Tuesday, July 5, 2011

SIKU YA JUMUIYA SAUT - Mtwara

Jumuiya za watu duniani zinajenga utamaduni wa kukutana kwa malengo mbalimbali. Kuimarisha umoja wao, kujenga uzalendo kwa jumuiya na kadhalika. SAUT Mtwara ni jumuiya ya wasomi; watu wanaoandaliwa kuwa wajenzi wa dunia. Kwa kuwa jumuiya ya aina hiyo ina jukumu kubwa la kujielimisha zaidi ili kuondoa ujinga binafsi na kuisaidia jamii yake, basi inafaa mara mojamoja kupata nafasi ya kujipumzisha. Tarehe 4 Juni, 2011 ilikuwa ni siku ya jumuiya hiyo.

Kulikuwa na shughuli kadha wa kadha kuishi siku hiyo; ikiwa ni pamoja na hotuba anuwai za kitaaluma na maonyesho toka idara za hapo chuoni.

Sehemu ya wanajumuiya ya Saut wakianza sherehe za siku yao kwa maandamano.

No comments:

Post a Comment