Thursday, July 7, 2011

KAZI YA TANU NA TANZANIA YA LEO


Viongozi wa TANU
Flag of TANU.svg
Bendera ya TANU
Tarehe 7 mwezi Julai, 1954 (7.7.1954) ni siku ya kuzaliwa kwa chama cha kisiasa kilichosaidia kudai uhuru wa Tanganyika. Tanganyika National Union (TANU) kilikuwa Chama cha kisiasa kilichowaunganisha wananchi wengi wa kawaida wa Tanganyika na kuwa na nguvu ya pamoja kupigania uhuru wao.

Chama hicho kilikuwa na imani na ahadi za mwanachama. Nazipenda hasa ahadi za mwanaTanu. Ahadi hizo kwa hakika inafaa ziwe ndo TUNU za taifa letu la jamuhuri ya muungano wa tanganyika na Zanzibar- Tanzania. Ahadi za TANU ambazo zimeasiriwa na Chama cha Mapinduzi, (CCM), ni mali ya watanzania wote kwa sababu zililenga kuikomboa nchi na wananchi wote kwa pamoja bila kujali itikadi zao za kisiasa, rangi, dini, wala kabila. Chama cha TANU na pia CCM ndani ya mfumo wa chama kimoja kilikuwa ni mali ya waTanzania wote na hivyo basi ahadi hizo za mwanaTANU ni mali ya waTanzania wote.

Hivi leo tunapokuwa katika mfumo wa vyama vyingi ni dhahiri kuwa vyama vya kisiasa vina katiba, imani na miongozo mbalimbali ya kisiasa, hiyo ni vyema kwa ushindani wa kisiasa. Tanzania kama nchi, pmoja na kwamba ina mwongozo mama-Katiba, inafaa iwe na TUNU ambazo zitafuatwa na wananchi wote bila kujali itikadi zao za kisiasa. Ahadi za mwanaTANU zinaweza kutufaa sana.

AHADI ZA MWANATANU

(1)Binadamu wote in ndugu zangu na Afrika ni moja

(2) Nitaitumikia nchi yangu na watu wake wote

(3) Nitajitolea nafsi yangu kuondosha umaskini, ujinga, magonjwa na dhuluma.
(4) Rushwa ni adui wa haki, sitapokea wala kutoa rushwa.
(5) Cheo ni dhamana, sitatumia cheo changu wala cha mtu mwingine kwa faida yangu.
(6) Nitajielimisha kwa kadri ya uwezo wangu na kuitumia elimu yangu kwa faida ya wote.
(7) Nitashirikiana na wenzangu wote kujenga nchi yetu.
(8) Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko.
(9) Nitakuwa mwanachama mwaminifu wa TANU na raia mwema wa Tanzania na Afrika.


No comments:

Post a Comment