Tuesday, February 28, 2012

Kumbe wabunge wetu ni maskini vile !

Jengo la kisasa la Bunge la Tanzania huko Dodoma
Mbunge ni mwakilishi wa moja kwa moja wa wananchi wengine kwenye chombo rasmi cha kuwasilishia mawazo na maoni ya wakaazi wa nchi wenzake. Kwa hivi ni mtu muhimu katika jamii, japokuwa anabaki kuwa mtumishi wa wananchi, kwani wao ndio hasa wanaompatia ridhaa ya kuwaongoza.

Sasa ili mtu huyu aweze kufanya kazi yake vizuri ni vyema kwa hakika kuwa na mazingira stahiki ya kufanya kazi zake kwa weledi na hasa kwa uzalendo unaojidhihirisha kabisa.

Ili kuwa mbuge kwa Tanzania, tunahitaji mtu mwenye kuwa na sura na mfano wa watu anaowawakilisha ndio maana enzi zile wakaitwa 'ndugu' hivi leo ni waheshimiwa. Pamoja na kufanana na waajiri wake kwa maana ya kuyafahamu vyema mazingira yao na inafaa zaidi akiishi huko huko na wala si mjini tu, inafaa awe na nafasi kiasi ya kiuchumi kiasi ili mambo mengine yanayohusu kazi yake aweze kuyamudu kwa pesa zake mwenyewe. Si saw kila kazi ihitaji kodi za watanzania, hapo ndio has inafaa ajiulize anaifanyia nini Tanzania?

Makala hii imechochewa na taarifa niliyoiona kwene televisheni hivi karibuni na hatimaye kuingia kwenye mtandao wa youtube ikielezea japo kwa kifupi tu hali ngumu kiuchumi ya ndugu zetu wabunge. Hayo yamedhihirishwa na kiongozi wa bunge hilo la Tanzania alipoongea na wananchi wa jimbo lake huko Njombe. Kwa habari zaidi tazama hapa

Kwa hakika jambo hili nimeniacha na maswali mengi kuliko majibu. Kwanini watangaza nia hutumia nguvu na wakati wao mwingi vile kujinadi mbele ya wapiga kura ili wapate nafasi hii yenye umasikini wa kutupa?

Je, wengi wao huenda bungeni bila kujua kuwa kuna umasikini wa kiwango hicho?

Uwezekano mwingine wa suala hili ni kuwa watangaza nia na hatimaye wabunge wetu ni watanzania wenye uzalendo sana na  hakika maslahi ya taifa letu yamo mioyoni mwao kiasi kwamba pamoja na umasikini ulio bungeni, ambao nadhani watakuwa wakiufahamu kwani kwa hali ya kawaida mtu hufanya kwanza utafiti wa kile anachokitatuta, bado huamua kwenda bungeni kwenye umasikini wa kutupa.

Wabunge ni wawakilishi wa moja kwa moja wa watanzania. Na hivi wanabeba sura ya nchi yetu; bunge pale Dodoma likiwa kazini inamaanisha kuwa Tanzania yote kupitia majimbo ipo pale katikati ya nchi hii tukufu, na hivyo wawakilishi hawa lazima kuwajali vilivyo. Sasa kwa kuwa kiongozi wa moja ya nguzo kuu za uongozi wa taifa letu amesema kuwa kuna umasikini katika chombo hicho, itakuwa vigumu kwa hawa watumishi wetu kufanya kazi vizuri. Inafaa tutatue tatizo hili kwa kuwawekea wazalendo na watanzania wenzetu hawa mazingira mazuri ya kufanya kazi. Kwa kuwa tuna uzoefu wa kutatua matatizo yetu wenyewe basi natulitatue njia mojawapo ni kuunda tume kwaajili ya kuchunguza ukata unaowakabili waheshimiwa wetu.

Kupitia uchunguzi huo tupate mwongozo wa nini cha kufanya...
Picha zote kwa hisani ya google!

Wednesday, February 22, 2012

Uelewa kwa vitendo!

Wanachuo wakionyesha uelewa kwa vitendo chuoni STEMMUCO
Hapa kaka akifanya kweli
Wanachuo wakionyesha uelewa kwa vitendo chuoni STEMMUCO
Dada hakubaki nyuma katu!

Monday, February 20, 2012

Elimu ya Majanga - Zima Moto!

Ndugu Ibrahim Badiri - Mtaalamu wa kikosi
Cha zima moto Manispaa Mtwara-Mikindani
akitoa mafunzo juu ya majanga hususani moto
Baadhi ya wanachuo wa Stella Maris Mtwara University College (STEMMUCO) walipata mafunzo juu ya majanga na hasa juu ya moto.

