kitumishi. Kama asemavyo mwanafalsafa nguli John Locke kwamba mwanasiasa mzuri ni yule anayefahamu moyoni mwake kuwa kazi hiyo ni mkataba baina ya mwanasiasa na wananchi.

MADUDU

Pamoja na kula viapo wanandoa huvikiuka viapo vyao na kuvunja ahadi zao za ndoa na kuanzisha nyumba ndogo ambazo ni kinyume na ahadi zao za ndoa. Kama ilivyo kwa wanandoa, wanasiasa wetu wengi pia hukiuka na kuvunja ahadi na viapo vyao kwa kuchakachua rasilimali zetu na kushiriki kwenye ufisadi na wizi mkubwa mkubwa tu. Mfano wa uchakachuzi hapa ni pamoja na kushiriki katika ESCROW, EPA, RICHMOND na wizi mwingi unaowakesesha wananchi haki zao. Hivyo basi wanasiasa na wanandoa wote kwa nafasi zao hufanya madudu na kukiuka viapo vyao.

Thursday, November 19, 2015

German Universities Now All Free of Tuition Fees - Vyuo Vikuu Vyote Ujeruman Hakuna Ada sasa

Reichtag
Universities in Germany are now free of tuition fees for all including international students. Yesterday, Lower Saxony became the last of seven German states to abolish their tuition fees, which were already extremely low.
German universities had been charging for tuition since 2006. The measure proved unpopular, and German states began dropping them one by one. It is now all gone throughout the country, even for foreigners.
This means that now, both domestic and international undergraduate students at public universities in Germany are able to study in Germany for free, with just a small fee to cover administration– usually between €150 and €250 (US$170-280)  – and other living expenses costs per semester (food, transport, accommodation, entertainment, course materials and other necessities).
Germans barely had to pay for undergraduate study even before tuition fees were abolished. Semester fees averaged around €500 ($630). It is now gone.
Free education is a concept that is embraced in most of Europe with notable exceptions like the U.K., where the government voted to lift the cap on university fees in 2010, and tripled the tuition fees therefore. The measure has reportedly cost more money than it brought in. The Guardian reported last March that students are failing to pay back student loans.
Maybe for now, learning German might be the best financial choice an high school student can make.
Move to Germany with a student visa by using the step by step virtual assistant to the German student visa or reading about visa for international student in Germany on migreat.com.
Read more about Scholarships for Filipinos in Germany // Scholarships Para sa Mga Filipino sa Germany
Got questions about studying in Germany? Ask Migreat Communities in Germany.

TANZANIA YETU YA FURAHA - Atomic Jazz Band

Picha kwa hisani ya Google

Tanzania ni nchi ya aina yake na tuna wajibu wa kuifanya isonge mbele hasa. Atomic Jazz Band walifanya kazi hiyo vizuri kwa kutunga wimbo unaodumu daima. Wimbo wao utuhamasishe tutumie vyema vipaji vyetu ili tuijenge nchi hii.

Monday, November 16, 2015

A Nigerian Scholar Solves 156-Year-Old Mathematics Puzzle

Image courtesy of google
In what can be regarded as a rare achievement and possible entry in Guinness world of records, a Nigerian scholar, Dr Opeyemi Enoch, has successfully solved the 156 -year- old Riemann Hypothesis, the most important problem in Mathematics.
With this breakthrough, Dr Enoch, who teaches at the Federal University, Oye Ekiti (FUOYE), has become the fourth egghead to resolve one of the seven Millennium Problems in Mathematics.
The Kogi State-born mathematician had, before now, worked on mathematical models and structures for generating electricity from sound, thunder and Oceanic bodies.
A statement in Ado Ekiti, the Ekiti State capital yesterday, said Dr Enoch presentation of the Proof on November 11, 2015 during the International Conference on Mathematics and Computer Science in Vienna, Austria becomes more symbolic coming on the exact day and month 156 years after the problem was delivered by a German Mathematician in 1859.
The Riemann Zeta Hypothesis is one of the seven Millennium problems set forth by the Clay Mathematics Institute with a million Dollar reward for each solved problem for the past 16 years.
The statement reads in part, "Dr Enoch first investigated and then established the claims of Riemann. He went on to consider and to correct the misconceptions that were communicated by Mathematicians in the past generations, thus paving way for his solutions and proofs to be established.
"He also showed how other problems of this kind can be formulated and obtained the matrix that Hilbert and Poly predicted will give these undiscovered solutions. He revealed how these solutions are applicable in cryptography, quantum information science and in quantum computers."
Three of the problems had been solved and the prizes given to the winners. This makes it the fourth to be solved of all the seven problems.
Dr Enoch had previously designed a prototype of a silo for peasant farmers and also discovered a scientific technique for detecting and tracking someone on an evil mission.
Enoch has succeeded in inventing methods by which oil pipelines can be protected from vandalism and he is currently working on Mathematical approaches to Climate Change.
The home link to this story: http://allafrica.com/stories/201511160834.html?utm_campaign=trueAnthem:+Trending+Content&utm_content=564a324004d301547840c792&utm_medium=trueAnthem&utm_source=twitter

Saturday, November 14, 2015

What a Talent! Andrea Bocelli

Pourqoui Paris, Why Paris, Kwanini Paris?

Crowds in Paris
Picha kwa hisani ya BBC
Mwezi Januari mwaka huu 2015, dunia ishuhudia mauji ya wafanyakazi wa jarida la Charlie Hebdo jjijni Paris. Ufaransa na nchi nyingi za magharibi waliyaita mashambulizi hayo kama ni mbinu kuzuia uhuru wa kujieleza. Msingi ambao nchi nyingi zilizoendelea zinaona ni haki muhimu mno kwa binadamu na ambayo katu hakuna taifa lililostaarabika litakubali kuiacha haki hiyo ipotee. Hivyo nchi hizo hujinasibu kuwa zipo tayari kutumia gharama kubwa kutetea haki hiyo; ila tusisahau kuwa haki inafaa iendane na wajibu pia. Watu wengi tuliunga mkono wa wale ndugu wa lile jarida kwa maneno ya kifaransa #jesuisCharlie" kuwa mi ni Charlie ama nawaunga mkono wafanyakazi wa Charlie Hebdo.

Wakati Ufaransa na dunia kwa ujumla inaanza kusahau habari za mauji ya wafanyakazi wa Charlie Hebdo. Jiji lile lile la Paris linakutana na mashambulizi mauaji makubwa na ya kutisha mno ndani ya miezi kumi tu toka tukio la mwisho, ukiachia majaribio ya mashambulizi yaliyozimwa kwenye treni miezi ya hivi karibuni. Mashambulizi haya yameacha zaidi ya watu 120 waliopoteza maisha na mamia wengine wengi waliojeruhiwa.

media
Picha kwa hisani ya RFI
Ni dhahiri kuwa mauaji haya yanaacha maswali mengi kuliko majibu kwa sasa. Uchunguzi ukikamilika bila shaka tutafahamu vyema kuhusiana na mauaji hayo. Moja ya maswali yanayojitokeza ni kwanini ushambuliwe mji wa Paris? Kwanini Paris? Itafaa siku za usoni tuangalie watu na mfumo wa maisha ya Paris; linalosemekana kuwa moja kati ya majiji ya starehe zaidi duniani. Bila shaka Ufaransa itatumia uwezo na rasilimali zinazohitajika kupata kufahamu mengi zaidi juu ya hili na kuimarisha usalama duniani.

Kwa sasa tunasema poleni sana wakazi wa Paris na nchi ya ufaransa kwa ujumla. roho za marehemu waliofariki dunia wapumzike kwa amani, amina.