Katika mhadhara huo uliofanyika chuoni hapo, ndugu Badiri alisema watanzania wengi hawana elimu ya kujiokoa toka kwenye majanga na hivyo basi tatizo kama la moto linapotokea inakuwa vigumu kujiokoa.

Mtaalamu huyo alichanganua aina za moto: moto utokanao na mada za kioganiki, moto utokanao na hitilafu ya umeme, moto utokanao na gesi na moto utokanao na madini na vyuma mbalimbali. Kupambana na moto alisema kila aina ya moto huzimwa kwa kizima moto mahususi.

Moto wa vifaa vya kioganiki huweza kuzimwa kwa maji, poda / unga mkavu maalumu, mchanga
Moto wa umeme huzimwa kwa poda/unga mkavu maalum,
Moto wa gesi, kama ule wa kituo cha mafuta huzimwa kwa mchanga, poda / unga mkavu maalum
Moto wa madini huzimwa kwa poda/ unga mkavu maalumu.

Baadhi ya wana STEMMUCO wakifuatilia mafunzo hayo
Hata hivyo mtaalamu huyo alisema njia hizi hufanyika zaidi kama huduma ya kwanza na pia kwa moto ambao bado haujawa mkubwa, hulenga zaidi moto ambao ndo kwanza unaanza.

Sunday, February 19, 2012

Binadamu hujiumba

A man, as a general rule, owes very little to what he is born with - a man is what he makes of himself.










































Kanuni ya maisha ni kwamba, binadamu hutegemea kwa kiasi kidogo mno kile anachozaliwa nacho, kimsingi binadamu anaamua yeye mwenyewe kuwa anavyotaka yeye mwenyewe.

Alexander Graham Bell.

Mwenyezi Mungu anatuumba mara moja na kutupatia pumzi ya uhai. Pumzi hiyo ya uhai nd'o has maisha yenyewe; hiyo ndo hasa sayansi bado haiwezi kuelezea ni nini hasa. Tunapozaliwa tunakuwa tumekamilika idara zote za miili yetu. Hata hivyo maamuzi ya binadamu awe nani ni suala na maamuzi binafsi lakini muhimu hasa kama tunapenda maisha yetu yawe na maana na kuleta furaha na maana kwa maisha ya watu wengine.
 
Kuvumbua, kuibua, kuja na wazo jipya na kadhalika ndo hasa mambo amabayo tunatakiwa tuyafanye ili kweli maisha yetu yawe na maana kabisa. Kutafuta na kukusanya mali kwa bidii zote (hili ndilo jambo ambalo wengi wetu hulifanya) ni muhimu na vyema kabisa ili kuupiga vita umaskini na uhohehahe lakini pesa isiwe ndio lengo letu kuu; pesa itumike tu kuboresha maisha ya jamii ya wanadamu kote duniani.
 
Hivi leo vijana wengi hapa Tanzania hatufahamu hasa nini maana ya maisha yetu tunadhani lengo la maisha ni kusaka pesa tu "mkwanja" hasa tukikutana na maneno na ushawishi wa vijana wa Marekani ama bara Ulaya, "Jitahidi kupata mali maishani ama kufani". Kamwe hili si lengo la maisha, jambo muhimu tukumbuke kila mwanadamu ana nafasi ya kujiumba na kuwa anavyotaka awe! 

Friday, February 3, 2012

Maneno ya kujenga na kuimarisha zaidi

Maneno ya kujenga na kutia moyo kwa vijana na wengine wote wenye nia ya kujiendeleza yanapatikana katika mtandao wa Advance Africa ambao hutoa taarifa ya nafasi nyingi za masomo ya juu zaidi. Kwa wanaopenda kujifunza juu ya nafasi hizo wasome hapa


If you think you are beaten, you are.
If you think you dare not, you don't.
If you like to win but think you can't,
It's almost a cinch you won't.

If you think you'll lose, you're lost.
For out in the world we find

Success begins with a fellow's will.
It's all in the state of mind.

If you think you are out classed, you are.
You've got to think high to rise.
You've got to be sure of your-self before
You can ever win the prize.

Life's battles don't always go
To the stronger or faster man.

But sooner or later, the man who wins
Is the man who thinks he can.

C. W. Longenecker.


        "When one door closes another door opens; but we so often look so long and so regretfully upon the
                                      closed door, that we do not see the ones which open for us."

 Alexander Graham Bell.