Saturday, November 7, 2015

Jina la Uwaridi - The Name of The Rose - Le Nom de la Rose






The Name of The Rose (Kiingereza), ll Nome Della Rosa(Kiitaliana), Der Name der Rose(Kijerumani), Le Nom de la Rose (Kifaransa) Jina la Waridi : Filamu nzuri mno. Filamu iliyoandaliwa toka kwenye kitabu tajwa hapo juu kilichoandikwa na mwandishi muitaliana Umberto Eco. Kitabu chake kinaeleza mambo anuwai ikiwa ni pamoja na namna ya kufumbua tatizo lililoigubika monastery moja ya wafransikani. Ndugu mdogo William wa Baskerville akisadia na mnovisi wake Christian Slater anasaidia kutoa ufumbuzi wa tatizo hilo kitaaluma, kiteolojia, kifalsafa. Anatumia mbinu za Aristotle, mafundisho ya kiteolojia ya Thomas wa Akwino na uwezo wake wa kiakili. Kwa hakika ni filamu nzuri mno. Wakati watengeneza filamu wetu wanaendelea kufanya kazi mbali mbali na kuandaa filamu wajifunze toka kwenye filamu nzuri kama hii. 



The Land of Riches and Opportunities


Image by google

Tanzania is a land of riches and indeed many opportunities and yet the country is counted among poor countries of the world. Tanzania is the home of the roof of the continent; mount Kilimanjaro, the country houses one of the world's natural wonders of Serengeti, Ngorongoro Crater, the beautiful islands of Zanzibar to mention but just a few... and Knud Vilby in his book  'Independent? Tanzania's challenges since Uhuru' writes on...

Image by the courtesy of google
"Tanzania is one of the most peaceful, stable and democratic countries in Africa. Nevertheless, the country faces almost insoluble problems. The African continent is one of a huge variety of difficulties and potentials. The problems of Tanzania tell us something about the huge challenges facing many other countries in the continent..."
e
o


Ngorongoro Crater
Part of the Zanzibar island

Nini Muhimu Zaidi Uchaguzi Mkuu?



Tunapoelekea uchaguzi mkuu wa viongozi wa nchi yetu kuna mambo ambayo inafaa wanasiasa na wapiga kura tuyazingatie. Kuna maswali tunayopaswa kujiuliza:
1. Kwanini takwimu zinaonyesha uchumi unakuwa lakini bado kuna umasikini?
2. Vyama vituambie vitatumia mfumo upi wa uzalishaji mali? Je, ni ujamaa na kujitegemea,      Ubepari, Ubepari uchwara, ama mfumo upi?
3. Kuna jitihada zipi kupunguza kwa dhati umasikini mkubwa wa vijijini? (NBS 2012) inasema zaidi ya asilimia 70 ya watu wanaishi vijijini na kuwa karibu asilimia 90 ya watu hao ni masikini.
4. Miundo mbinu mibovu inatukosesha mapato mengi
    - Barabara vijijini mbovu hivyo usafirishaji mazao kupeleka sokoni inakuwa taabu
    - Reli ziboreshwe na kusafirisha mizigo mizito ili barabara zidumu muda mrefu na kupunguza ajali
5.Bandari ziboreshwe zaidi kupata biashara za nchi jirani
6. Elimu na wazazi wote wawasaidie vijana wetu kuongeza uthubutu, waongeze moyo wa kusoma vitabu zaidi kupata maarifa, wajifunze lugha za kishindani ili kushindana na vijana wenigne kote duniani
7. Watueleze watatumia vipi rasilimali nyingi zulizonazo kuondoa kabisa umasikini nchini. Tuna watu wengi (nguvu kazi), ardhi kubwa, bahari, maziwa, mito, jua (umeme jua), madini anuwai, gesi asilia, vivutio vingi vya utalii kwa uchache tu mlima Kilimanjaro, Serengeti, Ngorongoro, Ruaha, Mikumi, etc..Visiwa vya Zamzibar...

Baadhi ya viongozi wa siasa Tanzania wakiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Dar es Salaam,
31/08/2015